Kwanini konyagi huwa inalazwa?

Kwanini konyagi huwa inalazwa?

Kulazwa kwa Konyagi mezani ni tamaduni ya mtaani iliyojaa maana ya kiheshima, ukali wa kinywaji, au ubabe wa wanywaji.

Ni style tu ya kuonyesha upekee kwamba msije mkamuangusha huyu mwamba ngoja tumlaze - Ni street culture, si lazima iwe na maana rasmi.

Na hii tuliyolaza je? Sijaona Mikono hapa wala utamaduni wa mtaani.

678E923C-8BDC-43E3-B1C8-DA3FC8C5C181.jpeg
 
Kwasababu ya Muundo wa Chupa yake.
Ukiisimamisha inakaa ila sio stable.
Ukiilaza inatulia na inakuwa stable.
Maana Kitako chake kidogo...
Pia hard liquors nying zenye mgongo mnyoofu na kitako kidogo hulazwa.

Na zenye chupa za Round husimamisha maana kitako kina stable base.

Tuachane na hizo sababu za ajabu hapo juu.

Hulazwa ili kushindana tu na yule jamaa aliyenyayua mikono, ionekane kuwa umemshinda.
Na pia ukinywa imesimama kuna kiungo kitasimama wakat huo huo, bora ilale na Kiungo kilale,
Kitaenda kuamsha dude huko mbelen.
Konyagi ndogo inasimama mezani vizuri tu, hata ile kubwa sehemu isiyotingishika kama meza za kaunta inasimama mezani vizuri tu.
 
Salaam alyekum,

wakati sosho media zimejaa taarifa zisizo na tija sijui gwaji boy, sijui gen z binafsi naona ni kama kelele za chura ambazo hazimzuiii kuendelea na kazi huo ulikuwa utangulizi lakini swali langu ni kwanini konyagi huwa inalazwa? …..ukizingia kwenye comment principle yangu ni ile ile “ntakutafuta ntakupata na nitakufurahisha”
No reform no election
 
Chupa ipo bapa ile ukiisimamisha meza ikicheza kidogo tu inaanguka, chupa zote za bapa na chache za pembe tatu huwa zinalazwa. Hazipo stable.
Konyagi ndogo ipo stable, ile kubwa kwenye meza ya kaunta inasimama vizuri tu.
 
Konyagi ndogo inasimama mezani vizuri tu, hata ile kubwa sehemu isiyotingishika kama meza za kaunta inasimama mezani vizuri tu.
Sawa bro!
Ila hap hujajibu hoja kwanini inalazwa.

Umetoa tu condition.
 
Nafikiri hayo ni maamuzi yenu binafsi, Hiyo whisky haijazoeleka kulazwa.

Sehemu nyingi nimeona konyagi ndiyo imezoeleka kulazwa.
Sawa.
Kwahiyo kinywaji cha Kulaza tu ni Konyagi , na inakubid kwakuwa sio maamuzi yako binafsi?.

Hard Liquors nying hulazwa kwasababu ya Muundo wa chupa, hakuna cha ubabe , utamaduni wala ukali wa Kinywaji.
 
Wabongo huwa hawaulizi.. wakiona waliowatangulia wanafanya hivi, nao hufanya vile vile bila kuuliza sababu ya kufanya vile.

Mtu tu kuamua kujilazia bapa yake, mtu kaona akajua ndo utaratibu.

Wengi hawawezi kitu kinaitwa "questioning the premise".

Ni wachache sana ukishawaweka katika reli ya "kati ya A na B unachagua ipi?" wanaweza kukuhoji kwa nini wachague, kwa nini uchaguzi uwe A au B, kwa nini wasiwe,e juchagua vyote A na B au kingine tofauti C?
 
Nimejibu, ni mbwembwe tu za walevi, wengine huwa wanaipiga chini kwenye kitako kabla hawajaifungua.
Haujajibu.

Umetoa comdition kuwa inaweza ikasimamishwa. Ndogo kuwa iko stable na kubwa kuwa meza ya Counter itakaa.

Sasa kwann weng wanalaza?
 
Nimejibu, ni mbwembwe tu za walevi, wengine huwa wanaipiga chini kwenye kitako kabla hawajaifungua.
Ile sio mbwembwe ile ni physics Mkuu, Henry's law,the solubility of a gas in a liquid is proportional to the partial pressure of that gas above the liquid.

Ile paaah!, inafanya inakuwa rahisi zaidi kukifungua kifuniko kwa zenye mifuniko ile. Kumbuka.sio chupa zote zinafanana viuniko ndio maana bado sio zote zinapigwa chini.

Hiyo ni worldwide sio bongo tu.
 
Ile sio mbwembwe ile ni physics Mkuu, Henry's law,the solubility of a gas in a liquid is proportional to the partial pressure of that gas above the liquid.

Ile paaah!, inafanya inakuwa rahisi zaidi kukifungua kifuniko kwa zenye mifuniko ile. Kumbuka.sio chupa zote zinafanana viuniko ndio maana bado sio zote zinapigwa chini.

Hiyo ni worldwide sio bongo tu.
Sawa mkuu, nilikuwa sijui kama ile kupigwa kibao kwa chini ni elimu ya physics ifunguke vizuri!🤣
 
Back
Top Bottom