Ubutu wa kufikiri ndio mpaka wa leo bado tuna kasumba za ubaguzi, ukitazama wachangiaji wengi pamoja na huyo Mwakyembe, wanajaribu kutowa taswira kuwa RA si mzalendo?
Jee, uzalendo wa Tanzania unapimwa kwa rangi ya mtu? dini ya mtu au ukabila wa mtu?
Upuuzi wa siasa hizi ndio unaoifanya hii nchi bado iwe nyuma na utajiri wote iliyokuwa nao! leo tunalalamika ooohh eti Rostam sio mzalendo, sababu? rangi yake au dini yake au kabila lake?
Wakati huo huo tunaona mikakati ya kukaribisha wawekezaji kutoka nje, ambao wengi wameshafanya madudu ya ajabu, mifano ipo mingi tu, haina haja ya kuirudia. Wakati huo huo tunaona ''wazalendo'' ikiwa tu, kwa rangi zao ni wazalendo, wakifanya madudu, ufisadi na ubadhirifu ambao hausemeki, hapa pia sina haja ya kutaja majina, mifano na mingi na haina haja ya kuirudia.
Ufisadi, mafisadi, hawana rangi, uzalendo wa rangi, wala dini, wala ukabila. Ukisha kuwa fisadi, umeshapingana na vitabu vyote vya dini na vya sheria za kibinadamu, halikadhalika, utapoanza kuhukumu watu kwa rangi zao, kabila zao na dini zao bila ya kuwa na ushahidi kuwa wametumia hayo kwa kufisadi, utakuwa na wewe ni fisadi mmoja wapo.
Leo waTanzania wanaojitapa kuwa si wabaguzi wanafikia kuhukumu kwa rangi? hebu niambieni, fisadi ana rangi gani? Kama ni rangi, mbona tunawafata wenye mitaji huko ulaya na merekani kuwakaribisha kuwekeza? isn't it a double standard?
Upuuzi wa kujihami uzalendo kwa ajili ya rangi tuuache, wengi wenye rangi tofauti na RA hawana uzalendo hata chembe.
Leo tukianza rangi, kesho tutaanza, huyu mngoni huyu asili yake si hapa, huyu mmakonde huyu asili yake si hapa, huyu mzanaki huyu asili yake si hapa! hiyo ndio dhambi ya kuanza kuutazama uzalendo kwa rangi zetu.
Sioni mantiki ya mtu kama Mwakyembe kuanza na kujitetea kikampuni cha-wazalendo, huo ni upuuzi wa hali ya juu, at the same time hiyo technology anayoisemea italetwa na wazalendo? si ndio hayo hayo? na hata baadhi ya wamiliki wa hiyo kampuni ni hao hao. Tusidanganyane, hakuna siasa wala uzalendo katika hili la RA na Mwakyembe, wanajificha nyuma ya pazia la siasa lakini ukweli wanaujuwa wao na washirika wao!