Earthmover
JF-Expert Member
- Sep 28, 2012
- 25,977
- 25,303
mkuu utaniua na kicheko bhana
....Mkuu jamaa kakimbia ukunga kule Mvomelo
mkuu utaniua na kicheko bhana
Lumumba FC mnajifanya wajuaji wa katiba ya Chadema wakati wenye katiba yao wako kimya, kamuulize traitor Mwigamba akuonyeshe kipengele cha ukomo wa uongozi kiko ibara ya ngapi.Hivi Chadema mnakiendesha chama kwa misingi ipi.
Nyie wenyewe mnasema chama chenu ni cha demokrasia, akitokea mtu kuhoji mwendendo wa matumizi ya ruzuku mnasema ni msaliti.
Mbowe kama anaungwa mkono wanachama watu wengi mbona amechakachua katiba ya chama kuhusu uchaguzi. Kwa mujibu wa Mkulima.
Kazi nzuri mwenyekiti Mbowe,wewe ni jemedari wa vita na tunakuunga mkono katika harakati zako kwakuwa Chadema iko salama ikiwa chini ya uenyekiti Wako. Wengine bado hawajajipambanua kama ni baridi au Moto!
Mkuu,
Kuna familia imewekeza pesa zake nyingi kuendesha shughuli za chama hiki. Ukiwaambia waachie uongozi utakuwa unatafuta ugomvi nao.
Chama cha wote kinajulikana.
Chadema ni chama kinachoendeshwa katika misingi ya kilaghai.
Kila anayehoji ulaghai huo anapachikwa jina la "msaliti".
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman Mbowe amesema chama hicho hivi sasa kinakumbana na viongozi wasaliti wasiojua wajibu wao wa kulikomboa Taifa.
Akihutubia kongamano la wadau na viongozi wa Kanda ya Kaskazini kiongozi huyo amesema sababu kubwa ya usaliti huo ni uroho wa madaraka kwa baadhi ya watu.
Mwenyekiti huyo anayeongoza chama kikuu cha upinzani nchini amesema kwa sasa chama hicho hakitavumilia viongozi wasaliti na badala yake watakuwa wanaelezana ukweli na kuchukua hatua stahiki kila inapobidi.
Kauli hii ya Mbowe itakuwa msumari wa moto kwa baadhi ya viongozi wanafiki na wanaotumika kutaka kuvuruga chama hicho.
Mbowe ni kiongozi ambaye anaungwa mkono na idadi kubwa ya wafuasi wa CHADEMA kote nchini kutokana na kazi kubwa anayofanya kuimarisha chama hicho kiasi ambacho Mwenyekiti wa CCM Rais Kikwete akiwahutubia watendaji wa CCM hapo jana amehofia chama chake kuondolewa madarakani kupitia sanduku la kura mwaka 2015.
Source:ITV Habari
Hatushangai 'zeMarco'...Tunajua wewe upo kundi la 'majangili' kama Chief dentist wenu mkuu...! Chadema haijawahi kufuga majangili...majangili wapo sehemu moja tu ya kisiasa duniani...ni ndani ya CCM. Wanajangili rasilimali za umma, rushwa, ufisadi, utekaji nyara, ugaidi...uporaji viwanja, uzulumati...! Sifa zote hizo, ingekuwa CDM wanabeba sifa 2 kati ya hizo tuneweza kuthamini uwezo wako wa kudadavua kama 'ulaghai'! CCM kwa sifa zote tajwa juu...bado unatoka nyumbani kila siku na kupita njiani kama mtetezi wa chama jangili kama hicho??....Mbowe anao uwezo kiuongozi kuliko viongozi wa-5 wa ngazi ya juu ndani ya CCM, ndiyo maana CCM yote inahaha kuvuruga...! Ila ukoo wa panya...wote wezi! wananchi wanajua, ukoo wa majangili je?...hadi mtoto, mjukuu na kitukuu...! CCM wanajiona ni kama kambale, wote wana sharubu, hadi aliyeanguliwa leo....wezi! JK wenu kawaambia mjiandae 2015...'chali'....bora nawe jiandae tu kisaikolojia....! mwache Mbowe na uongozi wake aikomboe nchi toka kwa majangili hawa wa kimataifa!
Wewe ni miongoni mwa wanaonufaika na uenyekiti wa maisha wa Mbowe.
Chama cha Demokrasia kinapoogopa kufanya uchaguzi ujue kuna tatizo kubwa...
chiaguzi za ngazi tofauti katika chama zapaswa kufanyika,sanduku la kula litaamua nani anahitajika katika ngazi mbalimbali chamani,haiwekani mtu anashikilia nafasi miaka 10 no uchaguzi hii sio democrasia,chama cha siasa ni chama cha watu na sio cha ukoo au familia furani,ukifanyika uchaguzi hao wanaotwa wasaliti watatoweka.
Uchaguzi mnafanya lini?Lumumba FC mnajifanya wajuaji wa katiba ya Chadema wakati wenye katiba yao wako kimya, kamuulize traitor Mwigamba akuonyeshe kipengele cha ukomo wa uongozi kiko ibara ya ngapi.
For your information tumepania kuwapukutisha traitors wote hadi baba lao libaki peupe.
Uchaguzi mnafanya lini?
Thats non of your business utafanyika pale wanaChademba watakapoamua na sio maelekezo toka Lumumba.Uchaguzi mnafanya lini?
Mkuu Selungo usishangae huyo naye ni mhitimu wa chuo kikuu. Lumumba wameifanya chuo kimoja hapa nchini kuwa cha kwao.Taaluma kwao si hoja,ila ukiwa kada wa CCM utapewa alama za juu.Kiongozi!
Unahisi vipi kama ungerudi darasani kwa miaka mingine mitatu ili kujifunza kuandika sentensi fasaha? maana licha ya kuja na povu kibao, bado hau eleweki umeandika nini, eti?
Kwa hiyo una taka kusema mi-CCM ndio inapo safishia rungu, eti?
Mkuu inawezaekana Lumumba hawamtaki na vile vile asiwe na tija kwa wapigakura ( yaani wananchi, ukizingatia kwamba msingi wa yote haya ni Ikulu 2015)Chadema kamwe hakitaongozwa na mawazo kutoka Lumumba! Yule ambaye Lumumba hawamtaki ndiye atakayeongoza Chadema!
Mbona kinawanyima usingizi nyie LB7