Tribute to Mwana JF Mwenzetu William Malecela Le Mutuz, Alikuwa Mtu wa Watu

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,498
113,604
Update ya Msiba wa Mwana JF Mwenzetu, William Malecela (Le Mutuz).

Kwanza natoa pole sana kwa familia ya Mzee John Malecela kwa msiba mkubwa na mzito wa mtoto wake, William Malecela, kwa jina maarufu Le Mutuz, aliyefariki leo asubuhi jijini Dar es Salaam. Msiba upo nyumbani kwa Baba yake Mzee John Malecela, pale Sea View. Nimepita pale na kufanikiwa kupata Ratiba ya Kumuaga.

Kwa mujibu wa msemaji wa familia Le Mutuz ambaye ni kaka wa Le Mutuz, aliyejitambulisha kwa jina moja tuu la Kaka Misano, amesema mwili wa marehemu utachukuliwa Hospitali ya Muhimbili Saa 2:00 Asubuhi na kupelekwa nyumbani Sea View kwa Ibada Fupi ya Kifamilia.

* Saa 3:00 asubuhi - Mwili utaondolewa nyumbani kuwasili Ukumbi wa Karimjee Saa 3:30.

* Saa 4:00 - Saa 6:00 - Shughuli za kuaga hapo Karimjee

* Saa 7:00 Mwili unaondoka Ukumbi wa Karimjee kupelekwa Airport, tayari kwa safari ya Dodoma.

* Saa 11:00 jioni - Mwili Utawasili Dodoma

Siku ya Jumanne kutakuwa na Ratiba za Dodoma.

Mazishi yatafanyika Mvumi Mission Dodoma, Siku ya Jumatano saa 9:00 Alasiri.

Kwa wote walioguswa na msiba huu mkubwa wawasiliane na familia wapewe utaratibu wa kutoa mkono wa pole.

My Take. My Tribute
Huu ndio msiba mkubwa wa pili kwa mwana JF maarufu baada ya Regia Mtema.

Kwasababu msiba wa Regia, wana JF, tulijitoa na kujitokeza, natoa wito kwa wana JF, kesho tujitokeze kwa wingi Karimjee.

Wenye kuweza kumsindikiza Dodoma, tumsindikize. Wana JF wa Dodoma, mtuwakilishe Mvumi Dodoma siku ya mazishi, na itapendeza kama kutakuwa na shada la JF.

My Personal Tribute to Le Mutuz:

Mimi nimesoma Shule ya Msingi Oyster Bay na watoto wote wa Mzee Malecela. Nilikuwa darasa moja na Jaji Mwendwa Malecela. Rais Hussein Mwinyi alitutangulia madarasa mawili, alikuwa darasa moja na Dr. Seche Malecela.

Nikiwa O Level Tambaza, Senyagwa alikuwa A level PCM, alipomaliza na kupiga DIV 1 ya point 3 na kujoin UDSM, Dr. Hussein Mwinyi na Seche, Mh. Silvester Koka walijiunga Tambaza PCB. Ni shule hii ya Tambaza kule juu summit, ndiko mimi niliko jifunzia kufanya mambo fulani, si unajua tena foolish age!.

Nikaja kuwa MC wa harusi ya dada yake, mmoja wa ma binti wa Malecela na mpaka leo, mpaka kesho from time to time na m visit Jaji Mwendwa..

Ni mpaka nilipokwenda jijini New York, nchini Marekani kwenye Ubalozi wetu UN pale New York, ndipo nikatambulishwa kwa shemeji yetu Mke wa Le Mutuz, ndipo nikamfahamu William.

Tukaja kukutana tena JF alipokuja kugombea ubunge wa Bunge la Africa Mashariki, akanitafuta, nikampa support

Kuna wakati nikiwa Dodoma akanikaribisha home kwa Dingi pale Dom, kisha tuka drive all the way from Dom to Dar so we got to know better, ndipo nikajua kumbe jamaa, don't drink!, don't smoke, just chilling tuu and have good time!.

From there tukawa marafiki, kama vilivyo vikombe kabatini kuna wakati tukapishana kauli, akanifungia madirisha!. Alikuwa mwepesi kukasirika, hachelewi kukiwasha ila pia mwepesi kusamehe!.

Tukaja kupatanishwa na mwana JF Sactus Mtsimbe, kuna wakati alituhifadhi mimi na Le Mutuz pale ofisini kwake, Tancot House hivyo tukapatana.

Ni Le Mutuz ndie aliyenitambulisha mimi kwenye YouTube channel, na video hii ya Le Mutuz ndio video yangu ya kwanza YouTube.



Ingekuwa video ni Mwanamke, tungesema ni video ya Le Mutuz ndio imeizindua YouTube Channel yangu. Thanks for that.

Na baada ya hapo akanipa bonge la shavu LE Mutuz: Special Salute To Paschal Mayalla!

Mara ya mwisho kuonana na Le Mutuz ni kwenye msiba wa Baghdellan pale Magomeni mwaka jana, alikuja na chuma fulani kikali sana na Davis Mosha!.

Kiukweli kabisa kwa jinsi Le Mutuz alivyo mtu wa watu, sijapenda mahudhurio hafifu niliyoyaona hapo nyumbani. Nilipategemea kukuta watu kufurika wakiwamo ma babez na washure wakiongozwa na Davis Mosha, labda tusubirie hiyo kesho, ila kwa sasa kitu muhimu sana ni kutoa mkono wa pole kwa familia.

Mkuu William Malecela Le Mutuz,
Umepigana vita vilivyo vitakatifu,
Mwendo umeumaliza,
Imani umeitunza.

Sisi tulikupenda, lakini Bwana amekupenda zaidi,
Bwana alileta, Bwana ametwaa,
Jina lake Lihimidiwe.

Buriani ya Kuonana.
Paskali
Baadhi ya mabandiko yangu na mwamba huyu
 
Mwanzo nilimuona ni mtu wa maana, baadae maisha yake ya mitandaoni yakanifanya nimdharau, nimpuuze na kumuona mtu wa hovyo. Kumbe sikuwa sahihi.

Nilipoongezeka hekima kidogo nikaanza kuelewa kuwa changamoto na mapito ya maisha yanaweza kukuvuruga na ukawa au ukaonekana mtu wa hovyo. Kila mtu ana namna yake ya kukabiliana nazo na kila mmoja ana namna anavyoathiriwa nazo.

Wengine huhitaji watu wakuwasaidia kuvuka, wengine huweza kuvuka wenyewe, wengine huzama mazima.

Mfano; umeachwa na mwenza mkiwa ughaibuni. Anaunda timu kukuchafua na kuwajenga watoto wakuchukie.

Unaamua kurudisha majeshi nyuma kwa kurudi nchini kwako huku mifuko imechacha, hapo una stress na depression. Unakuta watu wa rika lako au wadogo kuliko wewe tayari wana maisha. Kumbuka umetoka majuu, jamii yako inategemea kuwa umerudi na mafanikio, kwa kuwa ni kinyume chake unahisi wata/wanakudharau. Hujui uanzie wapi na stress zako. Unaingia kwenye denial.

Mungu anakusaidia unapata riziki za hapa na pale ila depression inakutuma ufanye maonesho na maigizo ya maisha mazuri pia ukomae na bebez kwa kuwala au kupiga nao picha tu na kusambaza ili tu kumlingishia mtaraka wako kuwa kakuacha ila mademu wanakukubali na unakula bata na wewe ni maarufu. Pia kuwasuta wote wanaohisi huna lolote.

Kumbe unazidi kuharibu. Watu wa maana wa rika lako wanakuona hufai na wanaanza kukuepuka, huku wale wadogo wanakuona mtu mzima hovyo. Umri unaenda, na stress zinazidi. Hapo huamini tena katika mahusiano, ndoa wala familia. Unaona wakati umeenda na kila kitu kimeshavurugika.

Maisha yana mambo mengi. Unaweza kuwa mtu mwema tu ila familia, mwenza, kazi, misukosuko vikakuvuruga na kukutoa kwenye reli. Usipopata msaada wa kupokea hali na kuanza upya unaweza dhani unayajenga, kumbe ndio unaharibu na kuongeza stress zaidi.

R.I.P William
 
Update ya Msiba wa Mwana JF Mwenzetu, William Malecela, "Le Mutuz "

Kwanza natoa pole sana kwa familia ya Mzee John Malecela kwa msiba mkubwa na mzito wa mtoto wake, William Malecela, kwa jina maarufu Le Mutuz, aliyefariki leo asubuhi jijini Dar es Salaam...
Mtoto wa waziri Mkuu mstaafu anachangiwa huku kuna wanjf kibao hawana hata pesa ya chakula wanakuja humu kuomba misaada wanaambulia matusi tu.

Paschal hii double standard mpaka lini kama vipi wote wachangiwe

USSR

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pascal haya maneno no yako kweli!!!!!👇👇👇👇👇👇👇
(Mkuu William Malecela Le Mutuz,
Umepigana vita vilivyo vitakatifu,
Mwendo umeumaliza,
Imani umeitunza,

Sisi tulikupenda, lakini Bwana amekupenda zaidi,
Bwana alileta, Bwana ametwaa.
Jina lake Lihimidiwe)

......................................................
NI AFRIKA PEKEE MAREHEMU HUSINGIZIWA MAZURI YOTE.

Poleni wafiwa Mungu awafariji
 
Mkuu William Malecela Le Mutuz,
Umepigana vita vilivyo vitakatifu,
Mwendo umeumaliza,
Imani umeitunza,

Sisi tulikupenda, lakini Bwana amekupenda zaidi,
Bwana alileta, Bwana ametwaa.
Jina lake Lihimidiwe

......................................................
NI AFRIKA PEKEE MAREHEMU HUSINGIZIWA MAZURI YOTE.

Poleni wafiwa Mungu awafariji
Vita gani vitakatifu bwana.
 
Update ya Msiba wa Mwana JF Mwenzetu, William Malecela, "Le Mutuz "

Kwanza natoa pole sana kwa familia ya Mzee John Malecela kwa msiba mkubwa na mzito wa mtoto wake, William Malecela, kwa jina maarufu Le Mutuz, aliyefariki leo asubuhi jijini Dar es Salaam.

Msiba upo nyumbani kwa Baba yake Mzee John Malecela, pale Sea View.

Nimepita pale na kufanikiwa kupata Ratiba ya Kumuaga.

Kwa mujibu wa msemaji wa Familia, ya William Malecela, Le Mutuz, ambaye ni Kaka wa Le Mutuz, aliyejitambulisha kwa jina moja tuu la Kaka Misano. amesema Mwili wa marehemu utachukuliwa Hospitali ya Muhimbili Saa 2:00 Asubuhi na kupelekwa Nyumbani Sea View na Ibada Fupi ya Kifamilia.

Saa 3:00 asubuhi Mwili utaondolewa nyumbani kuwasili Ukumbi wa Karimjee Saa 3:30.
Saa 4:00 - Saa 6:00 ni shughuli za kuaga hapo Karimjee

Saa 7:00 Mwili unaondoka Ukumbi wa Karimjee kupelekwa Airport, tayari kwa safari ya Dodoma.

Mwili Utawasili Dodoma Saa 11:00 jioni

Siku ya Jumanne kutakuwa na Ratiba za Dodoma.

Mazishi yatafanyika Mvumi Mission Dodoma, Siku ya Jumatano saa 9:00 Alasiri.

Kwa wote walioguswa na msiba huu mkubwa wawasiliane na familia wapewe utaratibu wa kutoa mkono wa pole.

My Take. My Tribute
Huu ndio msiba mkubwa wa pili kwa mwana JF maarufu baada ya Regia Mtema.

Kwasababu msiba wa Regia, wana JF, tulijitoa na kujitokeza, natoa wito kwa wana JF, kesho tujitokeze kwa wingi Karimjee.

Wenye kuweza kumsindikiza Dodoma, tumsindikize. Wana JF wa Dodoma, mtuwakilishe Mvumi Dodoma siku ya mazishi, na itapendeza kama kutakuwa na shada la JF.

My Personal Tribute to Le Mutuz.
Mimi nimesoma Shule ya Msingi Oyster Bay na watoto wote wa Mzee Malecela.

Nilikuwa darasa moja na Jaji Mwendwa Malecela.

Rais Mwinyi alitutangulia madarasa mawili, alikuwa darasa moja na Dr. Seche Malecela.

Nikiwa O LevelTambaza Senyagwa alikuwa A level PCM, alipomaliza na kupiga DIV 1 ya point 3 na kujoin UDSM, Dr. Husein Mwinyi na Seche, Mh.Silvester Koka walijiunga Tambaza PCB.

Ni mpaka nilipokwenda jijini New York, nchini Marekani kwenye ubalozi wetu UN pale New York, ndipo nikatambulishwa kwa shemeji yetu Mke wa Le Mutuz, ndipo nikamfahamu William.

Tukaja kukutana tena JF. alipokuja kugombea ubunge wa Bunge la Africa Mashariki, akanitafuta, nikampa support.

From there tukawa marafiki, kama vilivyo vikombe kabatini kuna wakati tukapishana kauli, akanifungia madirisha.

Tukaja kupatanishwa na mwana JF Sactus Mtsimbe, kuna wakati alituhifadhi mimi na Le Mutuz pale ofisini kwake, Tancot House hivyo tukapatana.

Ni Le Mutuz ndie aliyenitambulisha mimi kwenye YouTube channel, na video hii ya Le Mutuz,
ndio video yangu ya kwanza YouTube, ingekuwa video ni Mwanamke, tungesema ni video ya Le Mutuz ndio imeib...ri YouTube Channel yangu!. Thanks for that.

Mara ya mwisho kuonana na Le Mutuz ni kwenye msiba wa Baghdellan pale Magomeni mwaka jana.

Kiukweli kabisa kwa jinsi Le Mutuz alivyo mtu wa watu, sijapenda mahudhurio hafifu niliyoyaona hapo nyumbani, nilipategemea kufurika ma babez na washure wakiongozwa na Davis Mosha, labda tusubirie hiyo kesho, ila kwa sasa kitu muhimu sana ni kutoa mkono wa pole kwa familia.

Mkuu William Malecela Le Mutuz,
Umepigana vita vilivyo vitakatifu,
Mwendo umeumaliza,
Imani umeitunza,

Sisi tulikupenda, lakini Bwana amekupenda zaidi,
Bwana alileta, Bwana ametwaa.
Jina lake Lihimidiwe

Buriani ya Kuonana.

Paskali

Ila we na lemutuz mnafanana akili.
 
Back
Top Bottom