Kwanini Tanzania tuliamua kumtumia twiga mnyama legelege kwenye nembo ya taifa?

Hoja fikirishi. Ni kama ina karibia ukweli.

Lakini Twiga japo anaonekana mrembomrembo miongoni mwa wanyama mwitu sio mlegevu kama alivyoelezwa.

Simba humudu wanyama wengi kweli, lakini kwa Twiga hammudu kirahisi.

Zipo video Simba anauwawa na Twiga. Mateke miguu ya nyuma na mbele huyatumia vizuri sana.

Ule urefu wake huonekana kama mlemavu akikimbia, lakini ndio mbio zenyewe.

Haonekani kuwa mnyama mbabe lakini nae pia anajua kujihami.

Tukiacha hayo ya Twiga. Ni kweli waTanzaia yafaa tujitafakari, tujipange kurukia ngazi ya juu ya maendeleo na ustawi.

Ulegelege, kutojali, kupuizia, kuridhika kwa vitu vidogo, kufikiria zaidi ya leo tu, uoga nk ni vitu tunavyo sana.

Tubadilike sasa.
 
Twiga ni mnyama legelege, mzuri anayevutia lakini hafaidiki na uzuri wake. Mrefu, anaona mbali na anaishia kuona tu.

Kwa kweli utambulisho wowote unaoamua ukutambulishe utabeba taswira na tabia yako.

Tanzania ni taifa ambalo ni legelege, haliko aggressive kwa lolote. Watu wake ni masikini, elimu duni lakini lina utajiri wa kutisha.

Tunamtumia twiga kujitambulisha, twiga yuko taratibu sana kwenye kujongea. Na sisi maendeleo yetu kwenye kila sekta ni ya taratibu sana. Usiwasikilize wanasiasa wanaosema tuko kwenye uchimi wa chini wa kati, jiangalie wewe binafsi.

Twiga na ukubwa na urefu wake hayumo hata kwenye the big five. Kwanini hatukutumia mnyama kama Simba, au ndege tai, au hata tembo?

Bora tungemtumia nyegere (honey badger) mnyama mbishi, mbabe, ambaye akiwa na jambo lake halali mpaka amelitimiza, mnyama asiyeogopa chochote duniani.View attachment 2490848

Kwa kumtumia twiga tumekuwa kama mwanamke mzuri asiyekuwa na akili, zinazoumia ni sehemu zake za siri. Sisi na uzuri wetu na utajiri wa rasilimali tulionao, hatutaki kujitaabisha kuzibadilisha rasilimali zetu kuwa pesa, tunataka pesa za mikopo na misada (hii ni sifa ya ma slay queen) wapige tu mizinga.
Twiga Anakula majani ya kwenye miti tu anaacha manyasi mengi ardhini kwasababu anaona uvivu kuinama. Twiga Ni sisi kabisa, tuna visingizio vingi sana vya kutufanya tusifanye kazi.


Ni aibu nchi haina hata mpango wa maendeleo wa miaka 20. Hiyo mipango ya miaka mitano mitano ni upi tumeufanikisha kwa asilimia mia moja?

Tunahitaji mabadiliko makubwa ya kimfumo, ifike mahala wanaoshindwa kutusogeza mbele tuwakatae kwa nguvu zote.

CCM na katiba ya mwaka 1977 vimeshindwa kuboresha hali za wananchi na kukuza uchumi, ni wakati sasa wote tuungane pamoja kuiweka CCM kando.

KAZI NDIO MSINGI WA MAENDELEO. NCHI MASIKINI HAIWEZI KUENDELEA KWA MSINGI WA FEDHA. NCHI MASIKINI HAIWEZI KUJITAWALA KAMA INATEGEMEA MSAADA KUTOKA NCHI ZA NJE- J. K. NYERERE

Hayo ni maneno ya Nyerere yaliandikwa kwenye Uwanja wa Mapinduzi, Uwanja wa Sokoine, kwa aibu ya kusutwa na dhamira CCM wameyafuta maneno hayo.
Tanzania siyo legelege kama unvyoona wewe labda wewe mtoa mada ndiyo legelege
 
Twiga ni mnyama legelege, mzuri anayevutia lakini hafaidiki na uzuri wake. Mrefu, anaona mbali na anaishia kuona tu.

Kwa kweli utambulisho wowote unaoamua ukutambulishe utabeba taswira na tabia yako.

Tanzania ni taifa ambalo ni legelege, haliko aggressive kwa lolote. Watu wake ni masikini, elimu duni lakini lina utajiri wa kutisha.

Tunamtumia twiga kujitambulisha, twiga yuko taratibu sana kwenye kujongea. Na sisi maendeleo yetu kwenye kila sekta ni ya taratibu sana. Usiwasikilize wanasiasa wanaosema tuko kwenye uchimi wa chini wa kati, jiangalie wewe binafsi.

Twiga na ukubwa na urefu wake hayumo hata kwenye the big five. Kwanini hatukutumia mnyama kama Simba, au ndege tai, au hata tembo?

Bora tungemtumia nyegere (honey badger) mnyama mbishi, mbabe, ambaye akiwa na jambo lake halali mpaka amelitimiza, mnyama asiyeogopa chochote duniani.

View attachment 2490848

Kwa kumtumia twiga tumekuwa kama mwanamke mzuri asiyekuwa na akili, zinazoumia ni sehemu zake za siri. Sisi na uzuri wetu na utajiri wa rasilimali tulionao, hatutaki kujitaabisha kuzibadilisha rasilimali zetu kuwa pesa, tunataka pesa za mikopo na misada (hii ni sifa ya ma slay queen) wapige tu mizinga.
Twiga Anakula majani ya kwenye miti tu anaacha manyasi mengi ardhini kwasababu anaona uvivu kuinama. Twiga Ni sisi kabisa, tuna visingizio vingi sana vya kutufanya tusifanye kazi.


Ni aibu nchi haina hata mpango wa maendeleo wa miaka 20. Hiyo mipango ya miaka mitano mitano ni upi tumeufanikisha kwa asilimia mia moja?

Tunahitaji mabadiliko makubwa ya kimfumo, ifike mahala wanaoshindwa kutusogeza mbele tuwakatae kwa nguvu zote.

CCM na katiba ya mwaka 1977 vimeshindwa kuboresha hali za wananchi na kukuza uchumi, ni wakati sasa wote tuungane pamoja kuiweka CCM kando.

KAZI NDIO MSINGI WA MAENDELEO. NCHI MASIKINI HAIWEZI KUENDELEA KWA MSINGI WA FEDHA. NCHI MASIKINI HAIWEZI KUJITAWALA KAMA INATEGEMEA MSAADA KUTOKA NCHI ZA NJE- J. K. NYERERE

Hayo ni maneno ya Nyerere yaliandikwa kwenye Uwanja wa Mapinduzi, Uwanja wa Sokoine, kwa aibu ya kusutwa na dhamira CCM wameyafuta maneno hayo.
Haaaaahaaa
 
Tanzania siyo legelege kama unvyoona wewe labda wewe mtoa mada ndiyo legelege
Tanzania ni imara kwenye nini? Kama ni michezo, Tanzania ni mdebwedo ile mbaya, kama ndio kwenye akili, Watanzania wanaamini maji yanaweza kugeuza risasi iwe maji, sasa wamekuja na mpya, wanaamini eti maji yanayoitwa maji ya upako yanawez kutatua shida zako zote ikiwa ni pamoja na kukupa hela za miujiza
 
Tulizingua sana. Tumekaa kitwigatwiga tu. Nashauri tunapochagua ndege wa taifa tusikosee tena. Sagittarius Serpentarius atatufaa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom