Nawe utakuwa unasumbuliwa na ushamba tu na wala si kingine!!
Ushamba unawafanya watu wadhani brutality ndio uanaume wakati huo ni ushamba tu!!
Ushamba ndo unawafanya watu waone mwanaume asiyepiga mwanamke ni dhaifu!!
Ushamba ndo unawafanya watu waone kupiga mwanamke ndo uanaume!!!
Ushamba ndo unawafanya watu wakatae kuoa wasomi eti kwa sababu "wasomi wanajifanya kujua sana"!!
Ushamba ndo unawafanya watu wadhani mwanaume anayemsikiliza wife/girlfriend wake huyo mwanaume ni dhaifu, na anapelekeshwa!!
Ushamba ndo unawafanya watu waone mwanamke akikubishia basi huyo ni jeuri hata kama ni kweli ulichofanya ni upumbavu lakini usipingwe eti kisa ni mwanaume!!!
Ushamba ndio unawafanya watu wadhani mwanamke hana sauti kwenye jamii!!
NI ushamba huu huu ndio unawafanya watu waamini wanaume ndio wanastahili kurithi na wanawake hawastahili!!!
Ushamba ndo unawafanya watu wadhani feminism ni ukorofi!!
My girlfriend or wife will always be MY BEST FRIEND!!
So, nitakuwa very stupid endapo nitataka my girlfriend or wife awe kama Msukule kwangu, anayekubali kila ninachosema au kutaka hata kama ni cha kipumbavu!!!
For me I'll feel blessed mwanamke akinikosoa, na nikiangalia nakubalia kabisa kwamba she's right and I was not kuliko unakuwa na jitu ambalo mwanaume ukishatoa maamuzi ya kipumbavu, yanapita hivyo hivyo na kuja ku-backfire kwa familia!!
Na nitakuwa very stupid nikianza kurusha ngumi kwa MY BEST FRIEND coz' kama alichofanya ni completely intolerable, my best option will always be to let her go, and trust me, she'll always be my best friend no matter what!!!
And guess what... am now in my 40's, lakini sijawahi kuachana na mwanamke kwa visa, and am proud of it coz' I know how to manage difficult situation!!!!
Na kama alivyosema cariha hapo juu, watu aina yenu mnasumbuliwa na insecurity and inferiority complex, na kwahiyo mnataka kutambulika kama wanaume not based on your responsibility as a man but by being physically TOO TOUGH over a woman... huo ni ushamba tu!!
I don't have to do anything stupid to prove my manhood which will always be judged based on my responsibility as a man!
Again, I love a feminist women, na sio mwanamke unayeweza kumpelekesha pelekesha tu kama msukule, na hajui hata haki zake!! Na kama hajui haki zake, na hawezi kupigania haki zake at a family level, ni namna gani anaweza anaweza kupigania haki za familia wakati ambapo mumewe yupo kwenye mazingira yasiyomwezesha to stand for his family?!