Kuna Viongozi wasaliti CHADEMA - Mbowe

Kuna Viongozi wasaliti CHADEMA - Mbowe

Its None of your business and keep distance please!

Chadema is for Chadema only and not of your type!


Kwanza haya maneno ni ya kibaguzi sana,pil8 kwa chama chenye watu makini hakiwezi kuwa na watu wenye maneno mepesi,kashfa na ya kijinga kama haya yako,maneno yako haya yanawakatisha tamaa wale watu wenye mawazo ya kujiunga na chadema,na chama chochote kile lazima kwenye katiba yake kiwe na mkakati wa kuongeza idadi ya wanachama!acha umbumbu na ukabila!
 
Patient is the key kwa sababu viongozi wasaliti na waongo wanakuja kwa njia nyingi.

Jf in akisima cha mambo yote na ukweli wa watu waongo na wasaliti mara nyingi hujitokeza kama ukivyojitokeza kwenye hii thread.

Gonga hapa upate ukweli mwingine,

https://www.jamiiforums.com/complai...afanuzi-kutoka-kwa-mods-na-uongozi-wa-jf.html

Wakilalamika zaidi wanaweza kupatiwa muda kama ilivyotokea kwenye hii thread,

https://www.jamiiforums.com/jamii-i...iri-ya-mwenendo-wa-zitto-iliyopo-chadema.html

Hii ndiyo JF ambayo ukweli wote hupatikana kwa njia ya keypad/keyboard.
 
chiaguzi za ngazi tofauti katika chama zapaswa kufanyika,sanduku la kula litaamua nani anahitajika katika ngazi mbalimbali chamani,haiwekani mtu anashikilia nafasi miaka 10 no uchaguzi hii sio democrasia,chama cha siasa ni chama cha watu na sio cha ukoo au familia furani,ukifanyika uchaguzi hao wanaotwa wasaliti watatoweka.

Mkuu una haki zaidi ya asilimia 100 kutoa mawazo yako. Na ni kweli unayoyawaza. Lkn nduguyangu angalia haya:
1. kwa sasa na hapo baadae hali ya CDM itakuwa ngumu tunaelekea ktk chaguzi mbalimbali. hivyo inawezekana hawa viongozi wakahairisha uchaguzi ili kuangalia na hali halisi ilivyo. Cha muhimu ni kuwataarifu wanachama wake.
2. Ifahamike kuwa kama kweli ni kutaka kukinusuru chama maana maadui ni wengi (kila kona ya nchi hii) basi hata inawezekana uchaguzi ukasogezwa nyuma. hii isiwe kisingzio tu cha kusema chama ni cha watu fulani!!!
3. Ikumbukwe ndani ya chama kuna viruses wachache ambao madhara yake hatuyajui yataleta nini!!!
Kwa hiyo kulaumu ni rahisi lkn kumbe hali ni ngumu kuliko unavyofikri! subira uvuta kheri!!!!!!!!!!!!
 
chadema si mtu ni taasisi kama kuna yoyote anaenda kinyume na nia thabiti ya kukipeleka chama mbele aondolewe mara moja regardless yeye ni nani hata kama alikua tunampenda sana huko nyuma!!!!
 
jibu mwanana. hata kama uchaguzivungefanyika leo.itakuwacni upuuzi mkubwa kuendesha uchaguzi kwa shinikizo la wasaliti wapenda madaraka ,"na mawakala wa wakoloni weusi..........safari ya kuusaka ukomboz itaongozwa na watu wanaoaminika kwamba wanaamini ktk ukomboz..sio wapuuzi na wazandiki wanaomini katika usaliti huku wakijipambanua kinafiki kuwa wanamujumuhi wa Afrika ( Pabafricanist).

kitu muhm kutambua ni kwamba si lazima uwe mwenyekiti wa chamaili uweze kuleta mabadiliko makubwa ktk nchi. kama kyk nafas uliyopo unaongoza usaliti tukikupa uenyekiti bila shaka utaongoza mkakati mpana wa kuviza mapambano ya ukombozi na kuua hamasa ya umma kutafuta uhuru uliotekwa nyara na wasaliti wa nchi.... WATU HAWA NI AINA YA wasaliti walioiangusha na kuisambaratisha URUSI

We can easily give in to the evil forces of traitors. we must soldier on these revelations are ttue signs whch indicate tht victory against the betrayors of our independence is close to realization...History of our struggle for second liberation will keep record of their betrayal of the very course of freedom fighting...

inaumiza sana kuona kuna watu badala ya kuongeza nguvu ili tuikamilishe safari kwa kishindo kikubwa, wao wako busy kutafuta umaarufu binafsi na kufanya kila hila kukwamisha mapambano...historia itatunza kumbukumbu ya vitendo vyao..

Hakuna sababu ya kuwa na viongozi wasaliti, binafsi natambua mchango was Freeman katika mageuzi ya nchi hii. Mwigamba hata M4C anakwambia alianzisha yeye so walianzisha wao
 
Chadema ni chama kinachoendeshwa katika misingi ya kilaghai.

Kila anayehoji ulaghai huo anapachikwa jina la "msaliti".

Ze mako kukaza misuli ya shingo hapa jf kutakufanya uende haja kubwa kwemye chupi bure, cheameni wenu keshasema hali ni mbaya wewe bado unafikiri kuna wa kumbadilisha mawazo jf
 
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman Mbowe amesema chama hicho hivi sasa kinakumbana na viongozi wasaliti wasiojua wajibu wao wa kulikomboa Taifa.

Akihutubia kongamano la wadau na viongozi wa Kanda ya Kaskazini kiongozi huyo amesema sababu kubwa ya usaliti huo ni uroho wa madaraka kwa baadhi ya watu.

Mwenyekiti huyo anayeongoza chama kikuu cha upinzani nchini amesema kwa sasa chama hicho hakitavumilia viongozi wasaliti na badala yake watakuwa wanaelezana ukweli na kuchukua hatua stahiki kila inapobidi.

Kauli hii ya Mbowe itakuwa msumari wa moto kwa baadhi ya viongozi wanafiki na wanaotumika kutaka kuvuruga chama hicho.

Mbowe ni kiongozi ambaye anaungwa mkono na idadi kubwa ya wafuasi wa CHADEMA kote nchini kutokana na kazi kubwa anayofanya kuimarisha chama hicho kiasi ambacho Mwenyekiti wa CCM Rais Kikwete akiwahutubia watendaji wa CCM hapo jana amehofia chama chake kuondolewa madarakani kupitia sanduku la kura mwaka 2015.

Source:ITV Habari

Uongo na porojo tu, angekuwa yu mkweli si angewataja!

My take; ambae si wa Kaskazini yeyote ni msaliti.
 
Mbowe ndiyo mroho wa madaraka ndiyo maana kamudu kubadili katiba ili aendelee kuwa mwenyekiti wa chadema.
haiingii akilini unapowaita wenzako wasaliti wakati wewe umehusika kubadili mpaka katiba ili ubaki uongozini hii ni aibu kwa mbowe na uroho wa madaraka uliokithiri.

African Politicians! Hivi Mh Mbowe anapowaita wenzake wasaliti na waroho wa madaraka, ni nani ambaye yuko katika siasa hasiyetaka madaraka yanayoambatana na uanasiasa wake? Yeye alilazimishwa kuwa mwenyekiti wa Chama hicho na je mbona sasa anawaita majina machafu wenziwe wanaodai tu taratibu za kidemokrasia ndani ya chama zifanyike. Chama chochote cha siasa ambacho kinajipambanua kuwa ni cha kidemokrasia lazima kiheshimu misingi ya kidemokrasia ambayo ni pamoja na kuwaruhusu watu kutoa maoni mbadala hata Kama huyapendi wala hayakupendezi, pia kuwapa nafasi watu kuchagua kwa mujibu wa taratibu viongozi wawatakao.

Ukianza kupindisha taratibu hizo ili usalie madarakani basi ujue wewe ndio msaliti na mroho wa madaraka.

Mtaongea yote,mtasema yote,lkn hayatakuwa na madhara kwetu maana mlishatutangazia kupitia viongozi wenu akiwamo Wasira kwamba mnataka CDM ife,nani hataki ahojiwe kuhusu ukomo wa madaraka?Muulizeni Mwigamba atawajibu jinsi demokrasia ilivyo kwrnye vikao vya chama,Muulizeni hata baraza kuu lililopita hali ilikuwaje kwa wajumbe kutoa yaliyo ya moyoni,lkn kwa hili mlilomtuma Mwigamba ni ujinga tu,na njaa,anajua kabisa taratibu zetu zilivyo,hoja zote ni kwenye vikao,malalamiko yote ni kwenye,vikao,iweje aende kwenye mitandao kama sio kutumiwa na maccm?leo hii issue imegeuka storu ya mjini,mmsahau juzi juzi tu Bukoba ilikuwaje magamba,mwenzenu wa ZNZ mmempora kadi tu kea kuwaambia msimamo wake kuhusu serikali tatu,tofauti na la Mwigamba,kwenye kikao hakusema juu ya tuhuma anamaliza kueasilisha anaingia kwenye mtandao anasema vingine.
Mbowr bafo ,wenyekiti bora,ataendelra kuwa mwrnyekiti bora,na kamwr hatutakubali CDM idhofishwe na wachumia tumbo.
 
Patient is the key kwa sababu viongozi wasaliti na waongo wanakuja kwa njia nyingi.

Jf in akisima cha mambo yote na ukweli wa watu waongo na wasaliti mara nyingi hujitokeza kama ukivyojitokeza kwenye hii thread.

Gonga hapa upate ukweli mwingine,

https://www.jamiiforums.com/complai...afanuzi-kutoka-kwa-mods-na-uongozi-wa-jf.html

Wakilalamika zaidi wanaweza kupatiwa muda kama ilivyotokea kwenye hii thread,

https://www.jamiiforums.com/jamii-i...iri-ya-mwenendo-wa-zitto-iliyopo-chadema.html

Hii ndiyo JF ambayo ukweli wote hupatikana kwa njia ya keypad/keyboard.

Nakuona uko kazini na furushi lako la dhambi! Unahama kila mtaa.
Kuwa makini na operation kimbunga?!
 
Kamanda Freeman A. Mbowe.

Mbona umekuwa tena mtu wa kulia lia kwenye vyombo vya habari.

Kama kweli wapo hao viongozi Chadema wataje tukate mzizi wa fitina.
 
Last edited by a moderator:
Inasikitisha sana kama Tanzania bado tuna watu wa aina yako.

Watu wa aina yako ndio hatari kubwa sana unadangnaywa unachekelea tu. Si awataje, yanini anapiga porojo tu.

Na siku akiwataja ukikuta mmoja wa Kaskazini uje kutueleza, labda Mtei?
 
Chadema kamwe hakitaongozwa na mawazo kutoka Lumumba! Yule ambaye Lumumba hawamtaki ndiye atakayeongoza Chadema!

Watumwa wa Mboe wakibanwa utasikia mara Lumumba mara buku saba,jibuni hoja,kwanini ndani ya CDM watu wakihoji swala la DJ na Babu inaonekana wasaliti???kuwa na mawazo tofauti si usaliti.au CDM mali ya watu flani.
 
Maadui hawana uwezo wa kutuamulia.Kama hao wasaliti na vibaraka wao ni wazuri basi waenda wakagombee huko Lumumba.

Kwanza uliona wapi Jeshi makini likabadili Majenerali katikati ya vita kwa kufuata matakwa na hila za maadui?

Kama suala ni uchaguzi basi subiri hao vibaraka wao waingie mbele ya sanduku la kura waone cha mtemakuni

mbona hawakihoji CUF Lipumba kila siku?? chadema bora kulikuwa na mtei, msukuma Bob makini na sasa mbowe!
 
Kamanda hivi kuna ubaya gani wanachamaa akihoji ukomo wa uongozi ni makosa?

pia kulikuwa na ubaya gani baadhi ya wajumbe wa nec- magamba kuhoji na kutaka mwenyekiti wa chama asiwe rais?

halafu ikawaje mwisho wa siku?
la mwenzako jekundu, je lako?!
ama kweli nyani....................................
 
Chadema mna maadui ndani ya chama na wanafanya kazi kwa kutumia akili sana. msidhani wanafanya kazi hiyo kwa utashi wao bali kwa utashi wa waliowatuma.

Ukifuatilia jinsi matukio machache yalivyofululizana katika siku hizi chache na hasa tuhuma ambazo zinaelekezwa kwa viongozi wakuu ama moja kwa moja ama kwa njia isiyo moja kwa moja utgundua kuwa kuna mipango na mikakati madhubuti katika hayo. Hayo wala siyo 'coincidence'. Mfano, moja: tuhuma kwamba vyama havijawasilisha hesabu zao kwa ajili ya ukaguzi, na kwamba CDM ni mojawapo katika vyama hivyo. Pia kwamba makatibu wakuu wa vyama hivyo wanatakiwa kwenda kwenye kamati ya bunge kujieleza. Pili: Mbowe kumiliki nyuma ya kifahari huko Uarabuni. Tatu, tunakutana tena na suala la Mwigamba kumtuhumu mwenyekiti wake na katibu mkuu, yote hayo ni mambo yaliyopangwa kiufundi sana. Nne, vyombo vya habari tunaviona navyo ni sehemu ya mikakati kwani vinatoa habiri zinazokinzana na kushindwa kutoa habari za upande wa pili.

Nawaasa viongozi mtulie, mtafakari na mjipange upya.
 
mkuu kuna njia sahh za kuhoji esp kwa kiongozi kama yeye
njia aliyotumia sio sahihi
 
Chama cha DEMOKRASIA na MAENDELEO........demokrasia ya kushika hatamu ya uongozi...
 
Back
Top Bottom