Lazima tuwekane sawa kuhusu UKIMWI

SERIKALI imepiga marufuku wahubiri wa dini na waganga wa jadi wanaojitangaza kuwa wana uwezo wa kutibu ugonjwa wa UKIMWI, kwani kufanya hivyo ni kuendelea kuchochea maambukizi ya ugonjwa huo ambao hadi sasa hauna tiba wala chanjo.

Akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalumu, Lucy Mayenga (CCM) kuhusu watu wanaojitangaza kutibu UKIMWI wakati hauna tiba, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Aisha Kigoda alisema watu hao ni wapotoshaji kuhusu hali halisi ya ugonjwa huo.

Alisema wananchi wawe makini na watu hao na wazingatie maagizo yanayotolewa na serikali kupitia wahudumu wake wa afya kuwa, UKIMWI hauna tiba yoyote zaidi ya dawa za kuongeza kinga ya mwili.

Akijibu swali la Msingi la Mbunge wa Viti Maalumu, Margareth Mkanga (CCM), aliyetaka kujua lini serikali itasitisha matumizi ya Kadi za Bluu zinazotumiwa na waathirika wa UKIMWI wakati wa kutibiwa kwani zinawanyanyapaa, Naibu Waziri huyo alisema kwa sasa serikali haina mpango wa kusitisha matumizi yake.

Alisema kuwa kadi hizo zinawasaidia wagonjwa wa UKIMWI kupatiwa tiba hata katika vituo ambavyo hawakuwa wakivitumia awali, kwani kwa kuonyesha vitambulisho hivyo, hutambuliwa na kupatiwa tiba.

Naibu waziri huyo alisema vitambulisho si sababu ya kuwepo kwa unyanyapaa, unatokana na uelewa wa jamii husika kuhusu ugonjwa huo kwani wapo wagonjwa wa kifua kikuu ambao nao pia hutibiwa kwa kutumia kadi za kijani.

Kwa upande wa wahudumu wa afya ambao wanaonyesha unyanyapaa kwa wagonjwa wa UKIMWI baada ya kuwaona wakitibiwa kwa kadi hizo za bluu, Naibu Waziri alisema serikali haitakuwa tayari kuwavumilia na kuahidi kuwachukulia hatua ikiwa ni pamoja na kuwafukuza kazi.
Kumbe hata nyie ni member, duh
 
Siku moja nilikuwa katika ofisi fulani nataka kufanya kazi, kabla sijaanza ile kazi, dada moja wa office ile akaniambia kwamba anayetumia office hiyo ni muadhirika wa UKIMWI, angalia vizuri sana hapo mezani unavyofanya kazi na kushugulika, ni kweli nilishangaa yule jamaa ni kigogo lakini ana viwembe mezani kwake, kuna pini ameziweka tu bila mpango na mambo mengine ambayo ukigusa unaweza kuchomwa na kuweza kuambikizwa labda

Kuona vile sikuendelea kufanya ile shuguli, nilimwomba huyu mama abebe mzigo wake aulete kazini kwangu kwa pale ni ngumu kuendelea nayo kwa sababu ni mtu ambaye ninatembea na kuzunguka naweza kujisahau na kushika vitu vyake alinikubalia

Kwa hiyo hii ndio jamii ya watu tuliokuwa nao katika jamii yetu wameadhirika na ugonjwa Fulani lakini, anaweka mitego au chambo kwa wenzake waingie katika mambo yake ambayo kwa kweli hayavutii mbele ya jamii iliyostarabika hata kidogo hata kama anacheo gani

Huo ni ukumbusho tu -- KUMBUKA KWAMBA

Tarehe 1 Desemba kila mwaka ni siku ya UKIMWI duniani, siku hiyo watu mbalimbali hukumbushana na kuelimishana kuhusu Ugonjwa wa UKIMWI na kushirikiana katika mambo mengi ambayo nia yake au malengo yake ni kupunguza maambukizo ya UKIMWI sio kuzuia, kuzuia ni ngumu kwa sababu watu wengi wameshaadhirika na wengi wao wamejificha majumbani, maofisini, mashuleni, vyuoni na sehemu zingine nyingi sana ndio maana tunaongelea kupunguza na sio kuzuia.

Kuzuia maambukizi ya UKIMWI au ugonjwa wowote wa zinaa ugumu wake unakuja kuwa ngumu kwa sababu ni jukumu la mtu binafsi ( personal ) yeye mwenyewe ajizuie sio wewe umwambie aache , na mbaya zaidi watu wengi wanaoambukiza au kuambukizwa ukimwi ni watu wenye akili timamu na wengi wao wanajijua wameadhirika na kuendelea kuambukiza wengine na wengine kadri ya siku zinavyozidi kwenda

Kwa upande wa wale watu wenye kipato kidogo wao hawana wasiwasi , si ARV ziko ? kwahiyo atafanya anachojua yeye akiadhirika anapesa kidogo, za kuweza kuzitumia anunue hizo dawa za kuongeza nguvu na mambo kama hayo pamoja na madawa mengine mengi ambayo masikini wa kawaida sio rahisi apata, I wish kungekuwa hakuna ARV watu wengi wangeona hali halisi ya mtu anayeadhirika yukoje inakuwaje .

Wengi wameadhirika tunatembea nao njiani , wamependeza , wanavutia , wana furaha na mambo mengine mazuri lakini siri wanazijua wao wenyewe kwa hapa Tanzania hakuna mtandao maalumu wa kuwaweka wazi watu wanaosumbuliwa au walioadhirika na ukimwi , mfano USA kuna website maalumu yenye majina ya wagonjwa wote wa ukimwi kwahiyo unaweza katika tovuti ya serikali na kuangalia majina halisi na mahala wanapoishi waadhirika.

Hali hiyo na ujuzi huo umesaidia kupunguza maambukizi na kuzuia kabisa maambikizi kwa baadhi ya watu na jamii zingine , kila mtu sasa najua nani ameadhirika na anakuwa makini katika mahusiano yake na maisha yake ya kawaida bila hofu bila hiyana yoyote .

Wakati hapa naendelea kuandika , kuna mambo nafikiria kuhusu aina za jamii ambazo ziko hapa duniani kuhusu huu ugonjwa wa ukimwi , MWINGINE ATASEMA AHH NAJUA KUNA UKIMWI KWAHIYO ?? , HUYU NAE ATAKUJA NA LAKE , NAJUA UPO NA NINATUMIA KONDOM , MPENZI WAKE NAYE ANASEMA AHH BWANA MIMI NAMWAMINI MPENZI WANGU , MZAZI WAKE ANASEMA MIMI NIMEKUWA NA MKE WANGU KWA MUDA MREFU KWAHIYO SIWEZI KUADHIRIKA , NA MTOTO WAKE NAYE ATASEMA SIKU HIZI KUNA ARV NIKIPATA UKIMWI NTATUMIA ARV NIISHI MUDA MREFU .

Vituko kibao na majigambo kibao ambayo hayana msingi wala maana ukifikiria kwa umakini zaidi , lakini yote tisa , la kumi na mwisho ni mtu kujua kwamba ukimwi upo , utaendelea kuwepo na kusambaa zaidi kama hujaadhirika basi rafiki yako ameadhirika , ndugu yako , mpenzi wangu au jirani yako , mfanyakazi mwenzako na watu wengine ambao huwa unakutana nao mitaani au sehemu za mihangaiko yako .

Inahitajika jitihada za dhati na za uhakika kuweza kupunguza na kufanya ugonjwa wa ukimwi historia na usiendelee kuuwa na kuambukiza ndugu zetu na jamaa zetu wengine wa karibu , hawa tunawapenda , wengine ndio wametusomesha mpaka kufikia hapa tulipo , wengine wanatufundisha mashuleni , wengine tunashirikiana nao katika mambo kadhaa , tunaenda kuendelea kushirikiana nao kwa vitu vingi zaidi ili kujenga jamii na taifa lililo kuu na lisilo na wagonjwa wa UKIMWI .

UKIMWI UPO , UTAENDELEA KUWEPO , KUANGAMIZA WATU NA KULETA MADHARA KATIKA JAMII NYINGI , DUNIANI , NA WEWE NI TARGET YA UKIMWI , LAKINI UNAWEZA KUUKWEPA USILENGWE NJIA ZINAJULIKANA NA ZIKO WAZI KABISA .
Hakika maandishi yanaishi! Pumzika kwa Amani Member
 
Mika
Nilisikiliza kipindi cha Femina Talkshow cha wiki hii kwa masikitiko makubwa sana. Kuna dada mmoja mlemavu alipata ukimwi na kutelekezwa na familia yake. Mwanadada huyo aliamua kueleza wazi kuwa ni muadhirika akitegemea kupata msaada kutoka kwa familia yake. Chakushangaza ni kwamba alinyanyapaliwa na kutengwa na familia yake. Kwa sasa analelewa na mtu aliye wa familia yake. Ni ndugu wa kutoka kijiji kimoja. Mambo kama hayo yapo kwenye familia nyingi. Ndio maana tulio wengi tunaogopa kujitangaza. Kwani kujitangaza ni kunyanyapaliwa na jamii na pia kutengwa. Huyu mlemavu alijitoa mhanga na kujitangaza. Alikuwa na ujumbe mzito kwa wa-Tanzania. Kwani tulio wengi tunadhani walemavu hawana ukimwi? Dunia imebadilika. Hakuna mlemavu, watoto wa shule wala nani. Wote wanao. All are vulnerable to HIV/AIDS.

Ni wajibu wetu kama jamii kuwahudumia waadhirika wa ugonjwa huu kwa hali na mali. Kwani wote ni watarajiwa wa ugonjwa huo. Nilisoma jana kwenye jamii forums kwamba kuna mtoto alikuja papai na kupata HIV. Uchunguzi ulipofanyika uligundua kwamba aliyemuuzia mtoto huo papai alikuwa na jeraha liliokuwa linatoa damu. Kwa hali hiyo mtoto alipata ukimwi kwa nia hiyo. No one is safe against this killer disease.

Ninatoa pongezi kwa kipindi cha Femina Talk Show hiki kwani kinatoa mambo muhimu yanayozikumba jamii zetu. Kwa hiyo tujifunze kupitia kipindi hiki.
[/QJF itaishi milele
 
SERIKALI imepiga marufuku wahubiri wa dini na waganga wa jadi wanaojitangaza kuwa wana uwezo wa kutibu ugonjwa wa UKIMWI, kwani kufanya hivyo ni kuendelea kuchochea maambukizi ya ugonjwa huo ambao hadi sasa hauna tiba wala chanjo.

Akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalumu, Lucy Mayenga (CCM) kuhusu watu wanaojitangaza kutibu UKIMWI wakati hauna tiba, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Aisha Kigoda alisema watu hao ni wapotoshaji kuhusu hali halisi ya ugonjwa huo.

Alisema wananchi wawe makini na watu hao na wazingatie maagizo yanayotolewa na serikali kupitia wahudumu wake wa afya kuwa, UKIMWI hauna tiba yoyote zaidi ya dawa za kuongeza kinga ya mwili.

Akijibu swali la Msingi la Mbunge wa Viti Maalumu, Margareth Mkanga (CCM), aliyetaka kujua lini serikali itasitisha matumizi ya Kadi za Bluu zinazotumiwa na waathirika wa UKIMWI wakati wa kutibiwa kwani zinawanyanyapaa, Naibu Waziri huyo alisema kwa sasa serikali haina mpango wa kusitisha matumizi yake.

Alisema kuwa kadi hizo zinawasaidia wagonjwa wa UKIMWI kupatiwa tiba hata katika vituo ambavyo hawakuwa wakivitumia awali, kwani kwa kuonyesha vitambulisho hivyo, hutambuliwa na kupatiwa tiba.

Naibu waziri huyo alisema vitambulisho si sababu ya kuwepo kwa unyanyapaa, unatokana na uelewa wa jamii husika kuhusu ugonjwa huo kwani wapo wagonjwa wa kifua kikuu ambao nao pia hutibiwa kwa kutumia kadi za kijani.

Kwa upande wa wahudumu wa afya ambao wanaonyesha unyanyapaa kwa wagonjwa wa UKIMWI baada ya kuwaona wakitibiwa kwa kadi hizo za bluu, Naibu Waziri alisema serikali haitakuwa tayari kuwavumilia na kuahidi kuwachukulia hatua ikiwa ni pamoja na kuwafukuza kazi.
Je, ilifanya kazi au ilikuwa propaganda tu?
 
Back
Top Bottom