Kwa mliooa wanawake waliowazidi umri

Kwa mliooa wanawake waliowazidi umri

Mwanume usione mwanamke mnaelingana au aliekuzidi uri... Kibaiolojia wanawake wanakua haraka kuliko wanaume... Ata kuzeeka iko hivyo hivyo... Ata mwanamke akijitunzaje!!! Baada ya miaka kadhaa ataonekana mzee kuliko wewe. Ndo mwanzo wa kuona aibu kutembea nae yanaanza!!
Inabidi mzidiane angalau miaka mingapi??
 
Kuoa ni makubaliano au hiyari sasa kama ameoa umri mkubwa au mdogo ameafiki huyo me/ke na macho anayo anaona
 
Mbona mnazidi kunkatisha tamaa asee mara hivi mara vile sasa yupi ndo wa kuoa daah ngoja ntafute wa kunzalia tu
Wakuoa ni yule ulo mpenda naye akakupenda kwa mapenzi ya dhati na mkawa mnaendana tabia na malengo.Hizo ndio sifa za muhimu.ukimpenda mtu hata maswala ya umri hutayafikiria
 
Kwa mtizamo wangu kuna "perfect age for mates"...inatakiwa Mwanaume awe na kati ya miaka 3-5 zaidi ya mwanamke.

Ikiwa zaidi ya hapo itafika wakati mwanaume utakua unaona kama unaishi na mdogo wako (unamlea).

Ikiwa chini ya hapo, kuna tatizo ya "superiority complex" kwa pande zote mbili. Hata kama kuna vitu mnatofautiana basi mmoja wapo kati yenu atachukulia kwamba anauwezo zaidi yako. Kitu kigumu katika mahusiano ni kujiona wote sawa na kitu kimoja.

Kuna "factors" zingine wazungu wanaita "outliers"...kuna watu wana maarifa na busara(akili ya maisha) zaidi ya wastani wa miaka yao. Mfano mwanamke au mwanaume mwenye miaka 20 lakini akili yake inao uwezo sawa na mtu wa miaka 30. Hii inatengeneza matabaka ya watu wa rika lao kwasababu wanawaona kwa kiasi fulani wana akili za kitoto. Wengi wao hupendelea kutembea na wapenzi walio wazidi umri.

Ni vigumu kutumia kigezo cha umri kwa matakwa ya ndoa (unless for biological reasons)

Mahusiano (ndoa) ni suala la kisaikolojia zaidi kuliko baiolojia, mira na desturi zimeweka miiko na mifumo ambayo inafunga watu ambao sio wa kawaida (average people)...

Ikiwa unahitaji mahusiano na ndoa yenye mafanikio ni vigumu lakini inawezekana (inahitajika bahati pia). Umri sio kigezo kuna "physiology" pia, mchunguze mwenzio kama ana chembechembe za "dwarfism" au "giantism". Ingawa katika hayo mawili kuna mapungufu yanayo jitokeza, "early boomers" na "late boomers" ambapo huchangiwa sana na vyakula mnavyotumia kila siku.

"Ego and honesty" hichi ni kigezo kikubwa katika mahusiano kuliko vyote, kama mtaweza kutengeneza mshababiano mzuri basi mtafika mbali.
 
Ndoa ni kama nguo za wadada kila mtu na yake kulingana na alivyo. We angalia ipi itakukaa vizuri na kukupendeza
 
Kama utakuwa vizuri kiuchumi, halafu ukaoa mwanamke aliyekuzidi umri kati ya miaka 5 mpaka 10, utafurahia sana ndoa yako. Hawa huwa wanakufanya kujisikia wewe mfalme.
Angalizo: ukikaa Naye kwa muda mrefu, hutoweza tena kuwa na mwanamke uliyemzidi umri, Kwani hatowezo kukufanyia yale mwanamke aliyekuzidi umri aliyokuwa akikufanyia.
 
Wanawake wana mature haraka kuliko wanaume, ndio maana mwanamke mwenye miaka 18 anaweza ishi na mwanaume wa miaka 40 but not the opposite.
 
juzi nimeachana nae aisee maana huwa ni ma hitler kila kitu anataka akuongoze achana nao mkuu..tena ukikuta anakuzidi mawe utahenya
Tatizo umeoa mtu mzima halafu unafanya utoto. Akikukemea unamwona mbabe, hirler nk. Ukioa mtu mzima fanya ya kiutu uzima tu.
 
Mimi napenda mwanamke aliyenizidi umri
Hii ni kweli kabisa
Kuna tatizo wakuu
 
Mwanume usione mwanamke mnaelingana au aliekuzidi uri... Kibaiolojia wanawake wanakua haraka kuliko wanaume... Ata kuzeeka iko hivyo hivyo... Ata mwanamke akijitunzaje!!! Baada ya miaka kadhaa ataonekana mzee kuliko wewe. Ndo mwanzo wa kuona aibu kutembea nae yanaanza!!
Mimi ndo nawapenda walionizidi umri yani wanajielewa sana
 
Back
Top Bottom