Kwako Kaka William Malecela

Kwako Kaka William Malecela

- Well, Mkuu sana Masa heshima yako na ahsante sana kwa ujumbe wako, naomba kusema hivi:-

1. CCM ni chama kikubwa sana kuliko Mukama na Nape, waliowavua ujumbe wa NEC na CC mafisadi sio Mukama na Nape, isipokuwa ni chama cha CCM collectivelly.

2. Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye ndiye Rais wa Jamhuri kwa sasa, ndiye mtendaji mkuu wa chama CCM na amesema wazi kabisa kwamba maneno ya Nape ni yake pia, kwenye siasa za taifa hapo ndio mwanzo na mwisho, hakuna mwingine tena hata awe Mukama, Mwenyekiti ndio; FULL STOP WA YOTE!

3. CCM kujivua magamba, ninaliamini kwa 100% kwanza tayari lilishaanza na sasa ni process tu kwenye kusomga mbele na kujivua na ni kwa speed ya CCM sio ya Chadema au anybody else! na kama kweli Rais wa sasa haamui maamuzi bila hao mapacha, basi wangekuwa bado wapo CC na NEC, na kama kweli Lowassa ana nguvu kama inavyosemekana basi angekua Makamu wa Mwenyekiti wa CCM Taifa, siku aliponyimwa hivyo nafasi ukienda kuanglia records humu JF utaona nilisema wazi kwamba ulikuwa ndio mwisho wake politically, sasa jiulize nani aliymenyima hiyo nafasi?

4. Kuhusu Tawi, kwa kweli kama nilivyoahidi nipo mbioni kulifungua very soon bado some very few touches ninazipitia kabla halijasimama, na mimi binafsi sina nia ya kuongoza tawi hilo, nitaliongoza kwa muda tu kuelekea kusimama na kuwaachia wengine maana in the wake ya habari za ushiriki wangu hapa JF last two weeks, nimeongezekewa sana na shughuli ambazo sasa zinaanza hata kunizidi kimo kwa sababu watu wanahitaji sana msaada wa mawazo! So!

- Mwisho naomba kutoa ushauri wangu wa bure hapa JF, kwamba wakati umefika kwa baadhi yetu kujitoa nje to the public ili mfahamike na muweze kutumika kulisaidia taifa letu changa, maana hapa kuna watu kama wewe na wengine wengi ambao wana mawazo makubwa sana, lakini wenye shida hawawezi kukutafuta na hili jina, I mean ni ushauri wa bure tu!


William @ NYC, USA.
Hatuwezi kukulaumu.CCM ndio iliyokufikisha hapo.Wakati ikikupatia mkate na siagi wenzio ilituacha tule ugali na upupu.Nafikiri pia hujui kama kwetu upupu umekuwa mboga.
Kaka najua kwa hii "political inbreeding" ya tanzania upo kwenye warithi wa ufalme hivyo huwezi kuupinga utawala mbovu wa CCM.
"SIKIO LA KUFA HALISIKII DAWA" bado kitambo kidogo hizo ndoto za ufalme tutazitowesha.
 

- Binafsi ninasema bado CCM tunahitaji Mwenyekiti wa chama kuwa ndiye mgombea u-Rais wa Jamhuri, bado hatujawa strong enough kusimama kikatiba ya chama chetu, maana unaweza kufanya hivyo only tu kama uko strong kikatiba ya chama, miaka 50 bado ni michache sana, wenzetu huku wana miaka 300 na kitu sasa ndio maana wanaweza ku-afford mwenyekiti wa chama kutokua Rais.

- Again, CCM is bigger that Rais wa sasa na anybody, sasa hatuwezi kutenganisha kofias just because of Rais wa sasa, kama Salim is that good angekua amechaguliwa na wananchi kushika nafasi hiyo, I mean hoja zingine sometimes you wonder kama kweli wanaozitoa wanaitakia mema CCM.

William @ NYC, USA.
Kaka naona kamchango kananukia uoga wa style fulani kwa mbali,kwa yeyote mwenye mapenzi ya dhati kwa ccm hawezi kupigia chapuo mfumo huu anamizi wa m/kit kuwa mgombea wa urair hasa inapotokea una kuwa na mtu bogus kwenye nafasi hiyo kama ilivyo sasa.Mtu ambaye si competent ndipo inapowalazimu kutumia mbinu chafu,rafu zisizo za lazima ili mradi jamaa aukwae urais..Na hili la chama cha ccm kuwa ni kikubwa unattumia vigezo vipi.Kaka tafakarii chukua mapema ccm is a dying party,unaparade uhai wa kitu ambacho wenzako nd'o wanakiteremsha k kaburini kukizika .Kweli maajabu hayataisha chinini za jua.
 
Nashukuru sana Mchungaji! Bado nasubiri majibu ya Wlliam; Mchungaji kutokana na majibu yako unadhani kijana aliyekulia ndani ya CCM na ambaye uovu na magamba unayoyasema ndio yaliyomkuza, kumsomesha, na kumlea anaweza kushindwa kufa na haya Magamba?Kumbuka kuwa tofauti na wewe na mimi tunaokula kula vumbi hapa na kusubiri mgao wa Umeme William kupitia Magamba ya CCM uenda hakawa toka kuzaliwa hajawai hata kula mihogo! (sahamani sana Wliliam Naomba husichukulie kuwa nakuongea wewe so direct, ila nakutumia kama jukwaa kufika ujumbe)[/SIZE]

Inbreeding within CCM has ruined the thinking capacity. Family politics - Nepotism is an honor within Chama Cha Magamba- "Mwenzetu" na "CCM ina wenyewe" You need grassroot before you can practice active politics, William is in favor of that. Mazee you need family connections, CCM watalithishana madaraka hili liko very evident, Kama tulivyokwisha ona Makamba, Kikwete, Nnauye, Msuya, Mwinyi, Mzindakaya, Pinda, Simba, Kitwana Kondo, Kighoma Malima, Ndejembi..... endless list....ongezea hapo
 
Kinachoiponza CCM (hususani makada wao, kama huyu) ni kudhani kuwa wanaweza kuwadhihaki watanzania siku zote na mahali popote!

Matatizo ya CCM na ya watanzania hayataweza kutatuliwa kwa kufungua matawi ughaibuni. CCM wanapaswa kujua consumers wake wanataka nini? Consumers (watanzania) hawataki watawi yaongezeke, kwani yanaongeza vichaka tu! Wanataka Mti utoe matunda! Wanataka maji ya uhakika na salama, Umeme, foleni zipungue, bidhaa na huduma mbalimbali zipatikane kwa unafuu na ziwafikie wananchi wengi, hasa wa vijijini.

Wananchi wanataka wanaohujumu mali ya taifa wachukuliwe hatua! CCM inawabembeleza... C'mon, tuwe serious japo kidogo!!
 
Kaka William Malecela

Bila shaka uko salama na unaendelea na majukumu ya kila siku ya kimaisha. Nimeona leo nikuandikie waraka wa kirafiki kuhusiana na hali ya kisiasa na maisha yetu huku Tanzania. Nilikusoma siku chache zilizopita ukifahamisha umma jitihada zako za kuanzisha tawi la CCM huko uliko. Wengi walikupongeza na wengine kama kawaida walikubeza na kwenda mbali zaidi. Nakumbuka kwenye lile bandiko uliweka kauli mbiu ya kuvua magamba na CCM mpya. Nadhani Kaka Wiliam unajua sasa zile zilikuwa ni sanaa tu, Mukama na Nape wamekuwa wakitofautiana na muafaka na nani na lini hatua zitachukuliwa zidi ya wale waliokiweka chama chenu hapo kilipo. Mukama alienda mbali zaidi kudai hakuna listi ya watakao vuliwa magamba. Kumbuka huyu ndiye mtendaji mkuu wa shughuli za kila siku za chama na sekretariat nzima.

Bila shaka hakuna anachofanya Kikwete bila Rostam, Chenge na Lowassa kujua. Hawa watu wameshiriki kwa karibu sana na Kikwete na kufanikisha CCM-Mtandao Kushika dola. Haikuwa rahisi watu hawa kutengana kirahisi kama wengi tulivyotaka iwe. William ningeweza kukuandikia PM ila nimeona wacha na wanaJF wengine walione na watachangia. CCM na Magamba ilikuwa ni sanaa, kama ambavyo mwenyekiti wenu amekuwa akicheza na jukwaa kufurahisha hadhira. Alianza na semina elekezi Ngurudoto, kwa top govt officials, tunajua kashfa za ngono zilizofanyika kule 2006. Juzi katembelea wizara na kuamsha utendaji wa kazi, sasa amekuja na semina elekezi Dodoma, anarudia yale yale, kwenye formal logic hali inaitwa Tautology, hakuna tija wasiofanya kazi awapige chini, ngonjera zake zina gharama sana kwa wapiga kura. Nina wasi wasi CCM itagawanyka mikononi mwake na Muungano na Zanzibar utavunjika kabla ya 2015.

Kaka ningekushauri ufunge hilo tawi njoo tuungane kwa mambo yenye maslahi kwa taifa! Tuwe watanzania na si waCCM. Taifa lije mbele kama watanzania shida za umeme zinatokana na ufisadi zinatupata wote.

Ilikuwa niandike mengi wacha niwahi mazishi kuna kada wa CCM amekufa hapa mtaani

Respect

Mdogo wako Mch Masa

Mchungaji ushauri mzuri sana, ila unataka aende chama gani? na kwa nini? au apiganie maslahi kwa njia gani??
 
Mchungaji ushauri mzuri sana, ila unataka aende chama gani? na kwa nini? au apiganie maslahi kwa njia gani??

Kamanda!

Nataka asiweCCM awe Mtanzania apiganie Maslahi bila kuweka mbele CCM.
 
Asante Rev Masa kwa ujumbe wako kwa Ndg yetu Billy..............

.............wachangiaji wote wa hii mada tuko pamoja sana........kuna kitu nimeki-observe kwenye hii mada.....naendelea kuangalia for any consistency.......
 
- Well, Nape amesema mafisadi wataondolewa CCM, Nape ni my loongtime friend tunatoka mbaali sana na huu mchezo wa siasa and I trust him kwa sababu at one time in 2005 mimi na yeye we were offered big rewards kama tungejiunga na kundi flani la siasa tukakataa kwa kauli moja, nimeongea naye na ninamuamini 100%, kama sio hivyo Nape asingekubali kuchukua hii nafasi ya CCM!

- Mtatizo ya umasikini yapo hata huku ndugu yangu, ndio maana mimi ninajali sana tunakokwenda sio tulikotoka!


William @ NYC, USA.

Na wewe unamsimamo mmoja na nape juu ya wachagga? maana naona mna fikra moja!
 
Bwana WM usikate tamaa na hizo porojo. CCM sasa imepata makamanda wa kupambana na kelele za Dr. Slaa. Hawa watu walizoea wao kupiga makombora na akina Makamba kutulia, siku hizi tz mambo mswano, Dr. Slaa akitoa kashfa kuhusu ufisadi wa CCM, Nape anajibu na vielelezo wa UFISADI wa Dr. Slaa.

Nape alisema ccm haichezi ngoma ya chadema kumbe ni muongo anaicheza kama unavyotuthibitishia katika red
 
Bwana WM usikate tamaa na hizo porojo. CCM sasa imepata makamanda wa kupambana na kelele za Dr. Slaa. Hawa watu walizoea wao kupiga makombora na akina Makamba kutulia, siku hizi tz mambo mswano, Dr. Slaa akitoa kashfa kuhusu ufisadi wa CCM, Nape anajibu na vielelezo wa UFISADI wa Dr. Slaa.

Nape alisema ccm haichezi ngoma ya chadema kumbe ni muongo anaicheza kama unavyotuthibitishia katika red

- Thread mpya karibu 100 za Nape JF, anayecheza ngoma ya mwenziwe ni nani hapa?


FMEs!
 
Huyu William ni matunda ya taxpayers wa Tanzania tangu tupewe UHURU.
Dada zake 3 wana nafasi nzuri serikalini kutokana na sifa za baba,sio utendaji mzuri,HII NI FACT.

Angalia yule wa NIMR,Mahakama na yule wa UN hapo New York.

Kwa hiyi huyu William atatetea status quo mpaka siku ya kufa.


 
Huyu William ni matunda ya taxpayers wa Tanzania tangu tupewe UHURU.
Dada zake 3 wana nafasi nzuri serikalini kutokana na sifa za baba,sio utendaji mzuri,HII NI FACT.

Angalia yule wa NIMR,Mahakama na yule wa UN hapo New York.

Kwa hiyi huyu William atatetea status quo mpaka siku ya kufa.



- Nje ya hoja ya msingi, Wa-Tanzania wote tumesoma bure under Mwalimu, hawakusomeshwa watoto wa viongozi tu, isipokuwa kila mwananchi, Ulaya kuna wananchi wengi wa Tanzania sio watoto wa viongozi tu, Chadema in watoto na ndugu wengi wa viongozi wao infact mpaka wake zao pia, so stick to the ishu at hand badala ya kujaribu kubadili topic bila hoja za msingi!

- Unasema Mh. Mbowe kuwa Mwenyekiti wa Chadema ni kusimamia status quo ya baba mkwe wake, au Marehemu Baba yake aliyekuwa kuwa kiongozi wa TANU?


FMEs!
 
- Nje ya hoja ya msingi, Wa-Tanzania wote tumesoma bure under Mwalimu, hawakusomeshwa watoto wa viongozi tu, isipokuwa kila mwananchi, Ulaya kuna wananchi wengi wa Tanzania sio watoto wa viongozi tu, Chadema in watoto na ndugu wengi wa viongozi wao infact mpaka wake zao pia, so stick to the ishu at hand badala ya kujaribu kubadili topic bila hoja za msingi!

- Unasema Mh. Mbowe kuwa Mwenyekiti wa Chadema ni kusimamia status quo ya baba mkwe wake, au Marehemu Baba yake aliyekuwa kuwa kiongozi wa TANU?


FMEs!


Hii ni idiocy toka kwako.Mbowe simjui binafsi,kama unasema MTEI aliwalazimisha watu wa HAI kumpeleka bungeni ,that is insane.
Mbowe ni jina linalojitegemea,umefika CLUB BILICANAS?
Wala sidhani anaweza kutumia hela za kifisadi toka kwa WAHINDI kuingia bungeni!!!!!

Nilikuwa na respond propaganda za William ambaye yuko huko New YORK akila matunda ya TANU/CCM.
Nikasema kuwa dada zake 3 ,wapo kwenye nafasi nyeti kutokana na BABA YAO.Simple that.
Kulinganisha Freeman na Malecela sisters ,you are out of common sense
 
Hii ni idiocy toka kwako.Mbowe simjui binafsi,kama unasema MTEI aliwalazimisha watu wa HAI kumpeleka bungeni ,that is insane.
Mbowe ni jina linalojitegemea,umefika CLUB BILICANAS?
Wala sidhani anaweza kutumia hela za kifisadi toka kwa WAHINDI kuingia bungeni!!!!!

Nilikuwa na respond propaganda za William ambaye yuko huko New YORK akila matunda ya TANU/CCM.

Nikasema kuwa dada zake 3 ,wapo kwenye nafasi nyeti kutokana na BABA YAO.Simple that.
Kulinganisha Freeman na Malecela sisters ,you are out of common sense

- Idiocy ni kuongelea vitu usivyovijua na kudai ni ukweli, Mh. Mbowe ni mtoto wa muasisi wa TANU na pia ni Mkwe wa Muasisi wa Chadema, kwa hiyo kama unaongelea status quo ungeanza na huko upande wa pili kwanza.

- Nimefanya kazi ya ubaharia kwa muda mrefu sana kabla sijaamua kuhamia New york, na kulala nje na kwenye magari na kusota sana pale Port Authority, mpaka kuwa na maisha niliyonayo sasa if that is matunda ya TANU na CCM then uko sawa sawa mkuu, ila in the future uliza kwanza kabla ya kukurupuka, I mean ungeweza kuniuliza kwenye inbox kuhusu maisha yangu badala ya ku-assume tu na kukurupuka!


William @ NYC, USA.
 
- Idiocy ni kuongelea vitu usivyovijua na kudai ni ukweli, Mh. Mbowe ni mtoto wa muasisi wa TANU na pia ni Mkwe wa Muasisi wa Chadema, kwa hiyo kama unaongelea status quo ungeanza na huko upande wa pili kwanza.

- Nimefanya kazi ya ubaharia kwa muda mrefu sana kabla sijaamua kuhamia New york, na kulala nje na kwenye magari na kusota sana pale Port Authority, mpaka kuwa na maisha niliyonayo sasa if that is matunda ya TANU na CCM then uko sawa sawa mkuu, ila in the future uliza kwanza kabla ya kukurupuka, I mean ungeweza kuniuliza kwenye inbox kuhusu maisha yangu badala ya ku-assume tu na kukurupuka!

William @ NYC, USA.
hapo kwenye nyeusisiwezi kupinga hata kidogo
 
- Idiocy ni kuongelea vitu usivyovijua na kudai ni ukweli, Mh. Mbowe ni mtoto wa muasisi wa TANU na pia ni Mkwe wa Muasisi wa Chadema, kwa hiyo kama unaongelea status quo ungeanza na huko upande wa pili kwanza.

- Nimefanya kazi ya ubaharia kwa muda mrefu sana kabla sijaamua kuhamia New york, na kulala nje na kwenye magari na kusota sana pale Port Authority, mpaka kuwa na maisha niliyonayo sasa if that is matunda ya TANU na CCM then uko sawa sawa mkuu, ila in the future uliza kwanza kabla ya kukurupuka, I mean ungeweza kuniuliza kwenye inbox kuhusu maisha yangu badala ya ku-assume tu na kukurupuka!


William @ NYC, USA.

Wewe una umri gani naona unapigia sdebe chama kinachoelekea kaburini.
Nadhani unafikiri wtanzania wanakula burgar kama wewe kuwa wanamuda wa kufikiri ili hali hata mlo mmoja ni shida kwa sasa.
Kama hujawahi kufikiri kijana wa tingatinga la Magamba, basi ccm iliachiwa Ben. Ila Akakiuka mashariti. Mchonga alimkataa mkwele na baba yako live! Halafu leo hii eti ndo mwenyekiti wa chama?
Piga ua garagaza ni lazima kimfie mikononi mwake hana ujanja maana kila dalili zipo na hakuna wa kukiokoa maana hayupo anayeweza kuyafuata masharti ya mchonga.
Tunakupa muda utatuambia kama hiki chama kitabaki by 2015 na pengine hata kabla ya hapo.

Kumbuka Mchonga alikuwa mtakatifu hakuna kitu alichokisema kikashindwa kuwa!
Alimchana EL live mkajifanya kichwa nguvu mkampa uPM mlionaalifika wapi!

Hamana namana ya kuizuia chadema tena maana ilikwisha tabiriwa na Mchonga ndiyo mbadala wa ccm! Jiandaeni na mazishi tu ya chama chenu maana ndo mnachoweza kufanya kwa sasa!
Mungu ibariki Tanzania, Mungu tupiganie dhidi ya hawa madharimu wanaotunyonya kwa muda mrefu sasa!
 
Wewe una umri gani naona unapigia sdebe chama kinachoelekea kaburini.
Nadhani unafikiri wtanzania wanakula burgar kama wewe kuwa wanamuda wa kufikiri ili hali hata mlo mmoja ni shida kwa sasa.
Kama hujawahi kufikiri kijana wa tingatinga la Magamba, basi ccm iliachiwa Ben. Ila Akakiuka mashariti. Mchonga alimkataa mkwele na baba yako live! Halafu leo hii eti ndo mwenyekiti wa chama?
Piga ua garagaza ni lazima kimfie mikononi mwake hana ujanja maana kila dalili zipo na hakuna wa kukiokoa maana hayupo anayeweza kuyafuata masharti ya mchonga.
Tunakupa muda utatuambia kama hiki chama kitabaki by 2015 na pengine hata kabla ya hapo.

Kumbuka Mchonga alikuwa mtakatifu hakuna kitu alichokisema kikashindwa kuwa!

Alimchana EL live mkajifanya kichwa nguvu mkampa uPM mlionaalifika wapi!

Hamana namana ya kuizuia chadema tena maana ilikwisha tabiriwa na Mchonga ndiyo mbadala wa ccm! Jiandaeni na mazishi tu ya chama chenu maana ndo mnachoweza kufanya kwa sasa!
Mungu ibariki Tanzania, Mungu tupiganie dhidi ya hawa madharimu wanaotunyonya kwa muda mrefu sasa!

- Haya ni maoni yako tu na ni haki yako kuwa nayo, ila elewa kwamba USA ni nchi imara kutokana na msingi uongozi imara walioachiwa na wa Rais wa kwanza George Washington, vipi sisi na uongozi wetu ni msingi tuliowekewa na nani?

- Kwamba Chadema itaiondoa CCM madarakani na hawa kina Marando, it is another wishfull thinking ninachojua ni kwamba Chadema walimuomba Slaa agombee urais ili awaongezee wabunge, lakini sio kwa sababu waliamini anaweza kushinda urais, CCM sio siri ilikuwa imelala sana, lakini sio sasa tena!

- Ninakula nini na Wa-Tanzania wanakula nini sijui kama ni ishu, ishu ni jinsi tunavyozitumia haki zetu za kikatiba wka manufaa ya taifa letu, na si kweli kwamba ni lazima uwe na mawazo ya ki-Chadema Chadema basi ndio unakuwa mzalendo, that is PATHETIC thinking!

William @ NYC, USA.
 
Kaka William Malecela

Bila shaka uko salama na unaendelea na majukumu ya kila siku ya kimaisha. Nimeona leo nikuandikie waraka wa kirafiki kuhusiana na hali ya kisiasa na maisha yetu huku Tanzania. Nilikusoma siku chache zilizopita ukifahamisha umma jitihada zako za kuanzisha tawi la CCM huko uliko. Wengi walikupongeza na wengine kama kawaida walikubeza na kwenda mbali zaidi. Nakumbuka kwenye lile bandiko uliweka kauli mbiu ya kuvua magamba na CCM mpya. Nadhani Kaka Wiliam unajua sasa zile zilikuwa ni sanaa tu, Mukama na Nape wamekuwa wakitofautiana na muafaka na nani na lini hatua zitachukuliwa zidi ya wale waliokiweka chama chenu hapo kilipo. Mukama alienda mbali zaidi kudai hakuna listi ya watakao vuliwa magamba. Kumbuka huyu ndiye mtendaji mkuu wa shughuli za kila siku za chama na sekretariat nzima.

Bila shaka hakuna anachofanya Kikwete bila Rostam, Chenge na Lowassa kujua. Hawa watu wameshiriki kwa karibu sana na Kikwete na kufanikisha CCM-Mtandao Kushika dola. Haikuwa rahisi watu hawa kutengana kirahisi kama wengi tulivyotaka iwe. William ningeweza kukuandikia PM ila nimeona wacha na wanaJF wengine walione na watachangia. CCM na Magamba ilikuwa ni sanaa, kama ambavyo mwenyekiti wenu amekuwa akicheza na jukwaa kufurahisha hadhira. Alianza na semina elekezi Ngurudoto, kwa top govt officials, tunajua kashfa za ngono zilizofanyika kule 2006. Juzi katembelea wizara na kuamsha utendaji wa kazi, sasa amekuja na semina elekezi Dodoma, anarudia yale yale, kwenye formal logic hali inaitwa Tautology, hakuna tija wasiofanya kazi awapige chini, ngonjera zake zina gharama sana kwa wapiga kura. Nina wasi wasi CCM itagawanyka mikononi mwake na Muungano na Zanzibar utavunjika kabla ya 2015.

Kaka ningekushauri ufunge hilo tawi njoo tuungane kwa mambo yenye maslahi kwa taifa! Tuwe watanzania na si waCCM. Taifa lije mbele kama watanzania shida za umeme zinatokana na ufisadi zinatupata wote.

Ilikuwa niandike mengi wacha niwahi mazishi kuna kada wa CCM amekufa hapa mtaani

Respect

Mdogo wako Mch Masa

Safi Reverend. Kaka William anajua sana unachomwambia isipokuwa anaogopa kugeuka asije muua mzee Sigwimisi kwa presha
 

- Haya ni maoni yako tu na ni haki yako kuwa nayo, ila elewa kwamba USA ni nchi imara kutokana na msingi uongozi imara walioachiwa na wa Rais wa kwanza George Washington, vipi sisi na uongozi wetu ni msingi tuliowekewa na nani?

- Kwamba Chadema itaiondoa CCM madarakani na hawa kina Marando, it is another wishfull thinking ninachojua ni kwamba Chadema walimuomba Slaa agombee urais ili awaongezee wabunge, lakini sio kwa sababu waliamini anaweza kushinda urais, CCM sio siri ilikuwa imelala sana, lakini sio sasa tena!

- Ninakula nini na Wa-Tanzania wanakula nini sijui kama ni ishu, ishu ni jinsi tunavyozitumia haki zetu za kikatiba wka manufaa ya taifa letu, na si kweli kwamba ni lazima uwe na mawazo ya ki-Chadema Chadema basi ndio unakuwa mzalendo, that is PATHETIC thinking!

William @ NYC, USA.

Mkuu labda kuna kitu kimoja kinakupita kidogo, pamoja na kuwa una upeo mzuri sana wa kuchanganuwa mambo, nadhani hizi ni athari za kushiriki siasa kimtandao zaidi kuliko phissically, na hata unapokuja nchini nadhani unakosa muda wa kutosha wa kupima na kujiridhisha ni kiasi gani Watanzania wamekata tamaa ya maisha.

Swala hapa sio CHADEMA, na yeyote anaedhani CHADEMA ndio mpinzani wa CCM basi anajidanganya yeye mwenyewe kwa makusudi au kwa kutokujuwa, Wananchi sasa hivi wanaangalia ni nani atakaewaunganisha kuelekea nchi ya kanani, maana ndani ya miaka 50 ya utawala wa CCM wameshindwa hilo. haiingi akilini kwa nchi tajili kama Tanzania wananchi wake wawe maskini wa viwango hivi, na kama Mkuu William unajidanganya kwamba CCM ina nafasi zaidi ya kuendelea kuongoza nchi nakupa pole sana labda kusiwe na katiba mpya Tanzania na tume huru ya uchaguzi. vijana wote ambao walikuwa hawana sifa za kupiga kura mwaka 2000 mwaka 2015 wote watapiga kura na ni hao ndio wengi siku hizi wapo kwenye vijiwe huku nyumbani tunavihita maarufu kama MAKEMPU.

Ili ni kundi kubwa la vijana wa dot com ambalo halina hajila na wanapenda maisha ya kisasa, na hawa huwezi kuwadanganya kwamba CCM ndio iliyokulea, hawa wote wanajuwa kwamba CCM ni chama cha mafisadi, na mtaji wa ccm ni vizee vichovu ambavyo vinaendelea kufa kwa kasi kubwa kutokana na maisha duni, kwa hiyo mtaji muhimu wa ccm unabaki kwa wanawake wa nyumbani walioishia darasa la nne na la saba, kwa mtaji huu ccm is out of power, kama kutakuwa na free n fair election.

Changamoto:
nakupa changamoto kama kweli unadhani ccm ipo tena mioyoni mwa watanzania, katika wapiga kura wenye sifa 20,000,000 ni kwa nini ccm ipate kura 5,000,000!? na je zaidi ya wapiga kura 10,000,000 hawakuonekana kwenye kupiga kura je wako wapi watu hawa? je unaweza kunipa final results kutoka NEC for 2010 General election? CCM iko madarakani kwa ridhaa ya vyombo vya dola na sio Wananchi.
Mimi binafsi kati ya kifo na ccm , mimi nachaguwa kifo.
 
Back
Top Bottom