jchofachogenda
JF-Expert Member
- Jan 8, 2012
- 537
- 123
Jamani wana Azania wenzangu naomba tujikumbushe kipindi kile tukiwa shuleni.Nakumbuka kipindi hicho ukifaulu kwenda Azania unaheshimika mtaa mzima.Ndio shule pekee ya serikali iliyokuwa na wanafunzi wa kiume pekee katika mkoa wa Dar es salaam.Si mnakumbuka nickname yetu ya shule ya Azaboys?Tulikuwa tunajiita wagumu hivyo masholi wa Jangwani sekondari hatukuwafagilia.Tulikuwa tunawasumbua sana walimu wetu kwa kukimbia masomo ya darasani na kwenda tuition.Je unamkumbuka yule mwalimu wa nidhamu aitwae Mchwampaka?Unamkumbuka mkuu wetu wa shule aitwae Andrew kwayu?Naomba mnikumbushe mengine wana AZABOYS.