Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,498
- 113,604
Update ya Msiba wa Mwana JF Mwenzetu, William Malecela (Le Mutuz).
Kwanza natoa pole sana kwa familia ya Mzee John Malecela kwa msiba mkubwa na mzito wa mtoto wake, William Malecela, kwa jina maarufu Le Mutuz, aliyefariki leo asubuhi jijini Dar es Salaam. Msiba upo nyumbani kwa Baba yake Mzee John Malecela, pale Sea View. Nimepita pale na kufanikiwa kupata Ratiba ya Kumuaga.
Kwa mujibu wa msemaji wa familia Le Mutuz ambaye ni kaka wa Le Mutuz, aliyejitambulisha kwa jina moja tuu la Kaka Misano, amesema mwili wa marehemu utachukuliwa Hospitali ya Muhimbili Saa 2:00 Asubuhi na kupelekwa nyumbani Sea View kwa Ibada Fupi ya Kifamilia.
* Saa 3:00 asubuhi - Mwili utaondolewa nyumbani kuwasili Ukumbi wa Karimjee Saa 3:30.
* Saa 4:00 - Saa 6:00 - Shughuli za kuaga hapo Karimjee
* Saa 7:00 Mwili unaondoka Ukumbi wa Karimjee kupelekwa Airport, tayari kwa safari ya Dodoma.
* Saa 11:00 jioni - Mwili Utawasili Dodoma
Siku ya Jumanne kutakuwa na Ratiba za Dodoma.
Mazishi yatafanyika Mvumi Mission Dodoma, Siku ya Jumatano saa 9:00 Alasiri.
Kwa wote walioguswa na msiba huu mkubwa wawasiliane na familia wapewe utaratibu wa kutoa mkono wa pole.
My Take. My Tribute
Huu ndio msiba mkubwa wa pili kwa mwana JF maarufu baada ya Regia Mtema.
Kwasababu msiba wa Regia, wana JF, tulijitoa na kujitokeza, natoa wito kwa wana JF, kesho tujitokeze kwa wingi Karimjee.
Wenye kuweza kumsindikiza Dodoma, tumsindikize. Wana JF wa Dodoma, mtuwakilishe Mvumi Dodoma siku ya mazishi, na itapendeza kama kutakuwa na shada la JF.
My Personal Tribute to Le Mutuz:
Mimi nimesoma Shule ya Msingi Oyster Bay na watoto wote wa Mzee Malecela. Nilikuwa darasa moja na Jaji Mwendwa Malecela. Rais Hussein Mwinyi alitutangulia madarasa mawili, alikuwa darasa moja na Dr. Seche Malecela.
Nikiwa O Level Tambaza, Senyagwa alikuwa A level PCM, alipomaliza na kupiga DIV 1 ya point 3 na kujoin UDSM, Dr. Hussein Mwinyi na Seche, Mh. Silvester Koka walijiunga Tambaza PCB. Ni shule hii ya Tambaza kule juu summit, ndiko mimi niliko jifunzia kufanya mambo fulani, si unajua tena foolish age!.
Nikaja kuwa MC wa harusi ya dada yake, mmoja wa ma binti wa Malecela na mpaka leo, mpaka kesho from time to time na m visit Jaji Mwendwa..
Ni mpaka nilipokwenda jijini New York, nchini Marekani kwenye Ubalozi wetu UN pale New York, ndipo nikatambulishwa kwa shemeji yetu Mke wa Le Mutuz, ndipo nikamfahamu William.
Tukaja kukutana tena JF alipokuja kugombea ubunge wa Bunge la Africa Mashariki, akanitafuta, nikampa support
Kuna wakati nikiwa Dodoma akanikaribisha home kwa Dingi pale Dom, kisha tuka drive all the way from Dom to Dar so we got to know better, ndipo nikajua kumbe jamaa, don't drink!, don't smoke, just chilling tuu and have good time!.
From there tukawa marafiki, kama vilivyo vikombe kabatini kuna wakati tukapishana kauli, akanifungia madirisha!. Alikuwa mwepesi kukasirika, hachelewi kukiwasha ila pia mwepesi kusamehe!.
Tukaja kupatanishwa na mwana JF Sactus Mtsimbe, kuna wakati alituhifadhi mimi na Le Mutuz pale ofisini kwake, Tancot House hivyo tukapatana.
Ni Le Mutuz ndie aliyenitambulisha mimi kwenye YouTube channel, na video hii ya Le Mutuz ndio video yangu ya kwanza YouTube.
Ingekuwa video ni Mwanamke, tungesema ni video ya Le Mutuz ndio imeizindua YouTube Channel yangu. Thanks for that.
Na baada ya hapo akanipa bonge la shavu LE Mutuz: Special Salute To Paschal Mayalla!
Mara ya mwisho kuonana na Le Mutuz ni kwenye msiba wa Baghdellan pale Magomeni mwaka jana, alikuja na chuma fulani kikali sana na Davis Mosha!.
Kiukweli kabisa kwa jinsi Le Mutuz alivyo mtu wa watu, sijapenda mahudhurio hafifu niliyoyaona hapo nyumbani. Nilipategemea kukuta watu kufurika wakiwamo ma babez na washure wakiongozwa na Davis Mosha, labda tusubirie hiyo kesho, ila kwa sasa kitu muhimu sana ni kutoa mkono wa pole kwa familia.
Mkuu William Malecela Le Mutuz,
Umepigana vita vilivyo vitakatifu,
Mwendo umeumaliza,
Imani umeitunza.
Sisi tulikupenda, lakini Bwana amekupenda zaidi,
Bwana alileta, Bwana ametwaa,
Jina lake Lihimidiwe.
Buriani ya Kuonana.
Paskali
Baadhi ya mabandiko yangu na mwamba huyu
Kwanza natoa pole sana kwa familia ya Mzee John Malecela kwa msiba mkubwa na mzito wa mtoto wake, William Malecela, kwa jina maarufu Le Mutuz, aliyefariki leo asubuhi jijini Dar es Salaam. Msiba upo nyumbani kwa Baba yake Mzee John Malecela, pale Sea View. Nimepita pale na kufanikiwa kupata Ratiba ya Kumuaga.
Kwa mujibu wa msemaji wa familia Le Mutuz ambaye ni kaka wa Le Mutuz, aliyejitambulisha kwa jina moja tuu la Kaka Misano, amesema mwili wa marehemu utachukuliwa Hospitali ya Muhimbili Saa 2:00 Asubuhi na kupelekwa nyumbani Sea View kwa Ibada Fupi ya Kifamilia.
* Saa 3:00 asubuhi - Mwili utaondolewa nyumbani kuwasili Ukumbi wa Karimjee Saa 3:30.
* Saa 4:00 - Saa 6:00 - Shughuli za kuaga hapo Karimjee
* Saa 7:00 Mwili unaondoka Ukumbi wa Karimjee kupelekwa Airport, tayari kwa safari ya Dodoma.
* Saa 11:00 jioni - Mwili Utawasili Dodoma
Siku ya Jumanne kutakuwa na Ratiba za Dodoma.
Mazishi yatafanyika Mvumi Mission Dodoma, Siku ya Jumatano saa 9:00 Alasiri.
Kwa wote walioguswa na msiba huu mkubwa wawasiliane na familia wapewe utaratibu wa kutoa mkono wa pole.
My Take. My Tribute
Huu ndio msiba mkubwa wa pili kwa mwana JF maarufu baada ya Regia Mtema.
Kwasababu msiba wa Regia, wana JF, tulijitoa na kujitokeza, natoa wito kwa wana JF, kesho tujitokeze kwa wingi Karimjee.
Wenye kuweza kumsindikiza Dodoma, tumsindikize. Wana JF wa Dodoma, mtuwakilishe Mvumi Dodoma siku ya mazishi, na itapendeza kama kutakuwa na shada la JF.
My Personal Tribute to Le Mutuz:
Mimi nimesoma Shule ya Msingi Oyster Bay na watoto wote wa Mzee Malecela. Nilikuwa darasa moja na Jaji Mwendwa Malecela. Rais Hussein Mwinyi alitutangulia madarasa mawili, alikuwa darasa moja na Dr. Seche Malecela.
Nikiwa O Level Tambaza, Senyagwa alikuwa A level PCM, alipomaliza na kupiga DIV 1 ya point 3 na kujoin UDSM, Dr. Hussein Mwinyi na Seche, Mh. Silvester Koka walijiunga Tambaza PCB. Ni shule hii ya Tambaza kule juu summit, ndiko mimi niliko jifunzia kufanya mambo fulani, si unajua tena foolish age!.
Nikaja kuwa MC wa harusi ya dada yake, mmoja wa ma binti wa Malecela na mpaka leo, mpaka kesho from time to time na m visit Jaji Mwendwa..
Ni mpaka nilipokwenda jijini New York, nchini Marekani kwenye Ubalozi wetu UN pale New York, ndipo nikatambulishwa kwa shemeji yetu Mke wa Le Mutuz, ndipo nikamfahamu William.
Tukaja kukutana tena JF alipokuja kugombea ubunge wa Bunge la Africa Mashariki, akanitafuta, nikampa support
Kuna wakati nikiwa Dodoma akanikaribisha home kwa Dingi pale Dom, kisha tuka drive all the way from Dom to Dar so we got to know better, ndipo nikajua kumbe jamaa, don't drink!, don't smoke, just chilling tuu and have good time!.
From there tukawa marafiki, kama vilivyo vikombe kabatini kuna wakati tukapishana kauli, akanifungia madirisha!. Alikuwa mwepesi kukasirika, hachelewi kukiwasha ila pia mwepesi kusamehe!.
Tukaja kupatanishwa na mwana JF Sactus Mtsimbe, kuna wakati alituhifadhi mimi na Le Mutuz pale ofisini kwake, Tancot House hivyo tukapatana.
Ni Le Mutuz ndie aliyenitambulisha mimi kwenye YouTube channel, na video hii ya Le Mutuz ndio video yangu ya kwanza YouTube.
Ingekuwa video ni Mwanamke, tungesema ni video ya Le Mutuz ndio imeizindua YouTube Channel yangu. Thanks for that.
Na baada ya hapo akanipa bonge la shavu LE Mutuz: Special Salute To Paschal Mayalla!
Mara ya mwisho kuonana na Le Mutuz ni kwenye msiba wa Baghdellan pale Magomeni mwaka jana, alikuja na chuma fulani kikali sana na Davis Mosha!.
Kiukweli kabisa kwa jinsi Le Mutuz alivyo mtu wa watu, sijapenda mahudhurio hafifu niliyoyaona hapo nyumbani. Nilipategemea kukuta watu kufurika wakiwamo ma babez na washure wakiongozwa na Davis Mosha, labda tusubirie hiyo kesho, ila kwa sasa kitu muhimu sana ni kutoa mkono wa pole kwa familia.
Mkuu William Malecela Le Mutuz,
Umepigana vita vilivyo vitakatifu,
Mwendo umeumaliza,
Imani umeitunza.
Sisi tulikupenda, lakini Bwana amekupenda zaidi,
Bwana alileta, Bwana ametwaa,
Jina lake Lihimidiwe.
Buriani ya Kuonana.
Paskali
Baadhi ya mabandiko yangu na mwamba huyu
- Watch TBC Live!. " William Malecela na Ndoto ya CCM Kutawala Miaka 50!. mode, ikikupendeza, lifugue bandiko hili kumuaga!.
- TBC: Mtaalamu wa meli, William Malecela atoa maoni yake ya kitaalam kuhusu usalama melini
- LE Mutuz: Special Salute To Paschal Mayalla!
- William Malecela: Watoto wa viongozi na uongozi wa taifa letu!
- Nini kinamsibu William John Malecela?
- Mzee John Malecela atua Jijini Dar kwa ajili ya kushiriki msiba wa Mwanaye