Masanilo
Platinum Member
- Oct 2, 2007
- 22,286
- 4,493
Kaka William Malecela
Bila shaka uko salama na unaendelea na majukumu ya kila siku ya kimaisha. Nimeona leo nikuandikie waraka wa kirafiki kuhusiana na hali ya kisiasa na maisha yetu huku Tanzania. Nilikusoma siku chache zilizopita ukifahamisha umma jitihada zako za kuanzisha tawi la CCM huko uliko. Wengi walikupongeza na wengine kama kawaida walikubeza na kwenda mbali zaidi. Nakumbuka kwenye lile bandiko uliweka kauli mbiu ya kuvua magamba na CCM mpya. Nadhani Kaka Wiliam unajua sasa zile zilikuwa ni sanaa tu, Mukama na Nape wamekuwa wakitofautiana na muafaka na nani na lini hatua zitachukuliwa zidi ya wale waliokiweka chama chenu hapo kilipo. Mukama alienda mbali zaidi kudai hakuna listi ya watakao vuliwa magamba. Kumbuka huyu ndiye mtendaji mkuu wa shughuli za kila siku za chama na sekretariat nzima.
Bila shaka hakuna anachofanya Kikwete bila Rostam, Chenge na Lowassa kujua. Hawa watu wameshiriki kwa karibu sana na Kikwete na kufanikisha CCM-Mtandao Kushika dola. Haikuwa rahisi watu hawa kutengana kirahisi kama wengi tulivyotaka iwe. William ningeweza kukuandikia PM ila nimeona wacha na wanaJF wengine walione na watachangia. CCM na Magamba ilikuwa ni sanaa, kama ambavyo mwenyekiti wenu amekuwa akicheza na jukwaa kufurahisha hadhira. Alianza na semina elekezi Ngurudoto, kwa top govt officials, tunajua kashfa za ngono zilizofanyika kule 2006. Juzi katembelea wizara na kuamsha utendaji wa kazi, sasa amekuja na semina elekezi Dodoma, anarudia yale yale, kwenye formal logic hali inaitwa Tautology, hakuna tija wasiofanya kazi awapige chini, ngonjera zake zina gharama sana kwa wapiga kura. Nina wasi wasi CCM itagawanyka mikononi mwake na Muungano na Zanzibar utavunjika kabla ya 2015.
Kaka ningekushauri ufunge hilo tawi njoo tuungane kwa mambo yenye maslahi kwa taifa! Tuwe watanzania na si waCCM. Taifa lije mbele kama watanzania shida za umeme zinatokana na ufisadi zinatupata wote.
Ilikuwa niandike mengi wacha niwahi mazishi kuna kada wa CCM amekufa hapa mtaani
Respect
Mdogo wako Mch Masa
Bila shaka uko salama na unaendelea na majukumu ya kila siku ya kimaisha. Nimeona leo nikuandikie waraka wa kirafiki kuhusiana na hali ya kisiasa na maisha yetu huku Tanzania. Nilikusoma siku chache zilizopita ukifahamisha umma jitihada zako za kuanzisha tawi la CCM huko uliko. Wengi walikupongeza na wengine kama kawaida walikubeza na kwenda mbali zaidi. Nakumbuka kwenye lile bandiko uliweka kauli mbiu ya kuvua magamba na CCM mpya. Nadhani Kaka Wiliam unajua sasa zile zilikuwa ni sanaa tu, Mukama na Nape wamekuwa wakitofautiana na muafaka na nani na lini hatua zitachukuliwa zidi ya wale waliokiweka chama chenu hapo kilipo. Mukama alienda mbali zaidi kudai hakuna listi ya watakao vuliwa magamba. Kumbuka huyu ndiye mtendaji mkuu wa shughuli za kila siku za chama na sekretariat nzima.
Bila shaka hakuna anachofanya Kikwete bila Rostam, Chenge na Lowassa kujua. Hawa watu wameshiriki kwa karibu sana na Kikwete na kufanikisha CCM-Mtandao Kushika dola. Haikuwa rahisi watu hawa kutengana kirahisi kama wengi tulivyotaka iwe. William ningeweza kukuandikia PM ila nimeona wacha na wanaJF wengine walione na watachangia. CCM na Magamba ilikuwa ni sanaa, kama ambavyo mwenyekiti wenu amekuwa akicheza na jukwaa kufurahisha hadhira. Alianza na semina elekezi Ngurudoto, kwa top govt officials, tunajua kashfa za ngono zilizofanyika kule 2006. Juzi katembelea wizara na kuamsha utendaji wa kazi, sasa amekuja na semina elekezi Dodoma, anarudia yale yale, kwenye formal logic hali inaitwa Tautology, hakuna tija wasiofanya kazi awapige chini, ngonjera zake zina gharama sana kwa wapiga kura. Nina wasi wasi CCM itagawanyka mikononi mwake na Muungano na Zanzibar utavunjika kabla ya 2015.
Kaka ningekushauri ufunge hilo tawi njoo tuungane kwa mambo yenye maslahi kwa taifa! Tuwe watanzania na si waCCM. Taifa lije mbele kama watanzania shida za umeme zinatokana na ufisadi zinatupata wote.
Ilikuwa niandike mengi wacha niwahi mazishi kuna kada wa CCM amekufa hapa mtaani
Respect
Mdogo wako Mch Masa