- Mkuu mimi ni member tu kama wengine hapa, lakini sio siri kwamba I have access kwa watawala wa vyama vyote vya siasa, kwamba ninaweza kutatua tatizo lolote hapana, lakini ninaweza kuwafikishia wanaohusika malalamiko. HOWEVER Mama Makinda alipopewa u-Spika nilisema hivi, amepewa kwa ridhaa ya Ikulu, meaning kwamba kwa uwezo wangu wa kusoma siasa, kuna mabadiliko makubwa yanakuja on mafisadi maana huyo sio chaguo lao,
- Matokeo yakawa mafisadi kuondolewa NEC na CC na sasa wako njiani kuondolewa kabisa CCM, ninasema hivi wanaondoka very soon kama hawajaambiwa tayari ni kwamba wataondolewa tu ndio maana wameshaombwa kuingia upinzani na kuna wakati walitishia kuanzisha chama chao, sasa wakati wao ni huu wakaanzishe chama chao maana wataondolewa very soon. So mkuu tunajidiliana na kupena moyo pia kwamba pole pole tutafika!
William @ NYC, USA.
mbona iko dhahiri kwamba mama Makinda ni chaguo la Mafisadi?
Pili nakuomba kaka mshauri mbunge wetu wa same mashariki akumbuke zile barabara zetu kwani Tangia uhuru tunaahidiwa tu zitajengwa kama ngonjera. Kuna ile ya mkomazi- kihurio- ndungu- kisiwani- same. Na kuna ya ndungu- mamba miamba- bwambo- saweni. Na bwambo suji-makanya. nyingine Mamba miamba-gonja- mbaga.
Najua sio rahisi kujenga zote kwa wakati mmoja ila bila hizi barabara maendeleo mitaa hiyo itakuwa ngumu. Nimeandika kwa sababu umesema una access na watawala na viongozi wote wapinzani na CCM. Mpelekee huu ujumbe anayehusika. mwambie kile kiwanda cha iliki ni usanii wa uchaguzi sasa afanye kazi uchaguzi umekwisha. Na mwambie Same imeshika mkia kwenye elimu kwenye ubunge wake. Same ilikuwa ndio kioo cha elimu TZ. Mwambie ni vigumu sana kuvuvuzela na kazi. Wananchi wanataka maendeleo walao kitu kimoja kwa mwaka wa fedha. utaifa mbele siasa nyuma.
Utaifa ukiwa kweli mbele tutaendelea, ila kuna njia panda ya utaifa na uzalendo pale ufunguo wa hazina akikabidhiwa mtu. Ndio maana wengi tunataka katiba mpya itakayotoa maelekezo ya kufikishana segerea kirahisi bila ubaguzi.
Swala la Jina la mwisho au majina ya wakubwa sio dhambi kuwa nayo tatizo kuna wakati watu wali abuse jamii kwa majina hayo, yalikuwa ndio yanaonekana ni watu zaidi ya wengine, jitihada zilikuwa hazihesabiwi kaka. Mfano mpaka leo kijana mwenzetu hajatuambia amepataje ubilionea kirahisi ili nasi tufanye. Hakuna shida kina Nape, na Makamba kupewa vyeo kama wamevifanyia kazi ila ukweli unajulikana ni mbereko ya chuma.
Naona unamategemeo sana na vijana hawa ila ukumbuke kuwa Chenge, Lowassa, Y Makamba, JK, Yona Nk nao walikuwa vijana siku moja tena walianzia umoja wa vijana wa wakati huo. Walipohamia serikalini kwa kofia ya CCM matokeo yake tunayaona.
Lazima chama kilichopo madarakani kikubali kuwa mfumo wa utawala umeshindwa, tunahitaji utawala wa sheria na katiba ifuatwe tena katiba ya wananchi. Matatizo yapo serikali ambapo huko hakuna kuwajibika, uzembe, ufisadi na matumizi mabovu ya mali za taifa. huko ndiko kwenye ngozi za kuchunwa. Mwenyekiti wa CCM analijua hilo ila hataki kufanya kazi. Swala la kufikiri uvuvuzela wa Nape utawapa nafuu CCM sidhani.
Kelele za wananchi ni huduma bora na maisha walioahidiwa hayatokei. Mfano halamshauri ya Ndesa-pesa ndio halmashauri bora kwa sasa usafi, mipango mijini nk. CCM wao wanapita kuuza sura eti kisa mmemwondoa Makamba mkamwingiza makamba. Kwani hizo sura za akina Nape zinawasha Umeme, zinaleta maji au zina jenga barabara? CCM ni wajibu wao kujibu mashambulizi kiutendaji badala ya kivuvuvzela?
Niatawashangaa sana CDM wakiwa madarakani, wananchi wakapiga kelele ufisadi ufisadi, uzembe , rushwa na tip za hao wanapewa na wananchi eti wakaanzisha uvuvuzela wa kutetea mambo yaliyo wazi. Nategemea CDM itamwajibisha mzembe, fisadi, mla rushwa, na mtu yeyote atakayesaidia kuingiza nchi hasara. hiyo ni kazi ya mtawala, sio kutoa ahadi kila asubuhi, ooh tumewafukuza wakati wapo. ooh ngoja muone lini? ooh mafisadi hawapo tena come on !!