Kwenye Maisha yako yote, ogopa kukataliwa na Mungu

Kwenye Maisha yako yote, ogopa kukataliwa na Mungu

Furaha na amani ya moyo inategemea na matarajio yako ya maisha(expectations)na wale wanaokuzunguka, kama ulikuwa unategemea kumiliki baiskeli tu maishani ukija kumiliki pikipiki huwezi kuwazia au kuumia sana kukosa gari, kama ulikuwa unategemea kuajiriwa kuwa mtumishi wa Halmashauri tu huwezi kuwazia sana kufika wizarani, kwenye mashirika ya ndani ya kmataifa bungeni au Ikulu, kama hukuwahi kuwazia hata kumiliki nyumba yako huwezi kuwaza na kuumia kuhusu kumiliki ghorofa n.k n.k

Kama unatoka jamii za Pwani Lindi na Mtwara huwezi kuwa na mawazo sana jinsi jamii iliyokuzunguka inavyokutazama maendeleo yako kama ukiwa unatoka Kaskazini.
Unaandika vitu vizuri sana kosa lako ni kupinga uwepo wa MUNGU MWENYEZI
 
Unaandika vitu vizuri sana kosa lako ni kupinga uwepo wa MUNGU MWENYEZI
Hakuna mahali popote napinga uwepo wa mungu, nachukia ujinga na pomposity inayaondamana na wafia dini wakijidai na kujifanya wana majibu ya mambo yote yote ya ulimwengu zaidi ya wanasayansi na critical thinkers.
 
Unaandika vitu vizuri sana kosa lako ni kupinga uwepo wa MUNGU MWENYEZI
Mnahangaika sana kuongelea habari za huyo Mungu na kumtetea ili aonekane yupo.

Huyo Mungu kama yupo, Si aje yeye mwenyewe kujitetea kama ana huo uwezo!

Mnajitungia dhana za kufikirika ambazo hazipo, halafu mnaanza kuzitetea kufosi uwepo wake.

Huyo Mungu kama kweli yupo, ajitetee mwenyewe sio kutegemea wanadamu wamtetee.
 
Maisha ambayo mnadai Mungu yupo, Ndio watoto na wanawake wanafanyiwa ukatili na huyo Mungu anabaki kimya tu!

Rejea Eipstein files, huyo Mungu alikaaga kimya tu! Alishindwa kuwanusuru wale watoto.

Rejea vita vya  Gaza, maelfu ya watoto waliuwawa. Na huyo Mungu wenu akabaki kimya tu! Bila kusaidia chochote.

Maisha ambayo yanadaiwa kuna uwepo wa Mungu ndio hayana maana kabisa.

Na uwepo wa huyo Mungu hauna maana kabisa. Kwa sababu Mungu huyo anashindwa kudhibiti maovu yasifanyike duniani.

Mungu hana maana! kwenye maisha yaliyojaa ukatili na uovu ambao angeweza kuudhibiti.

Uwepo wa Mungu mwema, mwenye upendo na huruma, Hauna maana Kwenye Dunia iliyojaa uovu na ukatili.
Sema Mzee Infropreneur haya mambo ni magumu sana kuyaamini. Nilisoma bible Mungu alitoa order kwa waisrael wakiongozwa na Yoshua kuwaua watu wote wa mji wa Yericko pamoja na mifugo yao. Yaani wauteketeze mji wote wasibakishe kitu. Ilikuwa GENOCIDE mbaya sana. Na kweli waisrael wakateketeza hadi vichanga. Huenda ni Mungu pia anaamuru vichanga vya Gaza viuwawe.
 
Sema Mzee Infropreneur haya mambo ni magumu sana kuyaamini. Nilisoma bible Mungu alitoa order kwa waisrael wakiongozwa na Yoshua kuwaua watu wote wa mji wa Yericko pamoja na mifugo yao. Yaani wauteketeze mji wote wasibakishe kitu. Ilikuwa GENOCIDE mbaya sana. Na kweli waisrael wakateketeza hadi vichanga. Huenda ni Mungu pia anaamuru vichanga vya Gaza viuwawe.
Sasa huyo Mungu sio mwema. Wala sio mwenye upendo na huruma.

Mungu anaye ruhusu Genocide ni Mungu mkatili, muuaji na hana hata chembe ya huruma.

Huyo Mungu hafai kabisa anastahili KUFURUSHWA huko alipo.
 
Maisha ambayo mnadai Mungu yupo, Ndio watoto na wanawake wanafanyiwa ukatili na huyo Mungu anabaki kimya tu!

Rejea Eipstein files, huyo Mungu alikaaga kimya tu! Alishindwa kuwanusuru wale watoto.

Rejea vita vya  Gaza, maelfu ya watoto waliuwawa. Na huyo Mungu wenu akabaki kimya tu! Bila kusaidia chochote.

Maisha ambayo yanadaiwa kuna uwepo wa Mungu ndio hayana maana kabisa.

Na uwepo wa huyo Mungu hauna maana kabisa. Kwa sababu Mungu huyo anashindwa kudhibiti maovu yasifanyike duniani.

Mungu hana maana! kwenye maisha yaliyojaa ukatili na uovu ambao angeweza kuudhibiti.

Uwepo wa Mungu mwema, mwenye upendo na huruma, Hauna maana Kwenye Dunia iliyojaa uovu na ukatili.
Uovu ufanye wewe alafu unataka Mungu afanye unavyotaka wewe
Umkatae Mungu alafu utake afanye unavyotaka wewe
Aliyekuumba wewe na vyote vinavyoonekana na visivyoonekana unajiona umemzidi akili
 
Siku ukikutana na watu wasioamini mungu wanaoishi maisha ya maana kuliko wewe utaelewa jinsi ulivyokuwa kwenye box la fikra za ujinga wa kidini.
Unajua maisha ya maana? Unafikiri walio na magari na manyumba ndio wana maisha ya maana sana kuliko wasiyokuwa nayo? Au hujui hata wapumbavu hufanikiwa hayo unayofikiri ni ya maana sana?
 
Uovu ufanye wewe alafu unataka Mungu afanye unavyotaka wewe
Kwa nini Mungu aliumba binadamu wenye uwezo wa kutenda maovu?

Huyo Mungu alishindwaje kuumba binadamu wema tu, watakao mtii na kutenda mema siku zote na wakati wote?
Umkatae Mungu alafu utake afanye unavyotaka wewe
Aliyekuumba wewe na vyote vinavyoonekana na visivyoonekana unajiona umemzidi akili
Huyo Mungu angekuwa na akili, asingeumba binadamu wenye uwezo wa kutenda maovu.

Badala yake, angeumba binadamu wema tu.
 
Haiwezekani hiyo kitu.
Ni vile concept ya Mungu ni complicated

Akili haiwezi ku operate bila kutambua uwepo wa Mungu. Ndio maana inamipaka.

Concept ya Akili nayo ni pana na haina mwisho kama ilivyo Iman kwa sababu unaelezea moja ya character ya Mungu.

mkuu kuna jamaa anaitwa Daniel Everett. mfatilie alikutana na nini alipokutana na kabila la piraha huko ndani ya amazon,Brazil

Wewe kama mchambuzi ukielewa mkasa wa huyo jamaa ndo labda utaelewa hiyo hoja unayopewa hapo


Kwa kuweka kionjo, huyu alienda kueneza dini lakini alirudi nyumbani dini kaacha na kawa mtafiti wa lugha, maana hilo kabila hata concept ya kuhesabu hawana

View: https://youtu.be/BNajfMZGnuo?si=fWMAXZ8loxE25rVj
 
Back
Top Bottom