Kutoka Bungeni: 2006 - 2010

Kutoka Bungeni: 2006 - 2010

yaani takukuru ina uchafu? hii haingii akilini. Haiwezekani taasisi nyeti kama hii iwe na matatizo ya kupaswa kuchunguzwa. Masilingi hana hoja kwenye hili. Haiwezekani kila taasisi inayotuhumiwa jambo baya basi ianze kujichunguza! Mbuna hajashauri Ikulu ijichunguze? Mbona watu wamesema kuhusu wabunge kugongana na hawajataka wachunguzwe!
 
yaani takukuru ina uchafu? hii haingii akilini. Haiwezekani taasisi nyeti kama hii iwe na matatizo ya kupaswa kuchunguzwa. Masilingi hana hoja kwenye hili. Haiwezekani kila taasisi inayotuhumiwa jambo baya basi ianze kujichunguza! Mbuna hajashauri Ikulu ijichunguze? Mbona watu wamesema kuhusu wabunge kugongana na hawajataka wachunguzwe!

Takukuru, Ikulu na taasisi yoyote ile ya umma aliye mbele hajulikani. Wananchi tumepoteza imani na vyombo hivi maana ni uwongo tu kila kukicha bila woga wala aibu. Halafu wenyewe pamoja na kuwa wanafahamu kwamba Watanzania hatukubali uwongo wao bado tu wanasema uwongo. Hakuna hata mkubwa mwenye busara akawaambia jamani eh! Watanzania hawakubaliani na hadithi tunazowapa tubadilishe mwelekeo au tubadilishe hadithi yetu!!! Hii ni siri ya serikali, ile ni siri ya serikali, siri siri siri....🙁. Serikali imewekwa madarakani na Watanzania sasa mnafanya siri dhidi ya wale tuliowaweka madarakani!? Mkjj kwa maoni yangu hakuna cha kuchunguza ni kufukuza kazi wote tu maana kazi tuliyowapa imewashinda.
 
Basil Msongo, Dodoma
Daily News; Tuesday,July 01, 2008 @00:04

MBUNGE wa Muleba Kusini, Wilson Masilingi (CCM), ametaka ufanyike uchunguzi kuhusu kauli za Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema) kuwa viongozi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) hawaelewani, na kwamba fomu za mali za viongozi zilizopo kwa Spika wa Bunge zinatofautiana na zilizopo katika Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Amesema ikithibitika ni uongo, Mbunge huyo aombe radhi. Masilingi alisema kauli ya Kabwe kuhusu Takukuru lazima itolewe maelezo na akahoji Kabwe amefahamu vipi kuwa kuna mgawanyiko mkubwa na mgongano baina ya wafanyakazi wa taasisi hiyo wakati hafanyi kazi huko.

Masilingi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, alisema anaamini Kabwe ana uhakika na aliyoyasema na kwa kuwa hafanyi kazi Takukuru lazima wafanyakazi wa taasisi hiyo wamemueleza hayo. Alisema lazima pia uchunguzi ufanywe kufahamu Kabwe amefahamu vipi kuwa kuna fomu za mali za viongozi wa umma zilizopo katika Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ambazo zinachezewa na ni tofauti na zilizopo katika Ofisi ya Spika wa Bunge.


Masilingi lazima ujue kwamba watu wanauchungu sana na jinsi mnavyogawana hiki kidogo tulichojaliwa na Mungu. Na ndiyo maana wameamua kuto information ili wasikilizwe kilio chao. Tena UKOME kabisa kutoa kauli za kutishatisha. Lengo ni nini wakati anasema hawa viongozi wa TAKUKURU hawaelewani je huna habari kwamba vijana wanaoonekana wanapenda haki wanahamishiwa mbali sana kama kuwaadhibu. TAKUKURU inafanya yale yale aliyokuwa anafanya IGP Mahita kila askari akitaka haki fulani adhabu yake Lindi au Mtwara kwani huko Lindi na Mtwara hakuna watu? Acheni kabisa kufanya haki kama kigezo cha kuwanyamazisha wanaharakati.
 
Last edited:
Mmhhh!!! TAKURURU???? hiyo si ndo imeoza kabisa.Nakumbuka pale Singida afisa mmoja wa takururu alimkamata polisi mmoja akipokea rushwa,lakini baada ya kupewa rushwa na polisi huyo kesi ikaisha.Yaani mimi huwa naugua kizunguzungu
 
Masilingi nae kaongea leo.. eeeeh mpigieni vigelegele na makofiiiiiii, kumbe na yeye yupo!!! Haya anaweza kukaa sasa kwenye yale makochi mazuri ya jengo letu jipya la bunge (japo na makochi haya yameshawangiwa, labda wafikirie kujenga jengo jipya na hayo ya sasa yatumike kuanzisha nursery school).
 
kama takukuru imeshindwa kutoa ufumbuzi wa hizi rushwa kubwa mapaka leo. wana matatizo.
Hakuna haja ya kusemwa bungeni.
ni wazi.
Hatujaona makundi ya watu kufutiwa kesi, au kupewa adhabu kwa rushwa kubwa.
Au wanasera ya usiri?
tunataka mtu akisafishwa tujue, na mtu akiadhibiwa tujue pia.
Kwani utu wa hao vibosile ni tofauti na wa hao mahakimu wanaoandukwa kwenye magazeti wakikamatwa na laki mojamoja?
 
Post Zionajirudia mno...

Mod kama inawezekana Merge hii Thread na Zitto azua Jambo Bungeni iliyoanzishwa na Bubu ataka kusema...

Tuweze jadili katika cmstari mmoja.

Heshima mbele.
 
yaani takukuru ina uchafu? hii haingii akilini. Haiwezekani taasisi nyeti kama hii iwe na matatizo ya kupaswa kuchunguzwa. Masilingi hana hoja kwenye hili. Haiwezekani kila taasisi inayotuhumiwa jambo baya basi ianze kujichunguza! Mbuna hajashauri Ikulu ijichunguze? Mbona watu wamesema kuhusu wabunge kugongana na hawajataka wachunguzwe!

Mkuu Mtata sana wewe...

Nadhani ujumbe umefika kwa Walengwa. Pamoja
 
Masilingi ndugu yangu, tangu ulipo temwa kwenye kabineti umejirundika kwenye migomba na rubisi huko Muleba hata hujui kinacho endelea TZ yetu?

Hivi kweli hujui TAKUKURU kuna mgawanyiko mkubwa? Jitahidi basi walau uwe unatembelea JF uwe update kidogo na kinacho endelea nchini kwako! vinginevyo wakati ukuta ndugu yangu utajikuta uko nje kabisaaaa ya dunia yetu Tanzania!
 
Mashilingi Hana Jipyaa, Jimbo Lake Linanyelelewa Na Tibaigana, Wote Ni Walevi Wa Rubisi. Anachozungumza Zito Ndicho Kilichoko Moyoni Mwa Watanznia Wote. Polisi Rushwaa, Takukuru Rushwaaa, Tume Ya Maadili Rushwaaa! Rais Rushwaaaa! Sijui Tuanze Na Nani? Labda Kanisa Na Misikiti Itusaidie Tena
 
Zitto azua jambo bungeni
Basil Msongo, Dodoma
Daily News; Tuesday,July 01, 2008 @00:04

MBUNGE wa Muleba Kusini, Wilson Masilingi (CCM), ametaka ufanyike uchunguzi kuhusu kauli za Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema) kuwa viongozi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) hawaelewani, na kwamba fomu za mali za viongozi zilizopo kwa Spika wa Bunge zinatofautiana na zilizopo katika Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Amesema ikithibitika ni uongo, Mbunge huyo aombe radhi. Masilingi alisema kauli ya Kabwe kuhusu Takukuru lazima itolewe maelezo na akahoji Kabwe amefahamu vipi kuwa kuna mgawanyiko mkubwa na mgongano baina ya wafanyakazi wa taasisi hiyo wakati hafanyi kazi huko.

Masilingi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, alisema anaamini Kabwe ana uhakika na aliyoyasema na kwa kuwa hafanyi kazi Takukuru lazima wafanyakazi wa taasisi hiyo wamemueleza hayo. Alisema lazima pia uchunguzi ufanywe kufahamu Kabwe amefahamu vipi kuwa kuna fomu za mali za viongozi wa umma zilizopo katika Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ambazo zinachezewa na ni tofauti na zilizopo katika Ofisi ya Spika wa Bunge.

Masilingi aliyasema hayo baada ya Kabwe kumaliza kuchangia hoja ya makadirio ya matumizi ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma kwa mwaka wa fedha 2008/2009 iliwasilishwa jana bungeni mjini Dodoma. Kabwe alisema taarifa za mali za viongozi wa umma zinachezewa katika sekretarieti hiyo na hivyo suala hilo lichunguzwe pamoja na kuchunguza tofauti ya fomu zilizopo huko na zile alizonazo Spika wa Bunge.

“Siri zetu zote, mali zetu zote, madeni yetu yote zinafahamika....” alisema Kabwe na pia akawaeleza wabunge kuwa kuna umuhimu wa kuiangalia upya Takukuru kwa kuwa kuna matatizo makubwa ndani ya taasisi hiyo. Kwa mujibu wa Mbunge huyo, viongozi wa taasisi hiyo hawaelewani na watumishi wa chini, kuna Kamati ya kuwawinda wanaoisema Takukuru na kwamba mgawanyiko huo unasababisha Takukuru ishindwe kushughulikia kesi za ufisadi.

Pia alisema Bunge linapaswa kupitia upya sera na Sheria ya Usalama wa Taifa kwa kuwa hivi sasa Idara hiyo hairuhusiwi kuchukua hatua, inatoa ushauri tu. “Pesa za EPA ziliibwa kwa cash, Idara ya Usalama wa Taifa ilikuwa inafahamu,” alisema Kabwe na kusema kuwa Meremeta haihusiani na Usalama wa Taifa hivyo serikali kupitia Bunge lazima iwaeleze ukweli Watanzania akidai kuwa Meremeta ni wizi wa waziwazi.

Masilingi alisema anavyofahamu hakuna tofauti ya rushwa kubwa na rushwa ndogo, anafahamu kuna watu wanaoichukia Takukuru na isipokuwapo taifa litaangamia. Alisema watu wanawatuhumu wenzao kuwa ni mafisadi nao wachunguzwe wasije wakasakwa wanaotuhumiwa kumbe wengine wapo, na akasema kuna mafisadi na vifisadi.

“Mimi sichukii mtu akisema fisadi fisadi, tusije tukasema fisadi fisadi tukawapita mafisadi,” alisema Masilingi na kuitaka Takukuru ichunguze kwa makini kabla ya kuwakamata watuhumiwa. Alisema watumishi wa umma wanapaswa kujiamini, wasiogope kujenga maghorofa au kununua magari ya kifahari kwa sababu ya hofu ya kuitwa mafisadi.

Msemaji wa Kambi ya Upinzani katika wizara hiyo, Grace Kiwelu alisema wananchi wengi hawaamini kuwa Takukuru ni chombo cha kupambana na rushwa, bali taasisi ya kulinda mafisadi.

“Kambi ya upinzani inaitaka serikali ianzishe mchakato wa kuichunguza Takukuru yenyewe kwa lengo la kujisafisha, kuona kama yenyewe ni safi, jambo ambalo kimsingi linaashiria kuwa haiko safi ndiyo maana inashindwa kuchukua hatua kwa watuhumiwa mbalimbali,” alisema.

Mbunge wa Kibaha Mjini, Dk. Zainab Gama (CCM), alisema inapaswa kufuatilia taarifa za rushwa serikalini, mahakamani na kwamba hata kama zinawahusu wabunge wachunguzwe. Dk. Gama alisema kuna umuhimu wa kuwa na kamati ya Bunge inayoshughulikia rushwa kama ilivyo kwa Kamati ya Bunge ya Ukimwi, na pia Takukuru wawe wanatoa taarifa bungeni kuhusu utendaji wao.

Haya niliyategemea baada ya kusoma ile speech ya zitto. kazi imeanza tena, kijana mwenzetu anafanya wazee mafisadi kujiabisha hadharani. Nasubiria kuona game plan ya ccm kwenye hili.

Credibility ya Pinda imekwisha kabisa na sasa wanatafuta "mtoto wa mkulima" mwingine asafishe njia.

Kazi kweli kweli
 
Huyu Kilaza hivi ni Mashilingi au Vijisenti? yaani katika nondo zote zile alizopigilia Zito kuhusu Meremeta, huyu Kilaza alichoona ni muhimu kuzungumzia kwa gharama za walipa kodi ni mgongano kati ya wafanyakazi wa TAKUKURU na sio mapesa ya MEREMETA ambayo ndio msingi wa hoja ya Zitto. Kama huyu jamaa aliwahi kuwa waziri wa utawala bora enzi za Mkapa sasa ndio naanza kuelewa, ilikuwaje kashfa zote hizi za KIWILA, EPA, MEREMETA na matakataka mengine yaliweza kutokea bila ya serikali kushtuka.
 
Takukuru haina maana yoyote na ingebidi ni vema ikavunjwa. Mlarushwa na mafisadi wako serikalini ambayo ndi inamteuwa PCCB. sasa PCCB itamchunguza serikali. Itaanzia wapi?. PCCB haikuanzashwa kwa matakwa ya ananchi bali kwa shinikizo la nchi wahisani.
 
Masilingi huyu si yule mbunge wa Muleba?
Kwanza usafi wake yeye tu unatia shaka. Alikuwa waziri wa takukuru wakati wa BWM na anajua wazi kuwa haya ni malalamiko ya kweli kwani aliyaacha bila ya kuyashughulikia akitegemea atarudi kwenye cabinet. Bahati yake mbaya alisoma vibaya alama za nyakati kama wafanyavyo wana ccm wote. Akalalia kwa Sumaye akidhani atakuwa ndiye president na akakuta hesabu imetibuka.
Hata hivyo ni huyu huyu ambaye wakati wa uchaguzi inasemekana wakati wa kula (Kura)za maoni ya chama chake cha majizi alitembea usiku kucha akigawa pesa kwa wajumbe yeye mwenyewe! ili ateuliwe kugombea kupitia ccm kwani ajui tunamfahamu? Sijui yeye tumweke kundi gani Fisadi/Kafisadi?
 
...Masilingiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii anataka kuturudisha mwaka 47 nini?? Kama Takukuru wanachemka hataki watu waseme!!!
 
Back
Top Bottom