Kyela: Dr. Mwakyembe amtolea Uvivu Rostam

Kyela: Dr. Mwakyembe amtolea Uvivu Rostam

Gozi gumu,
..
Mkuu soma maandiko yako utaona jibu umeliandika mwenyewe.. Ametajwa na nani kisha unasema Ametajwa kuhusika na.. wewe umeipata wapi hiyo kama hakutajwa..
Hoja ilikuwa Dowans na sio Richmond! na kama haya mashirika hayahusiani imekuwaje kesi ya Dowans yarudishwe maswala ya Richmond ambayo kesi imekaliwa bungeni..Je, mnakubali kuna uhusiano..au?..
Hakuna hata sehemu moja ya maelezo ya kamati ya Nishati na madini (Mwakyembe) kuhusiana na Dowans wamegusia Richmond au hata kumtaja Rostam isipokuwa Dowans na kile walichokuwa wakiuza..Leo yeye karudishiwa kesi nzima ya Richmond wakati hakuna mtu aliyeuliza kuhusiana na Richmond.. mbona hamtaki bunge ilizungumzie swala la Richmond tena kesi mmeifunga tayari..Kama kweli mnataka ushahidi na ukweli kuhusiana na Richmond liambieni Bunge lifungue mara moja kesi ya Richmond tutamjua mchawi nani!..Ya Dowans yabakie Dowans na utapeli wake..Na mkitaka kuunganisha yote then hata Mwakyembe ana haki ya kuunganisha toka kule anakokufahamu yeye iwe hata Igunga!

Mkandara, Pengine hukuwa mfuatiliaji mzuri wa hili sakata. Huku kuchafuana kumeletwa na gazti kusema kuwa Mwakyembe hatueleza kuwa alikuwa na intererst wakati akitumikia Kamati ya Richmond Fullstop.
Current issue ya Dowans kamati ya Mwakyembe haikuwa muhusika bali ya Zitto na ya Shelukindo, umeelewa?
 
Game Theory,
Mkuu kama Mwakyembe alikula mchango wa Rostam asingeinua hata kidole, tunawajua wote waliokula hizo fedha wanaingia Bungeni na kuuchapa usingizi kusubiri kura za kupinga hoja zote zinazohusiana na Rostam..Wanajulikana mkuu wangu, Mwakyembe hayupo ktk hesabu hizo wala Rostam asingemwacha unajua yaliyomkuta Mtikila...tena basi hata kugombea tu Ubunge ilikuwa shughuli kubwa hawakumtaka kabisa asimame isipokuwa yule msomi mwingine aliyekula hela akapigwa chini.....mara umeshalisahau vagi ile!

Alikuwemo ndani ya KAPU LA CCM.
 
Alitumia muda mwingi kumtukana Rostam.

Waungwana,

Miye bado nasubiri matusi ambayo Mwakyembe alimtukana fisadi Rostam maana katika habari zote niliziona hadi sasa kuhusiana na aliyoyazungumza Mwakyembe akiwa Kyela sijaona yoyote iliyozungumzia matusi yaliyovurumishwa na Mwakyembe.
 
Vita vya Rostam na Mwakyembe amevianzisha Rostam mwenyewe na hii vita sio ya mwakyembe pekee ni wengi wako kwenye vita hii kwani kundi la Rostam likiongozwa na Lowasa linawaonea wengi.

Kiini cha mgogoro huu kimeanzia kwenye research results za power pool ea, Rostam alitaka kuiba results na baadhi ya wadau akishirikiana na Lowasa, walivyoshindwa waliamua kuhakikisha kuwa mradi ule hautafanikiwa, moja wanahakikisha hakuna bank au serikali ya tanzania kuisaidia kampuni ile.
pili, hawapati sehemu yeyote ya kuwekeza mradi huo, vita yao ikaanzia singida.

Tatu watawapaka matope wote wanaoshiriki mradi huo kwa kutumia magazeti walioyaanzisha na wabunge waliowaingiza bungeni na wafuasi wao mawaziri kama Ngeleja nk.

Nne kwa sababu mradi huo hauna vigogo wanaotambulika basi haufai tanzania.

Hapa hakuna maslahi kwenye kamati bali kuna ile dhana ya mweusi asiwe na kampuni kwani huwa wanawasumbua sana waburushi wachache.
Ikumbukwe baada ya uhuru wa bendera bado mtanzania hajapata uhuru wa kiuchumi ndio maana leo hakuna mweusi mwenye nguvu ya kweli kupigana na mafisadi kwani wengi wanategemea hawa mafisadi kuishi, kufanyakazi, na kuwa wanasiasa. Najua hoja itakuwa kinepi ni mmbaguzi la hasha hii ni hali halisi haya ndiyo yaliyotokea mareakani mweusi kutawaliwa baada ya ubaguzi kwisha kwa sababu za kiuchumi vilelvie Afrika ya kusini bado mweusi ana njia ndefu kabla hajawa na nchi lazima tubadilishe mtizamo wetu kwenye uchumi na kuwaona na tusio wategemea kuwa wanaweza

Tusipokata hii chain hatuwezi kuendelea. hatuwezi kuwa na wabunge ndani ya bunge walionunuliwa na kina rostam, jeetu kama tu wale wa Mobutu.

Naomba kuwasilisha hoja

Naamini kama hiyo vession yako ni sahihi Mwakyembe angekuwa salama kuieleza yeye mwenyewe kabla ya kushutumiwa na hata baada ya shituma basi angekuwa muwazi moja kwa moja. Issue hii unayoisema hakujitaja hata baada ya kujitetea na shutuma only to be surfaced by the third part DR. Slaa.
Mwakyembe alikuwa anaficha nini? Mtu safi anakuwa muwazi hata anapokosa sembuse anapojihisi kuwa msafi kama ajihisivyo Mwakyembe.
 
HUYU JAMAA ni mswahili mwenzetu kweli??????? maana hiyo lugha aliyotumia inatia mashaka, kajipange upya, STORY yako haieleweki na KAMWE huwezi kumlinganisha RA na Nyerere USHINDWE NA ULEGEEE

pengine ni mweusi kuliko Chenge Mramba,Mgonja na Balali.
 
Hiyo miziki yako kacheze na wenzio huko Bilicanas na kwingineko. Huna ushauri wa kusaidia lolote hapa wewe. Hata kama unatu-disguise, I think this has gone too far; kumshauri mtanzania yeyote afuate mifano ya RA, you can only be one of the killlers of this country. I prefer not to hear anything from you bwana.

Shishye, kwanza Bilicanas ni wapi? Wengine tuko shamba huku Sikonge hatujui huko wenzetu wa mjini mnaenda kucheza miziki. Yes, Mwakyembe afuate mfano wa RA na akae kimya. Ukikaa kimya maana yake unasema ndiyo na hapa na upepo unavyokwenda unaweza siku ya mwisho ukasema nilikuwa na maana hii. Ukishasema basi hilo halifutiki tena. RA hasemi kitu hata siku moja. Ila wee utaipata tu habari yake. So asitupe karata zake za mwisho mezani mwaka 2009, hadi mwakani atakuwa kaishiwa karata na kuwa mtupu.


.......eti nini?.........ajifunze kutoka kwa RA.....halafu aende "KUTUBU"!!! (wow.......thats incredible!!).........inaelekea wamfahamu vyema sana huyu RA.........."RA anacheka na kila mtu........"

duuh aisee.....mafisadi kiboko

Yes, umeshasikia RA katukana mtu? Sanasana anakwenda kanisani kujisafisha tu. Yeye harushi scud direct ila anatumia wapambe wake. Ndiyo maana Mchungaji Kishoka akasema, mambo ya kumtukana RA atuachie sisi. Yeye amwage tu data kwa vijana na vijana wazifanyie kazi. Yeye abaki tu kucheka na RA, ile unaitwa "baba anacheka uso umekunjamana..."
Kutubu kwa wapambe wake ni muhimu. Kuna watu wengi kajitengenezea uadui wa kujitakia mwenyewe. Maneno gani haya wee msomi? So what? Ungelikuwa msomi ungelisimama jukwaani kumtukana mtu ambaye hakusoma? Sasa hiyo elimu yako inakusaidia vipi? Nduli Amin alimtukana sana Nyerere, na JKN akapeleka vijana wakamlima, sasa nani mbabe? Kama kweli yeye Msomi basi anyamaze na akae chini atafakari jinsi ya kummaliza RA na si kwenda kutoa matusi. CCM ni watu hatari sana, watammaliza Mwakyembe. Ndiyo maana nasema, atafute wapi kaangukia na akatubu. Sasa hivi kabaki peke yake masikini wakati 2005 alikuwa na watu wote waliokuwa wamechoshwa na OLD SCHOOL. Wakamleta msomi...... mambo ya Kyela wayasikia lakini???

- Rostam sio tishio tumeruhusu njaa yetu kwua tishio letu, sasa kama kawaida yetu tunajaribu kutafuta mchawi kila mahali badala ya kujiangalia sisi wenyewe, ni njaa yetu ndio tishio letu!

- Mama Clinton, majuzi amesema nini Mexico, ni tatizo lao US la kubwia unga sana ndio maana mpakani kuna matatizo, simple and clear tujiangalie wenyewe kwanza!

FMES!


FMes,

Nilishasema zamani sana. Ningelijaliwa kuwa Rais, ningeliwaachia Wahindi/Waarabu/Wazungu wote walioibia Tanzania. Ila wale wote walioweka sahihi mikataba na kuruhusu wizi huo basi ni risasi tu. Banki kuu ni MIPINGO, Serikali ni MIPINGO, Bunge ni MIPINGO, Usalama wa taifa ni MIPINGO, Tanesco ni MIPINGO, DAWASCO ni MIPINGO, Rais na PM ni MIPINGO nk nk. Sasa Mhindi kaibaibaje bila ya sisi wenyewe kumfungulia milango? Wenyewe kuchukua Makasha ya pesa na kumpa? Umeshaona sahihi ya RA? EPA tunasikia kuwa ni Mkapa aliagiza pesa zichotwe. Kesho wasikia Mzee mwacheni apumzike. Halafu mtu anaanza kupiga kelel ROSTAM AZIZ, shut up!!!!!!
 
Wahindi, Wazungu, Waarabu, Wachina na yeyote yule kama wamewafisadi Watanzania wote wanastahili kuchukuliwa hata za kisheria bila woga wowote. Sheria yetu haikuweka matabaka kwamba wezi wa rangi fulan hawastahili kuhukuliwa hatua za kisheria. Hivyo fisadi Rostam naye anastahili kupandishwa kizimbani na akionekana ana hatia basi afungwe na kufilisiwa mali yote aliyoipata kwa njia za haramu.
 
Kimya cha Rostam kinamsuta sana Mwakyembe...katika hili ilitakiwa Mwakyembe ndio awe kimya lakini la hasha....ni Rotam ndiye anyeonyesha usomi wa hali ya juu kutojibizana
 
Gonjwa letu tunalijua lakini tunajidai hatulijui..sasa kumlaumu Rostam ni kama escape route...kwa taarifa yenu hata kama kesho Rostam akienda kuishi sayari nyingine matatizo yetu na ujinga wetu utabaki pale pale

GT,

Ukweli unauma ati. Ila huo ndiyo UKWELI.

"Jamaa mmoja alifungwa jela na mkewe akaamua kusaliti ndoa. Aliposaliti akaenda jela kumwambia kuwa amemsaliti na kutembea na mwanaume mwingine. Anamwambia kwa sababu 'ukweli utakufanya uwe HURU'........"


Ukweli unauma jamani. Tuwe wa kweli na tumtafute FISADI hasa wa Tanzania. Tunachofanya sasa hivi ni kama Kuvunja gari lililotumika kubeba pesa na yule mtu ALIYEVUNJA BANK zetu tunasema ohh, kateleza kisiasa, ohhh mwacheni apumzike, ohhh yeyey ana .........

Hata Mwakyembe anamfahamu mwizi hasa wa Tanzania ila hawezi kumtaja. RA si Mu-irani, yeye rahisi kutajwa na mambo yanakwisha. Wale wanataka pesa basi, na kama nyie mnazigawa za bure BoT, why not. Hata mie ningelienda kuzibeba kama wanagawa. Bahati mbaya huku Sikonge utafaamiana vipi na Mama wa Kichaga.....????
 
Hata kama tuna matatizo alfu moja na moja kipeo cha alfu mia moja na moja,Rostam naye ni tatizo moja kati ya hayo.Na watu wengi tu watasema Rostam ana rank juu sana either practically au symbolically.

Kwa hiyo msitake ku spin kwamba kwa sababu tuna matatizo mengi basi tusimmulike Rostam.

Tukisema hivyo tutakosa hata pa kuanzia.Tuanzie wapi bwana wakati matatizo yetu lukuki?

Unataka kuchanganya maji ya nazi na soda?
 
Hata kama tuna matatizo alfu moja na moja kipeo cha alfu mia moja na moja,Rostam naye ni tatizo moja kati ya hayo.Na watu wengi tu watasema Rostam ana rank juu sana either practically au symbolically.

Kwa hiyo msitake ku spin kwamba kwa sababu tuna matatizo mengi basi tusimmulike Rostam.

Tukisema hivyo tutakosa hata pa kuanzia.Tuanzie wapi bwana wakati matatizo yetu lukuki?

Unataka kuchanganya maji ya nazi na soda?


Wazambia wameanzia na CHILUBA............ Hawa ndiyo WASOMI.
 
Hata kama tuna matatizo alfu moja na moja kipeo cha alfu mia moja na moja,Rostam naye ni tatizo moja kati ya hayo.Na watu wengi tu watasema Rostam ana rank juu sana either practically au symbolically.

Kwa hiyo msitake ku spin kwamba kwa sababu tuna matatizo mengi basi tusimmulike Rostam.

Tukisema hivyo tutakosa hata pa kuanzia.Tuanzie wapi bwana wakati matatizo yetu lukuki?

Unataka kuchanganya maji ya nazi na soda?

Hivi matatizo yetu yameanza lini?
 
Heee! Ng'waniyami, hukusikia viongozi wa ngazi za juu akiwemo PM akisema kuwa Kagoda wakifikishwa mahakamani nchi itatikisika? Halafu kumbuka JK yuko mikononi mwa huyu fisadi, yeye na EL ndo walioratibu shughuli yote ya kumweka madarakani na huenda wanajua siri zake nzito ndo maana hachukuliwi hatua yoyote. Fahamu hilo ndugu yangu.

kwa hivyo tukae kimyaa kelele zisizotowa ufumbuzi zinaonyesha busara gani?
 
Mkuu kitu gani ambacho hujaelewa mbona hakuna utata wowote. Kama umefuatilia mjadala huu kwa makini majibu yote yapo wazi hakuna shida inayoonekana kwa Dr. Mwakyembe kama unavyodai. Hakuna anacho kificha kashakiri anamiliki hiyo kampuni hatahivyo kauza share zake na uthibitisho wa doc sasa shida ipo wapi. Niukweli kampuni haijaanza kazi hakuna maslahi binafsi hapo tusimtafutie sababu

Soma habari za magazeti ya leo na umsikie kukiri kuwa bado ni mwanahisa. Sasa Mkuu niamulie kati yako na Mwakyembe yupi anasema ukweli?
 
Game Theory,
Mkuu haya ya maradhi yanatoka wapi?...
Sote tunajua kwamba hata kama HIV (Ufisadi) itaondoka Afrika bado watu tutakufa kwa maradhi mengine na kifupi ni kwamba ipo siku tutakufa tu iwe natural death au ajali..Afrika is doomed, tunajua na ni kutokana na watu kama Rostam...Hivyo haitufanyi kuwa sababu leo tusipambane ya HIV...
Hayo mabaya mengine yooote ni maradhi tofauti na HIV iwe Maleria au Kisonono, sisi hatuko huko kwa sasa, nguvu yetu sisi hapa JF sasa hivi tuna deal na HIV kwa nguvu moja..na Virus wake ndio huyo Rostam... awe kigeugeu abadilike kwa kila hali na rangi ajue kwamba tunafahamu kirusi hiki kiko vipi, dawa yake inatafutwa na hao wenye Ukimwi tayari wanajificha nyuma ya jina la Chama watakufa haraka zaidi...Gonjwa linazidi kusambaa ktk miili yao na hakika sasa hivi wanashindwa hata kujificha midomo imeshaanza kubadilika rangi..
Kimya cha Rostam kinamsuta sana Mwakyembe...katika hili ilitakiwa Mwakyembe ndio awe kimya lakini la hasha....ni Rotam ndiye anyeonyesha usomi wa hali ya juu kutojibizana
Rostam aseme nini wakati mpo watu kama nyie mnaoweza kusema hadi mapovu yawatoke wakati hamna taarifa yoyote kuhusiana na mtume wenu huyu Rostam..Hata Mwakyembe angekuwa na watu kama nyie nyuma yake, bila shaka angeuchuna tu. Wewe kama umeunganishwa kuuza Co, sawa mkubwa kwani mpo wengi sana..Tunajua hilo na hakika Mwenyezi Mungu atazidi kuwaumbua.
 
Kimya cha Rostam kinamsuta sana Mwakyembe...katika hili ilitakiwa Mwakyembe ndio awe kimya lakini la hasha....ni Rotam ndiye anyeonyesha usomi wa hali ya juu kutojibizana

Ulishasikia mwizi akajipeleka mahakamani mwenyewe!? 😕 Siku zote atajitahidi kadri ya uwezo wake kuficha madhambi yake ikiwemo pia kukaa kimya bila kutoa kauli yoyote.
 
Mkandara,

Ukitaka kuuwa mti, unaweza kuanza kukata majani kwani ni sehemu ya mti.

Ila huoni ni BUSARA zaidi kuchimba mizizi na kuikata au hata kumwagia ACID ile mizizi? Mizizi ikifa na mti kwishilia mbali. Sasa kuhangaika na haya MATAWI akina RA ambao wao kama wafanyabiashara wanataka kupata faida tu. Tungeliwa-CHILUBA hapa watu, akina RA watakufa natural death.

Naanza kuamini, Wazambia ni wasomi kuliko sisi. Kama Kyela ni karibu kabisa na Zambia, kwa nini Mwakyembe asiende huko kusomea? Au jina RA linauzika zaidi kwa wananchi? Akikimbia nchi je? Atawaambia nini Wakyela?
 
Wazambia wameanzia na CHILUBA............ Hawa ndiyo WASOMI.

Umewasahau Wamalawi kainchi kadogo lakini kametuzidi kwa kila kitu wanamsimamo lakini Bongoland tutaendelea kuogopana tu.
 
Back
Top Bottom