Kusema ukweli nchi ya Rwanda ni nzuri sana

Kusema ukweli nchi ya Rwanda ni nzuri sana

Hii hoja ya kwamba ni nchi ndogo mi wala sijawahi elewa mantiki yake ni nini?kwani hata kama wewe una nchi kubwa basi si hata resources ulizokua nazo zinalingana na eneo lako sasa kama vyote ni direct proportional kwanini usifanye maendeleo according to your resources?
Hoja yako ingekuwa na nguvu kama Rwanda tungelingana kwenye maeneo au Rwanda ingekuwa inaeneo kubwa kuliko Tz halafu inamiundombinu mizuri kila eneo..uchumi na pato zuri la kila raia na kukua kwa kasi ya 4G kuliko Tz..hapo sasa tungejitizama marambili mbili kwanini Rwanda wametuzidi kila kitu? ukubwa wa nchi hata maendeleo hali sisi tuna eneo dogo halafu tupo nyuma...
 
Ishu sio umaskiini Wala pato, ishu ni discipline na accountability, TZ chukulia mfano ripot ya CAG japo imepikwa madudu still yapo lakini hakuna anayejali, kosa kubwa LA dunia ambalo limefanyika TZ ni kuvuruga mahakama na bunge wallah hayo ni majuto makubwa kabisa Kwa watu wenyewe akili wanaofikiria mbali, hatuwezi kutoboa kamwe Kwa namna hii
Wenzako ndio Wana enjoy kwamba baada ya kuvuruga Bunge na Mahakama ndio wamepata unafuu wa kutawala na kudhibiti
 
Rwanda siyo nchi ndogo. Kieneo sawa ni ndogo. Lakini ina watu milioni 14. Imepita nchi nyingi kubwa kwa eneo kama Namibia na Botswana. Pia makazi ya wananchi na muonekano wao hawaonyeshi huo umasikini wa kutupwa. Hata kwenye slums na vijijini watu wanaonekana wana sura za 'matumaini'. Na hata kipato hatujapishana sana. Wao wana pato la mtu wastani dola 1,000 na sisi dola 1,300.
kieneo sawa ni dogo..Tuishie hapa.
 
Rwanda siyo nchi ndogo. Kieneo sawa ni ndogo. Lakini ina watu milioni 14. Imepita nchi nyingi kubwa kwa eneo kama Namibia na Botswana. Pia makazi ya wananchi na muonekano wao hawaonyeshi huo umasikini wa kutupwa. Hata kwenye slums na vijijini watu wanaonekana wana sura za 'matumaini'. Na hata kipato hatujapishana sana. Wao wana pato la mtu wastani dola 1,000 na sisi dola 1,300.
Usiongee upuuzi nenda kibeho huko wanakula hadi mizizi.
 
Hii hoja ya kwamba ni nchi ndogo mi wala sijawahi elewa mantiki yake ni nini?kwani hata kama wewe una nchi kubwa basi si hata resources ulizokua nazo zinalingana na eneo lako sasa kama vyote ni direct proportional kwanini usifanye maendeleo according to your resources?
Excuse ya viongozi wetu na watetezi wao.
 
Si uhamie huko?likianza tarumbeta huko utakesha unakatika tu.
Pazuri mjini tu hapo Kigali.
Nenda kule kwa hutu,na batwa wanaishi km sokwe
Miji yote mizuri. Nimeangalia Gisenyi na Musnze, miji inayofuatia kwa ukubwa, ni miji standard hasa. Vijijini watu wana ndizi na chai na ng'ombe. Pengine vijiji vyetu watu masikini kuliko huko Rwanda vijijini.
 
Miji yote mizuri. Nimeangalia Gisenyi na Musnze, miji inayofuatia kwa ukubwa, ni miji standard hasa. Vijijini watu wana ndizi na chai na ng'ombe. Pengine vijiji vyetu watu masikini kuliko huko Rwanda vijijini.
Ushafika Kiwira wewe?Hiyo wilaya ya Rungwe inalisha hiyo Nchi miaka,
Hapo hatujaja Tokyo,Kyela ,Uporoto,Swaya,Songwe,Chunya,Utengule,Ileje,Mbozi kwa mwashambwa, Makambako
Hako kanchi unakabeba kwa mbeleko tu.
Kuna ndizi Mbeya wanakula Nguruwe,na sijui km unazijua mkono wa tembo?
Ndizi moja mnakula ukoo mzima.
 
Nimekuwa nafuatilia video za nchi ya Rwanda, hata za huko vijijini. Kwa kweli hii ni nchi nzuri sana. Baada ya miaka kumi ikiendelea hivi itakuwa muonekano wa nchi za Ulaya hata kuzidi.

Kila kitu unaona kimepangwa na wapangaji wanaojali watu wao. Mambo yote yanaonyesha kuwa kuna order.
Nimejifunza kuwa ukidhibiti rushwa kila mtu ndani ya nchi anaamka na kufanya mambo kwa manufaa ya wote. Rushwa inavunja moyo wenye nia ya kuendeleza nchi.


Taifa lolote lenye Rais Genius, Wananchi Genius na Kabila Genius kama la Tutsi (Tanzania ni la Wazanaki) kamwe haliwezi kuwa baya kama moja hivi la Jirani lenye Wapumbavu tokea juu mpaka chini.

Long live Rwanda
Long live President Kagame
Long live Rwanda Citizens
Long live Zanaki Tribe in TZ
Long live Tutsi Tribe in Rwanda
Long live GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE
 
Hoja yako ingekuwa na nguvu kama Rwanda tungelingana kwenye maeneo au Rwanda ingekuwa inaeneo kubwa kuliko Tz halafu inamiundombinu mizuri kila eneo..uchumi na pato zuri la kila raia na kukua kwa kasi ya 4G kuliko Tz..hapo sasa tungejitizama marambili mbili kwanini Rwanda wametuzidi kila kitu? ukubwa wa nchi hata maendeleo hali sisi tuna eneo dogo halafu tupo nyuma...
Sijui umeelewa mantiki ya hoja yangu,nasema hivi hata kama sisi tuna eneo kubwa la km za mraba kuliko rwanda basi hata resorces tulizokua nazo zinalingana na ukubwa wa eneo letu,sasa kwanini tunashindwa kufanya maendeleo yanayofanana na utajiri tuliokua nao?kwamba sisi pekee duniani ndo tuna eneo kubwa la km za mraba na ndio maana maendeleo inakua mtihani kuliko nchi ndogo? acheni kumeza mawazo mfu ya wanasiasa wetu ambao pamoja na exposure yote waliyokua nayo lakini wameshindwa kujifunza kwa wenzetu waliofanikiwa.
 
Fatilia na pato la kila raia..Nchi ipo vizuri kimiundombinu lakin raia ni masikini wakutupwa..halafu Rwanda ni nchi ndogo sana ni sawa na Mkoa mmoja wapo wa Tz.
Dar ni ndogo mbona haina Miundombinu Bora ?

Somalia ni nchi ndogo mbona imejaa umasikini ?

Burundi ni nchi ndogo mbona imejaa umasikini ?


Toeni pongezi Kwa nchi ya Rwanda
 
Sijui umeelewa mantiki ya hoja yangu,nasema hivi hata kama sisi tuna eneo kubwa la km za mraba kuliko rwanda basi hata resorces tulizokua nazo zinalingana na ukubwa wa eneo letu,sasa kwanini tunashindwa kufanya maendeleo yanayofanana na utajiri tuliokua nao?kwamba sisi pekee duniani ndo tuna eneo kubwa la km za mraba na ndio maana maendeleo inakua mtihani kuliko nchi ndogo? acheni kumeza mawazo mfu ya wanasiasa wetu ambao pamoja na exposure yote waliyokua nayo lakini wameshindwa kujifunza kwa wenzetu waliofanikiwa.
Achana na hao wapumbavu wanaotumia size ya nchi kama kigezo cha nchi kuendelea. Burundi ni nchi ndogo ila ni masikini.


Somalia ni nchi ndogo ila Haina lolote la maana


Eritrea ni nchi ndogo pia ila imejaa umasikini.


KAma kigezo cha udogo wa nchi ndio ingekuwa sababu ya nchi kuendelea basi Burundi, somalia au Eritrea ingebidi ziwe na maendeleo pia.
 
Sijui umeelewa mantiki ya hoja yangu,nasema hivi hata kama sisi tuna eneo kubwa la km za mraba kuliko rwanda basi hata resorces tulizokua nazo zinalingana na ukubwa wa eneo letu,sasa kwanini tunashindwa kufanya maendeleo yanayofanana na utajiri tuliokua nao?kwamba sisi pekee duniani ndo tuna eneo kubwa la km za mraba na ndio maana maendeleo inakua mtihani kuliko nchi ndogo? acheni kumeza mawazo mfu ya wanasiasa wetu ambao pamoja na exposure yote waliyokua nayo lakini wameshindwa kujifunza kwa wenzetu waliofanikiwa.
Huyo uliyemjibu hii reply ni moja ya watanzania wenye ufahamu mdogo sana kuhusu maendeleo ya Taifa kwa ujumla, angalia hapo kwenye comment yake ya kwanza amekimbilia kusema eti Rwanda ni taifa la mafukara, wakati mada inazungumzia hasa mandhari na mpangilio wa miundo mbinu.

Kwake yeye anaamini mtu mmoja mmoja akiwa na pesa ya kuhonga na kunywa bia ndio maendeleo yenyewe hayo, kwake yeye maendeleo anayoyatambua ni ya mtu mmoja mmoja kumiliki pesa basi.

Angalia hata Id yake anajiita "MONEY IS EVERYTHING" ina reflect fikra zake, na mara nyingi watu kma hawa wakipewaga kitengo wanakuwaga ni wezi na wabinafsi wakubwa.
 
Huyo uliyemjibu hii reply ni moja ya watanzania wenye ufahamu mdogo sana kuhusu maendeleo ya Taifa kwa ujumla, angalia hapo kwenye comment yake ya kwanza amekimbilia kusema eti Rwanda ni taifa la mafukara, wakati mada inazungumzia hasa mandhari na mpangilio wa miundo mbinu.

Kwake yeye anaamini mtu mmoja mmoja akiwa na pesa ya kuhonga na kunywa bia ndio maendeleo yenyewe hayo, kwake yeye maendeleo anayoyatambua ni ya mtu mmoja mmoja kumiliki pesa basi.

Angalia hata Id yake anajiita "MONEY IS EVERYTHING" ina reflect fikra zake, na mara nyingi watu kma hawa wakipewaga kitengo wanakuwaga ni wezi na wabinafsi wakubwa.
hahahahahahaha !! Ndugu kwanin usiende kuishi huko? Hali yakuwa maendeleo ya nchi yako huyaoni..Unadhani TZ ya miaka 1990 ndo ya leo? Unaejiona unaupeo wa kufikiri umeisaidia nini nchi yako kutokana na uwezo wako wa kufikiri..kwani huyaoni au unajifanya kipofu.
 
Huyo uliyemjibu hii reply ni moja ya watanzania wenye ufahamu mdogo sana kuhusu maendeleo ya Taifa kwa ujumla, angalia hapo kwenye comment yake ya kwanza amekimbilia kusema eti Rwanda ni taifa la mafukara, wakati mada inazungumzia hasa mandhari na mpangilio wa miundo mbinu.

Kwake yeye anaamini mtu mmoja mmoja akiwa na pesa ya kuhonga na kunywa bia ndio maendeleo yenyewe hayo, kwake yeye maendeleo anayoyatambua ni ya mtu mmoja mmoja kumiliki pesa basi.

Angalia hata Id yake anajiita "MONEY IS EVERYTHING" ina reflect fikra zake, na mara nyingi watu kma hawa wakipewaga kitengo wanakuwaga ni wezi na wabinafsi wakubwa.
Nenda huko ukaishi kama huoni maendeleo ya nchini kwako sahv barabara za lami kila kona..huduma za afya mpaka ngazi ya kata..maji japo yakusua ila yapo..umeme mpaka vitongojini..n.k. TZ ya 1990 ndo unaiyona leo? Au ndo wale wa 2000 msiojitambua mmekuta kila kitu kipo..halafu ningekuona unaakiri zaidi kama ungeweka mlinganisho hapa.
 
Rwanda siyo nchi ndogo. Kieneo sawa ni ndogo. Lakini ina watu milioni 14. Imepita nchi nyingi kubwa kwa eneo kama Namibia na Botswana. Pia makazi ya wananchi na muonekano wao hawaonyeshi huo umasikini wa kutupwa. Hata kwenye slums na vijijini watu wanaonekana wana sura za 'matumaini'. Na hata kipato hatujapishana sana. Wao wana pato la mtu wastani dola 1,000 na sisi dola 1,300.
Mbona wabongo ndo maskini wa kutupwa kuliko hao Wanyarwanda. Lol
 
Back
Top Bottom