Kutoka Dodoma!

Kutoka Dodoma!

Kwa kuongezea evidence kwenye hoja ya Mwanakijiji kwamba Mbunge akitaka kuhama seat hupeleka ombi kwa uongozi wa Bunge ili apangiwe seat nyingine. Kuna Mbunge alishaomba na ilitangazwa kwenye ukumbi. Mama Anne Kilango-Malecela aliomba kuhama mahali alipokuwa akikaa baada ya Marehemu Amina Chifupa (RIP) kufariki na ilitangazwa kwenye ukumbi na alipewa seat nyingine. Kwa hiyo alichokifanya Chenge sicho kinachofanyika na ndiyo maana nilisema kwamba Spika na Katibu wa Bunge wasingekurupuka kupeleka swala polisi na UWT kama ofisi yao ingekuwa na hizo taarifa za Mzee wa Vijisenti kubadilisha seat.
 
Hatahivyo,nimeshtushwa sana na pendekezo lako la namna ya kuwashughulikia hawa wahujumu uchumi.Ni kweli, hawa watu wanakera na wanatia hasira mno.Lakini kama tukichukua mapendekezo yako ya kuwatwanga risasi, tena hadharani,duuuuh!Mkuu nadhani hapo umeenda mabali sana.

Mkuu najua kuo sasa hivi uko Dodoma, ninasema hivi ukisoma kwa makini historia za Empire nyingi sana za zamani huko Europe, ni kwamba almost siku zote wafalme au viongozi wao wa hizo Empire, walikuwa wako vitani, lakini kuna wakati walikuwa wakishinda vita na kutawala kwa muda wa miaka kama kumi mpaka 30,

Mkuu historia yao iko very clear kuwa wakisha shinda vita, walikuwa na tabia ya kuwapiga risasi au kuwa-eliminate wale wote waliowasaidia katika kushinda vita, kwa sababu inapswa kuwa very clear kwa kiongozi yoyote yule duniani kuwa wasaidizi wa vita, sio watawala, kwa hiyo dawa ni kuachana nao mara tu power ikipatikana, ukisoma kitabu cha Jerry Ralwings, yuko very clear on hilo, walipofanikiwa kupindua nchi tu, basi mshikaji wake wa karibu General Oqnqwipa alikimbia mwenyewe kabla Ralwings hajawakamata washikaji wake wote waliomsaidia na kuwaua kwa risasi, anasema ndio maana aliweza kutawala mpaka alipoamua ku-retire!

Mkuu wangu I am revolutionist wa vitendo sio maneno matupu, Muuungwana alipaswa kuachana na hawa washikaji the minute aliposhinda tu, kwa sababu sasa hivi asipoaangalia wataiushia kumpumzisha yeye, maana sasa wana nguvu nzito sana ya Mkapa nyuma yao!
 
Mkuu nakumbuka Sam Mangwana alikuja jiunga na kundi moja wapo kati ya Kamalee au LipwaLipwa yakiwa chini ya himaya ya Verkys..

Mkuu wangu Bob,

Heshima mbele, najua kuwa unayapata haya alkini hapa umechanganya kidogo mkuu, Sam Mangwana alikuwa akipiga muziki wa bakulutu yaani watu wazima, Orch. Lipwa Lipwa ambayo mwanzoni ilikuwa chini ya Nyiboma Mayidoda ilikuwa inapiga muziki wa Cavasha, yaani wa vijana kwa hiyo Sam Mangwana singeweza ku-fit in,

Baada ya Nyiboma kutoka kuwa kiongozi wa Orch. Lipwa Lipwa, alihamia Orch. Kamale, na kukutana na kina Mulemba na Ricos Kizunga, na Tshimanga Assosa, kule Orch. Lipwa Lipwa ikachukuliwa na kina Mbumbi Malanda, Vata Mombasa, Mongoley, kina Nsayi Nono Nkuka, na kina Benanzooo,

Sam Mangwana, hakuwahi kupiga hizo bendi kwa sababu zilikuwa ni vijana mno kulinganisha na staili ya Sam Mangwana ya kizeee!

Anyways, back to the ishu ya Dodoma, wakuu tukutane kesho wakuu ingawa nitakuwa safarini lakini nitajitahidi nikizipata ku-break in hapa JF na kuhabarishana, ikibidi lakini otherwise labda jioni nitakapokuwa free,

Asante Wakuu!
 
Another stupid Idiot suggest that we wait for the Police and Takukuru whatever you call it ..........................................what the hell do you think? We are not in Zimbabwe where the police is the law.

Mkuu wangu Dua,

Nilikuwa sijaiona hii, yaani nimekufa mbavu na ninaenda kulala sasa! Exactly what we call kumkoma nyani bila kumuangalia usoni, masikini ollo!Hovyooooo!
 
Najuta kwa nini nimeugua jana na juzi naona kama dunia imenipita...lakini nashukuru Mungu am ok nimesoma hizi habari huku mwili ukisisimuka...duuh mambo yanazidi kuwa mabaya.

On bright side, ni kuwa haya mambo yanatokea na tunapata habari...kwanza nashukuru wana JF na mkulu FMES mzee wa madata....zamani, hizi habari zilikuwa hazipatikani, haina maana kuwa hakukuwepo mafisadi au vituko bungeni,bali upevuko ulikuwa kidogo hata ufisadi haukuwa mkubwa hivi.

Chenge,mimi kwa mawazo wangu nafikiria kafanya kitendo hicho kwa sababu ninazofikiria tatu.

(1)Anataka kupotosha wimbi la maswali ya ufisadi...sasa tuna na tutazungumzia uchawi.
(2)Amejenga hofu kwa wabunge wengi sasa...ukiangalia kuwa Chifupa, Balali wamekufa kimaajabu (mtamazo wangu).
(3)Ukiangalia background yake...sheria. Hamuoni kuwa jamaa anajijengea hoja ya kuwa yeye ni insane?.

Chiligati!!!!! jamani hawa mawziri wetu sijui wana matatizo gani yaani ni hawajui kabisa kuongea...kwanza Sofia Simba na sasa huyu Chilli ningeshauri wapewe intensive course ya PR.

Mungu Ibariki TANZANIA,Mungu wazidishie JF nguvu...AMEEN.
 
lho mie niliondoka kw amasaa kama ma nne tu kurudi nimekuta nimepitwa na pages kama 6 sijui 7 nane on this topic...loh!!
yan hawa wachawi wauaji wasijaribu ku spinia topic kirahis i hivii watueleze hata kama alikua anahamishwa seat iweje security camera zilizimwa???it means its something it was pre planned to ka mwanzo!!wasituzingue that easily!!!

wana mpango wa kuua wangapi sasa??wallahi mie nasema hatA Kwenye hivyo vikao wallahi nsingekua nagusana na mtu maana hw far can we be assured kwenye hivyo vikao vya kunyunyuziwa hivyo havijawekwa??if bungeni viliwezwa wekwa!!??
 
This is treason, this is coup d'etat!

Serikali imetekwa nyara, Serikali imepinduliwa, Taifa linaburuzwa!

I can careless if it is Uchawi, P210, Radioactive or whatever mchawi kuchapa nyumba kwa matako, this is serious business kuwa Taifa limetekwa Nyara wakati muhimu ambapo tunapaswa kujadili mipango ya maendeleo na kujiendesha kwa mwaka mpya wa fedha unaoanza July 1 2008.

Waliohusika na kuleta vurugu hizi au kusitisha Ufanyakazi wa Serikali kupitia Bunge, wafunguliwe mashitaka ya Uhaini, kama jinsi Serikali inavyotaka kuwafungulia mashitaka Wabunge wa Pemba ambao waliwasilisha barua ya kutaka Serikali ya Pemba huru kutoka SMZ.

Naungana na Moelex kusema, yanaytokea sasa ni makosa ya Kiongozi Mkuu, Rais wa Nchi, Amiri Jeshi Mkuu na MWenyekiti wa CCM Jakaya Mirisho Kikwete.

Kama Kikwete asingekuwa mdhaifu, mbabaishaji na kukosa ushujaa na ukakamavu kuachana na hili kundi la manyang'au mafisadi maharamia ambao wanaiteka nchi yetu kwa Sheria, Katiba na Rasilimali zetu, tusingefika hapa tulipo ambapo shughuli muhimu za kuendesha Serikali zinagota kutokana na hofu ya uchawi au sumu.

Narudia tena, kilichofanyika ni Uhaini na waliohusika wahukumiwe hukumu ya kifo.

Tumechoka kudhalilishwa na kuburuzwa. Nchi imekuwa ni kituko na tunaacha kujenga Taifa kwa woga wa kijinga ambao nia kubwa ni kuendelea kufunika madhambi ya Watuhumiwa wa Ufisadi.

Lets stone them or burn them as we do the old ladies in Shinyanga, hawa wachawi Wantusu hawaitakii mema nchi yetu. Be it Rostam, Karamagi, Lowassa, Mramba, Mkapa, Meghji, Chenge, Apson or whomever who is behind this nonsense, they should be hanged in public and stoned to death.

Kuendelea kumpa adui shavu la pili kuna kikomo.
 
Mkuu najua kuo sasa hivi uko Dodoma, ninasema hivi ukisoma kwa makini historia za Empire nyingi sana za zamani huko Europe, ni kwamba almost siku zote wafalme au viongozi wao wa hizo Empire, walikuwa wako vitani, lakini kuna wakati walikuwa wakishinda vita na kutawala kwa muda wa miaka kama kumi mpaka 30,

Mkuu historia yao iko very clear kuwa wakisha shinda vita, walikuwa na tabia ya kuwapiga risasi au kuwa-eliminate wale wote waliowasaidia katika kushinda vita, kwa sababu inapswa kuwa very clear kwa kiongozi yoyote yule duniani kuwa wasaidizi wa vita, sio watawala, kwa hiyo dawa ni kuachana nao mara tu power ikipatikana, ukisoma kitabu cha Jerry Ralwings, yuko very clear on hilo, walipofanikiwa kupindua nchi tu, basi mshikaji wake wa karibu General Oqnqwipa alikimbia mwenyewe kabla Ralwings hajawakamata washikaji wake wote waliomsaidia na kuwaua kwa risasi, anasema ndio maana aliweza kutawala mpaka alipoamua ku-retire!

Mkuu wangu I am revolutionist wa vitendo sio maneno matupu, Muuungwana alipaswa kuachana na hawa washikaji the minute aliposhinda tu, kwa sababu sasa hivi asipoaangalia wataiushia kumpumzisha yeye, maana sasa wana nguvu nzito sana ya Mkapa nyuma yao!

Mkuu,kwanza ni kwamba bado sijatua Dodoma.Nimehitimu shahada yangu mwezi uliopita.Kwasasa bado nabeba maboxi kwa muda hapa kwa Mzee Bush nikichanga nauli ya kurudia nyumbani Tanzania.Panapo majariwa ya Mwenyezi Mungu, nitakuwa Dodoma wiki ya kwanza ya mwezi wa nane.

Nafurahi kusikia kwamba wewe ni mwanamapinduzi wa kweli.Kimsingi,hata mimi napenda watu wa aina yako.

Mkuu nimekuelewa juu ya hizo historia.Ni kweli unayoyasema.Likini historia hiyohiyo inathibitisha wazi kuwa sio wote waliowaangamiza wasaidizi wao walikuwa na nia njema ya kufanya hivyo.Wengine walikuwa wakifanya hivyo kwa hofu ya kugeukwa na wale waliowasaidia kushinda vita.Ni hii ilitokea sana kwa wale waliokuwa wakiwafahamu vema nje na ndani na hivyo kuhatarisha uhai wa tawala zao.Umetoa mfano wa huyu rais wa zamani wa Ghana, Jerry Ralwings.Sasa huyu bwana ni mmoja wa hao watawala waliowaua wasaidizi wao kwa hulka zao za kidikteta tu na wala sio kwa nia njema.Nimesoma na waghana wengi sana hapa Marekani.Kwa kweli namna wanavyozungumzia utawala wa kidikteta wa Jerry na idadi ya wanasiasa aliowaua katika kipindi cha utawala wake,hutatamani hata kutumia rejea yoyoye toka kwake.Jerry alikuwa ni mshenzi na myama.Kuna mghana mmoja nimesoma naye darasa moja ambaye mjomba wake alikuwa ni mmoja wa wahanga wa utawala wake.Akikusimulia vitendo viovu vya utawala wa Jerry, utasikitika sana.

Kwa hiyo mkuu ninachotaka kusema ni kwamba, sio watawala wote waliwateketeza wasaidizi wao kama njia bora ya kujiwekea mazingira mazuri ya kutawala.Bali wengine walifanya hivyo kutokana na hulka zao za kifashsti na kutopenda mawazo mbadala.Maana mtu kama Jerry, sio tu kwamba aliwaua wale waliomsaidia tu,bali aliendelea kufanya hivyo katika kipindi chote cha utawala wake kwa wale wote walioonekana kuwa mwiba kwenye utawala wake.Sasa siamnini mkuu kama unaweza kuufagilia utawala wa watu aina ya kina Jerry.

Sasa nikirudi kwa muungwana, kuna mambo ya kuyaangalia kabla ya kumlaumu kuwa kwanini asiwatose waliomsaidia muda mfupi baada ya kushinda.

Jambo la kwanza ni la kibinadamu kabisa.Wahenga walisema "akufaae kwa dhiki ndiye rafiki".Sasa mkuu hili halina ubishi kabisa kwamba,katika hali ya kawaida kwa binadamu mwenye akili timamu,huwezi kuacha kumfikiria kwanza kumkumbuka mtu aliyechangia mafanikoa yako ya aina yoyote ile katika maisha.Sasa hii si hulka ya kibinadamu tu bali ni ya kiMungu pia.Najua wewe ni msomaji wa biblia.Unajua habari ya msamaria mwema,kuwatembelea wafungwa,wagonjwa,na kuwasaidia wenye njaa.Na kuna mahali biblia imezungumza kabisa umuhimu wa kuwasaidia kwanza watu wa nyumbani kwako .Ninachotaka kukazia hapa ni kwamba,suala la kuwakumbuka kwanza waliokusaidia katika mahitaji yako ni la kawaida na la kiungwana zaidi,ukiachilia mbali mifano ya madikteta wachache kama kina Jerry.Na hili lipo mahali pote katika ulimwengu wa siasa.Kwa hiyo muungwana hakufanya jambo jipya.Na tumbuke kuwa sio wote waliomsaidia muungwana ni tatizo katika utawala wake.Wako wanamtandao wengine wanachapa kazi vizuri kabisa bila shaka yoyote.

Sasa ni bahati mbaya sana kwamba,vinara wa mtandao ndio walioharibu.Na bahati mbaya sana kwamba vinara hao wamekuwa watu wa karibu na muungwana kwa kipindi kirefu.Sasa hapa ni pagumu sana kwa kweli.Nasema hivyo kwa kuwa nafahamu fika kuwa kuna mambo ya siri yaliyokuwa yanafanywa na vinara hawa na muungwana alikuwa hajui lolote.Hapa nazungumzia tabia binafsi za vigogo wa mtandao.Mkuu naomba uelewe kuwa wewe unaweza kuwa mtu wangu wa karibu kwa muda mrefu, lakini usijue mambo ninayoyafanya sirini.Kwa hiyo,ninachotaka kusema ni kwamba, si muungwana tu aliyewaamini na kujiridhisha na watu wake.Watanzania wengi tu tuliwaamini makada hawa.Ndio maana kama utakumbuka wakati jina la el linasomwa na spika bungeni kuwa pm,bunge zima lilipuka kwa vifijo(ingawa wengi pia walitegemea hivyo).Zikapigwa kura za kumthibitisha bungeni.Akaungwa mkono wa wabunge wote wakiwemo kina Zito,Slaa na wabunge wa upinzani wengine.Sasa,hii maana yake nini? Maana yake ni kwamba kabla ya zogo la Richmond, hakuna aliyekuwa na shaka yoyote juu maadili ya uongozi ya el na wenzie.

Kwa hiyo mkuu muhimu kwa sasa ni kwa muungwana kuwa makini na watu anaowaamini ili wasimharibie.Ahakikishe anajiridisha sana na watu anaowapa majukumu ya kumsaidia.Najua ameliona hilo na amejipanga vizuri.

Mkuu suala la hawa jamaa kuwa na nguvu kubwa kwa sasa wakisaidiwa na Mkapa,mimi sidhani kama wanaweza tatizo kwa muungwana na CCM kwa ujumla.Mkuu mimi naijua CCM vizuri sana.Kwa mtizamo wa haraka haraka na wa nje,unaweza kudhani nguvu ya hawa watu ni kubwa na yenye athari kwa chama.Lakini nakuhakikishia kwa namna ninavyokijua chama,muungwana wala hawa hofu kwa sababu, kwa muundo na mfumo wa chama, muungwna sasa hivi ndiye mwenye nguvu,rasilimali na uwezo wa kufanya chochote kuliko mtu wala kikundi chochote ndani ya chama na serikali.Hata hao watu wanalijua vema hilo.Ni kweli kwa ujinga wao,wanaweza kutumia pesa na ushawishi mwingine wakafanikiwa kulata vurugu kidogo.Lakini mwisho wa siku wao ndio wataumia zaidi.Ni suala la muungwana kuamua tu.Akiamua wote hao watakufa kisiasa ndani ya dk chache sana.Kwa tunaomjua muungwana sio wa mchezo hata kidogo.Na wao wanalifahamu hilo.Wachokoze wakione cha moto!
 
this is serious business kuwa Taifa limetekwa Nyara wakati muhimu ambapo tunapaswa kujadili mipango ya maendeleo na kujiendesha kwa mwaka mpya wa fedha unaoanza July 1 2008.

Waliohusika na kuletavurugu hizi au kusitisha Ufanyakazi wa Serikali kupitia Bunge, wafunguliwe mashitaka ya Uhaini, .

Naamini kabisa,kwetu weusi uchawi na ngono ni kitu ambacho ni kipaumbele kabisa...sasa nafikiri Muungwana alipokuwa huko U.K. labda alikutana na yule aliyekuwa spin doctor wa Tony Blair...somebody Campbell (nimekumbukia yule mchezaji mahiri wa Portsmouth)na akampa hii spin inayotembea sasa hivi...maanake hakuna mtu anaongelea bajeti...sinclair...kiwira...EPA..nk... hata jf angalia wangapi wako kwenye hii thread.

doc.jpg


Nina wasiwasi kama vituko vinginevyo vilivyotokea bongo na hili litaishia kijiweni hakuna atakayewajibishwa......hiyo ndio bongo.
 
Mr Tom,
Mkuu penigne unaifahamu CCM lakini humfahamu Kikwete! ...
Hivi sasa Kikwete hana ubavu kabisa na analindwa na serikali kama rais lakini chama hakina uwezo wa kukemea mabaya... hakina! kwa sababu wahusika wakubwa ni wale wenye kuendesha chama chenyewe...
Mtu yeyote mwenye ubavu hawezi kuweka suluhisho kati yake na wahalifu yaaania ana shake hands na enemy wake...
Labda useme tu kuwa hawa watu hawawezi kuingamiza CCM kama chama lakini kulingana na mtaji uliopo labda tokee Nabii Mussa mwingine... CCM ipo hatarini sana kupoteza heshima yake kwa wananchi kama KANU. Ni swala la muda tu hivi sasa..
Kwa hiyo rudi nyumbani na hiyo digrii yako ukayaone mambo, kwanza tapelekwa kwenye TV ya kienyeji kisha kesho yake nadhani nawe utapanga safari ya Bagamoyo!... makao makuu ya chama.
 
Mr Tom,
Mkuu penigne unaifahamu CCM lakini humfahamu Kikwete! ...
Hivi sasa Kikwete hana ubavu kabisa na analindwa na serikali kama rais lakini chama hakina uwezo wa kukemea mabaya... hakina! kwa sababu wahusika wakubwa ni wale wenye kuendesha chama chenyewe...
Mtu yeyote mwenye ubavu hawezi kuweka suluhisho kati yake na wahalifu yaaania ana shake hands na enemy wake...
Labda useme tu kuwa hawa watu hawawezi kuingamiza CCM kama chama lakini kulingana na mtaji uliopo labda tokee Nabii Mussa mwingine... CCM ipo hatarini sana kupoteza heshima yake kwa wananchi kama KANU. Ni swala la muda tu hivi sasa..
Kwa hiyo rudi nyumbani na hiyo digrii yako ukayaone mambo, kwanza tapelekwa kwenye TV ya kienyeji kisha kesho yake nadhani nawe utapanga safari ya Bagamoyo!... makao makuu ya chama.

Mkandara, CCM wameshapoteza heshima yao kwa wananchi tangu kashfa mbali mbali zilipoanza kuwaandama watendaji mbali mbali wa chama na serikali. Watanzania wengi tulitegemea viongozi wa serikali ambao ndio hao hao viongozi wa CCM wangechukua hatua madhubuti ili kuonyesha kashfa zilitokea kama EPA, Richmonduli, Kiwira n.k. hazina utetezi ndani ya chama na serikali na wahusika watachukuliwa hatua za kisheria ili kulinda heshima ya chama na serikali, lakini hivyo sivyo ilivyokuwa. Waliohusika na EPA bado wanapeta mtaani, waliohusika na richmond bado wanaitwa waheshimiwa wabunge na wanaingia katika vikao vya NEC na CC. Waliohusika na ununuzi wa rada bado wanajidai na vijisenti vyao. Yote haya yamechangia kwa wananchi kutokuwa na heshima na imani na chama cha mafisadi.
 
Bubu Ataka kusema,
Mkuu labda kunielewa vizuri, ebu nambie ni viongozi gani wa chama unawazunguzia ambao hawamo ktk scandal hizi!...mimi sioni mtu kabisa... hivyo wachukuliwe hatua na nani? nambie hata mtu mmoja mwenye ubavu wa kuwasimamisha hawa jamaa kundi la Mkapa! kama sio wao ndio viongozi wa chama chenyewe. Pinda hana ubavu kichama, Kikwete kakamatiwa kamba, Karume maji yako shingoni na huyo Shein ndio hana hata sauti! NANI kweli anaweza kuwasimamisha watu hawa mahakamani kama sii wao ndio viongozi wa CCM. Unafikiri Mkapa kenda bungeni kwa bahati mbaya?... yupo pale kuona nani ataweza kusimama dhidi yake na kusimama mbele ya macho yake kumkoma nyani yule -Nani atoe hoja inayohusiana na Mkapa..nani! trust me swala la Mkapa limekwisha! alisema kajiuzuru siasa imekuwaje karudi?.... mkuu tazama na soma nyakati! imani na heshima siii issue tena watu wanaogopa..
Tumekwishaaaaa!
 

Watanzania wengi tulitegemea viongozi wa serikali ambao ndio hao hao viongozi wa CCM wangechukua hatua madhubuti ili kuonyesha kashfa zilitokea kama EPA, Richmonduli, Kiwira n.k. hazina utetezi ndani ya chama na serikali na wahusika watachukuliwa hatua za kisheria ili kulinda heshima ya chama na serikali, lakini hivyo sivyo ilivyokuwa.

Waliohusika na EPA bado wanapeta mtaani, waliohusika na richmond bado wanaitwa wameshimiwa wabunge na waingia katika vikao vya NEC na CC. Waliohusika na ununuzi wa rada bado wanajidai na vijisenti vyao.

Nilisema mwanzoni katika post zangu kadhaa kuwa JK alipoingia IKULU alikuwa na nia na ari kubwa sana kubadilisha mambo mengi tu.....Nilimwamini......lakini kusema kweli sasa anasikitisha sana hajui la kufanya amekosa mwelekeo na ni dhoofu sana...nguvu imemwishia, aidha kazidiwa nguvu na wana mtandao au kiti kimemlevya, na nina wasiwasi kama hajaingia basi ataingia katika hili kapu la mafisadi, na haswa hili suala la Sinclair,Tudor ndio limenifanya kusaidia kubadilisha mawazo yangu juu yake.

Yaani Rais wetu,jamani hayo matukio yote hakuna moja nimesikia akilikemea, hata anapotua hotuba zake humwoni akionesha hata ishara. Yeye hubaki akikenua meno na kutoa jokes ambazo kwa maajabu huwa zinamchekesha yeye tu, wala sio kadamnasi ya wanyemsikiliza, kama vile kilakitu ni shwari.....ina maana hasomi,haoni au hasikii kilio cha wananchi?.... Au ni kiburi....alikuja na mikono nyuma tukampa kura.

Hii yote inatokana na CCM, kuwa na vigogo wazito na wana vijisenti kupita kiasi, na nina wasiwasi kama hiki chama kitaishiwa nguvu hapa karibuni, unless vyama vya upinzani wakaamua kuacha ubinafsi(kugombania kiti) na wakafanya uzalendo wa kujiunga pamoja, ili kukiangusha chama hiki kilichojaa na mafisadi wa kunuka. Vinginevyo itakuwa ndoto tu.

Hivi, nauliza haya mamikutano ya CCM inayofanyika kila mara nani anazilipia gharama? na ina gharama kiasi gani?.Maana wanakuwa wana mikutano mingi tu, na hatuyaoni maamuzi yeyote yale.
 
Mwanatanu,
Mkuu nasema hivi Kikwete kashikiwa kamba na hawa jamaa hana ujanja hata kidogo. Akijifurukuta tu wajanja wanaachia kamba anayoning'inia, kenda chini na kuangukia pua.. na huyo Sitta anajua fika kwamba Kikwete akidondoka yeye hana mkate nyumbani...
Mzee wangu Pius Msekwa ndiye nadhani anayewaweka meza moja hadi sasa hivi laa sivyo kumesha kuchwa!... Msekwa mwenyewe naanza kufikiria tofauti nafasi aliyopewa pengine ni katika kuleta suluhu ndani ya chama hicho kwa sababu yupo kote..
 
Bubu Ataka kusema,
Mkuu labda kunielewa vizuri, ebu nambie ni viongozi gani wa chama unawazunguzia ambao hawamo ktk scandal hizi!...mimi sioni mtu kabisa... hivyo wachukuliwe hatua na nani? nambie hata mtu mmoja mwenye ubavu wa kuwasimamisha hawa jamaa kundi la Mkapa! kama sio wao ndio viongozi wa chama chenyewe. Pinda hana ubavu kichama, Kikwete kakamatiwa kamba, Karume maji yako shingoni na huyo Shein ndio hana hata sauti! NANI kweli anaweza kuwasimamisha watu hawa mahakamani kama sii wao ndio viongozi wa CCM. Unafikiri Mkapa kenda bungeni kwa bahati mbaya?... yupo pale kuona nani ataweza kusimama dhidi yake na kusimama mbele ya macho yake kumkoma nyani yule -Nani atoe hoja inayohusiana na Mkapa..nani! trust me swala la Mkapa limekwisha! alisema kajiuzuru siasa imekuwaje karudi?.... mkuu tazama na soma nyakati! imani na heshima siii issue tena watu wanaogopa..
Tumekwishaaaaa!

Tatizo siyo nani mwenye ubavu. Kuna mwenye ubavu zaidi ya Rais wa nchi ambaye vyombo vyote vya dola viko chini yake? CCM kama sikosei kina taratibu zake za kuwaadhibu wale wote ambao wamekiuka taratibu za chama walizojiwekea. Pia serikali ina taratibu zake ambazo wale ambao wamezikiuka kama wahusika wa EPA, Richmonduli n.k. Nyakati gani nizisome? Unapokuwa Mwenyekiti wa chama na Rais wa Jamhuri ya Muungano na vyombo vyote vya dola viko chini yako basi wananchi wako siku zote watategemea umchukulie hatua za kisheria yeyote yule aliyekiuka sheria za nchi na kujipatia utajiri kwa njia za haramu bila kujali alikuwa na wadhifa upi au ana wadhifa gani. Hivyo Watanzania wote ndicho tunachokitegemea toka kwa Rais tuliyemchagua kutuongoza.

Kama huyo Rais tuliyemchagua hawezi kulinda sheria za nchi kwa kuwachukulia hatua za kisheria na hata kuwafilisi wale waliovunja sheria za chama na serikali, basi Rais huyo hatufai Watanzania! Maana si ajabu woga aliokuwa nao ni kwa sababu na yeye anahusika kwa namna moja au nyingine katika kuvunja sheria za nchi na kujipatia utajiri katika njia za haramu. Sheria za nchi zinatakiwa zifuatwe na mkubwa na mdogo, tajiri na maskini na aliye na wadhifa na kapuku. Kama hazifuatwi basi kuna uwezekano wananchi kuanza kuchinjana wenyewe kwa wenyewe maana nchi haina sheria.
 
JF 3 - Kasheshe/Mafisadi 0

Mkuu Field Marshall ES;

Kwi kwi kwi...

Heshima mbele mkuu!!!
Kumbe na mimi niko kwenye kundi hilo la mafisadi... du burudani kweli kweli mkuu!!!
Natamani na mimi ningekuwa na vijisenti... na niwe na uwezo hata wa kununua Bajaji Mkuu!!!

Muda si muda matokeo yatatoka... ubaya ni kwamba penalty mkifungwa mtakataa mtasema referee amewaonea...
 
Mkuu Mtanzania,


dawa ni kuwakamata na kuwalazimisha wao na familia zao walipie risasi za kuwatwanga mbele ya public, tena ikiwezekana pale Sanamu Monument, yes piga risasi tu, kwa sababu look what they are doing to us now? tumeacha kuongelea a strong an big agenda za taifa kama EPA na Kiwira, lakini sasa tunaongelea uchawi na ujinga wa a Harvad man Chenge, yaani the Harvads, kina Obama wanakaribia kuwa marais wa kwanza weusi huko USA, hili lijinga ndoo kwanza linaenda ku-promote uchawi nationally!

Binafsi, sioni siasa ya chama hapa, ninachooona ni taifa kwanza hapa kuna wabunge am,bao wamepania na wako intact, kuna CCM na wa upinzani pia wanashirikiana ingawa kwa siri, kuweka agenda za wananchi kwa manufaa ya taifa, na ninawaombea Mungu awabariki na wafanikiwe!


Naunga mkono na mguu hapa. The Ndesamburo solution. That's what we need here.
 

Yaani Rais wetu,jamani hayo matukio yote hakuna moja nimesikia akilikemea, hata anapotua hotuba zake humwoni akionesha hata ishara. Yeye hubaki akikenua meno na kutoa jokes ambazo kwa maajabu huwa zinamchekesha yeye tu, wala sio kadamnasi ya wanyemsikiliza, kama vile kilakitu ni shwari.....ina maana hasomi,haoni au hasikii kilio cha wananchi?.... Au ni kiburi....alikuja na mikono nyuma tukampa kura.

Bush akijibu swali la Sky News Political editor Adam Boulton's

THE PRESIDENT: Let me say this to you about all this popularity stuff. First of all, popularity is fleeting. And I want it to be said about George W. Bush that when he finished his presidency, he looked in the mirror at a man who did not compromise his core principals for the sake of politics, or the Gallup poll, or the latest, you know, whatever. And you can't lead in this world if you're chasing something as temporary as a popularity poll.

Je inawezekana alimpa shule kidogo Muungwana hapa?

KikweteBush.jpg
 
Back
Top Bottom