Kwanini Levina Mukasa alijiua UDSM?

Kwanini Levina Mukasa alijiua UDSM?

kweli mkuu, inawezekana kabisa hakuna hata mafaili Police....... Kwa hapo criminal case itakuwa ngumu!! Lakini la madai nafikiri linawezekana kabisa ............ na chuo au Wizara husika ikalipishwa fidia!! Kama issue ilifikia mpaka kwenye ngazi za utawala wa chuo basi kuna uzembe mkubwa sana ulifanyika. Hata hao akina Victor na Omari wanaweza kupelekwa kama mashahidi kwenye kesi hiyo ya madai.

Madai inawezekana kabisa, hata chuo kinawajibika. Usalama wa wanafunzi ulikuwa mikononi mwa chuo. And under that harassment the university was responsible to act
 
so ndo ilikuwa KKK ya mlimani wakati huo na ilikuwa nadhumuni lipi na kinanani walikuwa ma founder wa hii?...kati ya maswali ya kujiuliza huenda hata wakina Ulimboka na wote waliopata mateso ya kinyama pale mabwepande ni source kama sio product ya PUNCH
Binafsi nilivyoiona PUNCH hakikuwa chombo cha wanafunzi peke yao. Kama nilivyosema awali, kwanza lugha iliyotumika katika makala zake ilionekana kusheheni ujuzi wa fani mbalimbali (madaktari, wahandisi, waandishi wa habari, wachumi, polisi, usalama wa taifa, n.k). Kuna matoleo mengine yalikuwa ni ya uchunguzi wa kina wa jambo (investigative), kiasi kwamba mwanafunzi wa kawaida asingekuwa na uwezo wa kifedha kukamilisha uchunguzi huo. Makala nyingine ziliianika serikali au taasisi zake, jambo ambalo lilikuwa gumu kuwezekana pasipo mkono wa nje ya Mlimani.

Lingine linaloonesha kuwa PUNCH hawakuwa wanafunzi peke yao, ni ule uwezo wa kutundika makala hizo sehemu nyeti, kama jengo la utawala pasipokushikwa wahusika.

PUNCH vile vile ilikuwa ni vent ya kuikosoa serikali katika mazingira ya chama kimoja na uchache wa vyombo vya habari. Enzi hizo watu, wakiwemo watawala, walipanda magari kuja Mlimani kusoma matoleo ya PUNCH.

Nakiri kabisa kuwa PUNCH ilikuwa na madhara ya kibaguzi (hasa kwa wasichana-waliokuwa wachache vilevile), lakini kuna na mambo mazuri (postive) ambayo PUNCH imechangia katika ustawi wa Taifa hili.

Nguvu ya PUNCH nilivyoiona, lazima ilikuwa na patrons wenye nguvu, nje na ndani ya Chuo, ingawa sisemi Shivji alikuwa mmoja wao.
 
R.I.P Levina!

so saaad..yaan nimesikitika sana sana nakumbuka UDOM kulikua na.kundi lililokua linajiita Mungiki ambapo weng kwenye kundi hilo walisoma Ilboru Arusha..hawa ndo walikua vinara wa migomo na kama chakula kikipandishwa bei cafteria wanapitisha vikaratas chini ya milango wakiwatahadharisha watu kutokwenda ole wake uende cafteria utakiona..kwa bahat weng wao waligundulika na kufukuzwa chuo..jamani makundi kama haya ni ya kukemea kwenye jamii jamani haswa vyuoni na kwenye shule za sekondari..
 
Miaka ya mwishoni mwa 80 na mwanzoni mwa 90 karibu taasisi nyingi za elimu zilikuwa na makundi kama haya.

Wanafunzi wengi haswa wa kiume walikuwa na makundi ya siri au yanayojulikana na lengo kubwa la makundi haya ilikuwa ni kufanya tu vitendo vya kihuni na haswa kwa wasichana au wanawake.

Wengi wanaweza wakawa wanaikumbuka Tambaza(WU-TAMBA CLAN) ya wakati huo kabla wanafunzi wake hawajasambazwa mashule mengine na O-Level kuvunjwa rasmi.

Shule kama Ilboru ilikuwa na makundi ya wanafunzi wavuta bangi ambao walijitenga na kuishi katika bweni moja kiasi kwamba mwanafunzi mgeni ukiingia huko ni kama umepelekwa gereza la Sona na kukutana na kina Theodore Bagwell (T-Bag).
Aisee walivyoisambaratisha tambaza ilikua vema kabisa manake wale vijana walikua wamefika pabaya.Nakumbuka hii issue ya levina inasikitisha sana
 
Based on the preponderance of the evidence, nafasi ya kushinda kesi ya madai ni kubwa zaidi kuliko ya jinai.

Kwenye jinai hapo itakuwa rahisi sana kutilia shaka usababishi wa moja kwa moja wa watuhumiwa.

Tumsaidieje mama yake apozwe kidogo.
 
Hahaha!! hayo majina ukiyasikia tu unajua kabisa si salama

Kuna siku mwaka 1993 au 1994 wanafunzi wa WU-TAMBA walitembeza mkong'oto karibia shule zote za msingi na sekondari.

Nakumbuka siku hiyo ilikuwa ni hekaheka mjini hapa, wanafunzi na waalimu walipigwa bila kusahau mali za shule nyingi ziliharibiwa.

Heeee haya yalitokea hapahapa tanzania mkuu?

Dizaini zamani wanafunzi wa kiume walikua wanaume hasa sio vishalobalo vya siku hizi hata ngumi havijui kuikunja
 
Heeee haya yalitokea hapahapa tanzania mkuu?

Dizaini zamani wanafunzi wa kiume walikua wanaume hasa sio vishalobalo vya siku hizi hata ngumi havijui kuikunja

Yalitokea hapa hapa Tanzania tena Dar es Salaam, wakati wa awamu ya mwisho ya Rais Mwinyi.

Haijawahi kutokea wanafunzi wakorofi kama hawa ninaowaeleza wa Tambaza, sijui chanzo kilikuwa ni nini haswa!!!
 
So sad, kundi hilo liliendelea hadi miaka ya 2000 japo hali ilibadilika kiasi kwani hadi wanaume walikuwa wakitolewa Punch. Pia kuna wanawake walianzisha kundi lao "MOTHER OF THE LAND" Walikuwa wakiwatoa wanaume sana sana japo haikuwa strong kama PUNCH Original. Wengi sana walifikia uamuzi wa kukatisha maisha yao japo takwimu sahihi zinaweza zisiwepo.

Safari ya Usawa wa Kijinsia na kumaliza unyanyasaji wa kijinsia ni ngumu sana kwa kuwa wapo wanaofanya hivyo bila kujua ni unyanyasaji na wapo wanawake wanaofurahia na kuchekelea kwa kuona mwanamke mwenzie ananyanyasika. Mungu azilaze pema roho za marehemu walitutangulia kwa unyanyasi wa kijinsia wa aina yoyote.
 
Asante kwa kutukumbusha hiki kisa, kisa ambacho kilimsikitisha yoyote mpenda haki. Lakini tukio hili, ulikuwa ndio mwisho wa Mzee Punch. Nilikuwa namjua Levina kwa karibu sana. Mimi mwenyewe wakati huo nilikuwa hapo chuoni na nilikuwa naishi Hall moja na Levina. Yote yaliyomtokea kabla ya kuamua kujiua nilipata nafasi ya kuyafahamu na kwa namna moja au nyingine nilijitahidi kuweka mambo sawa ili hali aliyokuwa nayo Levina isije ikaleta madhara, bahati mbaya mhusika akunielewa lakini baada ya Levina kuwa amekunywa sumu, huyu mtu alinifuata na kujuta ni kwa nini hakufuata ushauri wangu, mtu huyu ndiye pekee aliyekuwa na uwezo wa kuepusha alichoamua kukifanya Levina.

Wakati ule, kaka yake Levina ambaye wanashare Baba na Mama Mr. Deo Mukasa alikuwa mwaka 3, Bcom. Na yeye hakuweza kuyaokoa maisha ya mdogo wake, kwani hakujua kama mdogo wake angeamua kufanya alichokifanya.

Ukware wa kijana wa kikurya Saloti kwa mgongo wa Mzee Punch ulimtoa roho binti wa watu. Watu tulikasirika na ilibidi Ma-engineer wazikimbie meza walizokuwa wanadai ni wao tu wanaopashwa kukaa.

RIP Levina.

Tiba
 
Ushahidi wa kuridhisha upo? Manake soga za humu tu si ushahidi.

Na vipi kuhusu statute of limitation kwenye civil suits? Na hapo itakuwa ni aina gani ya civil suit?

Longest time in such civil suits is 12 years, but the minister can extend the period of limitation not exceeding.......years(????) need research!
 
Longest time in such civil suits is 12 years, but the minister can extend the period of limitation not exceeding.......years(????) need research!

And when did the girl take her own life? Twenty some years ago, right?
 
Back
Top Bottom