Kyela: Dr. Mwakyembe amtolea Uvivu Rostam

Kyela: Dr. Mwakyembe amtolea Uvivu Rostam

Dk. Mwakyembe: Nitapambana na Rostam


• Amtaka asiwe bubu kujadili hoja anapokuwa bungeni

na Moses Ng'wati na Richard Kilumbo, Mbeya
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
MBUNGE wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe (CCM), amesema atapambana kwa hoja na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz nje na ndani ya Bunge hadi kieleweke.

Dk. Mwakyembe, alitoa kauli hiyo jana katika mkutano mkubwa wa hadhara, ulioandaliwa na wananchi na kufanyika katika viwanja vya Siasa mjini hapa, kwa lengo la kulaani kauli zinazotolewa dhidi yake kupitia vyombo vya habari vinavyomilikiwa na Rostam.

Alisema mbinu anayoitumia sasa Rostam pia wa CCM, ya kumchafua kupitia vyombo vyake vya habari, inatokana na ububu alionao anapokuwa bungeni. Dk. Mwakyembe alisema licha ya Rostam kuamua kuanzisha Bunge lake kupitia vyombo vya habari anavyovimiliki, hawezi kukaa kimpya, huku akiona watu wachache wakitumia uwezo wao kifedha alizodai wamezipata kwa njia ya ufisadi wakitaka kuiendesha nchi kama wanavyotaka.

Aliendelea kusema kuwa Watanzania wanatambua wazi kuwa fedha katika akaunti ya madeni ya nje (EPA), zaidi ya sh bilioni 40, zilichotwa na Kampuni ya Kagoda, aliyodai inamilikiwa na Rostam kwa maslahi na faida ya watu wachache.


Mbunge huyo machachari, alisema hawezi kuvunjika moyo kutokana na mbinu chafu zinazofanywa na kundi la watu wachache aliodai kuwa ni mafisadi, za kutaka kuvuruga kazi nzuri ya Kamati Teule ya Bunge aliyoiongoza kuchunguza mkataba wa zabuni ya Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond, iliyosababisha aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, kujiuzulu.

Mawaziri wengine waliojiuzulu kutokana na kashfa hiyo ni pamoja na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na Dk. Ibrahim Msabaha ambaye alikuwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Kama alivyotoa ufafanuzi katika mkutano wake na vyombo vya habari wiki mbili zilizopita, Dk. Mwakyembe alisema hakuna suala la ugongano wa maslahi kwa kutotangaza maslahi aliyonayo kwenye Kampuni ya kuzalisha umeme wa upepo ya Power Pool East Africa Ltd.

"Shutuma zinazotolewa na Rostam Aziz kupitia vyombo vyake vya habari zinashangaza, maana hakuna mgongano wa maslahi na sijavunja kanuni za Bunge, kwani kampuni inayosemwa kwamba nina hisa nayo ni ya wazalendo wa Kitanzania wapatao 50 wa ndani na nje ya nchi, hapa hakuna mgongano wa maslahi na kama kuna wanaobisha, warejeshe hoja hiyo bungeni ili tufumue yaliyojificha," alisema Dk. Mwakyembe.

Alisema malumbano yanayotokea sasa ni matokeo ya baadhi ya watu waliotemwa bungeni baada ya ripoti ya kamati yake, ambao hawakuridhika na kazi hiyo, hivyo kujaribu kulipiza kisasi kupitia vyombo vyao vya habari.

"Unajua wakati tunawasilisha ripoti yetu, kuna mambo hatukuyasema kwa sababu kuna watu walioamua kusema basi yaishe, wakaachia ngazi, hivyo hatukutoa mambo yote, sasa kama wanaona hawakutendewa haki, turudi bungeni tukatoe yale tuliyoamua kuyaacha," alisema Dk. Mwakyembe.

Mkutano huo uliohudhuriwa na maelfu ya wananchi wa Kyela, wakiwamo viongozi wa vyama vya upinzani, ulitawaliwa na mabango ya kumlaumu Rostam na watu waliodai kuwa ni mafisadi, huku wakiapa kufa na mbunge wao (Dk. Mwakyembe) waliodai kuwa anaonewa na mafisadi.

Baadhi ya mabango ambayo yalibebwa na baadhi ya wanachama wa upinzani, yalimtaka Mbunge huo kujitoa CCM na kujiunga na vyama vingine vya upinzani ili kuungana na wabunge wa kambi hiyo katika kukabiliana na vita dhidi ya ufisadi.

Awali, mkutano huo ulipangwa kuanza kwa maandamano, lakini yalikataliwa na polisi kwa sababu za kiusalama.

Hii ni mara ya pili kumshutumu hadharani Rostam kwamba anatumia vyombo vyake vya habari kupotosha umma na kumchafua kisiasa.

Hatua ya Mwakyembe kujibu tuhuma hizo, inakuja baada ya magazeti mawili ya kila siku (Si Tanzania Daima) kuchapisha habari zinazomhusisha yeye na umiliki wa hisa 1,000,000 zenye thamani ya sh bilioni 1.5 katika Kampuni ya Power Pool East Africa Ltd.

Mbali ya habari hizo kuandikwa katika magazeti hayo mawili, moja la binafsi na jingine la serikali, nyaraka kadhaa zinazomhusisha Mwakyembe na kampuni hiyo, zimesambazwa katika mtandao wa intaneti.

Mbali ya Mwakyembe, taarifa hizo zinamtaja Mbunge wa Lupa, Victor Mwambalaswa ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya TANESCO, kuwa miongoni mwa wanahisa wa kampuni hiyo binafsi ambayo wakati fulani Dk. Mwakyembe alipata kuwa mtendaji mkuu wake.

Taarifa hizo zinajaribu kujenga hoja zinazojaribu kumuondolea Mwakyembe uhalali wa kuendelea kudai kupambana na ufisadi ndani na nje ya Bunge, ilhali yeye mwenyewe akionekana kuwa na ukwasi mkubwa unaotiliwa shaka.

Taarifa hizo zinaonyesha kuwa, Mwakyembe licha ya kuwa na hisa nyingi katika kampuni hiyo, ameisaidia katika mambo mbalimbali ambayo hata hivyo hayakufafanuliwa, wakati akiwa katika wadhifa wa mtendaji mkuu.

Taarifa ambazo Tanzania Daima imezikusanya kutoka miongoni mwa wabunge kadhaa zinaonyesha kwamba, lengo kuu la kusambaza nyaraka hizo ni kujaribu kumnyoshea kidole Mwakyembe na kumuondolea uhalali wa kuendelea kupigania sekta ya nishati ilhali yeye mwenyewe akijua kuwa na maslahi.
 
Brazameni haya ndiyo mambo gani tena!!!!!? 🙁. Pamoja na kuwa hukuwepo hapa kwa muda mrefu baada ya kutekwa nyara huko Brazil lakini si unajua hizo picha ulizoziweka hapa zina mahali pake maalum? Sasa mbona umeziweka hapa!!?

Wacha tuwe na hasira maana wakati mwingine haya mambo yanaudhi na kutia uchungu wa hali ya juu. Mtu anatutapeli karibu shilingi 300 bilioni (kama huyo fisadi angeuza na ile mitambo yake michakavu) lakini leo yeye anaonekana bora kuliko Mwakyembe.

Huyo Malecelea ni mnafiki, wakati sijamsikia akitoa tishio la kuwafukuza mafisadi waliojaa ndani ya CCM eti leo anatishia kumfukuza mtu chamani kwa kulumbana kwenye magazeti!!!!
 
aliendelea kusema kuwa watanzania wanatambua wazi kuwa fedha katika akaunti ya madeni ya nje (epa), zaidi ya sh bilioni 40, zilichotwa na kampuni ya kagoda, aliyodai inamilikiwa na rostam kwa maslahi na faida ya watu wachache.

source;tanzania daima

"rostam nenda mahakamani mwakyembe anakuchafulia jina anakusingizia unamiliki kagoda"

kutoka ippmedia
mwakyembe abebwa jimboni

to hell with newhabari...
 
halafu mkiambiwa kuwa standards zimeshuka JF mnasema ohhhh sijui nini sijui nini...nimeuliza ni mahakama gani katika Jamhuri ya Muungano ya Tanzania imemtia hatiani Rostam Aziz kwa tuhuma za wizi,utoaji rushwa,ufisadi, ubadhirifu etc....sijapewa jibu

Hivi zile bara bara mbovu kule Mkuranga nayo tumlaumu Rostam? Hivi matatizo ya Tanzania wa kulaumiwa ni Rostam? Pesa kuibiwa BOT tumlaumu Rostam?

acheni hizo...


btw:

Hii style ya Rostam kutojibizana na Mwakyembe naona inamfrustrate sana Mwakyembe maana its been one week Mwakyembe anazungumza yeye tuu kwenye media na Rostam hamjibu kitu

sasa Mwakyembe na taaluma yake ya sheria anaonekana anabwatuka kama mtikila vile..very entertaining indeed
 
halafu mkiambiwa kuwa standards zimeshuka JF mnasema ohhhh sijui nini sijui nini...nimeuliza ni mahakama gani katika Jamhuri ya Muungano ya Tanzania imemtia hatiani Rostam Aziz kwa tuhuma za wizi,utoaji rushwa,ufisadi, ubadhirifu etc....sijapewa jibu

Mkuu vipi? kuna ushahidi mwingi tu umewekwa hapa jamvini unaodhihirisha kuwa Rostam ni fisadi bila shaka. Threads nyingi tu hapa za Kagoda ni ya Rostam, Richmond/Dowans etc!?

JF hatusubiri ushahidi wa mahakama, kila member anaweza kutoa hukumu (conclusion) yake kutokana na ushahidi uliopo hapa jamvini. Hii ndiyo mahakama yetu.
 
halafu mkiambiwa kuwa standards zimeshuka JF mnasema ohhhh sijui nini sijui nini...nimeuliza ni mahakama gani katika Jamhuri ya Muungano ya Tanzania imemtia hatiani Rostam Aziz kwa tuhuma za wizi,utoaji rushwa,ufisadi, ubadhirifu etc....sijapewa jibu

Hivi zile bara bara mbovu kule Mkuranga nayo tumlaumu Rostam? Hivi matatizo ya Tanzania wa kulaumiwa ni Rostam? Pesa kuibiwa BOT tumlaumu Rostam?

acheni hizo...


btw:

Hii style ya Rostam kutojibizana na Mwakyembe naona inamfrustrate sana Mwakyembe maana its been one week Mwakyembe anazungumza yeye tuu kwenye media na Rostam hamjibu kitu

sasa Mwakyembe na taaluma yake ya sheria anaonekana anabwatuka kama mtikila vile..very entertaining indeed

GT unafurahisha.

Kwanza unasema Rostam ana i own nchi, halafu unashangaa kwa nini hajapelekwa mahakamani!

Of course katika strategy za communication Rostam anam set up Mwakyembe, lakini kumbuka hii textbook strategy inaweza isifanye kazi Tanzania ambapo hiyo "dignified silence" ya Rostam inaweza kuchukuliwa kama kukosa cha kujibu. Of course Rostam anaweza kuwa anatafuta cha kupeleka kwa his CCM pawns ili kujenga case ya kum excommunicate Mwakyembe kutoka CCM.

Isitoshe uchafu wa Rostam unajulikana fika.Sasa kama unataka kumtetea on the basis of lawyerspeak na concepts za fairness na "innocent until proven guilty" katika system ambayo umesema kashainunua unaonyesha your true colors.

Mwakyembe anakosea vitu fulani, lakini in no way makosa ya Mwakyembe yako sawa na level ya institutionalized grand corruption ya Rostam.
 
Naishiwa Pumzi kuona Gen xers wanadiriki kumsemea RA. Kweli ni mfanyabiashara - lakini hata biashara kuna morals!!!!! RA anaonyesha hivyo; jibu hapana !!!!
 
Alegee kwa jina la yesu,nyerere na RA wapi na wapi? Alafu wewe umepewa kidogo nini? Mwakyembe yupo sahihi,lazima tusimame kikatiba. Kama kakutuma umpigie debe,kajipange upya!!
 
Inabidi nimshauri dada yangu safari hii ahairishe kwenda likizo........kwi kwi kwi kwi, mpaka uchaguzi mkuu upite......asije akakumbwa na matinga tinga bure........na kipunga cha huko basi tena......
 
Wana JF,

Kutokana na habari za uhakika ni kuwa:-
Mwakyembe alibebwa na watu wengi sana kuwa pale alipo. Siku hizo alikuwa mtu mwenye akili sana na mawazo mazuri sana. Alisikiliza watu na kuchukua ushauri wao. Hii ilimsaidia sana kuwa mbunge na mtu mashuhuri. Mara baada ya kuwa MBUNGE ndipo Mwakyembe mtu akawa amezikwa na Mwana siasa akazaliwa. Akafanya mambo ya Bush kuwa ama uko na mie ama hauko na mie. Ukijifanya wee ni mtu neutral basi wewe pia unakuwa adui yake. Washauri wake wote akawazika hai katika kaburi la SAHAU. Wengine walikuwa ni wafanyabiashara wasiojali nani ni mbunge wao yaani wanakula huku na huku kama Mengi. Yeye hawa wote wakawa maadui zake wakubwa.

Biada ya miaka 4, muda umefika wa kurudisha makaratasi ili WAHASIBU wakuchambue umeifanyia nini taranta yako ya miaka 5 uliyopewa. Akiangalia mbele, nyuma, kushoto9 na kulia anakuta ile timu iliyomuweka pale yote kashaitibua, kaisaliti. Walimsihi asifanye hivyo, yeye akaona wanachemka na yeye ni MSOMI. Msomi kama yeye hawezi kuhangaika na wazee walioishiwa (Kama Malecela vile). Wazee wakaja kuwa vibosile tena na jamaa akawa analialia.

Nafikiri Dr Mwakyembe angelifaa ajifunze kutoka kwa RA. Rostam yule yeye anacheka na kila mtu. Wee mtukane tu ila baadaye anacheka na wewe na kama vile hakijafanyika kitu ila ukikaa vizuri kwenye anga zake, timu yake INAKULIMA.

Anavyofanya sasa, hata CHADEMA itabidi wamteme. Itakuwa kama wanamleta Wangwe mpya ndani ya CHADEMA. Itakuwa ni kuhesabu tu siku kabla jamaa hajaanza kurusha maugomvi yake ya magambo. Wahaya wanasema "USIJIGAMBE MBELE YA WAGAMBIRWA".

Mwakyembe, tafuta wapi ulipoangukia na nenda ukatubu......... Usipopaona au ukifikiri bado umesimama basi kweli umeishiwa. Wapambe wake mwambieni Dr, umeanguka chini sana. Hii FMes kaielezea vizuri sana. Fuateni wosia wake na msaidieni Dr. Vinginevyo ni kuwa MWAMPAKA MAFUTA NA MGONGO WA CHUPA. Atajiona Babu K. kumbe "wamhogo" yaani WAPIII!!!!!

Nakuachia huu wimbo wa Gambler, unaoasa watu wajue muda wa kukimbia meza ya kamali. Vinginevyo ujuwe wee si mcheza kamali wa kwelikweli.

[ame=http://www.youtube.com/watch?v=kn481KcjvMo]YouTube - Kenny Rogers - The Gambler[/ame]
 
mambo ya nchi hii yanachosha,yanakera,lakini mimi nadhani kuna kitu kinaendelea huko CCM,ndo maana wanaanza kuanikana ovyo ovyo,binafsi siifurahii hiyo tabia ya kupigana vijembe walioianzisha isije ikawa changa la macho wanatuzubaisha tuache kufatilia issues za maana na ku-concentrate kwenye hayo malumbano yao,hiyo CCM yao iliyosema itawaita na kuwakalisha chini kwa sababu ni wana CCM wote ilifanya hayo?
Jamani hizi fighting zao sio za bure kuna kitu but lets watch this movie,i think something is about to happen in this poor country Tanzania
 
Wana JF,

Kutokana na habari za uhakika ni kuwa:-
Mwakyembe alibebwa na watu wengi sana kuwa pale alipo. Siku hizo alikuwa mtu mwenye akili sana na mawazo mazuri sana. Alisikiliza watu na kuchukua ushauri wao. Hii ilimsaidia sana kuwa mbunge na mtu mashuhuri. Mara baada ya kuwa MBUNGE ndipo Mwakyembe mtu akawa amezikwa na Mwana siasa akazaliwa. Akafanya mambo ya Bush kuwa ama uko na mie ama hauko na mie. Ukijifanya wee ni mtu neutral basi wewe pia unakuwa adui yake. Washauri wake wote akawazika hai katika kaburi la SAHAU. Wengine walikuwa ni wafanyabiashara wasiojali nani ni mbunge wao yaani wanakula huku na huku kama Mengi. Yeye hawa wote wakawa maadui zake wakubwa.

Biada ya miaka 4, muda umefika wa kurudisha makaratasi ili WAHASIBU wakuchambue umeifanyia nini taranta yako ya miaka 5 uliyopewa. Akiangalia mbele, nyuma, kushoto9 na kulia anakuta ile timu iliyomuweka pale yote kashaitibua, kaisaliti. Walimsihi asifanye hivyo, yeye akaona wanachemka na yeye ni MSOMI. Msomi kama yeye hawezi kuhangaika na wazee walioishiwa (Kama Malecela vile). Wazee wakaja kuwa vibosile tena na jamaa akawa analialia.

Nafikiri Dr Mwakyembe angelifaa ajifunze kutoka kwa RA. Rostam yule yeye anacheka na kila mtu. Wee mtukane tu ila baadaye anacheka na wewe na kama vile hakijafanyika kitu ila ukikaa vizuri kwenye anga zake, timu yake INAKULIMA.

Anavyofanya sasa, hata CHADEMA itabidi wamteme. Itakuwa kama wanamleta Wangwe mpya ndani ya CHADEMA. Itakuwa ni kuhesabu tu siku kabla jamaa hajaanza kurusha maugomvi yake ya magambo. Wahaya wanasema "USIJIGAMBE MBELE YA WAGAMBIRWA".

Mwakyembe, tafuta wapi ulipoangukia na nenda ukatubu......... Usipopaona au ukifikiri bado umesimama basi kweli umeishiwa. Wapambe wake mwambieni Dr, umeanguka chini sana. Hii FMes kaielezea vizuri sana. Fuateni wosia wake na msaidieni Dr. Vinginevyo ni kuwa MWAMPAKA MAFUTA NA MGONGO WA CHUPA. Atajiona Babu K. kumbe "wamhogo" yaani WAPIII!!!!!

Nakuachia huu wimbo wa Gambler, unaoasa watu wajue muda wa kukimbia meza ya kamali. Vinginevyo ujuwe wee si mcheza kamali wa kwelikweli.

YouTube - Kenny Rogers - The Gambler

Hiyo miziki yako kacheze na wenzio huko Bilicanas na kwingineko. Huna ushauri wa kusaidia lolote hapa wewe. Hata kama unatu-disguise, I think this has gone too far; kumshauri mtanzania yeyote afuate mifano ya RA, you can only be one of the killlers of this country. I prefer not to hear anything from you bwana.
 
Sasa naona uoza wa Mwakiembe ,Mwakiyembe alizarau Mwiba sasa mguu umeanza kumwota tende,chansi ambayo anaitafuta haipo tena atabakia kubweka kwenye majukwaa tu, wazungu wanasema too late.

Mwakiembe ni mmoja kati ya mafisadi na anafaa kulaumiwa na wananchi au WaTanzania wote kwa ujumla ,kila anapobahatika kupanda jukwaani husema wazi kuwa mengine hawakuyatoa kwenye kamati yao au hawakuyaandika ,waliamua yaishe ,sasa Mkuu Mwakiyembe hayo yalikwisha ,sidhani kama yatakusaidia kwa sasa ,uliyaficha au mliyaficha ili kuwaficha wananchi wanaotaka kujua ukweli wa viongozi waliohusika na wizi,Mwakiyembe ulificha hilo ni kosa la jinai ,moja kwa moja kwa kauli zako hizo ambazo umekuwa unazirudia rudia tayari una kosa la kujibu kwenye sheria ,kwa kuficha ukweli ambao ungewaweka uchi wahusika na ubadhirifu.Na Wananchi wangewaelewa waliyoyatenda kwa kutumia vyeo vya serikali,wananchi wangeelewa kuwa hawafai kuwepo uraiani,wananchi wangeelewa kuwa wapo waliomo ndani ambao wanaweza kusema ukweli,Mwakiembe na wenzio mpo ndani lakini mmeshindwa kuuanika ukweli ,je wenzio wanayajua uliyokuwa umeamua usiyaanike ? SI ajabu wakakuruka.

Hivyo hayo makelele yako unayoyatoa sasa ni kutafuta msamaha kwa wananchi ,ulipewa dhamana ya kuchunguza na waTanzania wakakuamini kumbe uliwadanganya au ulipewa chochote ili mengine usiyataje sasa unaonekana kama una waBlackmail wahusika kwa kuwatisha wasiendelee kupambana na wewe na zaidi ni harakati za kuwania Uraisi kwa tiketi ya CCM kati ya makundi yenu ,ndio patashika zote hizi tunazoziona ,Mwakiembe hufai na kama Chadema watamkumbatia mtu huyo basi nao watabakia kubeba lawama ,huyu ana kesi ya kujibu kujua kwanini aliwahifadhi wahujumu uchumi na aliyokuwa hakuyataja ambayo yanaonekana ni makubwa zaidi kwa jinsi anavyowatisha nayo inaonekana kama amekamata mpini wa upanga na akina Lowasa na wenziwe wamekamata makali kwamba akivuta tu wote wataishia jela bila ya kesi ,ndio maana yake ,haiwezekani kila akikurupushwa anakumbushia dhamana aliyoichukua ya kutoyaanika mambo mengine.

Namalizia kwa kusema Mwakiyembe umekosea sana na hufai kuwa kiongozi hata wa timu ya mpira unaweza ukaiuza timu kama ulivyoiuza Nchi kwa kutoa ripoti isiyokamilika kwa kuwa tu wewe na marafiki mmeamua yaishe ili wahusika wasiishie pabaya na hakuna jipya ila uliendeleza fanatic ideas za kulindana.

Wewe Mwakiembe na Rostum nyote ni wafuasi wa CCM ,ugonvi wenu hautusaidiii kwa sasa tunatafuta Chama mbadala kitakachoweza kuwashughulikia nyote katika mezani ya ukweli na sheria sawa kwa wote. Hakuna yameisha wakati nchi imeoza,maji hakuna ,umeme hakuna,vifaa vya mahospitali hakuna ,infrastructure mbovu ,kwa kuwa uwamuzi wenu ni kuwa tulindane na yaishe ili mtama usizidi kumwagika,lakini sasa mzigo wa uliyoyafichaa unahangaika nao unatafuta pakuutua.
 
Last edited:
Nakubariana na wewe 100 kwa 100 watu wametumwa humu (kagoda imetema)kwa mfano bebu fuatilia thanks tha FMES kwenye hii thread utagunduwa kitu..... utabiri wangu unatimia

Kwa hiyo mtu kupewa "thanks" na FM ES ndio kuonesha kutumiwa na Kagoda. Basi hili jamvi litakosa uhuru lililokuwa nalo, manake itafikia wakati watu wataambiana naomba uondoe "thanks" zako kwa posts zangu. Kuzungumza mapungufu ya Mwakyembe, hakufanyi uwe upande wa Rostram. Ina maana Mwakyembe akikosea watu wasiseme, manake watakuwa upande wa mafisadi?. Hapa tunazalisha mafisadi wengine ambao hawatakiwi kuguswa, manake ukiwagusa kama wamekosea unakuwa fisadi. Hatuwezi kwenda hivyo, kifanya jema unasifiwa, ukikosea unakosolewa bila kuangalia nyuma kuwa ulifanya jema.
 
kwa hiyo matatizo ya Tanzania yanatokana na Rostam?

GT,

Unaondoka kwenye mada ya ufisadi wa Rostam na kutaka ku obfuscate issue kwa kuingiza issue complex ya "Matatizo ya Tanzania yanaletwa na nani"

Ingawa ni kweli kwamba hakuna mtu mmoja aliyesababisha matatizo ya Tanzania (wote tuko responsible kwa jia moja au nyingine) hili halimuondolei Rostam ukweli kwamba yeye ni mchafu kiasi cha kutapisha.

Ni kweli wote tuna makosa ukichukua view ya "zero tolerance" towards corruption and incompetency, lakini inabidi tuwe prudent na practical.

Huwezi kumfananisha kijana aliyepo Ulaya, ambaye makosa yake yanaweza kusemwa kinadharia kwamba hajarudi nyumbani kupambana na ufisadi sawa sawa (this is actually debatable) na makosa ya fisadi kama Rostam anayefanya ufisadi wa mamilioni ya dola.

Moja ya strategy ya kujisafisha ni ku point out maovu ya wengine, katika kuangalia maovu haya, inabidi tuweke vitu katika mizani.Ndiyo maana nimesema sikatai kwamba Mwakyembe ana mapungufu yake, na tumeyasema sana katika ile thread ya press conference ya Mwakyembe, lakini sasa tunamgeuzia kibao Rostam naye.Ukiwaweka katika mizani, uchafu wa Rostam unaupita uchafu wa Mwakyembe by far.

Ukijaribu kusema Rostam hajaleta matatizo ya Tanzania (some people would argue that in the order of gravity Rostam ndiye mhujumu uchumi namba moja) unakosa point ya kwamba hatuhitaji mtu mmoja ambaye ameleta matatizo ya Tanzania ili tum indict na kum shame hapa, ukitafuta mtu huyo hutampata.

Ukichukua approach hiyo ya "Kwani Rostam ndiye kaleta matatizo ya Tanzania" utahalalisha kila aina ya ufisadi.Ni kama yule muuza madawa haramu ya kulevya anayesema "nimekuta madawa yanauzwa, hata mimi nikiuza au nisipouza wengine watauza, kwa hiyo ni bora niuze tu ili nipate faida". Ingawa inawezekana yanayosemwa na muuzaji madawa huyu kwa kiasi fulani yatakuwa kweli, hii justification haimuondolei responsibility na answerability kwa matendo yake.

Tanzania ilikuwa na matatizo kabla ya Rostam kuzaliwa, na probably ingeweza kuwa na matatizo hata bila ya Rostam, lakini tunachojua ni kwamba Rostam kachangia kiasi kikubwa sana katika matatizo ya sasa, na hawezi kujisafisha asichukue sehemu yake ya responsibility hii.
 
Last edited:
kila siku mnamshambulia mwakyembwe! mi naona hakuna msafi kati yetu kila mmoja anajua kwenye nafsi yake nini anafanya. acheni haya tufanye kazi jamani
 
he sasa tunakwenda wapi naona malumbana haya mwisho mwisho wake nini hasa?

Mwisho wake ni kutokomeza ufisadi, kama ufisadi hauishi malumbano haya na mengine kama haya hayaishi, na hayatakiwi kuisha.
 
Back
Top Bottom