Nakushauri Somea sheria nenda kafanye kazi mahakamani.
Kuna hakimu mmoja(mwanamke) mahakama ya mwanzo mkoa mmoja alimfurusha mwanamama mjuaji aliyeachika kwa kwa hiari yake hapohapo mahakamani, baada ya aliyekuwa mumewe kuugua sana alirudi kumuuguza baadae akafariki.
Ndugu wakaenda kuzika na kwenye mirathi akasema yeye ndiye atakuwa msimamizi familia ikakata kauli kutomtambua maana kisheria aliachika ila yeye kwa uelewa wake kwa sababu alimuuguza anayo haki kusimamia mirathi.
Shauri lilipelekwa mahakamani na hakimu (mwanamke) alimpasha sana pale mahakamani na kumfurusha akidai sheria haimtambui maana tayari alidai taraka na kumuacha mume kwa hiari yake. Ni vyema ujifunze na sheria kuongeza knowledge