MWAKA WA SHETANI,NANI ALAUMIWE?Hakika mungu wetu kaamua kutupigania watzAmeonyesha kuwa kumbe anajiamini na anaweza kusema ukweli hata kama ataonekana mbaya.
Pili Mbunge wa Nkasi Poniano Nyami amesema kuwa ataleta hoja binafsi Bungeni kama serikali haitatoa majibu ya kuridhisha kuhusiana na SPM mgololo -kwa wale waliosoma hoja ya Dr.Slaa mtakumbuka hili la SPM.
lets wait another man is coming in front.........
Mimi bado sijaona cheche zozote kwenye kauli za Kimaro.
Alichosema hakina tofauti na alichosema Mama Killango na Anna Abdallah...Kwamba pesa zirudishwe na pia kuna wanaopinga ufisadi ila kwa upole!
Hata hivyo ni siasa tu!
Kwani at the same time ameongea maneno ya Anna Abdala kwamba kuna wabunge wasiozungumza kwa ukali ila na wao wanapinga ufisadi!
Kwa maana hiyo ujumbe wake ni wa kuwaunganisha ccm esp baada ya Killango na Anna Abdallah kulumbana...Mmoja akisema pesa zirudishwe kama alivyosema Kimaro...Na mwingine akisema kuna wale wanaojidai wanauchungu kwa kuzungumza kwa ukali kama alivyosema Anna Abdallah na Kimaro kusema the same!
Kwa kifupi Kimaro ni Kilabdallah!
Kwamba yeye ni nusu killango na nusu Anna Abdalla!
Politics and more politics!
Ushahidi uko wazi...Atakayesema MAFISADI WAKAMATWE NDIYE WA KUUNGWA MKONO!
Ni ushauri tu.
mwaka huu bungeni kumoto
huenda sasa watu wakaanza kuogopa kugombea ubunge.
ilikuwa ishaanza kuhesabika ubunge ni kula tu sasa kazi ipo
Subira yavuta heri! Pamoja na kuwa CCM kuwa chama cha mafisadi bado kuna baadhi yao humo ni wazuri na kila wanapofanya juhudi za kutetea maslahi ya nchi ni lazima tuwapongeze badala ya kuwakatisha tamaa. Kuwakatisha tamaa kutawafanya hata wale wanaotaka kuingia upande wakutetea maslahi ya nchi kufikiria mara mbili mbili kama siyo mara 10 10, maana watasema angalia fulani na fulani walizungumza hapa bungeni kutetea maslahi ya Watanzania lakini hawakupata support yoyote toka kwa wananchi bali Watanzania waliwazodoa tu!! Kuwa na subira!
mmh Sijui Ila Hawa Star Tv Huwa Mara Nyingi Hawaonyeshi Bunge Jioni.wakuu, Heshima Mbele.
Nimekua Mfuatiliaji Wa Hii Forum Kwa Muda Mrefu Kama Observer, Lakini Hali Ya Taifa Ilipo Imenilazimu Nianze Kuchangia Huu Mjadala.
Huyu Mheshimiwa Inaonekana Amekua Mwiba... Binafsi Leo Nimeshuhudia Matangazo Live Ya Bunge Kupitia Tbc1 Yakikatishwa Wakati Alipokua Anashusha Makombora Around Saa Moja Na Dakika Kumi Hivi Jioni Na Badala Yake Yakawekwa Matangazo. Ilianza Kuzimwa Camera Wakati Yeye Anaongelea Issue Ya Tanzanite Sorting, Sauti Ikabaki. Then Wakakata Na Sauti Yake.
After About Fifteen Minutes, Matangazo Ya Bunge Yakarudi Tena Live Tbc1. Wakati Tbc1 Haipo Hewani, Hata Star Tv Nao Hawakua Wakionesha Bungeni Live.
To Me It Was More Than A Coincidence. Lakini Nimeogopa Kua Judgemental On Tbc1.
Wanaofaham Zaidi Wanaweza Kutusaidia Nini Haswa Kilitokea.
Kama kuna mtu ana video hizo awasiliane nami na tutasaidia jinsi ya kuziupload ili watu wengine waweze kuziona. Sijui ilikuwaje TV zetu zote tatu zilizokuwemo kwenye JumpTV zikaamua kuchomoa zote! Labda waliona tunafaidi sana.
Kama kuna mtu ana video hizo awasiliane nami na tutasaidia jinsi ya kuziupload ili watu wengine waweze kuziona. Sijui ilikuwaje TV zetu zote tatu zilizokuwemo kwenye JumpTV zikaamua kuchomoa zote! Labda waliona tunafaidi sana.
We the PEOPLE or "Yuo" to be specific...Said the same thing during Killango's statements!
And i told you guys to be sceptical!
TRUST BY VERIFY!
Niki verify statements zake sioni jipya!
Hata hivyo kama tulivyofanya kwa Killango..Then ni wazi tutafanya tena kwa Kimaro!
However...We should be aware that time is running out na bado fisadi hajaguswa!
Mush,kama ungekuwepo Bungeni ukasikia na tone ya Kimaro, ninaamini ungekwua na mawazo tifauti kwa sababu alichokisema ukikisikia moja kwa moja kina tofauti sana na hiki tunachokiandika ili wenzetu mlio nje muelewe kinachoendelea.
Pia, ukioanisha maneno ya Kimaro jioni na yale yaliyosemwa na Mzindalaya asubuhi (ipo thread yake niliianzisha) utabaini kuwa there is something going on.
Pia juzi Naibu Spika alitamka ndani ya Bunge kuwa katika kipindi hiki kilichosalia hadi uchaguzi mkuu "MOTO UTAWAKA BUNGENI".
Nadhani kwa pamoja, kauli hizi na mambo mengine yanayotokea, yanaashiria kitu fulani kikubwa ingawa hakijafika katika level ambayo wewe unaitaka(ya Mkapa kuguswa moja kwa moja au kukamatwa). Lakini nikipima hali ya mambo hapa, nadhani ni suala lamuda tu, tutafika hukohuko unakokuzungumza wewe.
Mush,kama ungekuwepo Bungeni ukasikia na tone ya Kimaro, ninaamini ungekwua na mawazo tifauti kwa sababu alichokisema ukikisikia moja kwa moja kina tofauti sana na hiki tunachokiandika ili wenzetu mlio nje muelewe kinachoendelea.
Pia, ukioanisha maneno ya Kimaro jioni na yale yaliyosemwa na Mzindalaya asubuhi (ipo thread yake niliianzisha) utabaini kuwa there is something going on.
Pia juzi Naibu Spika alitamka ndani ya Bunge kuwa katika kipindi hiki kilichosalia hadi uchaguzi mkuu "MOTO UTAWAKA BUNGENI".
Nadhani kwa pamoja, kauli hizi na mambo mengine yanayotokea, yanaashiria kitu fulani kikubwa ingawa hakijafika katika level ambayo wewe unaitaka(ya Mkapa kuguswa moja kwa moja au kukamatwa). Lakini nikipima hali ya mambo hapa, nadhani ni suala lamuda tu, tutafika hukohuko unakokuzungumza wewe.
Akumbushia ahadi za mwana TANU.
Asema kuwa rushwa ni adui wa haki, asema kuwa ahadi zile ni muhimu na kila mbunge ameapa kuzilinda .
Asema wabunge wawe mstari wa mbele kupiga vita Ufisadi.
asema kuwa watanzania hawakuamini kuwa pesa za EPA ziliibiwa mpaka pale rais aliposema kuwa ziliibiwa na ni lazima wamuunge mkono kuhakikisha kuwa pesa hizo zitarudishwa.
anasema kuwa kuna watu wanasema kuwa kuna watu wanapayuka ,na hata wakipayuka ni haki yao na hata kama Microfone zikipasuka spika ataweka nyingine .
Asema kuwa kama wengine wanaongea kwa upole ,waseme maneno ya busara na yawaingie mafisadi mpaka rohoni mwao.
Asema kuwa kuna wabunge wanathubutu kuwatetea mafisadi ,hii ni aibu.
Asema kuwa nchi hii sio masikini na kama waarabu na mafuta yao basi sisi na madini yetu na hao wazungu wanaokuja hapa hawaji kutufanyia kazi,ila wanafanya kazi zao.
Asema kuwa hakuna usimamizi wa Tanzanite kwani hakuna anayehakikisha kuwa zinapatikana kiasi gani.
Alitembelea migodi ya Mererani na kukuta kuwa watanzania wanateseka sana kwani hata wakati wa kuchambua Tanzanite mikono yao inakuwa imefungwa na hata kama wakiwashwa hawawezi hata kujikuna .
Ataka ripoti ya tume ya Jenerali Mboma bungeni kuhusu kutatua mgogoro wa Kitalu B na C.
Amtaka waziri mkuu kupiga marufuku ununuzi wa fenicha kutoka nje ya nchi kwani hapa kwetu hatuna tatizo la mbao na hivyo akifanya hivy serikali itawekeza nchini kwani ndio wanunuzi wakubwa wa fenicha.
anaendelea kusema kuwa madukani kuna bidhaa feki nyingi sana asema kuwa waziri mkuu anatakiwa kulitupia macho.
Ununuzi wa magari ya serikali lazima yawe yananunuliwa kwenye pull na sio kila mmoja kujinunulia la kwake .