Mchele mchele na mazaga zaga mengine kibao sijui raba mtoni khaaa....Sie pia gari ilikuwepo ila mnaomba Dingi asiwe na safari zake vinginevyo ndio kuanza kutafuta usafiri lakini ulikuwa haukosekani maana mtaani ilitokea bahati watu wa rika moja tulikuwa tele basi ni kiasi cha kuambiana tu leo tunazuka wapi na usafiri wa uhakika uliandaliwa. Mie viwanja pia nilikuwa navipenda ila vingine vilikuwa havikongi kiu yangu ya muziki kuliko hiki kiwanja kimoja ambacho nikitoka pale nafurahia leo nimejirusha kwa raha zangu. Halafu hiki kiwanja wadada walikuwa hawakipendi sana wakidai wahuni wengi na vyangu doa pia, lakini muziki wake kama umefuata muziki tu ulikuwa bomba sana basi mie na wenzangu wawili tuliweza kuwashawishi wadada mpaka wakakubali kile kiwanja ndio pakawa HQ yetu ya kujirusha.