Duh mbona mapema mkuu wangu unaondoka hali bado twakupenda?..- Ndugu yangu sana Bob, sikusema Mbowe ajiuzulu, no way bado Chadema inamuhitaji sana na bado ana miaka mingi zaidi ya siasa, isipokuwa Dr. Slaa huu ni wakati muafaka kwake kuanza kufikiria kukaa pembeni na awaachie wengine watafute agenda mpya ya Chadema kwa taifa, maana ya ufisadi imesiha nguvu tayari!
- Nitakupigia weekend maana last week ulikuwa hupatikani kwenye simu! Na sasa naomba kutoka kidogo baaadaye wakuu wote!
William @ NYC, USA.
Hata hivyo ukirudi utayakuta haya..Dr.Slaa akae pembeni kwa sababu gani?..
Issue ya Ufisadi haiwezi kwisha ikiwa CCM wanacheza ngoma ya Dr.Slaa utafikiri wazungu wanavyocheza kiduku..Na wala sii swala la kisiasa tu Ufisadi ni lazima upigwe vita juu chini hadi imani ya watu irudi sio tu kwa CCM na viongozi wake bali kwa Taifa zima. Hvi vita sio vya Dr.Slaa hata kidogo, tazama mabillioni ya JK yalivyoyeyuka, Zana za kilimo kwanza zinavyopotea yaani wee acha tu. Ufisadi ni kwa kwenda mbele. Pengine unahitaji kutembea Bongo hata iwe kwa week tu utaipata fresh.
Hakuna sababu za kimsingi kwa Dr.Slaa kukaa pembeni wakati moto ndio umekolea, isipokuwa kuna watu pembeni ambao mimi nina mashaka na dhamira yao kwa sababu wanatumia sana jina lake lakini hawapo Chadema ati wao ni NEUTRAL na wanaunda kundi la kisiasa pasipo mrengo..Kwa maneno yao wanafuata mtu sio chama, hii kusema kweli inanipa shida sana kuelewa...