Kwanini Mzee Malecela alijulikana ghafla kama “Jumanne”?

Ukiacha la kuwadhibiti wapinzani katika chaguzi ndogo za majimbo, sijauona ubaya wa Mzee JM kama kiongozi kwenye chama na serikali.
 
Ukiacha la kuwadhibiti wapinzani katika chaguzi ndogo za majimbo, sijauona ubaya wa Mzee JM kama kiongozi kwenye chama na serikali.

Sema sasa wengi wetu tunaangalia sana 'pitfalls' kuliko mafanikio!
 
Kama kweli huna kashfa nzito ni vyema, lakini nilipouliza nilisema tuwe na kiongozi wa kulinganisha naye, tunaweza kusema mfano waliokuwa mawaziri wakuu waliopita na makamu wa CCM maana ndio alipofika. Tumekuwa na mawaziri wakuu hawa kama sikosei Sokoine (RIP), Kawawa, Msuya, Warioba, Sumaye, Salim A Salim na Kambarage (RIP) sijui pengine nimesahau unaweza kuongeza. Makamu wa vyama naona walio CCM watawafahamu zaidi .............tumlinganishe na hao kwenye kuchapa kazi na tumuhukumu kwa makosa ambayo ni ya kwake.

Ulipoanza na kauli "kama kweli huna kashfa nzito...." it looked as if huamini kuwa kweli sina kashfa,sio nzito tu,bali yoyote ile dhidi ya Malecela.

Kuhusu mchango wake ni mkubwa kwani kuna nchi hapa duniani wanamkumbuka kwa mengi mema aliyofanya, mimi binafsi namkumbuka alipokuwa waziri wa mambo ya nje na mambo yake alivyokuwa anafanya. Vile vile alipokuwa balozi wa Tanzania UK. Katika uongozi wake hajahusishwa na kulihujumu taifa kiuchumi, ufisadi na mambo ya rushwa sijasikia lakini kama kuna member anayo atuwekee hapa.

Je unaweza kunisaidia na mie kufahamu ni nchi gani hizo hapa duniani wanamkumbuka kwa mema aliyofanya?Na ni mema yapi hayo?

Je unaweza tena kunisaidia kufahamu hizo kumbukumbu za uwaziri wake wa mambo ya nje na alipokuwa balozi wa TZ hapa UK?

Sijawahi kusikia Malecela kahusishwa na rushwa au ufisadi,lakini swali langu ambalo hadi dakika hii hujalijibu ni NINI MCHANGO WAKE KATIKA KUPAMBANA NA RUSHWA NA UFISADI hasa kwa kuzingatia influence yake kubwa aliyokuwa nayo ndani na nje ya CCM?Nipatie japo mfano mmoja unaoonyesha kuwa Mzee huyo alikuwa anaichukia rushwa kwa dhati na hakuwaunga mkono mafisadi.Mfano mmoja tu,please.
 
Ili iweje?


Tunataka kujua ukweli wa maneno yako haya hapa:

Masatu said:
Moja ya kashfa za Malecela ni tuhuma kuhusu kiwanja cha Gymkhana ilipojengwa Sheraton ( Sasa Movenpick ) inasemekana mkuu pale kavuta na ujenzi wa Hotel katika "green" plot ile uligubikwa na mashinikizo yake.

Wataalam wa wizara ya ardhi na wa mazingira na asasi nyingine walipinga sana uvamizi ule

Mwaga data hapa na tumkome nyani giladi mchana kweupe.
 
Mlalahoi

Naona unazunguka na hoja ya msingi hakuna bali ni ubishi tu ili hali unabisha, mwenyewe unasema huna kashfa nzito kumuhusisha halafu unataka mimi tena nikutafunie chakula chako wakati unacho mdomoni. Angalia issue yangu ya mwanzo nilivyoandika halafu uje na madai.

Kuhusu mafisadi na kupambana na rushwa rejea nyuma kidogo tumeanza kuwa na mafisadi Tanzania lini na kwa kiwango gani? Unapomuongelea unam-compare na nani ambao walishika nyadhifa kama yeye? Vile vile nilikutajia mawaziri wakuu waliopita ili tuweze kuwa more open na kuchambua yale ambayo unamtuhumu.
 
...huyu jamaa nilimwona mwendawazimu na nikagundua kwa nini Nyerere alikuwa hampendi ni pale alipo suggest vinchi vidogo dogo kama Rwanda na Burundi ni visumbufu sana why not take them na kuweka serikali ambayo tunaweza kuiweka sawa,huyu jamaa kina Kagame hawataki kumsikia kabisa na angekuwa raisi ungeona uhusiano na hizo nchi ungekuwa kama sumu
 
koba,
tuna-deal na wendawazimu kina Kagame na Museveni sasa sijui kama diplomasia itafanya kazi muda wote.

sasa kama unasema Malecela mwendawazimu kwa kuwaza tu kupachika serikali Rwanda na Burundi. Halafu unadai hili inahalalisha chuki ya Baba wa Taifa dhidi yake?!!

Hivi umesahau kwamba Baba wa Taifa haikuishia kuwaza tu, bali alipachika serikali Uganda, Msumbiji,Zimbabwe[alimtoa mbio Nkomo],Seychelles .....

Ninavyoelewa mimi Malecela ametamka wazi kwamba Rwanda na Burundi haziwezi kutengemaa ikiwa Wahutu wataendelea kukandamizwa kama ilivyo sasa.

Kina Kagame hawataki kumsikia Malecela kwasababu kitendo chake cha kulaani uvamizi na uharamia walioufanya Congo-Kinshasa. Mali nyingi imeporwa na wananchi kwa mamilioni wamepoteza maisha. Pia vita hivyo visababisha ujambazi, wakimbizi, na uharibifu mkubwa wa mazingira, kwa upande wetu Tanzania.

Katika hali hiyo siwezi kumlaumu Malecela kwa kuota njozi ya kupachika serikali kibaraka Rwanda itakayofuata International Policies zetu.

Mlalahoi,
Nafikiri mambo mengi yakifisadi yaliyokuwa yanaendelea wakati Malecela ni Waziri Mkuu yalikuwa yanafanywa na watu waliokuwa karibu na Mzee Ruksa.

Maadamu hatuna ushahidi kwamba Malecela alikuwa mshiriki basi hiyo inatosha kama mchango wake. Hakuna waziri mkuu anayeweza kupingana na Raisi wake waziwazi.

Kama Mzee Ruksa angekuwa anapiga vita ufisadi, halafu Malecela akahujumu juhudi hizo basi tungekuwa na haki ya kumlaani Malecela.
 
Tunataka kujua ukweli wa maneno yako haya hapa:

Soma post yangu ya awali na kisumbue kichwa chako kidogo kusoma kwa makini utakuta jibu la swali lako... acha uvivu
 
Kuna mtu kaomba kashfa ya Malecela aelezewe lakini nimesoma mahala aliwai kuwaambia Watanzania go to hell je hii haitoshi kuwa kashfa nzito ?
 
Lunyungu,
kauli hiyo aliitoa miaka hiyo na baada ya hapo alishindwa Ubunge. Toka ameshindwa Ubunge amekuwa Mkuu wa mkoa,Balozi,na Waziri Mkuu na Makamu wa Raisi. Pia wananchi wamemrudisha tena Bungeni.

Ninavyosikia kauli hiyo aliitoa kutokana na mabishano yaliyotokea kuhusu usafiri wa reli ya kati. wakati huo alikuwa waziri wa mawasiliano. haujulikani huyo aliyekuwa akibishana naye alisema nini mpaka Malecela akatoa kauli hiyo.

The bottom line ni kwamba, usafiri wa reli ulikuwa better kuliko sasa hivi.

Hii kauli ya Malecela na ile ya Msuya zinakuwa exagerrated kwa malengo ya kisiasa. Majuzi Cleopa Msuya amehojiwa na ameeleza wazi kwamba he stands by what he said.

NB:
hivi huyu aliyesema "they can go to hell" na yule aliyesaini mkataba wa madini uliotuingiza hasara ya mabilioni yupi ana kashfa kubwa?
 
...huyu jamaa nilimwona mwendawazimu na nikagundua kwa nini Nyerere alikuwa hampendi ni pale alipo suggest vinchi vidogo dogo kama Rwanda na Burundi ni visumbufu sana why not take them na kuweka serikali ambayo tunaweza kuiweka sawa,huyu jamaa kina Kagame hawataki kumsikia kabisa na angekuwa raisi ungeona uhusiano na hizo nchi ungekuwa kama sumu

This was the best proposal for the Rwanda and Burundi crises. Hao waliogopa kupoteza vi-urais vyao. Waliona na hata leo wanaona vi-urais vyao kuwa ni muhimu zaidi kuliko ustawi wa watu wao.
 
...Jokakuu na Kitila i dont support uharamia au unyanyasaji wa wannchi wa hizo nchi kutoka pande zote either tutsi or hutu,lakini suggesting kwenda kuvamia hizo nchi na kuweka chini yetu ili kupata serikali makini kwangu huo ni wendawazimu na i doubt kama tunaweza kuwapiga hao jamaa kijeshi kirahisi kama inavyoonekana hapa...vita ya kagera tuu mpaka leo effect zake hazijaisha ndio uanze na hao tena ambao hata hawajakuchokoza.

Jokakuu historia ya wahutu na watuts ni very complex kwa mimi kuchukua any side ila you sound unajua sana hizo crisis za hii region ingawaje seems uko bias kidogo
 
This was the best proposal for the Rwanda and Burundi crises. Hao waliogopa kupoteza vi-urais vyao. Waliona na hata leo wanaona vi-urais vyao kuwa ni muhimu zaidi kuliko ustawi wa watu wao.

..kitila hii sasa naita shallow,jaribu kuangalia vizuri hao jamaa wanavyoendeea sasa kuanzia kwenye Demokrasi,uchumi na utawala wa sheria...kwa sasa kiuchumi tuko nyuma ya hizo nchi ukae ukijua,anyway jaribu kuchunguza kuliko kutoa statements kama hizo utashangaa na utachukia sana mafisadi
 
Soma post yangu ya awali na kisumbue kichwa chako kidogo kusoma kwa makini utakuta jibu la swali lako... acha uvivu

Naona huna hoja hapa yalikuwa ni uzushi tu, tuendelee na yaliyo muhimu.
 
This was the best proposal for the Rwanda and Burundi crises. Hao waliogopa kupoteza vi-urais vyao. Waliona na hata leo wanaona vi-urais vyao kuwa ni muhimu zaidi kuliko ustawi wa watu wao.

Tena ukumbue tumekuwa na wakimbizi zaidi ya millioni moja kwa muda mrefu sana na hii imefanya serikali ya TZ kutumia rasilimali zake kuthibiti uharamia kule maeneo ya mipakani ambazo zingefanya mambo mengine. Kagame na M7 ni watu hatari sana walikuwa wanawakataza waasi kwenda kwenye mazungumzo hata wakati Nyerere (RIP) hajafariki. Wao wanapigana halafu sisi ndio tunapata shida.
 
,lakini suggesting kwenda kuvamia hizo nchi na kuweka chini yetu ili kupata serikali makini kwangu huo ni wendawazimu
Kwa hiyo mkuu tulipovamia Uganda kumtoa Amin, na kuweka serikali yetu tulikuwa wendawazimu, juzi US walipovamia
Iraq na kuweka serikali yao nao ni wenda wazimu pia, au?

Malecela, alimwambia Mwalimu, straight in his face kuwa bila ya kuvamia nchi hizo kama tulivofanya Uganda, mpaka unaingia kaburini amani haitapatikana huko, Mwalimu kama kawaida yake akaiona opportunity ya kumshambulia adui wake, akapiga kelele niynig kuwa huo ni wenda wazimu, na sisi wananchi kama kawaida tukakubali tu mradi aliyesema ni Mwalimu.

Mkuu wangu jaribu kutafuta nafasi uongee na warundi wakueleze what Kagame did, ili kuwa hapo alipo sasa hivi, mikononi mwake ana damu za wananchi karibu millioni moja, Museveni anayoyafanya sasa hivi Uganda na Zaire, ni aibu hata kusema, na yes wote wawili walipigana na sana Malecela, asipate urais wakimtaka Sumaye. Wote wawili wanamuogopa sana Malecela, na hasa Kagame, mana mara nyingi sana mzee huwa anmwambia ambayo wengine wote duniani hawataki kumwambia, maana yeye ndiye aliyemuua Bagaza siku mbili baada ya kukutana na Malecela, ambapo alimuambia wazi kuwa Bagaza, "....akifa I am holding you responsible.....".

Kwa hiyo Malecela, kumshauri Mwalimu, kuzivamia nchi hizo na kuweka serikali yetu, ulikuwa ni wenda wazimu, basi Mwalimu aliyewahi kuivamia Uganda, mkuu Koba unamwitaje? Maana aliye-suggest kwako ni mwenda wazimu sasa aliyefanya tayari vipi?

2.
na i doubt kama tunaweza kuwapiga hao jamaa kijeshi kirahisi kama inavyoonekana hapa...vita ya kagera tuu mpaka leo effect zake hazijaisha ndio uanze na hao tena ambao hata hawajakuchokoza,Jokakuu historia ya wahutu na watuts ni very complex kwa mimi kuchukua any side ila you sound unajua sana hizo crisis za hii region ingawaje seems uko bias kidogo
Tanzania hatuwezi kushindwa kuwapiga hizo nchi kivita, the matter of fact katika dunia tunapewa nafasi ya juu sana kwa uhodari na ukali wa majeshi yetu, hakuna nchi yoyote hapa karibu inayoweza kutuchezea, kwa hiyo Mwalimu angekubali by now kwenye hizo nchi kusingekuwa na matatizo ambayo yanatugharimu hela nyingi sana za walipa kodi katika kugharamia wakimbizi wa kila siku wanaokuja nchini, ambayo ndio hasa ilikuwa argument ya Malecela, against Mwalimu kwamna serikali yetu mpaka leo inapoteza hela nyingi za maendeleo katika kugharamia wakimbizi.

Malecela, alipotaka kupewa kazi ya usuluhishi wa hao watu alikataa kwa kusema wazi kwamba anawaunga mkono Wahutu, kwa hiyo hawezi kutoa haki kwa Watusi, complex ilianzishwa na Wa-Belgiji kwa nia ya divide and rule, lakini Watusi nao wakaipeleka hiyo complex to the extreme, na walimsaidia sana Kagame, na hasa jeshi la UN ambao waliangalia upande mwingine wakimruhusu Kagame, kuua as much as of his fit, to this day Malecela humuita Kagame a thug, na hata Moi wa Kenya naye humuita jina hio hilo na mkuu huyo hukwepa mahali popote walipo hawa viongozi wawili.
 
Naona huna hoja hapa yalikuwa ni uzushi tu, tuendelee na yaliyo muhimu.

Ukisikia uvivu wa kufikiri ndio ushaambiwa ilikuwa ni open space na ikatolewa shinikizo kutoka juu.. sasa nani anamiliki open space kama sio serikali? fuata ushauri wako... endelea na mambo mengine.
 



Malecela, alipotaka kupewa kazi ya usuluhishi wa hao watu alikataa kwa kusema wazi kwamba anawaunga mkono Wahutu, kwa hiyo hawezi kutoa haki kwa Watusi

....i sure respect malecela kwa hili na kuwa mkweli,na sioni ubaya kuchukua side kama alivyofanya na kuamini watutsi ndio chanzo cha matatizo lakini mkuu(FM) unategemea kagame akae kimya huku watu wakichinjwa kiasi kile na mambo ya congo kule kabila baada ya kusaidiwa kumtoa mobutu na makubaliano yalikuwa lazima azuie interahamwe wasirudie walichofanya maana walipiga camp congo lakini yeye akawageuka na kuwapa silaha interahamwe ...mkuu huoni hapo ni deal chafu tuu kabila alicheza,anyway na hiyo ya kupigana na mushinda kirahisi hizi nchi mkuu hapo sina cha kusema lakini mmmh:rolleyes: !
 
unategemea kagame akae kimya huku watu wakichinjwa kiasi kile na mambo ya congo kule kabila baada ya kusaidiwa kumtoa mobutu na makubaliano yalikuwa lazima azuie interahamwe wasirudie walichofanya maana walipiga camp congo lakini yeye akawageuka na kuwapa silaha interahamwe ...mkuu huoni hapo ni deal chafu
Mkuu Koba,

Heshima mbele siasa ni mchezo mchafu sana, maana according to the dataz Kabila aliuliwa na mtoto wake ambaye ni rais wa sasa, Kagame na Museveni, walikuwa wakitafuta madini kule Zaire, ambayo sasa hivi Museveni is making a good use of it mpaka anasifiwa na wazungu kuwa ni a good president, maana wengi wao wanafaidika na hayo madini, Kabila alitaka kuleta tatizo kwenye hao wakuu wawili kuchukua madini bure, akaanza kujiweka sawa na Mugabe, hapo tu ndipo alipowaudhi Kagame na Museveni, hiyo ya intarahamwe na silaha ilikuwa ni propaganda tu za siasa,

Kagame, sasa hivi ni wanted na some courts in France, I mean sijui kuhusu kunyamaza kimya, lakini pia sielewi kuwa rais wa nchi huku ukiwa umeua wananchi karibu millioni moja, that sounds like the president is insane to me!
 
Back
Top Bottom