Kwanini Levina Mukasa alijiua UDSM?

Kwanini Levina Mukasa alijiua UDSM?

Hahahaa, Lizzy, huyu Smile ni Mtani wangu. Anataka sana kuolewa SIKONGE na Wanyamwezi wa huku. Ingawa yeye ni Mchaga, ila hata sijui utani na Wanyamwezi kaanza lini, ila basi tu imetokea Mnyamwezi kawa Mpare kwa kuFIKIA. Huu Mwaka hauishi, lazima mtu awe kama SAYARI ya SATURN...... Ili akubali kiharaka haraka, unamnyanyasa kwanza KIJINSIA kama Mzee Punch vile.... Mwisho, kumbuka sisi Wahandisi hata kutongoza hatujui, si umesoma mwenyewe? Hata kama ana miaka 18 na mie nina 58, unamnyanyasa hadi anajiona ni yeye ana 58 na mie nina 18 na kuwa namfanyia MSAADA tu kuwa naye, heheheee 🙂

1saturn.jpeg
images

Hii story kwa kweli nimeiandika kwa jinsi nilivyokuwa naikumbuka kwani wakati ikitokea, nilikuwa bado na kamasi puani.

Hahahaha wewe sasa utaharibu vijana kwa kuwapa maujanja. Kwanza unamshusha thamani alafu ndio unamchukua. Ndio maana wengi wanaonyanyaswa kwenye mahusiano huwa hawana ujasiri wa kujitoa.

Nwy nyie endeleeni kutaniana. Ila andaa hela ya kutosha maana wazee wetu hawa-PUNCH-ki kirahisi, labda kama utakuja na mjukuu kabisa.

. . . . . . .
Basi uko vizuri sana. Nasubiria wengine watiririke tujue zaidi.
 
Hahaha!! hayo majina ukiyasikia tu unajua kabisa si salama

Kuna siku mwaka 1993 au 1994 wanafunzi wa WU-TAMBA walitembeza mkong'oto karibia shule zote za msingi na sekondari.

Nakumbuka siku hiyo ilikuwa ni hekaheka mjini hapa, wanafunzi na waalimu walipigwa bila kusahau mali za shule nyingi ziliharibiwa.

Walifika hadi Bunge Primary....jamaniii mmh!!
 
aisee mimi sithubutu kurusha mguu wangu kwa mnyamwezi tena! hata uniambie utanipeleka wapi acha niishie kutalii mlima kilimanjaro na misitu yake basi!....khaaa kuna watu wana roho ngumu kama paka bwana


Mama nakwambia MOYO wa mtu ni msitu mnene sana! Yani weee acha tu!
 
Mwanamke mmejaliwa uwezo mkubwa sana kumtawala Mwanaume. Kama hujui wee uliza.

Mwisho kumbuka milele kuwa mie nimekuzwa na Mwanamke, hivyo nawaheshimu sana Wanawake wote duniani.

Sawa Mzee mwenzangu, ngoja nikukimbie na kiburudisho maana Weekend inaanza, ngoja nichukue Bugaluu yangu na Raizon langu nijivike nikaruke mangoma leo jioni. Afro langu linawaka si mchezo sasa hivi.


aisee mimi sithubutu kurusha mguu wangu kwa mnyamwezi tena! hata uniambie utanipeleka wapi acha niishie kutalii mlima kilimanjaro na misitu yake basi!....khaaa kuna watu wana roho ngumu kama paka bwana
 
Last edited by a moderator:
Mwanamke mmejaliwa uwezo mkubwa sana kumtawala Mwanaume. Kama hujui wee uliza.

Mwisho kumbuka milele kuwa mie nimekuzwa na Mwanamke, hivyo nawaheshimu sana Wanawake wote duniani.

Sawa Mzee mwenzangu, ngoja nikukimbie na kiburudisho maana Weekend inaanza, ngoja nichukue Bugaluu yangu na Raizon langu nijivike nikaruke mangoma leo jioni. Afro langu linawaka si mchezo sasa hivi.

ngoja nikale kuku kwanza
 
Last edited by a moderator:
Mhh...Hii habari imenisikitisha sana. Hivyo naomba uongozi wa UDSM pamoja na ule wa DARUSO mjiuzulu ili kulinda heshima yenu kama wanataaluma mbele ya jamii. Hii ni kutokana na kushindwa kudhibiti kundi haramu la PUNCH ndani ya hiyo taasisi kubwa ya elimu nchini .
 
thanks EMT kwa kutukumbusha, Enzi hizi za digital hadi kwa simu za techno kama mzee punch angekuwepoba bado angerahisisha mambo, R.I.P dada Levina.
 
Last edited by a moderator:
Mhh...Hii habari imenisikitisha sana. Hivyo naomba uongozi wa UDSM pamoja na ule wa DARUSO mjiuzulu ili kulinda heshima yenu kama wanataaluma mbele ya jamii. Hii ni kutokana na kushindwa kudhibiti kundi haramu la PUNCH ndani ya hiyo taasisi kubwa ya elimu nchini .

Kwahyo uongozi wa sasa wa UDSM na Daruso wajiuzulu au nimekuelewa vibaya.
 
Kuna miaka Mzee Punch alipunchiwa anafukuzwa na Masaai Warrior wa kike ambaye alikuwa amepunchiwa siku za nyuma;Kwa kweli ilikuwa vita!!!
 
Ooooh my God, kumbe huyu dada alifariki kwa style hii. I was young by then nadhan standard one, nilishuhudia mazishi yake pale hom biharamulo, mtaa wa rukaragata. Tulihudhunika sana, coz she was a very fun of mine, alikuwa akinifundisha kusoma mara alipoenda chuo kikuu na kuniahidi angeniledea vitabu akirudi, lakin alirudi ndani ya jeneza.
rest in peace dadaa,

unakumbukwa sana na mzee mkasa, mama yako, kaka zako bernard, mwombeki, padri faustine, osca na mdogo wako lidia.
 
Serikali nayo ilikua lege lege hadi anaacha wahuni wanatamba. Sahvi Mkandala hacheki na watu wa vurugu kama hao waulize walipoishia wanaharakati.Sasa hivi hata Revo Square kwishney.

Daaah akina Odong Odwar nao wamemtesa Mkandala! Bora tu kama amedhibiti zile mambo
 
so sad, kundi hilo liliendelea hadi miaka ya 2000 japo hali ilibadilika kiasi kwani hadi wanaume walikuwa wakitolewa Punch. Pia kuna wanawake walianzisha kundi lao "MOTHER OF THE LAND" Walikuwa wakiwatoa wanaume sana sana japo haikuwa strong kama PUNCH Original. Wengi sana walifikia uamuzi wa kukatisha maisha yao japo takwimu sahihi zinaweza zisiwepo. Safari ya Usawa wa Kijinsia na kumaliza unyanyasaji wa kijinsia ni ngumu sana kwa kuwa wapo wanaofanya hivyo bila kujua ni unyanyasaji na wapo wanawake wanaofurahia na kuchekelea kwa kuona mwanamke mwenzie ananyanyasika. Mungu azilaze pema roho za marehemu walitutangulia kwa unyanyasi wa kijinsia wa aina yoyote.

Nakumbuka pia 2004/5 wanafunzi wa Milambo secondari walienda usiku kuvamia wasichana wa tabora girls skul. Wasichana walichapwa na kumwagiwa kinyesi kilichobebwa kwenye ndoo na wanafunzi kutoka Milambo. It was very sad wapo waliopata ukilema mdogo kwa kupasuka midomo na majeraha mbalimbali.

Pia 2008 kuna mwnafunzi wa kike wa DUCE pale mabibo hostel alichomwa kisu na mwanaume aliyesemekana alikua mpenz wake lakini baadae huyo mwanaume alikataliwa kimapenz na huyo binti na hatimaye binti alichomwa kisu na kupoteza maisha yake.

It was a sad story na siku hiyo Dr Ndodi alikua uwanjani akiwafundisha wanafunzi mambo ya dawa na tiba asilia around saa 2 usiku.

Pinga ukatili wa kijinsia yanaweza kumkuta dada yako mama yako mwanao au ndugu wa karibu
 
Inasikitisha kwa waliokumbwa na dhahama za aina hii....
Punch ilikua nzuri kwenye siasa, nadhani hili la kudhalilisha halikua lengo lao la msingi...nadhani walitumia vibaya nia na uwezo wa punch!!!

Hilo la kudhalilisha ndiyo lilikuwa lengo la msingi kwani wakati wa Nyerere mazungumzo ya siasa vyuo vikuu yalikuwa limited.
 
Rest in peace Levina. Mwili wako ulitumika kwa ajili ya maslahi ya wachache Tanzania, wanasiasa na watawala wa hila Roho yako iwe nasi katika kupambana na udhalimu huu wa CCM katika nchni yetu maana ndio Punch wa leo katika Maisha ya leo.
 
Prof . shivji huyu huyu ninayemheshimu aliongea kauli dhaifu kama hiyo? Au alikuwa anamaanisha nini kuhusu saga hiyo labda sikuelewa??!!
bora umeuliza maana shivji nimesoma miaka mitatu pale midahalo mingi aliyowahi kuiendesha ikiwemo kigoda cha mwalimu nyerere hawezi kuonesha kauli ya kidhaifu hivyo haswa katia swala nyeti hvyo
 
Asante EMT , watu8 , Kashaijabutege , Kongosho na Pasco kwa kumbu kumbu hii nzuri yenye mafunzo mengi. Mungu amlaze pema peponi shujaa huyu Levina, natamani kusikia picha na historia yake ipo maktaba ya UDSM. Pia itakuwa ni busara kwa waliokuwa member wa hili kundi la PUNCH wakatubu hadharani na jamii itawasamehe, imewezekana SA na Rwanda, waige mfano huo.

Mbona mimi nakumbuka kama huyu alijirusha ghorofani? Ilitangazwa kwenye vyombo vya habari enzi zile ni radio tanzania.

Vile vile ilikuwa ni hot issue na kulikuwa na discussion kwenye magazeti (sina uhakika kama ni lile la mfanyakazi) kuhusu role ya punch pale chuo kikuu.

Kwa kweli hili tukio lilishtua watu wengi miaka ile na ilionyesha jinsi gani wanawake walikuwa wanadhalilishwa pale chuoni.

Wale vijana waliosababisha hiyo walifanywa nini, au waliachiwa kuendelea na degree zao bila zahama?
 
Back
Top Bottom