Mawele

Member
Jul 25, 2023
30
116
Video hii inaonesha mtu akichapwa fimbo huku akiambiwa "Hapa si bara" sababu za kuchapwa eti ni kwa kuwa amekula mchana chakula wakati wa Ramadhani.

Hivi Zanzibar, mnawachukuliaje watu wa bara? Ni watu baki au ni watu wasio na haki ya kukaa Zanzibar? Maana hapo ni ubaguzi wa wazi, kupanda mbegu ya chuki ambayo ni hatari kwa Taifa.

Kwani mtu ukifunga, ukaendelea na mfungo wako inakuathiri nini kwa asiyefunga kula?

Siyo sawa Kitendo cha kuwachapa au kuwafanyiwa vitendo mbalimbali vibaya watu wasiofunga mwezi wa Ramadhani.



Soma pia:

1) Yanayoendelea Zanzibar tusubiri majibu ya wahanga na kuzaa Gharika

2) Zanzibar: Akutana na kipigo baada ya kuonekana akila mchana!

3) PEMBA: Achapwa Mikwaju Kula Mchana Mwezi mtukufu wa Ramadhan

4) Serikali ya Mapinduzi Zanzibar yalaani vitendo vya unyanyasaji vinavyoendelea visiwani

5) Zanzibar yapiga marufuku mambo yafuatayo katika kipindi cha mwezi wa ramadhan
 
Hawa wakazi wa huko visiwani na viongozi wa huko ni wapumbavu sana. Wanajiona wao ni watu special sana. Sijajua kwann mamlaka zinawachekea takataka hawa.

Hadi polisi wa huko visiwani wanashirikiana na hawa raia kufanya ufala. Hizi sio tabia za kuungwana na sio sehemu ya tamaduni zetu sisi waafrika.
 
Nimeona klipu Moja ya kusikitisha Leo asubuhi ! Baba mmoja mtu mzima anacharazwa bakora mbele za watu kwa kuwa tu yeye hajafunga! Hilo halijanishtua Sana kilicho nisikitisha ni maneno ya wazanzibar kwa mtu huyu Ambae kwa haraka haraka nimegundua mi mzee wa makamo! Maneno kama huku sio bara ,huku sio kwenu ,nyinyi wa bara si mna kwenu? Hayo maneno yamenifanya nifikirie mara mbili kuhusu Ninani hasa anautaka muungano?
 
Unajua chuki ni kama ugonjwa kuna siku utakuumbua tu. Serikali isipokuwa makini na kuwakaripia Wazanzibari tutajikuta kwenye vita kubwa kati ya Tanganyika Vs Zanzibar na Wakristo Vs Wasalimu.
Hawawezi kuwakaripia kipindi hiki cha Uchaguzi......huzijui siasa za Tz?
 
Back
Top Bottom