Kwanini Mzee Malecela alijulikana ghafla kama “Jumanne”?

Nakubaliana na sifa zote anazomwagiwa Mzee Malecela, ambazo ni haki yake. Amehimili mengi.

Swali langu ni hivi Je Malecela atakumbukwa vipi kwa mwananchi wa kawaida mtaani,mwananchi ambaye hatosumbuka au kujali kama Maalim Seif ndie mrithi wa Makamba (hypothetically), mwananchi ambaye mazao yake yanaoza shambani kwa vile chama cha ushirika/wizara havina msaada kwake, mwananchi ambaye anaji-feel kulia anaposikia "takwimu juu ya takwimu" kuwa uchumi umepanda ilhali maisha yake yanazidi kuwa magumu,mwananchi ambaye anatamani kumtoa mtu meno anaposikia eti "maisha bora hayapatikani kwa kukaa vijiweni" ilhali yeye anadamkia shambani alfajiri na kurejea jioni akiwa hoi huku amepinda mgongo,mwananchi ambae ANAFAHAMU KUWA KUNA WATU WANATAFUNA NCHI YETU LAKINI HANA UWEZO WA KUFANYA CHOCHOTE KWA VILE YEYE SIO KIONGOZI...?(Swali la ziada hapo, je Malecela kama kiongozi anayeheshimika ndani na nje ya CCM alikuwa na mchango gani katika mapambano dhid ya wala rushwa, mafisadi, wabadhirifu, majambazi na wale wote wanaofanya mambo yanayoweza kulipeleka taifa pabaya?)


Swali jingine:

Je, Malecela kwa kutotamka mapema kuwa hana nia ya kuendelea na wadhifa wa makamu wa CCM, haiwezi kujenga picha miongoni mwa wananchi kwamba amebwagwa, and therefore tarnish his image as one of the most influencial leaders CCM has ever had?Nafahamu kuwa ALISHAAMUA KUJIUZULU lakini sikuona mantiki ya kukaa kimya ilopelekea kuwepo speculations za nani atamrithi. Sintiohangaa akijazushiwa kwamba ALILAZIMISHWA KUJIUZULU (which is completely untrue, lakini sometimes uzushi unaweza kuaminika iwapo mazingira yanaupendelea).

Mwisho,nadhani ingekuwa jambo la busara kama Malecela angefanya moja ya haya mawili:

a)Kuandika kitabu cha historia ya maisha yake,na kwa kutumia kitabu hicho pamoja na mambo mengine akafafanua mambo kadhaa ambayo yamekuwa yakisemwa dhidi yake.

b)Kuna hii kauli ya "wananchi can go to hell" ambayo no matter how one might try to downplay it,inaendelea kujichomoza kila wakati unapozungumizwa wasifu wa Malecela. Pengine ingekuwa vema akafafanua alikuwa anamaanisha nini (who knows, pengine alikuwa misquoted au misinterpreted) au kama alisema kwa jazba tu za kisiasa basi itakuwa uungwana kuwaomba radhi hao walioguswa na matamshi hayo.
 
Katika yote nasema Mzee John Jumanne Malecela hakuwa fisadi wala mla rushwa ila aliishi na kula na hata kuwatetea wala rushwa.Kwa hili sijui namweka wapi huyu Mzee .Ila siasa za mabavu , wizi wa kura nk ni vyake huyu mzee mwenye majina kama Tingatinga,nk.?
Ni vizuri kama umekubali kwamba ufisadi hakuwa nao.

Hili la kuwatetea wala rushwa sina uhakika nalo Labda unipe mfano alimtetea mla rushwa gani? Na Kama Yupo aliyemtetea Basi alikosea Lakini hilo halimfanyi kumuondelea na credit zake nyingine kama tutakavyofanya kutomuondolea udhaifu wake huo kama upo.

Malecela hata kwenye vikao wakati wa Mkapa ni yeye ambaye alikuwa na uwezo wa kumpinga pale alipopotoka na hata pale walipokuwa wakifokewa kina JK kama watoto wakati hawana Kosa KWA AJILI YA KUACHANGIA HOJA TU INAYOPINGANA NA WAZO LA Mh. ni yeye aliingilia na kuweka sawa.

Nafikiri kama nilivyokwishaandika awali Kama Binaadamu ana mapungufun yake lakini bado atakumbukwa na wengi ndani ya chama chake na Taifa kwa kulitumikia ktk nafasi mbali mbali na hata baada ya Mwalimu Kuondoka kutoonyesha tamaa ya kujilimbikizia mali Kama walivyofanya baadhi ya viongozi wa Nchi yetu. Hili linathibitisha kwamba hakuwa mnafiki na aliendelea kusimamia kile alichoamini na kupita kukihubiri kwenye majukwaa ya siasa,?

Na kwa Upande wa chama chake nafikiri kitamkumbuka zaidi na kinamuheshimu na ndiyo maana kimeamua kumpa U-CC,U-NEC WA KUDUMU. Na huu ni uthibitisho kamili wa kuthamini mchango wake ndani ya chama na huenda na ndani ya Taifa kwa upande wao ,hasa ukizingatia kwamba ni Chama pekee ambacho kimeshashika dola hadi sasa.
 
Murangia ; Mlalahoi

Hebu wekeni kashfa nzito za John Malecela hapa tukate issue, tuache kuzungukazunguka bila hoja ya maana halafu tuzilinganishe na za wengine. Lazima tuwe na kipimo sio kulalama tu na kurukaruka.
 
Murangia ; Mlalahoi

Hebu wekeni kashfa nzito za John Malecela hapa tukate issue, tuache kuzungukazunguka bila hoja ya maana halafu tuzilinganishe na za wengine. Lazima tuwe na kipimo sio kulalama tu na kurukaruka.

Kweli Dua, watuwekee kashfa za huyu mheshimiwa kama wanazo, hasa kuhusu rushwa na chafu mwingine unaolitafuna taifa.
 
Dua
JF Senior Expert Member
----------------------------------------------------------------

Murangia ; Mlalahoi

Hebu wekeni kashfa nzito za John Malecela hapa tukate issue, tuache kuzungukazunguka bila hoja ya maana halafu tuzilinganishe na za wengine. Lazima tuwe na kipimo sio kulalama tu na kurukaruka.


Shukrani mkuu Dua, ndio uzuri wa hiii forum siku zote kuna vichwa vikali, huwezi ukaleta nonesense ukategmea ku-get away with it hata uwe nani! Wakuu chuki za binafsi na Malecela, mkazimalizie huko pembeni hapa zinatakiwa hoja za msingi na zitajibiwa tu, unless vianze vioja!
 
Moja ya kashfa za Malecela ni tuhuma kuhusu kiwanja cha Gymkhana ilipojengwa Sheraton ( Sasa Movenpick ) inasemekana mkuu pale kavuta na ujenzi wa Hotel katika "green" plot ile uligubikwa na mashinikizo yake.

Wataalam wa wizara ya ardhi na wa mazingira na asasi nyingine walipinga sana uvamizi ule
 
Moja ya kashfa za Malecela ni tuhuma kuhusu kiwanja cha Gymkhana ilipojengwa Sheraton ( Sasa Movenpick ) inasemekana mkuu pale kavuta na ujenzi wa Hotel katika "green" plot ile uligubikwa na mashinikizo yake.

Wataalam wa wizara ya ardhi na wa mazingira na asasi nyingine walipinga sana uvamizi ule

Inasemekana heee? Angalau tunajua Malecela hayupo kwenye list of shame ambayo ilitolewa baada ya kufanyiwa kazi pevu. Hiyo ndiyo reference ya maana ya mafisadi TZ. Nyingine ndio hizi za inasemekana. Kutoa hisia na kuzusha ni kazi rahisi mno hasa katika siasa, kimbembe kipo kwenye kutoa tuhuma zenye angalau ushahidi wa mazingira. Hapo ndipo watz wengi hatuwezi. Ila kwa kusengenya hapo mtz umemfikisha!
 
Murangia ; Mlalahoi

Hebu wekeni kashfa nzito za John Malecela hapa tukate issue, tuache kuzungukazunguka bila hoja ya maana halafu tuzilinganishe na za wengine. Lazima tuwe na kipimo sio kulalama tu na kurukaruka.
Majibu mepesi:

Katika mchango wangu, sijamlalamikia Malecela bali nilikuwa nauliza swali. Hivi lugha yetu ya Taifa imekuwa ngumu kiasi hiki that hata swali nalo linageuka kuwa lawama?As to kuweka kashfa nzito za Malecela,mie sina hata moja, na hoja yangu haikuwa kama ana kashfa au la.However,ubora wa kiongozi sio kutokuwa na kashfa, na japo kuwa na kashfa kunaweza kuchafua jina la kiongozi haimaanishi kuwa uongozi wake hautakumbukwa (a living example ni Bill Clinton). Hate it or love it,kuna mtu anayeweza kunijibu swali langu kuhusu mchango wa Malecela katika mapambano dhidi ya rushwa, ufisadi, ujambazi, uhujumu uchumi, etc etc?Mwenye jazba apuuze swali hili,mwenye jibu anipatie.
Shukrani mkuu Dua, ndio uzuri wa hiii forum siku zote kuna vichwa vikali, huwezi ukaleta nonesense ukategmea ku-get away with it hata uwe nani! Wakuu chuki za binafsi na Malecela, mkazimalizie huko pembeni hapa zinatakiwa hoja za msingi na zitajibiwa tu, unless vianze vioja!
Pamoja na kutambua kuwa kila hoja yako huwa "imekwenda shule" naomba kutoafikiana na analysis yako kwamba kuuliza maswali (kama hayo niliyouliza) kuhusu Mzee Malecela ni NONSENSE.

Kwanini kumjadili Malecela iwe nonsense, especially kama mjadala wenyewe hautawaliwi na jazba, kashfa, dharau, matusi au uzushi? Na kwanini iwe SENSIBLE kumsifia tu Malecela lakini kuhoji vitu flani juu yake iwe NONSENSE? Anyway, katika zama hizi za uhuru wa kujieleza, mtu anaweza kusema chochote juu ya alichosema mwenzie (including any critical discussion on Malecela's legacy) lakini pia uhuru huohuo unaweza kutumiwa (vibaya?) na hao wanaokuwa criticized kudai kuwa kumtetea Malecela kwa "mahaba binafsi" ni NONSENSE as well.

Vioja ni pale tunapojaribu kukwepa mijadala ya kiutu uzima na kukimbilia kusema "kuna chuki binafsi".By the way, someone could have an excuse of having chuki binafsi na Malecela when he said "we can go to hell". And in the same line of thinking, kama ni ruksa kwa mtu kuwa na "mapenzi binafsi na Malecela" how then iwe dhambi kwa mtu mwingine kuwa na "chuki binafsi kwa Malecela"? If we can agree on that,then hao wenye mapenzi binafsi wayapeleke hukohuko just as we want wenye chuki binafsi "wazipeleke hukohuko"....simple logic,isnt it?

Kuna ugumu gani kuheshimu hoja za wenzenu pasipo kuzi-brand nonsense (knowing for sure kuwa hapatatosha hapa iwapo the same could have been said of whatever you say)?

Fair play,pleeeez!!!!
 
Kitila ndio maana nikasema "inasemekana" kwani ushihidi pekee nilionao ni "circumstantial" in the sense kwamba sakata la kiwanja kile lilltokea wakati Malecela akiwa Waziri Mkuu na kimsingi ile ni open playing ground kubadilisha matumizi ya ardhi ile na kujenga Hoteli inahitaji shinikizo kutoka juu...
 
Kitila ndio maana nikasema "inasemekana" kwani ushihidi pekee nilionao ni "circumstantial" in the sense kwamba sakata la kiwanja kile lilltokea wakati Malecela akiwa Waziri Mkuu na kimsingi ile ni open playing ground kubadilisha matumizi ya ardhi ile na kujenga Hoteli inahitaji shinikizo kutoka juu...

Haya mkuu, tuendelee. Inawezekana huyu mzee akawa na matatizo, lakini nafikri ufisadi sio mojawapo maana tungeshasikia. Hadi akina Kingunge tumewasikia na yale mambo yao fake ya parking system, lakini huyu mzee kimya. Tatizo langu na huyu mzee wetu ni pale alipotumia umaarufu wake kutuua sisi wapinzani tena kwa njia za haramu kabisa, ni hilo tu, otherwise I respect this mzee so much and there is so much young politicians could learn from him including myself!
 
Haya mkuu, tuendelee. Inawezekana huyu mzee akawa na matatizo, lakini nafikri ufisadi sio mojawapo maana tungeshasikia. Hadi akina Kingunge tumewasikia na yale mambo yao fake ya parking system, lakini huyu mzee kimya. Tatizo langu na huyu mzee wetu ni pale alipotumia umaarufu wake kutuua sisi wapinzani tena kwa njia za haramu kabisa, ni hilo tu, otherwise I respect this mzee so much and there is so much young politicians could learn from him including myself!

Mkuu,hapo umenichanganya kidogo.Hudhani kuwa kwa kutumia umaarufu wake kuua upizani kwa njia haramu ni passport tosha ya kumweka Malecela katika kundi la watu wanaopaswa kukumbukwa kudumaza demokrasia?Je alifanya hivyo kwa maslahi ya taifa au yake binafsi na chama chake?

If you wont mind,neglecting hiyo ya kuua upinzani kwa njia haramu,could you help me to know what can young and aspiring politicians (kwa mfano wa upinzani) learn from this man?
 
Mkuu Mlalahoi,

Katika historia ya bongo ni Sokoine tu aliyewahi kujaribu hilo, je alifanikiwa? Jawabu ni hapana aliishia kuwashika wauza colgate tu! rushwa bongo inaweza kupiganiwa na rais, kama rais hataki hakuna mtu mwingine yoyote aliye chini ya rais anayeweza hilo, unakumbuka Sokoine, alipotaka kuwashika wakubwa Mwalimu alikataa, nafasi ya makamu wa ccm haina uwezo wowote wa kuweza kupambana na rushwa, uamuzi ni wa mwenyekiti ambaye ni rais.

Kuhusu kuuuwa vyama vya upinzani, hiyo sio kweli maana Slaa na Zitto, wanapotoa orodha ya mafisadi wanakuwa wanacheza with in their political rights, sasa huwezi kusema kuwa wanajaribu kuiua CCM, kwa hiyo Tanznia hakuna mtu yoyote mweye huo uwezo wa kuua vyama vingine vya siasa.

CCM wamekuwa wakiwatumia viongozi wachache wa upinzani kuendeleza mambo yao, na pia upinzani nao wamejifunza hilo maana mambo ya mikataba na orodha za mafisadi, na wao pia wamepewa na baadhi ya viongozi wa ccm, kwa hiyo hakuna anyejaribu kuwaua wengine ila ni mchezo tu wa siasa unaochezwa kwa halali.
 
Moja ya kashfa za Malecela ni tuhuma kuhusu kiwanja cha Gymkhana ilipojengwa Sheraton ( Sasa Movenpick ) inasemekana mkuu pale kavuta na ujenzi wa Hotel katika "green" plot ile uligubikwa na mashinikizo yake. Wataalam wa wizara ya ardhi na wa mazingira na asasi nyingine walipinga sana uvamizi ule
Uwanja ulianza kujengwa kabla Malecela hajawa waziri mkuu, na umauzi wa mwisho ulikuwa ni wa Mwinyi, besides Mwalimu asingekosa kumuandika kwenye kitabu chake mkuu kuwa alikula hela kwenye hio deal, yakuchukua hela za rushwa huwa sio yake hayo wanaohusika na hayo wapo wengi sana hapa bongo hatuhitaji kuambiwa maana tunawaona tu wanavyokula nchi mkuu.
 
Binafsi naamini kuwa kuna mambo mawili tu ambayo hadi leo bado yanahitaji maelezo ilikuwaje yafanyike na kama mzee Malecela alikuwa na nafasi ya kuzuia yasitokee.

a. Zanzibar kujiunga IOC
b. Kundi la Wabunge 55 kutaka Serikali ya Tanganyika.

Nadhani kwa hayo mawili mzee Malecela alifanya makosa ambayo hakusamehewa, ni kama makosa ya Jumbe ambaye hadi leo hajawa restored!
 
a. Zanzibar kujiunga IOC

Huu kama mengine ulikuwa ni uamuzi wa rais wa Tanzania na rais wa visiwani, lakini mpaka leo hatujaambiwa tatizo la hiyo jumuiya ni nini? Mzee unaweza kutuamsha tatizo la hiyo jumuiya hasa ni nini? ninazijua nchi nyingi ambazo ni wanachama wa hiyo jumuiya na hazina matatizo yoyote, au tu ni kwa sababu Mwalimu alisema basi sisi ni kufuata tu bila kuuliza?

b. Kundi la Wabunge 55 kutaka Serikali ya Tanganyika.

Hili kundi lilikuwa likiongozwa na waliokuwa wakitaka madaraka, walipopewa kelele zikaisha, je Muungano uko salama sasa hivi?
 
Huu kama mengine ulikuwa ni uamuzi wa rais wa Tanzania na rais wa visiwani, lakini mpaka leo hatujaambiwa tatizo la hiyo jumuiya ni nini? Mzee unaweza kutuamsha tatizo la hiyo jumuiya hasa ni nini? ninazijua nchi nyingi ambazo ni wanachama wa hiyo jumuiya na hazina matatizo yoyote, au tu ni kwa sababu Mwalimu alisema basi sisi ni kufuata tu bila kuuliza?



Hili kundi lilikuwa likiongozwa na waliokuwa wakitaka madaraka, walipopewa kelele zikaisha, je Muungano uko salama sasa hivi?


Maswali muhimu hayo na ninatumaini tutaweza kuyapatia majibu au angalau kuyaangalia kwa ukaribu.
 
Moja ya kashfa za Malecela ni tuhuma kuhusu kiwanja cha Gymkhana ilipojengwa Sheraton ( Sasa Movenpick ) inasemekana mkuu pale kavuta na ujenzi wa Hotel katika "green" plot ile uligubikwa na mashinikizo yake.

Wataalam wa wizara ya ardhi na wa mazingira na asasi nyingine walipinga sana uvamizi ule

Masatu pale Gymkhana ilipojengwa Sheraton unaweza kutuambia kiwanja kile kilikuwa cha nani?


Majibu mepesi:katika mchango wangu,sijamlalamikia Malecela bali nilikuwa nauliza swali.Hivi lugha yetu ya Taifa imekuwa ngumu kiasi hiki that hata swali nalo linageuka kuwa lawama?As to kuweka kashfa nzito za Malecela,mie sina hata moja,na hoja yangu haikuwa kama ana kashfa au la.However,ubora wa kiongozi sio kutokuwa na kashfa,na japo kuwa na kashfa kunaweza kuchafua jina la kiongozi haimaanishi kuwa uongozi wake hautakumbukwa (a living example ni Bill Clinton).Hate it or love it,kuna mtu anayeweza kunijibu swali langu kuhusu mchango wa Malecela katika mapambano dhidi ya rushwa,ufisadi,ujambazi,uhujumu uchumi,etc etc?Mwenye jazba apuuze swali hili,mwenye jibu anipatie.

Kama kweli huna kashfa nzito ni vyema, lakini nilipouliza nilisema tuwe na kiongozi wa kulinganisha naye, tunaweza kusema mfano waliokuwa mawaziri wakuu waliopita na makamu wa CCM maana ndio alipofika. Tumekuwa na mawaziri wakuu hawa kama sikosei Sokoine (RIP), Kawawa, Msuya, Warioba, Sumaye, Salim A Salim na Kambarage (RIP) sijui pengine nimesahau unaweza kuongeza. Makamu wa vyama naona walio CCM watawafahamu zaidi .............tumlinganishe na hao kwenye kuchapa kazi na tumuhukumu kwa makosa ambayo ni ya kwake.

Kuhusu mchango wake ni mkubwa kwani kuna nchi hapa duniani wanamkumbuka kwa mengi mema aliyofanya, mimi binafsi namkumbuka alipokuwa waziri wa mambo ya nje na mambo yake alivyokuwa anafanya. Vile vile alipokuwa balozi wa Tanzania UK. Katika uongozi wake hajahusishwa na kulihujumu taifa kiuchumi, ufisadi na mambo ya rushwa sijasikia lakini kama kuna member anayo atuwekee hapa. FMES ambaye ni CCM damu anasema hadi leo hii huwa anawapa busara zake katika yale yanayotokea maana waswahili walisema jungu kuu halikosi ukoko.


Binafsi naamini kuwa kuna mambo mawili tu ambayo hadi leo bado yanahitaji maelezo ilikuwaje yafanyike na kama mzee Malecela alikuwa na nafasi ya kuzuia yasitokee.

a. Zanzibar kujiunga IOC
b. Kundi la Wabunge 55 kutaka Serikali ya Tanganyika.

Nadhani kwa hayo mawili mzee Malecela alifanya makosa ambayo hakusamehewa, ni kama makosa ya Jumbe ambaye hadi leo hajawa restored!

Zanzibar kujiunga na IOC unaweza kutufafanulia mchango wake hapo? Hilo la wabunge 55 vile vile kwani wengine hatukuwa Tanzania bali tulisoma tuwekee more data, nasi tuchungulie.
 
Mkuu,hapo umenichanganya kidogo.Hudhani kuwa kwa kutumia umaarufu wake kuua upizani kwa njia haramu ni passport tosha ya kumweka Malecela katika kundi la watu wanaopaswa kukumbukwa kudumaza demokrasia?Je alifanya hivyo kwa maslahi ya taifa au yake binafsi na chama chake?

If you wont mind,neglecting hiyo ya kuua upinzani kwa njia haramu,could you help me to know what can young and aspiring politicians (kwa mfano wa upinzani) learn from this man?

Pole sikuweza kujibu jana hii. Ni swali zuri na muhimu sana hili. Binafsi kitu kimoja nilichojifunza kwa huyu mzee ni kutokuwa king'ang'anizi katika maslahi ya taasisi dhidi ya maslahi binafsi.

Huyu mzee mara kadhaa amekubali mambo yaishe hata pale ambapo haki zake binafsi ziliporwa. Kwa mfano, katika nyakati za uchaguzi zote mbili za 1995 na 2005, huyu mzee alikuwa na uwezo wa kushinda kama angeenda katika vikao husika vya CCM. Lakini wazandiki wakamnyang'anya haki yake ya kugombea hivihivi na bado alikubali yaishe na kikubwa zaidi akaamua kutuliza mzuka wa wafuasi wake.

Ni yeye pekee katika ulimwengu wa siasa za dunia akiwa anashika nafasi ya makamu mwenyekiti yaani next to mwenyekiti aliyekubali kunyang'anywa haki ya kugombea urais huku akijua alikuwa na uwezo wa kushinda. This to me is a big sacrifice of individual interests; putting institutional interests above the individual interests.

Kama Marando na Mrema wangekuwa na moyo wa Malecelea leo hii upinzani Tanzania ungekuwa mbali sana. Lakini kwa kuwa hawa wawili waliyaona maslahi yao binafsi ni ya muhimu zaidi kuliko ya NCCR, waling'ang'ania uongozi; matokeo yake NCCR ikafa na wananchi kwa ujumla wakaupa upinzani adhabu. Hadi leo sisi tuliopo upinzani tuna-struggle kurudisha credibility ya opposition ambayo iliharibiwa na watu wawili tu: Mrema na Marando kwa maslahi yao binafsi.

Mzee Malecela naye alikuwa na uwezo kabisa wa kuisambaratisha CCM kama angeamua kushikilia maslahi yake binafsi na pengine ndio ungekuwa mwanzo wa kugawanyika kwa CCM.
 
Back
Top Bottom