Umeona! Adui wa mwanamke no.1 ni mwanamke mwenyewe. Nimefuatilia comments zote kwenye hii thread ila naona hili hawalifikirii. Focus zaidi imekuwa kwa mwanamme. Mwanaume hana ujanja bila ya mwanamke kukubali. Ingekuwa vizuri hili jambo waliangalie katika angles zote kwa maana ya roles ya mwanamke na mwanaume katika uchepukaji. Kwasababu wameegemea upande mmoja itakuwa ngumu kupata majibu ya maswali yao.
Pili hapa inaonekana kama wanaume ndo wachepukaji ingawa uzoefu unaonyesha hili tatizo nalo liko upande wa KE. Na wanaume wanalalamika kama wao wanavyolalamika.
Jambo la kuwashauri wanawake bila kuwa biased ni kwamba kuchepuka kwa mwanaume kunaweza kuwa na vyanzo viwili. Moja ni sababu inayotokana na mke na nyingine ni ya mwanaume mwenyewe kutokana na kushindwa kudhibiti matamanio.
Nikianza na sababu zinazotokana na mwanamke, wanawake wanapokuwa wameolewa hujisahau na kuona wamefika. Yale yote waliyokuwa nayo kabla ya ndoa hutoweka na kuona mume walishampata hawana haja ya kumuhangaikia. Hapa tatizo ndo linapoanzia. Wengine utakuta wanashindwa majukumu yao kwa mume na wakijaribu kurekebishwa huwa mbogo na wakati mwingine kumwabia mume ndo nilivyo. Hawawezi kufanya hata kazi ndogo ndogo za nyumbani na kutaka kila kitu wafanyiwe na wasichana wa kazu. Mwingine kama anafanya kazi atataka kuwa sawa na mwanaume na kutaka ku-dictate mambo ya nyumbani bila kujua kwamba hilo kwa mwanaume ni issue zaidi ya wanawake wengi wanavyofikiri. Wanawake wengine wanataka kuishi maisha ya kuigiza wanayoyaina kwenye tamthilia , n.k. Haya yote na mengine taratibu huanza kumfanya mwanaume kukuchoka. Na baadae atatafuta mbadala wako.
Pili wanaume by nature ni wadhaifu na mwanaume anapenda kwa kuona tofauti ilivyo kwa nwanamke ambaye yuko kihisia zaidi. Hii inaelezwa na jinsi mwanamke anavotumia muda mwingi zaidi ili kuleta mvuto kwa jinsia ya ME. Hiyo ni asili na huwezi izuia.
Wanaume wengine wana nguvu nyingi za kiume na mwanamke mmoja anaweza asimridhishe. Hili likichagiwa na mavazi ya siku hizi ya wanawake nalo limechangia sana kuamsha hisia za wanaume walio wengi.
La kufanya ni mwanamke kufanya sehemu yako kikamilifu ingawa bado hiyo haitamzuia mwanamke kuchepuka. Unaweza kuwa na strategy ya kupunguza uwezekano wa kupunguza vishawishi vya mwanaume kama vile kuwa naye sehemu ambazo si salama kwa ndoa yako. Hata hivyo mengine itabidi kumuachia muumba maana siyo rahisi kumdhibiti mwanaume kwa 100%.
Sasa hili nalo wanaume wanatofautiana jinsi ya kujizuia.
Sent using
Jamii Forums mobile app