Wana JF,
Kutokana na habari za uhakika ni kuwa:-
Mwakyembe alibebwa na watu wengi sana kuwa pale alipo. Siku hizo alikuwa mtu mwenye akili sana na mawazo mazuri sana. Alisikiliza watu na kuchukua ushauri wao. Hii ilimsaidia sana kuwa mbunge na mtu mashuhuri. Mara baada ya kuwa MBUNGE ndipo Mwakyembe mtu akawa amezikwa na Mwana siasa akazaliwa. Akafanya mambo ya Bush kuwa ama uko na mie ama hauko na mie. Ukijifanya wee ni mtu neutral basi wewe pia unakuwa adui yake. Washauri wake wote akawazika hai katika kaburi la SAHAU. Wengine walikuwa ni wafanyabiashara wasiojali nani ni mbunge wao yaani wanakula huku na huku kama Mengi. Yeye hawa wote wakawa maadui zake wakubwa.
Biada ya miaka 4, muda umefika wa kurudisha makaratasi ili WAHASIBU wakuchambue umeifanyia nini taranta yako ya miaka 5 uliyopewa. Akiangalia mbele, nyuma, kushoto9 na kulia anakuta ile timu iliyomuweka pale yote kashaitibua, kaisaliti. Walimsihi asifanye hivyo, yeye akaona wanachemka na yeye ni MSOMI. Msomi kama yeye hawezi kuhangaika na wazee walioishiwa (Kama Malecela vile). Wazee wakaja kuwa vibosile tena na jamaa akawa analialia.
Nafikiri Dr Mwakyembe angelifaa ajifunze kutoka kwa RA. Rostam yule yeye anacheka na kila mtu. Wee mtukane tu ila baadaye anacheka na wewe na kama vile hakijafanyika kitu ila ukikaa vizuri kwenye anga zake, timu yake INAKULIMA.
Anavyofanya sasa, hata CHADEMA itabidi wamteme. Itakuwa kama wanamleta Wangwe mpya ndani ya CHADEMA. Itakuwa ni kuhesabu tu siku kabla jamaa hajaanza kurusha maugomvi yake ya magambo. Wahaya wanasema "USIJIGAMBE MBELE YA WAGAMBIRWA".
Mwakyembe, tafuta wapi ulipoangukia na nenda ukatubu......... Usipopaona au ukifikiri bado umesimama basi kweli umeishiwa. Wapambe wake mwambieni Dr, umeanguka chini sana. Hii FMes kaielezea vizuri sana. Fuateni wosia wake na msaidieni Dr. Vinginevyo ni kuwa MWAMPAKA MAFUTA NA MGONGO WA CHUPA. Atajiona Babu K. kumbe "wamhogo" yaani WAPIII!!!!!
Nakuachia huu wimbo wa Gambler, unaoasa watu wajue muda wa kukimbia meza ya kamali. Vinginevyo ujuwe wee si mcheza kamali wa kwelikweli.
YouTube - Kenny Rogers - The Gambler