Willy,
Mafanikio mema mkuu. Usikatishwe na kelele za haters wa hapa JF.
Muhimu ni conviction yako katika hiyo kazi unayoomba. Ninaamini ukifanikiwa utasaidia kuingiza mtazamo mpya na mawazo mapya huko EA.
Kikubwa tu mkuu ukifanikiwa usituangushe. Watanzania ni mabingwa sana wa maneno lakini vitendo sifuri. Jikite kwenye kutatua matatizo na bahati mbaya kwenye EA yapo mengi sana.
Nimepitia majina ya wagombea na una qualifications zote za kutuwakilisha vizuri kuliko wengi wa hao waliopitishwa maana uzoefu ni mwalimu mzuri kuliko elimu ya madarasa. Inahitaji uwezo kuingia huko kwenye mameli na mpaka ukafika sehemu na kufanya mambo yako bila kubebwa na mtu. Hiyo ndio shule ya maana na ya kweli na sio kuwa na uwezo mkubwa wa kukariri ili kufaulu mitihani.
Wengine tungependa kuona watu wengi ambao wamepikika hapa JF wanachukua nafasi za uongozi kwa faida ya nchi yetu.
Mafanikio mema mkuu,
Mtanzania aka Mwakalinga.
Mtanzania
Kweli sie watz ni ma haters, lakini hii isiwe kigezo cha kutuzuia kuuliza watu maswali magumu na mepesi, nafikiri wewe ni muumini mzuri unayeamini kwamba kila anayetaka uongozi inabidi awe anaulizwa kwanza aliwahi kufanya nini na anategemea kufanya nini, kama hawezi kujibu hayo kunasababu tena nyingine ya kuongoza?
Mfano, anaongelea common visa ati akiongelea local watakuwa na free movement. Hapo sijamwelewa vizuri.
Je leo ukipata VISA ya UK utaenda UJERUMANI jibu ni hapana
Je raia wa UK anaweza kwenda ujurumani jibu ni ndiyo, anaweza fanya biashara huko jibu ni ndiyo. Na je ukipata VISA/working permit ya UJERUMANI unaweza fanya kazi Poland? jibu ni hapana.
Kuna kitu humo ndani amekielezea naomba nikili sijakielewa labda kama ana mda aje atuelezee tena. Yani hiyo common visa inauhusiano gani na local movement? na pia hiyo common visa itasaidia je kukuza uchumi?
Kingine anaongelea kama umeingia EAC basi usiogope usonge mbele, aa wapi bwana lazima uangalie na interest za nchi, mbona DAUDI KAMERUN alikataa ku sign ile sheria ya EU ya akina Sarkosy na Angela?
Unaposaini kitu ama kukikubali lazima uone nchi itanufaika kivipi? mfano hiyo common visa itawanufaisha wakenya tu, kwa sababu wao wana ndege yao na ni cheap kutua nairobi kuliko kutua Dar. Pili Nairobi ni karibu kwenda serengeti/kilimanjaro kuliko kutoka Dar.
Sasa wabunge lazima tuwaulize watalinda vipi masilahi yetu.