Kutoka Dodoma!

Kutoka Dodoma!

Mkuu heshima mbele, marekebisho kidogo, si unajua zamani nilikuwa DJ yaani mzee wa mic na kukwaruza santuri, hii ngoma originally ilipigwa na Sam Mangwana, with a guest star Franco Makiadi.

Mzee FMES,
Huu wimbo ni kwamba walitunga wote yaani Franco na Sam Mangwana na kuja kuuimba wote. Ikumbukwe kuwa huyu mzee alikuwa ni KISIMA cha wasanii. Wengi walipitia kwake kama akina Mayaula, Mangwana, nk.
 
Acha hizo bro, wewe kwenu ni Bukoba sio Bariadi, daganya wajinga sio wote hapa ni wajinga mkuu, kama tunazo za taifa itakuwa zako? Wewe endelea kujidanganya tu mkuu, hapa wengine sisi ni watu wazima tumeona mengi sana makubwa ya kwako ni madogo madogo sana kijana!

kinachokusumbua ni wivu wa kitoto, ulikuja kichwa kichwa saa umenasa, tena nilkuonya mapema hukutaka kusikia kuwa nitakuwekea kitanzi utajivika mwenyewe, mambo ya kurukia watu usiowajua unaona sasa mtu mzima aibuu!
 
Mkuu FMES

Hakuna sababu ya kujibizana na mahayawani; ati alikuwa anatafuta kiti, ......kwani aliambiwa atakuwa spika wa bunge au ilikuwa ni lazima aende usiku? Hawa mabaradhuli lazima wasafishwe. JK ni lazima achague Watanzania au MAFISADI. Tumekwisha ona mwelekeo wake kwa Sinclair et al. Aliwadanganya wadanganyika 2005 sio sasa wala haitakuja tokea tena hawa wana CCM kufanya watakalo. The buck stops kwenye ukweli na JF ukweli utawekwa tu no matter what.

FMES endelea kumkoma nyani hadi giladi maana hivyo vilima tumekwisha anza kuviona na vizingiti vilivyokuwa njiani vinafyekwa ki-roho mbaya kuanzia EL, Chenge, Mramba ..........
 
Kashikwaje pabaya!mmeshaambiwa kilikuwa kinatafutwa kiti!Hapa dawa ni kuachana na haya mambo na kuendelea kuchapa kazi!haya wewe evidence zako zipo wapi?zaidi ya maneno?

Kama kilikuwa kiinatafutwa kiti, kikao cha NEC wameamua hivyo, then Chiligati anasubiri uchunguzi wa polisi wa nini? Mbona hutmii akili kwa ishu ndogo sana hii?
 
Mkuu hollo heshima mbele,
Ukweli upi wakati maswali haya hatujajibiwa?

Hivi wabunge viti bungeni wanajitafutia wao wenyewe nafasi ipo wapi wakae au wanawekewa na watumishi wa bunge?
2. Kama wanajitafutia wenyewe sasa hayo majina kwenye viti yalitoka wapi?kiasi jamaa awe anaangalia jina lake?
3. Na kama kulikuwa na majina kumbe iliwezekana kabisa kuoneshwa kiti chake wakati ule ule rasmi wa kuingia bungeni
4. Kwa mtizamo reasonable kabisa hata mie nikienda pale bungeni leo sitatafuta kiti najua nitaoneshwa tu na makarani wa bunge sembuse mtu aliyekuwa waziri na inajulikana kabisa anarudi kuwa back bencher?
5. Kwa taarifa zilizopo ule ukumbi wa bunge una idadi ya viti kubwa kuliko wabunge waliopo,je kulikuwa na haja ya kutafuta kiti mapema?
6. kwani bunge wakati linaanza ile siku ya kwanza alikaa wapi?mpaka atafute kwa kukaa awamu ya pili ambako kungesomwa bajeti?au hata kama alikuwepo kwanini atafute kiti siku ambayo sio official kwa wabunge kuingia kwenye debate hall?
7. Kwa spika ama naibu spika nako ni back bencher?mbona alishawapta hata mawaziri au alitaka kuongoza bunge siku hiyo?
Maswali haya na mengine mengi yanazua circumstantial evidence kuwa huenda basi amehusika,na kwa wale waliosoma sheria ya ushahidi najua wamo wana sheria humu,kuna vitu kama res gestae kwenye ushahidi na pia section 3-20 ya sheria ya ushahidiTanzania ambapo kuna mambo ya ushahidi wa kusikia au kudhani yanaruhusiwa ili mradi yawe supported na other set of facts(yaani corroborated) hivi hamuoni kama chenge anatia shaka?
Jamani hivi kweli muda unaotumika kumdiscuss chenge inapatikana faida gani?zaidi ya maneno tu?kwanza hata katika vyombo vya habari iliandikwa vinavyohisiwa hivyo kulikuwa hakuna prouvement yoyote!Dawa ni kuforget abt that na kumove forward!
 
Tuambie kwa nini ni uongo? ukweli ni upi brother?... mimi hadi page ya 26 sijauona... zaidi ya mahisia kibao...
Habari ambazo zinashabihiana ni muhusika kwenye source zote mbili ni huyo huyo!!! Ambacho hatukijui ni Kumwagwa kwa unga au Kuonyeshwa kiti cha kukaa!!!
Sasa mkuu wewe unayejua ukweli tuambie...

Kasheshe,
Siku ukija kufiwa na mazishi yawe kesho yake, naomba ikifika USIKU WA saa NANE, basi uende makaburini na uanze kukagua wapi kesho utachimba kaburi. Kesho yake nafikiri utapata SIFA nyingi sana kutoka kwa MAJIRANI na ndugu na jamaa kuwa wewe kweli TAIMU IZI MANEY (Time is Cents..).
Nafikiri kuna wengine hawajasikia maneno ya KOLIMBA kuwa "Ukuta wa Berlin jamani umebaki kwenye Muzeum na sehemu za makumbusho kama SONY CENTRUM-Berlin".
 
Kama kilikuwa kiinatafutwa kiti, kikao cha NEC wameamua hivyo, then Chiligati anasubiri uchunguzi wa polisi wa nini? Mbona hutmii akili kwa ishu ndogo sana hii?
Polisi ni lazima isubiliwe kwa sababu ilishirikishwa!ila habari ndo hiyo Chenge is innocent!
 
Another stupid Idiot suggest that we wait for the Police and Takukuru whatever you call it ..........................................what the hell do you think? We are not in Zimbabwe where the police is the law.
 
mkitaka kutuzuga tuzugeni, lakini mkituzuga hakikisheni tunazugukika..

Baada ya Chenge kujiuzulu si alirudi alikokuwa anakaa mwanzoni kabla ya kuteuliwa Waziri? Kwani alipoingia Bungeni kabla ya kuwa Waziri alikuwa anakaa wapi mwanzo? si hapo aliporudi baada ya kujiuzulu? Ushahidi si huu hapa:

karamagi004.jpg


Sasa hiki kiti kingine anakitafuta kwa minajili gani wakati kiti chake alichokuwa nacho mwanzo (kabla ya kuwa Waziri) na ambacho alikirudia baada ya kuondoa bado kipo?

Nawashauri waje na kisingizio kingine. Please, jitihadini kidogo katika kuzuga basi...
 
Hollo,
Mkuu vipi tena yamekukuta yapi?..
Hiki ni kijiwe ambacho tunazungumzia maswala kama haya ya kina Chenge, hatujengi nyumba hapa sasa unaposema tu move on to move wapi?.. tuache kujadili msomi wetu ambaye kagubikwa na imani za kichawi?...
Wewe mtu mzima lini mtu akahama kiti wakati hakuna wabunge wengine ndani? na kama alikuwa akihama mbona hakukaa humo hadi wengine wajiunge naye maanake unapohama kiti unahakikisha watu wengine wasije kichukua..
Kisha basi hili swala la kuhama kiti linafanywa kila siku ya bunge inapokuwa tupu iweje leo huyu mkuu wamzushie yeye ktk kitendo ambacho ni cha kawaida unless kayafanya haya wakati usuokuwa wa kawaida na kapitia viti vingi akichagua sijui ama alitafuta kizuri zaidi kuwa karibu na Mwakyembe..
sasa labda tuseme hivi:- Chenge aliombwa na mhudumu wa Bunge kumsaidia kuweka majina ya watu ktk viti hivyo ndio maana alionekana akipita kila kiti!...lakini kabla bunge halijaanza waliamua tena kuyatoa majina hayo...
Nadhani hii itajibu maswali yote ya wananchi...
Mwambie naomba kuwa wakili wake! kwi kwi kwi!
 
Kikao cha Bunge la April Chenge alikuwa Bungeni kama Mbunge wa kawaida, je, alikaa kiti gani? Au Bunge la June ni maalum sana kiasi kwamba alikuwa anahitaji kukaa kwenye kiti kingine maalum?

Baraza la Mawaziri lilipovunjwa hatukuona mawaziri wakienda kuchagua seat za kukaa nyakati za usiku. Zoezi la kuchagua seat lilifanyika asubuhi walipoingia Bungeni na kuna wengine tuliwaona wakienda kukaa kwenye seat zao za uwaziri. Chenge siyo waziri wa kwanza kuachia ngazi, wapo wengine ambao waliachia ngazi na wakaenda kujichanganya kwa wabunge wengine, hatukushuhidia Lowassa, Karamaji na Msabaha wakienda kuchagua seat za kukaa usiku ama kwenye kiza. Hivi Chenge ana u-special gani ambao unamfanya ajichagulie seat na tena kwa kusindikizwa na Afisa wa Bunge na siyo wahudumu.

Kama kweli alifika mpaka kwenye seat ya Speaker, je, huko nako alienda kuchagua seat ya kukaa?

Sidhani kama Speaker ama Katibu wa Bunge wanaweza kuwa hawana akili/mambumbu kiasi cha kulifanya hili swala la Chenge liwe kubwa mpaka lifike mikononi mwa polisi na UWT. Kabla ya kulipeleka huko lazima walijiridhisha kwamba ni swala kubwa na liko nje ya uwezo wao na ndiyo maana waliamua kulisogeza kwenye vyombo vya usalama. Ina maana wakati wanapeleka hicho kideo polisi hawakuwa wamefanya uchunguzi wao wa awali ili kujiridhisha kwamba mtuhumiwa alikuwa anachagua seat ya kukaa? Mbona Chiligati anataka kulidhalilisha Bunge na Spika wake? Kibaya zaidi Katibu wa Bunge na wasaidizi wake wote wanasheria na Spika nae ni mwanasheria, sina hakika kama wangeweza kukurupuka na kulipeleka swala la mtu kuchagua seat mpaka lifike polisi na UWT. Hapa naona Chiligati ana lake jambo na kama Six na Katibu wa Bunge watakubaliana na maelezo hayo huo ndiyo utakuwa mwanzo wa kudharaulika kwa Bunge kama Taasisi na wao wenyewe kwamba huwa wanakurupuka kwenye kufanya maamuzi yao.

Mzee Chiligati naona anataka kuua soo na kupooza mambo maana ni aibu kubwa sana kwa CCM iwapo itathibitika kwamba Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya CCM (Mzee wa Vijisenti) amekumbwa na kashfa ya vijisenti, akalazimika kujiuzulu na kabla upepo haujatulia amejikuta kwenye kashfa nyingine ya kuzungukia seat za wabunge na Spika na tena nyakati ambazo wabunge wengine wote hawapo ukumbini. Ni aibu kwa CCM kwa kuwa jamaa ni mjumbe wa CC na NEC na alishinda kwa kishindo kwenye uchaguzi uliopita.

Maelezo ya mwanzo walisema alisahau kitu, sasa nadhani kideo kimewaonyesha kwamba alizunguka sana na wakabadilisha maelezo kwamba alikuwa anachagua seat ya kukaa. Hoja ya kusahau kitu ukumbini imeonekana haina mashiko na haiwezi kufunika aibu ya Mzee wa Vijisenti. Kweli mwaka wa balaa ni balaa tu! Mwaka huu ni mwaka wa mafisadi kuumbuka na watakuwa wanaumbuka mmoja baada ya mwingine.
 
Acha hizo bro, wewe kwenu ni Bukoba sio Bariadi, daganya wajinga sio wote hapa ni wajinga mkuu, kama tunazo za taifa itakuwa zako? Wewe endelea kujidanganya tu mkuu, hapa wengine sisi ni watu wazima tumeona mengi sana makubwa ya kwako ni madogo madogo sana kijana!

kinachokusumbua ni wivu wa kitoto, ulikuja kichwa kichwa saa umenasa, tena nilkuonya mapema hukutaka kusikia kuwa nitakuwekea kitanzi utajivika mwenyewe, mambo ya kurukia watu usiowajua unaona sasa mtu mzima aibuu!
Nimeamini kumbe za hata za taifa huzifahamu!wewe mimi hunifahamu usijidai unanifahamu!Give me a break!acha kubwabwaja hapa!habari bila data bila evidence imekufa!hiyo siyo scientific research!Fanyenyi kazi watanzania ili Taifa letu liende mbele!Maneno hayatatusaidia
 
mkitaka kutuzuga tuzugeni, lakini mkituzuga hakikisheni tunazugukika..

Baada ya Chenge kujiuzulu si alirudi alikokuwa anakaa mwanzoni kabla ya kuteuliwa Waziri? Kwani alipoingia Bungeni kabla ya kuwa Waziri alikuwa anakaa wapi mwanzo? si hapo aliporudi baada ya kujiuzulu? Ushahidi si huu hapa:

karamagi004.jpg


Sasa hiki kiti kingine anakitafuta kwa minajili gani wakati kiti chake alichokuwa nacho mwanzo (kabla ya kuwa Waziri) na ambacho alikirudia baada ya kuondoa bado kipo?

Nawashauri waje na kisingizio kingine. Please, jitihadini kidogo katika kuzuga basi...

Kwani mbunge hana haki ya kuhama sehemu aliyokuwa dhamani na kutafutiwa sehemu nyingine?ama kweli JK ana kazi
 
Hollo,
Mkuu vipi tena yamekukuta yapi?..
Hiki ni kijiwe ambacho tunazungumzia maswala kama haya ya kina Chenge, hatujengi nyumba hapa sasa unaposema tu move on to move wapi?.. tuache kujadili msomi wetu ambaye kagubikwa na imani za kichawi?...
Wewe mtu mzima lini mtu akahama kiti wakati hakuna wabunge wengine ndani? na kama alikuwa akihama mbona hakukaa humo hadi wengine wajiunge naye maanake unapohama kiti unahakikisha watu wengine wasije kichukua..
Kisha basi hili swala la kuhama kiti linafanywa kila siku ya bunge inapokuwa tupu iweje leo huyu mkuu wamzushie yeye ktk kitendo ambacho ni cha kawaida unless kayafanya haya wakati usuokuwa wa kawaida na kapitia viti vingi akichagua sijui ama alitafuta kizuri zaidi kuwa karibu na Mwakyembe..
sasa labda tuseme hivi:- Chenge aliombwa na mhudumu wa Bunge kumsaidia kuweka majina ya watu ktk viti hivyo ndio maana alionekana akipita kila kiti!...lakini kabla bunge halijaanza waliamua tena kuyatoa majina hayo...
Nadhani hii itajibu maswali yote ya wananchi...
Mwambie naomba kuwa wakili wake! kwi kwi kwi!


Mkandala wewe kata issue wacha kubishana na huyo .kwanza angalia madai yake then upime kama unataka kupoteza muda wako .Kata issue tuendelee atajifunza mbele ya safari .Watu huja hapa wakidhani n Darhotwire na chat za ajabu ajabu .Hapa ni Varisty bwana kuwa mwandishi wa mambo ya maana means akili yako inachoma kweli na inakamata Channels kibao .Vingenevyo utaishia kulia lia tu hapa .
 
Mzee FMES,
Huu wimbo ni kwamba walitunga wote yaani Franco na Sam Mangwana na kuja kuuimba wote. Ikumbukwe kuwa huyu mzee alikuwa ni KISIMA cha wasanii. Wengi walipitia kwake kama akina Mayaula, Mangwana, nk.

Mkuu vipi mbona husikii, hivi sijawahi kuesma mimi nilikuwepo huko Kinshasa, hebu ngoja nikupe darasa kijana maana sio kwenye siasa tu hata kwenye muziki nitakuumiza tu:-

1. Le Grande Franco Lwambo Lwanzo Makiadi Mandefu na Mandefu, ndio lililokuwa jina lake kamili,

2. Wapigaji wote wakubwa wa Congo Kinshasha, iliyokuja kuwa Zaire, karibu wote walitoka kwenye bendi ya Franco, yaani TP. Ok Jazz, isipokuwa tu Dr. Nico na kina John Bokeloo Isenge.

3. Sam Mangwana, ni mmoja wa waimbaji wa zamani wa Lwambo, enzi hizo alikuwa pamoja na Madilu, Simaroo, Josky Kiambukuta, Tabu Ley na kina Mayaula Mayoni, na hawa wote alikuja nao pale uwanja wa taifa in the 70s kasoro Tabu Ley ambaye tayari alikuwa na bendi yake kule Zaire.

4. Sam Mwangwana, alipotoka na hata akiwa peke yake, hakuwahi kuifikia level ya kimuziki ya Lwambo, maana Lwambo was too big kwenda chini kuimba waimbo kwa kushirikiana na Sam Mangwana, wenzetu wa-
Zaire au watu wa nchi za Francophone, huwa hwana tabia kama zetu za bongo za kujchanganya bila kujali Class, wao hujali Class, sasa kimuziki na kimaisha Sam Mnagwana, was too low of the Class kwa level za huko Zaire,

Kilichotokea ni kwamba Sam Mangwana, alikuwa ameenda Zimbabwe kwa muda mrefu, akawa amechacha sana, akarudi Kinshasa na kumuomba Verkyis Kimamangwana Wazela Mbongo Mateta, aliyekuwa then anamiliki bendi za Orch. Kamale, Orch. Lipwa Lipwa, Orch. Kiam, na Orch. Veve, kuwa amsaidie ili wapige naye album moja tu ili apate kuinuka tena, mkulu Verkyis akamkataa kabisa kuwa haweezi shusha jina lake kwa kupiga na Sam Mangwana.

Ndipo Sam Mwangwana, akatuma wapambe wakamuombeee kwa Lwambo, maana singeweza hata kwenda mwenyewe nyumbani kwa Lwambo, ndio Lwambo alipoambiwa akakubali tena kwa masharti kuwa Sam Mangwana atunge wimbo mmoja tu sio album nzima, amletee Lwambo ili auone na kumsaidia kupiga solo guitar na kuimba naye, which he did sasa njaa ya Sam Mangwana, akautengenezea album nzima na kusema kuwa ametunga na kuimba na Lwambo, lakini wimbo alioshiriki Lwambo ni mmoja tu, ambao kwa kilingala unasema hivi

"...balobaki eeeh biloba loba to lembi eee! lokuti yo kufa ye na ndokise moko moko, kusema sema walisema tumechoka, muwongo na mulosi ni watu wa kuchoma..."

Haya maneno mazito, Sam Mangwana, alkuwa anajaribu ku-get back to Verkyis aliyemkatalia kushirki naye au kumsaidia. Lakini kwamba alitunga Lwambo, hapana maana ingekuwa basi ile album ingejaa nyimbo zote akiwa Lwambo, badala yake ni huo wimbo mmoja tu!

Ahsante Mkuu
 
Quote:- Mwanakijiji

Sasa hiki kiti kingine anakitafuta kwa minajili gani wakati kiti chake alichokuwa nacho mwanzo (kabla ya kuwa Waziri) na ambacho alikirudia baada ya kuondoa bado kipo?

Nawashauri waje na kisingizio kingine. Please, jitihadini kidogo katika kuzuga basi...

Quote:- Hollo

Nimeamini kumbe za hata za taifa huzifahamu!wewe mimi hunifahamu usijidai unanifahamu!Give me a break!acha kubwabwaja hapa!habari bila data bila evidence imekufa!hiyo siyo scientific research!Fanyenyi kazi watanzania ili Taifa letu liende mbele!Maneno hayatatusaidia

Unajua ni aibu mtu mzima kuanza kuelimishwa upya kama mtoto mdogo!
 
Kwani mbunge hana haki ya kuhama sehemu aliyokuwa dhamani na kutafutiwa sehemu nyingine?ama kweli JK ana kazi

inabidi ufikiri kidogo...

Kila mbunge ana sehemu yake ya kukaa... kuna wabunge 320... kila mbunge anajua sehemu yake ya kukaa. Kukaa kwenye Bunge siyo kama kupanda daladala kwamba unajichagulia nafasi tu. Spika anapokaa mbelee akitaka kumuuliza mzee Malecela anajua pa kuangalia, akimtafuta Slaa anajua pa kuangalia kwa sababu jinsi wanavyokaa hawabadiliki kwa karibu miaka yao mitano.

Sasa mbunge akitaka kutafuta mahali pa kukaa hatafuta wanapokaa wengine (duh); tukikubali kuwa anaweza kufanya hivyo ina maana Chenge angeweza kwenda anapokaa Zitto na kumuambia "bwana mdogo nimekipenda kiti hiki move" halafu Katibu wa Bunge anabadilisha jina? Halafu Zitto na yeye anatoka anakiona kiti cha Lowassa na kumuambia "mzee nimekipenda kiti chako move"... na Lowassa.... to infinitum!

Kama Mbunge anatafuta mahali pa kukaa ni kutoa taarifa kwa uongozi wa Bunge na wanamuoambia nafasi zilizo wazi..SIYO zinazokaliwa na Wabunge wengine!!

Ukifikiria hili ndio utaona nadharia nzima kuwa alikuwa anatafuta mahali pa kukaa kwa kuangaliwa WANAKOKAA wabunge wengine haina msingi, ya kitoto, na inayokaribiana na ujinga (kama siyo ujinga).

Anayeaamini kuwa Chenge alikuwa anatafuta mahali pa kukaa kwa kuangalia wanakokaa wabunge wengine basi na yeye karogwa!
 
FMES,
Mkuu nakumbuka Sam Mangwana alikuja jiunga na kundi moja wapo kati ya Kamalee au LipwaLipwa yakiwa chini ya himaya ya Verkys..
 
Mkuu Mtanzania,
dawa ni kuwakamata na kuwalazimisha wao na familia zao walipie risasi za kuwatwanga mbele ya public, tena ikiwezekana pale Sanamu Monument, yes piga risasi tu,

Mkuu kwanza nakupongeza kwa kazi nzuri sana ya kutuhabarisha kwa yanayojiri mjini Dom ,hususani nyeti za kikao cha NEC.Kwa kweli tangu ulipoanza kututonya nyeti hizo, kila mara nimekuwa na shauku kubwa ya kufuatilia kwa karibu sana upekuzi wako huo.Kazi nzuri sana mkuu!

Hatahivyo,nimeshtushwa sana na pendekezo lako la namna ya kuwashughulikia hawa wahujumu uchumi.Ni kweli, hawa watu wanakera na wanatia hasira mno.Lakini kama tukichukua mapendekezo yako ya kuwatwanga risasi, tena hadharani,duuuuh!Mkuu nadhani hapo umeenda mabali sana.Najua una jazba mkuu, lakini nadhani adhabu hiyo inakiuka haki za binadamu.Kumbuka hata adhamu ya kifo inapigiwa upatu ifutwe kabisa duniani kote.

Naunga mkono kabisa haja ya kuwafilisi mali zao zote wao na wale wote walionufaika na hujuma zao pindi ikithibitishwa na vyombo husika kuwa ni kweli wana hatia. Nakubaliana nawe pia kwa dhati kabisa kwamba CCM ina wanachama wengi tu walio ndani ya bunge na nje ya bunge wenye nia na dhamira ya dhati kabisa ya kuwatumikia watanzania kwa uaminifu wa hali ya juu kabisa.Kwa hiyo sio sahihi kupoteza imani na CCM kama chama.Ni bahati mbaya sana kuwa wanaccm wachache waliobahatika kupewa dhamana ya kuwatumikia wananchi wakageuka kuwa mbwa mwitu wanataka kuwatafuna kondoo.Lakini tunashukuru Mungu kwamba safari yao sasa imeiva.Tuwape muda na kuwaunga mkono viongozi na wanaccm waliosafi wawasafishe wale wanaccm waliokwisha chafuka.

Hii mimi kwangu naona kwamba ndio suluhisho la kweli na linalotekelezeka kwa sasa kutokana na ukweli kwamba CCM dio chama chenye hatamu ya uongozi.Na sina hakika kama hatamu hiyo itatoka mikononi mwa CCM kwa siku za hivi karibuni.

Hivyo, sioni kufikiria kwamba CCM kuondolewe madarakani kama suluhisho linalotekelezeka kwa sasa.Kwa hiyo ni muhimu sana kwa sasa kuwaunga mkono kwa dhati kabisa wanaCCM waliodhamiria kwa dhati kukirejesha chama kwenye falsafa na misingi ya kuundwa kwake, kama chama cha wanyonge wa Tanzania.
Mkuu endelea kutuhabarisha yanayojiri huko Dom.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom