Kutoka Bungeni: 2006 - 2010

Kutoka Bungeni: 2006 - 2010

Imeonekana Unga Ulipelekwa Kwa Mkemia Mkuu Kwa Ajili Ya Uchunguzi Kuoka Bungeni Hauna Madhara Kabisa...kama Ni Mambo Ya Kishirikina Si Atujui Ila Unga Uko Poa Kabisa!!!!!!!!!kazi Kweli Kweli!!!
Mwananchi-source
 
Hizo ni hoja nzito, zilizotayarishwa kwa umakini na uchunguzi wa kina. Inadhihirisha kuwa kambi ya upinzani imebobea kwenye kufuatilia siyo tu ufisadi, bali masuala yote muhimu yanayogusa maisha ya watanzania kama ipasavyo kwa wanasiasa ambao wana lengo la kupigania mlalahoi. Hongera na mdumu kwenye msimamo huo. Iko siku watanzania wataamka na kuamua kuwapa kura zao wale wanaopaswa kuliongoza taifa hili kwa nia ya kuleta maendeleo kwa watanzania wote na si wao binafsi!
 
Wadanganyika nawasihi tujenge utamaduni wa kusoma hansadi katika tovuti mahiri ya Bunge maana japo hawakutuonesha laivu hotuba ya Dakta Slaa walishaificha hapa chini toka zamani kitambo - bofya uone: [media]http://www.bunge.go.tz/Polis/PAMS/Docs/HS-12-9-2008.pdf[/media]
 
If we could have more 20 politicians the type of Slaa, I believe we could be far in social service and development wise. If we need to have a sheer forward let us give the authorities to the leader who know what are they doing in the house and not going there just for allowance. It doesn't kick in my head even the primary pupils are now demonstrating protesting against increased commuter bus fares, is it fair?? Worse enough we have leaders but they decide to keep silent reason being their children are going to school by using Vx. So shall we make it???
 
Ukweli, Bunge lilikuwa limekwisha kupitisha kwa kauli moja, Azimio la kuanzishwa kwa Serikali ya Tanganyika Agosti 24, 1993 kwa maana ya kuwa na Serikali ya Muungano inayoundwa na Serikali hai zenye Mamlaka huru, za Tanganyika na Zanzibar, kama vile tu alivyotaka Rais Jumbe mwaka 1983.
Hata hivyo, Azimio hilo lilipigwa rungu zito na Mwalimu Nyerere na kunyamazishwa. Na kama ilivyokuwa kwa Jumbe, hapa napo mambo hayakuisha salama; safari hii Waziri Mkuu wa wakati ule, John Malecela (hongera kwa kutimiza miaka 75) na Katibu Mkuu wa CCM, Horace Kolimba, walipoteza nyadhifa zao na wengine kukutwa na umauti kwa sababu ya ama kunyamazia au kuunga mkono hoja / Azimio la G 55.

Je Wabunge wa leo wanaweza kuipalilia na kuiamsha hoja hii kwa kasi mpya na ari mpya ? Au wanaogopa kupoteza nyadhifa na kukutwa na umauti ?

Naomba kuwasilisha hoja .
 
Nawe mkuu Mwiba kwa kuchokonoa mambo!! haya hawayataki wao wameshika zanzibar ndo inataka muungano uvunjike, mara zanzibar ndo wanaoshinikiza serikali ya Tanganyika irudishwe mara vp... utafikiri haya yote hayakutokea, na wengine hawataki kuamini kuwa kikwazo cha maendeleo mazuri ya huu muungano ni hila tu za Mwalimu na nia yake mbaya tokea mapema. Labda mkuu Mwiba haja zako za "kichokozi" zinaweza saidia kuamsha bongo lala. Bismillah....
 
kwa wabunge wa sasa hawana time mkuu. wao wapo kuwekeza na miradi ya kufua umeme wa upepo na nini sijuwi, kwa hili usahau, ila chagizo zitoke kwa wabunge wa "upande wa pili" wasiokuwa na mradi wowote utakaowalazimisha kutangaza maslahi, wenzetu wapo bize kujadili hoja zinazolinda matumbo yao.
 
Tatizo lililopo fikira zipo zaidi kwenye kuvunja muungano, jambo ambalo sikubaliani nalo kimsingi. Kama haja ya muungano inarudi basi iwe kudumisha muungano. Azimio la G 55 kwa njia moja ama nyingine linato mwanya kwa kuanzisha mjadala.
 
KWa sasa waliobakia ni mafisadi tu maana kauli za vyama vyote vya upinzani vinasema Muungano una kasoro kubwa sana ,maana hata watoto wea shule wanadanganywa kuhusu sherehe za Uhuru ,wanaambiwa kuwa Tanzania ilipata Uhuru tarehe 9Dec wakati sio kweli ,iliopata Uhuru ni Tanganyika,halikadhalika kwa Zanzibar vilevile ,sasa vyama vya upinzani wameanza kuona ukweli huo ,kuwa Sultani CCM anadanganya hata watoto wa shule.
Kwa ufupi nawapongeza Vyama vya upinzani kwa kuona ukweli mafisadi lazima wafikishwe kikomo na kikomo chao ni kusambaratika kwa Muungano ili iundwe Tanganyika mpya hapo kutawezekana kujadiliwa hoja za Muungano na kutengenezwa vizuri sana. kwa sasa naona wapinzani wameweza kuitema kasumba ya CCM kulinda Muungano ,wameng'amua kuwa ni janja ya CCM tu ,hakuna kitu ,maana ikiwa huko Zenji hata ukamsikia CCM anasema kuwa Tanganyika lazima irudishwe ujue kuwa mambo ni magumu kwa CCM bara aidha itabidi wayakubali yale wanayoyataka Zanzibar na hapo WaTanganyika hamtakubali ikiwa serikali ya Muungano inafuata watakavyo WaZanzibari ,hili naamini kabisa hamtalikubali mtaona kama waonavyo WaZanzibari heri Muungano ufilie mbali ,lakini sivyo tunata kuuweka katika misingi imara kwa kuwepo kwa Tanganyika ,ni rahisi sana ,maana ukiulizwa Nchi zilizoungana zipo wapi ,Zanzibar ipo ,Je Tanganyika imekwenda wapi kusema ukweli kutakuwa hakuna jibu zaidi ya ubabaishaji tu.
Hivi kuna tatizo gani kurudisjhwa kwa Tanganyika hapa ndipo ninapotaka kufahamishwa ,wabunge wale 56 walifanikiwa kuirudisha Tanganyika ,sababu walizokuwa nazo wakati ule zitashindwaje leo ambako vyama vyote vya upinzani vinavyoongozwa na majority ya WaTanganyika vinasema Muungano ni batili ,wanasheria Muungano una matatizo utawasikia wakisema kuna hiki na kile vinakinzana, so ugumu upo wapi ,waongo mafisadi tulionao utawasikia wakiunda kamati tume,mara wanasheria mara waziri mkuu mara waziri kiongozi sijui wanakutana na walipofikia ni patamu ,lugha nzuri sana huwa wanaibuka nayo ,ghafla wanaingia mitini husikii chochote ,mpaka wakikurupushwa huzuka tena inakuwa kama wanasikiliza mshindo ,safari hii mshindo wandugu si mdogo ni mkubwa sana tena sana ,ndio nikasema haina haja ya yote ,kwa tulipo hakuna utakaemsikia kuwa Muungano ni mzuri hauna matatizo na ukimsikia hivyo ujue ni katika wale walindano matumbo yao ambao katika Chama Chao kumejaa mafisadi na mayai yao ni wao tu ,wakijitokeza vifua mbele kulinda kwa hali yeyote ile ,wakati wahindi saba wanawaendesha mbio na kuhangaika nao ,wanashindwa hata kuwa shughulikia itakuja kuwa Muungano ambao sasa walio wengi wameanza kuuelewa na kuona hata watoto wao wanapotoshwa mashuleni.
 
mwiba unadocuments za Azimio G 55 kama zipo tuwekee hapa. Ningependa kuzisoma
 
mwiba unadocuments za Azimio G 55 kama zipo tuwekee hapa. Ningependa kuzisoma
Kusema kweli sina labda hapa tuna wabunge machachari na pia kuna watu ni wajuzi wa kuweza pata hizo documents tatizo ikiwa serikali wanazi hesabu kuwa ni za siri ,sidhani kama yupo mtu atasubutu kuziweka hapa ,siku hizi wamekuwa waoga sana.
 
Labda ifanyike kula ya maoni, kujuwa ukweli!
He he he, hata maoni yakifisadi,
hamna chochote, ni kuidivete attention ya ufisadi tushughulike na muungano! Kweli tumazuzu!
 
Rais Kikwete ahadi za kuitafuta Tanganyika zimefia wapi?
Deogratius Temba

"MUUNGANO una kasoro zake, nilisema tutazimaliza, sikusudii kuunda tume ya kushughulikia kwa sababu kamati zilizowahi kuundwa zimebainisha kasoro za Muungano na namna ya kuzitatua." Hii ni kauli ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete.
Kila mmoja anayefuatilia kwa makini suala la Muungano huu ulioasisiwa Aprili 26, 1964, ataungana na Rais Kikwete kuwa Muungano una kasoro, unaumwa, tena upo taabani.

Ni vizuri kiongozi wa juu anapokiri waziwazi kuwa kuna tatizo na kutaka kuonyesha nia ya kulitatua. Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, aliwahi kutamka maneno haya: "Mficha madhara kilio kitamuumbua", hatuna haja ya kukanusha ukweli kama mtu anaumwa tuseme ukweli ili atafutiwe dawa.

Kwa muda wote huo na kwa sababu ya tabia ya kuficha maradhi kwa kigezo, kwani dhambi kuulizia masuala ya Muungano, tunakuwa tukijaribu kutibu tu dalili za maradhi ya muungano badala ya kutafuta chanzo chake.

Si mara moja kumeibuka mifarakano mingi kati ya serikali ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kuhusiana na mambo mbalimbali yakiwemo upatikanaji wa mafuta.

Muungano ulianza kukumbwa na misukosuko tangu siku za kwanza ya uhai wake. Tangu wakati huo awamu nne za utawala zimepita na baadhi ya kero ni zile zile kwa miaka 45. Hakuna aliyeweza kuzimaliza lakini napenda kusema kwamba naamini Rais Kikwete atapambana nayo tu.

Waasisi wa Muungano huo, Mwalimu Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume walisimamia Muungano na wakati mwingine ulianza kutetereka na kufikia mahali kutaka kuomba nguvu kutoka nje ya kwa ajili ya kuulinda.

Changamoto nyingi zimewakumba, malalamiko kuhusu kuwapo kwa Muungano huu yanazidi kukua kila siku, inawezekana ilikuwa kosa kuanzishwa kwake lakini pia kuuvunja ni kosa kubwa.

Kuna swali ambalo limejaa vichwani mwa wasomi na wanazuoni, leo wanajiuliza hivi, mawazo ya kuungana yalikuwa ya Mwalimu Nyerere au Sheikh Karume? Na kama yalikuwa ya kwao wenyewe, kwa nini walishindwa kuweka misingi imara ya kuulinda na kuwaweka baadhi ya nyaraka za msingi hadharani ambazo zingeweza kudhibiti mawazo ya baadhi ya watu wanaoupinga?

Ikumbukwe kuwa mwaka huu sherehe za Muungano zimeangukia Jumapili na Muungano huu huu uliasisiwa Jumapili 26, Aprili, 1964, na hicho kilikuwa kipindi cha siku 104, tangu Mapinduzi ya Zanzibar ya Januari 12, 1964.

Siku chache baada ya Muungano, Sheikh Karume alikaririwa na gazeti la Nationalist la Tanganyika akisema: "Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar utatufaidisha sote hautakuwa kikwazo kwa watu wa Zanzibar."

Binafsi nimekuwa nikijiuliza ni kitu gani kilichomsukuma Karume kutamka maneno hayo? ina maana alianza kuhisi kuwa Muungano kamwe hauwezi kuwafurahisha watu wa Zanzibar, licha ya kwamba Watanganyika hawana haja nao.

"Neno hautakuwa na kikwazo kwa watu wa Zanzibar lina maana kubwa linapokuja suala la Uzanzibari na Utanganyika ambao Mwalimu Nyerere aliukataa, lakini mzimu wake ndiyo hivi sa sa unautafuna muungano huu hadi leo.

Tumeona tayari dalili zinaonyesha kuwa kero za Muungano na kasoro zipo Zanzibar tu Watanganyika wamelala fofo, wanasema muungano uwepo usiwepo wao wanasonga mbele.

Kero ya kwanza ilitokea siku chache tu baada ya kuundwa kwake, Jamatatu, Aprili 27, 1964, MwalimuNyerere alitangaza Baraza la Mawaziri alitoa viti vitano kwenda Zanzibar kutoka kwenye baraza hilo.

Hali ilianza kuonekana siku chache na kisha kukatokea mgogoro wa Zanzibar na Tanganyika kuhusiana na suala la Jamhuri ya Kidemokrasi ya Ujerumani (GDR), ambapo Zanzibar ilitangaza kuitambua na kutoa utambulisho wake wa kibalozi, wakati Tangayika ilikataa kuitambua, ikawa inaitambua Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani Mashariki.

Jumanne, Mei 4, 1964 ikiwa ni siku nane tu baada ya Muungano na baada ya kuundwa kwa Baraza la Mawaziri, walikaa na kujadili juu ya suala la kuitambua Ujerumani, hawakuelewana ipasavyo, Muungno ukaendelea kutikisika, waasisi wakazidi kutafuta msaada wa nje kuumaliza hasa mataifa ya Marekani na Uingereza ambayo wanadaiwa kuwa ndiyo waliochochea nchi hizi kuungana.

Juni 12, 1964, balozi wa Uingereza Tanzania wakati huo, Wiliam Leonhart, alituma ujumbe kwenda Marekani ukisema anaomba Serikali ya huko imwombe aliyekuwa Rais wa Kenya, mzee Jomo Kenyatta, atumike katika kuimarisha Muungano.

Mdahalo wa kwanza juu mfumo na muudo wa Muungano ulianza kwa njia ya maoni juu ya katiba ya Jamhuri ya Muungano mwaka 1983/84, hapo ilibainika kwa mara ya kwanza viongozi wa juu wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakiongozwa na Rais Aboud Jumbe na wale wa serikali ya Muungano wakiongozwa na Mwalimu Nyerere walikuwa na mitazamo tofauti juu ya Muungano huo.

Jumbe na timu yake walitaka Muungano uwe na serikali tatu kwa maana ya serikali ya Tanganyika, Serikali ya Zanzibar iliyopo sasa, na serikali ya Muungano itakayokuwa ikishughulikia mambo ya Muungano tu.

Kutokana na ukorofi na mambo mengine, Sheikh Jumbe alilazimishwa kujiuzulu nafasi zote za uongozi wa nchi kuanzia urais, umakamu wa Rais wa Muungano na nafasi zote za kichama Januari 1984.

Baada ya Sheikh Jumbe kuondoka, hali haikutulia. Kuliibuka tena mambo mengine mapya wakati kundi la wabunge 55 maarufu kama G55, walipojitokeza na kwasilisha bungeni waraka wa kutaka kurejeshwa kwa serikali ya Muungano mwaka 1993.

Ni kweli kuwa Bunge lilikuwa limeshapitisha azimio la pamoja la kuanzishwa kwa serikali ya Tanganyika, Agosti 24, 1993 kwa maana kuwa kuwapo na serikai tatu kama alivyotaka Jumbe mwaka 1983.

Lakini Mwalimu Nyerere akaona kuna hatari ya Muungano kuishilia mbali kama atanyamaza. Aliamua kujitoa mhanga kupambana na kundi hilo hadi kulishinda. Hali hiyo ilisababisha aliyekuwa Waziri Mkuu wakati huo, John Malecela, na Katibu Mkuu wa CCM, Horace Kolimba kupoteza nyadhifa zao kwa kile kilichoelezwa kuwa walinyamazia makundi hayo hadi kuingia bungeni.

Leo hii tunapoadhimisha miaka 45, ya Muungano huo, mgogoro kama huo unaonekana katika suala la Zanzibar kutaka kujiunga na Jumuiya ya Nchi za Kiislamu (OIC) wakati Tanzania haitaki kujiunga nayo. Zanzibar imeanzisha Mahakama ya Kadhi lakini Tanganyika haikuwa tayari kuwa na mahakama hiyo, hizo ni tofauti za kimuungano.

Tumeona jinsi ambavyo hata waasisi walivyoshindwa kuuimarisha ipasavyo Muungano, hebu tujaribu kujiuliza kwa nini Mwalimu Nyerere kila mara alisema ni dhambi kubwa kuuvunja Muungno?

Kwa nini alitumia hata maneno ya kukatisha tamaa ya kusema kuwa ulevi wa madaraka na ujinga wa watu wachache unatawafanya watake kuuvunja Muungano? Aliona hayo tangu awali ikabidi atumie saikolojia ya vitisho.

Mwalimu ameshuhudia makundi kadhaa ya Wazanzibari na Watanganyika kutotaka kuutambua Muungano na kudai kurejeshwa kwa serikali ya Tanganyika.

Tumeona kutokana na magonjwa ya Muungano kutokutibiwa, magonjwa mengine yamekuwa yakiongezeka nakuna kundi limeibuka linataka kusherehekea siku ya Uhuru wa Zanzibar.

Hapo ndipo penye swali, kwa nini Wazanzibari wa leo wanagawanyika? Kwa nini hawataki kabisa kusikia mapinduzi na Muungano?

Hivi karibuni kumeitokeza kundi la wazee kutoka Pemba wakitaka kujitenga yaani Pemba ijitenge ni kisiwa cha Unguja, maana yake kujitenga huo kutaifanya Pemba kutambulika kama nchi au Jamhuri, na wangefanikiwa wangepaswa kutanga uhuru wa visiwa hivyo siku hiyo, wazee hao wamemwandikia Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Ki-moon, kueleza kilio chao.

Kwa bahati nzuri walipotaka kufanya maandamnao Februari wakati Ban akiwa nchini kuelekea katika ofisi za UN kudai haki hiyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Muhammed Seif Khatib, akafanikiwa kuwanyamazisha, lakini ieleweke kuwa kunapaswa kutafutwe dawa ya tatizo na si kuwanyamazisha.

Kama anavyosema Rais Kikwete, ambaye anamalizia miaka mitano ya utawala wake, akiwa bado hajaweza kutafauta dawa ya kuutibu Muungano, tunaingia kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, tukiwa na majeraha ya muungano hakuna suluhisho la matatizo.

Migogoro ya kupinga matokeo ya uchaguzi ni matokeo ya kutokutaka kutibu magonjwa ya Muungano, hayo ni moja ya magonjwa yanayouandama Muungano, tyunaelekea kutibu dalili na kuacha kuangalia chanzo cha ugonjwa.

Matumizi mabaya ya dola visiwani humo ni tatizo na ni kero mojawapo ya Muungano, huwezi kuongoza watu kwa kuwashambulia kila wanapopiga kura, wakimaliza unawaacha, haya ndiyo yanayowaumiza Wapemba.

Ni dhahiri kuwa muungano hauna shida kwa Wapemba kama wakipewa haki ya kufanya uchaguzi na kuchagua viongozi wao kwa uangalifu na umakini na wakamweka mtu wanayempenda madarakani, bila serikali ya Muungano kuingilia kati, au kupeleka jeshi la kupambana na raia.

Kero ya kudai kuwa mambo 11 ya Muungano hayako wazi, suala la mafuta, suala la Khatib kutaka kuwa rais si la kusababisha Muungano kuvunjika, kama viongozi wetu watakaa pamoja na kuangalia masuala ya msingi hasa ya Wapemba na kuwajali, kama watu wasio waasi.

Ni kweli kuwa huu ni Muungno wa kihistoria. Hakuna nchi au mataifa yaliyowahi kuungana na yakawa na muungano wa kudumu mzuri kama huu, lakini huu ni mzuri kwa nje lakini ukiingia ndani umejaa magonjwa zaidi ya 22.
Rais Kikwete ahadi zake na kundi lake la G55 za kuitafuta Tanganyika zimeishia wapi?
 
Mwakyembe kulipua bomu la Kiwira bungeni

Mwandishi Wetu Aprili 29, 2009

Raia Mwema~Muungwana na Vitendo

Ben Mkapa kuguswa

WAKATI wowote kuanzia leo, Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe atawasilisha hoja binafsi kuhusu mgodi wa Kiwira ili kuwatetea wafanyakazi wa mgodi huo ambao hawajalipwa mishahara yao kwa zaidi ya miezi 10, hali inayowafanya kushindwa kumudu gharama za maisha.

Dk. Mwakyembe amelazimika kuchukua hatua hiyo ambayo imekubaliwa na uongozi wa Bunge hususan Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashililah kutokana na kile kinachoelezwa kuwa shinikizo la wafanyakazi hao kwa mbunge wa eneo ulipo mgodi huo.

Wafanyakazi wa mgodi huo ambao wamepunjwa malipo ya mafao yao na kutolipwa mishahara kwa zaidi ya miezi 10 sasa, wanadai wamefikia hatua hiyo kutokana na ukimya wa Serikali katika kushughulia matatizo hayo.

Mbali na ukimya wa serikali, uamuzi wa wafanyakazi hao kumshinikiza mbunge wao pia unatokana na ukimya wa utekelezaji wa mapendekezo ya Kamati ya Rais iliyoundwa kuchunguza sekta ya madini iliyoongozwa na Jaji Mark Bomani, ujumbe wa Kamati ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Ludovick Utouh, pamoja na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini inayoongozwa na Mbunge wa Bumbuli, William Shellukindo.

Kwa nyakati tofauti kamati hizo zilitembelea mgodini hapo na kuzungumza na wafanyakazi na kuwaahidi kuwa matatizo yao yakiwamo ya kupunjwa malipo na kutolipwa mishahara yangepatiwa ufumbuzi wa haraka na kwamba taarifa zote zingefikishwa kwa Raia Jakaya Kikwete.

Hata hivyo, kinachowaondolea imani wafanyakazi hao ni ukimya uliotawala baada ya kamati hizo kuondoka mgodini hapo, wakiamini kuwa huenda mapendekezo ya Kamati ya Jaji Bomani na ujumbe wa CAG hayajafanyiwa kazi na wasaidizi wa Rais Kikwete ambaye wanaamini kuwa kama angeshauriwa vyema asingeweza kukaa kimya.

Raia Mwema imefanikiwa kuona barua ya wafanyakazi hao ya Aprili 15, mwaka huu yenye kumbukumbu namba TAMICO/KCP/VOL/11/0409 iliyotiwa saini na Mwenyekiti wao Daniel Kibona na Katibu wake Thomas Keyo ikiwa na saini za wafanyakazi wengine 54.

Katika barua hiyo, wafanyakazi hao wanamtaka Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, ambaye mgodi huo uko jimboni kwake, kulifikisha rasmi suala hilo bungeni kwa niaba yao , hasa baada ya kuona hata Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini nayo imekaa kimya.

Kwa mujibu wa kanuni za Bunge, katika hali kama hiyo ya shinikizo la wananchi, mbunge analazimika kuchukua maelezo ya wafanyakazi hao na kuyawasilisha bungeni kama hoja binafsi.

Barua hiyo inayomtwika mzigo huo Dk. Mwakyembe inataka kuchukuliwa kwa hatua za haraka kunusuru hali za wafanyakazi hao ambao wamedai katika barua kuwa wamekuwa ombaomba.

“Mbali na kupunjwa mafao yetu lakini mishahara ya miezi zaidi ya 10 hatujalipwa..Januari 14, mwaka 2008 Kamati ya Rais kuhusu madini iliyokuwa ikiongozwa na Jaji Bomani (Mark) ilitembelea mgodi na kushuhudia hali mbaya ya wafanyakazi na kuahidi kulifikisha suala hili kwa Rais.

“Oktoba 20, mwaka 2008, ujumbe maalumu wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ukiongozwa na Mama Msongwa, ulitembelea mgodi na kuridhika kuwapo kwa hali mbaya ya wafanyakazi waliahidi kushughulikia tatizo hilo na kulifikisha kwa Rais.

“Januari 17, mwaka huu, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ikiongozwa na Mbunge wa Bumbuli, William Shellukindo, ilitembelea mgodi na kushuhudia hali mbaya za wafanyakazi. Kamati hii ikaahidi kufikisha suala hili bungeni,” inaeleza barua hiyo na kuongeza kuwa;

“Mheshimiwa mbunge (Mwakyembe) pamoja na harakati zote hizo hakuna chochote kilichofanyika. Hali za wafanyakazi zinazidi kuwa mbaya..wafanyakazi wamechakaa mithili ya ombaomba.

“Wameshindwa kulipa ada na michango mingine ya shule kwa ajili ya watoto wao. Wapo watoto 107 wa kidato cha nne katika Sekondari ya KCM na sekondari nyingine ambao wameshindwa kulipiwa ada za mitihani kutokana na wazazi wao ambao ni wafanyakazi wa mgodi kukosa fedha hizo.”

Katika kuonyesha kukerwa na hali hiyo pamoja na ukimya wa Serikali, wafanyakazi hao wamesema; “Tumekuwa kama watumwa katika nchi yetu tusiokula matunda ya uhuru wa nchi yetu. Hii si haki hasa pale mgodi unapokuwa unamilikiwa na Serikali kwa ubia.

“Uvumilivu sasa umetushinda tumeamua kutembea kwa miguu kutoka Kiwira kwenda kumwona Rais tukaeleze wenyewe inawezekana timu zote zilizotembelea mgodi hazikufikisha ujumbe. Heri kufia njiani kuliko kufia kitandani, ” inaeleza sehemu ya barua ya wafanyakazi hao.

Katika mkutano uliopita wa Bunge, suala la Kiwira lilijitokeza japo si kwa uwazi na zaidi likiwa ndani ya wigo wa Kamati ya Nishati na Madini, ambaye ilitembelea mgodi huo pamoja na kuzungumza na wafanyakazi.

Gazeti hili liliwahi kuandika kuwapo kwa hali ya shinikizo la kutaka mgodi huo urejeshwe serikalini na wafanyakazi hao walipwe stahili zao zote.

Iliripotiwa pia na gazeti hili kwamba zilikuwapo juhudi za wazi za kuibana Serikali kiasi cha kulazimika kuanza kufikiria uamuzi wa kisheria na hata kutafakari fursa ya kumwondolea kinga Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, au kutafuta uwezekano wa kumhoji kuhusu mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira mkoani Mbeya, anaodaiwa kuwa na maslahi binafsi kupitia kampuni ya ANBEM na hata wanafamilia wake.

Kutokana na hali hiyo na hasa kile kinachobainika kuwa Bunge kupitia Kamati yake ya Nishati na Madini kuridhishwa na ushahidi katika nyaraka hizo, Bunge limetajwa kudhamiria kuibinya Serikali katika mambo makuu mawili.

Jambo la kwanza ni kushinikiza mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira kurejeshwa serikalini kutokana na sababu kadhaa lakini kubwa zaidi ni wawekezaji wanaopaswa kuendesha mgodi huo kubainika kuwa ni wababaishaji walioshindwa kutekeleza ahadi zao kwa Serikali.

Kati ya mambo yanayodhihirisha kuwa mwekezaji huyo kushindwa kuendesha mradi wa uzalishaji umeme kwa kutumia makaa ya mawe katika mgodi huo ni kushindwa kuwalipa stahili zao wafanyakazi wa mgodi, ambao hadi Kamati ya Bunge inatembelea mgodi huo, walikuwa wakidai mishahara mipya iliyotangazwa na Serikali kwamba kima cha chini kwa sekta ya madini ni Sh 350,000.

Kamati hiyo pia ilibaini kuwa mwekezaji huyo alishindwa kulipa mishahara waliopanga ambayo ni kima cha chini kuwa Sh 60,000 kwa muda wa miezi takriban nane sasa.

Lakini kubwa zaidi ni wawekezaji hao kushindwa kuzalisha umeme kwa mujibu wa makubaliano kati ya kampuni hiyo na Serikali kupitia TANESCO.

Kabla ya kubinafsishwa mgodi huo ulikuwa ukizalisha megawati 6 zilizokuwa zinaingizwa katika gridi ya taifa, lakini baada ya kampuni ya TanPower Resources Ltd kupewa mgodi walitakiwa wazalishe megawati 200 katika awamu mbili.

Awamu ya kwanza ilikuwa izalishe megawati 50 ifikapo Julai 2007 na uzalishaji wa megawati 150 zilizosalia ukamilike Machi, mwaka huu. Taarifa za uhakika zinabainisha kuwa hakuna chochote kilichofanyika hadi sasa na hasa ikizingatiwa kuwa awali umeme ulikuwa ukisambazwa na kutumika katika wilaya za Kyela, Ileje na Rungwe.

Kwa sasa inaelezwa kuwa uzalishaji umeme katika mgodi huo umeshuka kutoka megawati 6 za awali kabla ya ubinafsishaji hadi megawati moja na hivyo kusababisha matatizo ya umeme katika wilaya hizo tatu. Sababu hizi na nyinginezo ndizo chanzo cha Bunge kuweka shinikizo mgodi huo urejeshwe serikalini kutoka mikononi mwa mwekezaji huyo.

Jambo la pili ambalo Bunge linaweza kufanya ni kuishinikiza Serikali kumhoji Mkapa au hata kufungua milango ya kumwondolea kinga ya kushitakiwa.

Kama Serikali itashindwa kuridhia kufungua milango ya kumwondolea kinga ya kushitakiwa, basi Bunge limekusudia kuweka shinikizo kwamba Mkapa ahojiwe ili akiri au la kuliko kuacha mambo yabaki ‘hewani’ kama nchi haina uongozi.

Kwa mujibu wa tathmini ya mwaka 1998, mgodi ulikuwa na thamani ya Sh bilioni 4.2, wakati tathmini iliyowahi kufanywa mwaka 1991 na Taasisi ya Ardhi inaonyesha kuwa mgodi ulikuwa na thamani ya Sh bilioni saba.

Lakini katika ziara yake Januari mwaka huu, mgodini hapo, Kamati ya Bunge ilibaini kuwa pamoja na tathmini hiyo kufanyika, licha ya kwamba ilifanyika miaka mitano kabla ya kubinafsishwa, kamati ilishindwa kuelewa ni vigezo gani vilitumika kutupilia mbali uthamini huo na kuamua kuuza hisa kwa gharama ya Sh milioni 700 tu.

Habari zaidi zilizotufikia zinaeleza kuwa wakati wa ziara hiyo, Kamati hiyo ya Bunge ilipokea taarifa mbili zinazogongana kuhusu umiliki wa hisa za mgodi huo. Kilichobainika ni kwamba taarifa ya mwekezaji kudai kuwa amenunua hisa asilimia 70, Serikali asilimia 12 na nyingine asilimia 18 hazijanunuliwa.

Taarifa hiyo inadaiwa kugongana na ile ya wafanyakazi iliyotolewa kwa Kamati hiyo ya Bunge. Taarifa hiyo ya wafanyakazi inaeleza kuwa mwekezaji anamiliki asilimia 85 na Serikali asilimia 15.

Kutokana na mkanganyiko huo, kamati hiyo ilitoa taarifa yake iliyobainisha kuwa wajumbe wa kamati wameshindwa kuelewa juu ya utata wa umiliki huo wa hisa na wamelazimika kukusudia kuiomba Serikali ieleze wazi kuwa inamiliki hisa asilimia ngani.

Kubwa jingine lililogunduliwa na Kamati hiyo ya Bunge mgodini Kiwira ni taarifa ya mwekezaji kuonyesha kuwa Serikali ilitenga Sh bilioni 17 kwa ajili ya ukarabati, kabla ya ubinafsishaji kufanyika lengo likiwa ni kukarabati mitambo yote ya uzalishaji iliyotajwa kuwa ilikuwa imechakaa.

Hata hivyo, kamati ilipigwa na butwaa baada ya kuelezwa na wafanyakazi kuwa hakuna ukarabati wowote uliofanyika na zaidi ni kwamba jenereta moja ya kuzalisha umeme imechakaa na haifanyi kazi, wakati jenereta ya pili ina uwezo wa kuzalisha si zaidi ya megawati moja tu.

Mgodi wa makaa ya mawe Kiwira uliopo katika wilaya tatu za Rungwe, Ileje na Kyela, ulianzishwa kwa msaada wa kifedha na ufundi kutoka Jamhuri ya Watu wa China na ulizinduliwa rasmi na Rais wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi, Novemba mwaka 1988.

Mgodi huo unatajwa kuwa na uwezo wa kiusanifu wa kuzalisha makaa ghafi ya tani 150,000 kwa mwaka. Kiwango hicho cha uzalishaji hata hivyo kinaweza kuongezwa hadi tani milioni moja kwa mwaka. Makaa hayo hutumika kuzalisha umeme.
 
Mwakyembe kulipua bomu la Kiwira bungeni

Mwandishi Wetu Aprili 29, 2009


Ben Mkapa kuguswa

WAKATI wowote kuanzia leo, Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe atawasilisha hoja binafsi kuhusu mgodi wa Kiwira ili kuwatetea wafanyakazi wa mgodi huo ambao hawajalipwa mishahara yao kwa zaidi ya miezi 10, hali inayowafanya kushindwa kumudu gharama za maisha.

Dk. Mwakyembe amelazimika kuchukua hatua hiyo ambayo imekubaliwa na uongozi wa Bunge hususan Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashililah kutokana na kile kinachoelezwa kuwa shinikizo la wafanyakazi hao kwa mbunge wa eneo ulipo mgodi huo.

Wafanyakazi wa mgodi huo ambao wamepunjwa malipo ya mafao yao na kutolipwa mishahara kwa zaidi ya miezi 10 sasa, wanadai wamefikia hatua hiyo kutokana na ukimya wa Serikali katika kushughulia matatizo hayo.

Mbali na ukimya wa serikali, uamuzi wa wafanyakazi hao kumshinikiza mbunge wao pia unatokana na ukimya wa utekelezaji wa mapendekezo ya Kamati ya Rais iliyoundwa kuchunguza sekta ya madini iliyoongozwa na Jaji Mark Bomani, ujumbe wa Kamati ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Ludovick Utouh, pamoja na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini inayoongozwa na Mbunge wa Bumbuli, William Shellukindo.

Kwa nyakati tofauti kamati hizo zilitembelea mgodini hapo na kuzungumza na wafanyakazi na kuwaahidi kuwa matatizo yao yakiwamo ya kupunjwa malipo na kutolipwa mishahara yangepatiwa ufumbuzi wa haraka na kwamba taarifa zote zingefikishwa kwa Raia Jakaya Kikwete.

Hata hivyo, kinachowaondolea imani wafanyakazi hao ni ukimya uliotawala baada ya kamati hizo kuondoka mgodini hapo, wakiamini kuwa huenda mapendekezo ya Kamati ya Jaji Bomani na ujumbe wa CAG hayajafanyiwa kazi na wasaidizi wa Rais Kikwete ambaye wanaamini kuwa kama angeshauriwa vyema asingeweza kukaa kimya.

Raia Mwema imefanikiwa kuona barua ya wafanyakazi hao ya Aprili 15, mwaka huu yenye kumbukumbu namba TAMICO/KCP/VOL/11/0409 iliyotiwa saini na Mwenyekiti wao Daniel Kibona na Katibu wake Thomas Keyo ikiwa na saini za wafanyakazi wengine 54.

Katika barua hiyo, wafanyakazi hao wanamtaka Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, ambaye mgodi huo uko jimboni kwake, kulifikisha rasmi suala hilo bungeni kwa niaba yao , hasa baada ya kuona hata Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini nayo imekaa kimya.

Kwa mujibu wa kanuni za Bunge, katika hali kama hiyo ya shinikizo la wananchi, mbunge analazimika kuchukua maelezo ya wafanyakazi hao na kuyawasilisha bungeni kama hoja binafsi.

Barua hiyo inayomtwika mzigo huo Dk. Mwakyembe inataka kuchukuliwa kwa hatua za haraka kunusuru hali za wafanyakazi hao ambao wamedai katika barua kuwa wamekuwa ombaomba.

“Mbali na kupunjwa mafao yetu lakini mishahara ya miezi zaidi ya 10 hatujalipwa..Januari 14, mwaka 2008 Kamati ya Rais kuhusu madini iliyokuwa ikiongozwa na Jaji Bomani (Mark) ilitembelea mgodi na kushuhudia hali mbaya ya wafanyakazi na kuahidi kulifikisha suala hili kwa Rais.

“Oktoba 20, mwaka 2008, ujumbe maalumu wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ukiongozwa na Mama Msongwa, ulitembelea mgodi na kuridhika kuwapo kwa hali mbaya ya wafanyakazi waliahidi kushughulikia tatizo hilo na kulifikisha kwa Rais.

“Januari 17, mwaka huu, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ikiongozwa na Mbunge wa Bumbuli, William Shellukindo, ilitembelea mgodi na kushuhudia hali mbaya za wafanyakazi. Kamati hii ikaahidi kufikisha suala hili bungeni,” inaeleza barua hiyo na kuongeza kuwa;

“Mheshimiwa mbunge (Mwakyembe) pamoja na harakati zote hizo hakuna chochote kilichofanyika. Hali za wafanyakazi zinazidi kuwa mbaya..wafanyakazi wamechakaa mithili ya ombaomba.

“Wameshindwa kulipa ada na michango mingine ya shule kwa ajili ya watoto wao. Wapo watoto 107 wa kidato cha nne katika Sekondari ya KCM na sekondari nyingine ambao wameshindwa kulipiwa ada za mitihani kutokana na wazazi wao ambao ni wafanyakazi wa mgodi kukosa fedha hizo.”

Katika kuonyesha kukerwa na hali hiyo pamoja na ukimya wa Serikali, wafanyakazi hao wamesema; “Tumekuwa kama watumwa katika nchi yetu tusiokula matunda ya uhuru wa nchi yetu. Hii si haki hasa pale mgodi unapokuwa unamilikiwa na Serikali kwa ubia.

“Uvumilivu sasa umetushinda tumeamua kutembea kwa miguu kutoka Kiwira kwenda kumwona Rais tukaeleze wenyewe inawezekana timu zote zilizotembelea mgodi hazikufikisha ujumbe. Heri kufia njiani kuliko kufia kitandani, ” inaeleza sehemu ya barua ya wafanyakazi hao.

Katika mkutano uliopita wa Bunge, suala la Kiwira lilijitokeza japo si kwa uwazi na zaidi likiwa ndani ya wigo wa Kamati ya Nishati na Madini, ambaye ilitembelea mgodi huo pamoja na kuzungumza na wafanyakazi.

Gazeti hili liliwahi kuandika kuwapo kwa hali ya shinikizo la kutaka mgodi huo urejeshwe serikalini na wafanyakazi hao walipwe stahili zao zote.





Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa
Iliripotiwa pia na gazeti hili kwamba zilikuwapo juhudi za wazi za kuibana Serikali kiasi cha kulazimika kuanza kufikiria uamuzi wa kisheria na hata kutafakari fursa ya kumwondolea kinga Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, au kutafuta uwezekano wa kumhoji kuhusu mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira mkoani Mbeya, anaodaiwa kuwa na maslahi binafsi kupitia kampuni ya ANBEM na hata wanafamilia wake.

Kutokana na hali hiyo na hasa kile kinachobainika kuwa Bunge kupitia Kamati yake ya Nishati na Madini kuridhishwa na ushahidi katika nyaraka hizo, Bunge limetajwa kudhamiria kuibinya Serikali katika mambo makuu mawili.

Jambo la kwanza ni kushinikiza mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira kurejeshwa serikalini kutokana na sababu kadhaa lakini kubwa zaidi ni wawekezaji wanaopaswa kuendesha mgodi huo kubainika kuwa ni wababaishaji walioshindwa kutekeleza ahadi zao kwa Serikali.

Kati ya mambo yanayodhihirisha kuwa mwekezaji huyo kushindwa kuendesha mradi wa uzalishaji umeme kwa kutumia makaa ya mawe katika mgodi huo ni kushindwa kuwalipa stahili zao wafanyakazi wa mgodi, ambao hadi Kamati ya Bunge inatembelea mgodi huo, walikuwa wakidai mishahara mipya iliyotangazwa na Serikali kwamba kima cha chini kwa sekta ya madini ni Sh 350,000.

Kamati hiyo pia ilibaini kuwa mwekezaji huyo alishindwa kulipa mishahara waliopanga ambayo ni kima cha chini kuwa Sh 60,000 kwa muda wa miezi takriban nane sasa.

Lakini kubwa zaidi ni wawekezaji hao kushindwa kuzalisha umeme kwa mujibu wa makubaliano kati ya kampuni hiyo na Serikali kupitia TANESCO.

Kabla ya kubinafsishwa mgodi huo ulikuwa ukizalisha megawati 6 zilizokuwa zinaingizwa katika gridi ya taifa, lakini baada ya kampuni ya TanPower Resources Ltd kupewa mgodi walitakiwa wazalishe megawati 200 katika awamu mbili.

Awamu ya kwanza ilikuwa izalishe megawati 50 ifikapo Julai 2007 na uzalishaji wa megawati 150 zilizosalia ukamilike Machi, mwaka huu. Taarifa za uhakika zinabainisha kuwa hakuna chochote kilichofanyika hadi sasa na hasa ikizingatiwa kuwa awali umeme ulikuwa ukisambazwa na kutumika katika wilaya za Kyela, Ileje na Rungwe.

Kwa sasa inaelezwa kuwa uzalishaji umeme katika mgodi huo umeshuka kutoka megawati 6 za awali kabla ya ubinafsishaji hadi megawati moja na hivyo kusababisha matatizo ya umeme katika wilaya hizo tatu. Sababu hizi na nyinginezo ndizo chanzo cha Bunge kuweka shinikizo mgodi huo urejeshwe serikalini kutoka mikononi mwa mwekezaji huyo.

Jambo la pili ambalo Bunge linaweza kufanya ni kuishinikiza Serikali kumhoji Mkapa au hata kufungua milango ya kumwondolea kinga ya kushitakiwa.

Kama Serikali itashindwa kuridhia kufungua milango ya kumwondolea kinga ya kushitakiwa, basi Bunge limekusudia kuweka shinikizo kwamba Mkapa ahojiwe ili akiri au la kuliko kuacha mambo yabaki ‘hewani’ kama nchi haina uongozi.

Kwa mujibu wa tathmini ya mwaka 1998, mgodi ulikuwa na thamani ya Sh bilioni 4.2, wakati tathmini iliyowahi kufanywa mwaka 1991 na Taasisi ya Ardhi inaonyesha kuwa mgodi ulikuwa na thamani ya Sh bilioni saba.

Lakini katika ziara yake Januari mwaka huu, mgodini hapo, Kamati ya Bunge ilibaini kuwa pamoja na tathmini hiyo kufanyika, licha ya kwamba ilifanyika miaka mitano kabla ya kubinafsishwa, kamati ilishindwa kuelewa ni vigezo gani vilitumika kutupilia mbali uthamini huo na kuamua kuuza hisa kwa gharama ya Sh milioni 700 tu.

Habari zaidi zilizotufikia zinaeleza kuwa wakati wa ziara hiyo, Kamati hiyo ya Bunge ilipokea taarifa mbili zinazogongana kuhusu umiliki wa hisa za mgodi huo. Kilichobainika ni kwamba taarifa ya mwekezaji kudai kuwa amenunua hisa asilimia 70, Serikali asilimia 12 na nyingine asilimia 18 hazijanunuliwa.

Taarifa hiyo inadaiwa kugongana na ile ya wafanyakazi iliyotolewa kwa Kamati hiyo ya Bunge. Taarifa hiyo ya wafanyakazi inaeleza kuwa mwekezaji anamiliki asilimia 85 na Serikali asilimia 15.

Kutokana na mkanganyiko huo, kamati hiyo ilitoa taarifa yake iliyobainisha kuwa wajumbe wa kamati wameshindwa kuelewa juu ya utata wa umiliki huo wa hisa na wamelazimika kukusudia kuiomba Serikali ieleze wazi kuwa inamiliki hisa asilimia ngani.

Kubwa jingine lililogunduliwa na Kamati hiyo ya Bunge mgodini Kiwira ni taarifa ya mwekezaji kuonyesha kuwa Serikali ilitenga Sh bilioni 17 kwa ajili ya ukarabati, kabla ya ubinafsishaji kufanyika lengo likiwa ni kukarabati mitambo yote ya uzalishaji iliyotajwa kuwa ilikuwa imechakaa.

Hata hivyo, kamati ilipigwa na butwaa baada ya kuelezwa na wafanyakazi kuwa hakuna ukarabati wowote uliofanyika na zaidi ni kwamba jenereta moja ya kuzalisha umeme imechakaa na haifanyi kazi, wakati jenereta ya pili ina uwezo wa kuzalisha si zaidi ya megawati moja tu.

Mgodi wa makaa ya mawe Kiwira uliopo katika wilaya tatu za Rungwe, Ileje na Kyela, ulianzishwa kwa msaada wa kifedha na ufundi kutoka Jamhuri ya Watu wa China na ulizinduliwa rasmi na Rais wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi, Novemba mwaka 1988.

Mgodi huo unatajwa kuwa na uwezo wa kiusanifu wa kuzalisha makaa ghafi ya tani 150,000 kwa mwaka. Kiwango hicho cha uzalishaji hata hivyo kinaweza kuongezwa hadi tani milioni moja kwa mwaka. Makaa hayo hutumika kuzalisha umeme.
 
Mkapa ameshashauriwa arudishe jamani huu mgodi kwani nini lakini???ni aibu sasa.watu wanateseka jamani watanzania wenzetu wananyanyasika miezi 10 wanaishije??
 
Mkapa ameshashauriwa arudishe jamani huu mgodi kwani nini lakini???ni aibu sasa.watu wanateseka jamani watanzania wenzetu wananyanyasika miezi 10 wanaishije??

Halafu huyu mtu ni kwamba anakula bure, anasafiri bure, anatibiwa bure, hospitali yeyote ile duniani, ana wapishi, madereva na magari, wabeba briefcase, shamba boi, house boi, ana mshahara kama wa Kikwete almost, nyumba ya bure anapewa I'm sure, wachunga ngo'mbe, wafua nguo za ndani... bure.

Lakini bado na mgodi wa wizi lazima awe nao...
 
Tatizo la Dr. Mwakyembe alipata nafasi ya kufanya vitu bungeni akaficha kwa kuogopa kupindua serikali, sasa hivi hata akisema mkapa atasema ni sababu ya conflict of interest, alitakiwa hivi hawe amevisema alipopewa nafasi kwenye kamati na sio kusema kidogo, sasa watu wavitumia kumkaanga yeye.
 
Sasa hivi neno "bomu" si zuri sana kulitumia, hasa baada ya tukio la Mbagala.Unaweza kupandisha watu pressure bure.
 
Halafu huyu mtu ni kwamba anakula bure, anasafiri bure, anatibiwa bure, hospitali yeyote ile duniani, ana wapishi, madereva na magari, wabeba briefcase, shamba boi, house boi, ana mshahara kama wa Kikwete almost, nyumba ya bure anapewa I'm sure, wachunga ngo'mbe, wafua nguo za ndani... bure.

UMESAHAU ANA MABIBI WA BURE
 
Back
Top Bottom