Ben Saanane katika umri wako mdogo unaonekana kijana mahiri wa kujenga hoja na mwenye mvuto na ushawishi mkubwa kwa vijana ndani na nje ya CHADEMA lakini ninatoa angalizo moja kwako
Endapo Mwenyekiti Mbowe atagombea nafasi ya Uenyekiti basi ni bora wewe ukaacha kugombea uenyekiti wa vijana. Kwa kufanya hivi utakua umepunguza propaganda za CDM kuwa chama cha wachagga au wakaskazini. Kwa hiyo chagua moja, ama Zitto agombee Uenyekiti ili wewe uwe na uhalali wa kisiasa wa kugombea Bavicha au Mbowe agombee Uenyekiti wewe ukose kugombea Bavicha. Tathimini vita yako unayopigana nayo
Kwa hiyo sasa, kwa ushawishi ulio nao unaweza kushirikiana na uongozi utakaochaguliwa wa bavicha kutengeneza baraza imara la kuvuka uchaguzi mkuu. Ni bora hata ukagombea nafasi ya katibu Mkuu wa Bavicha kuliko nafasi ya uenyekiti itakayozidisha propaganda. Tutakibomoa chama kwa kuendekeza siasa za Ukanda na udini. Hapo kwenye udini hakuna tataizo ndani ya chama kama ukabila na ukanda
Pia ungependeza zaidi ungejikita kwenye nafasi za kichama kama kurugenzi na idara ndani ya chama halafu ukaachana na Bavicha. Waunge mkono watakaojitokeza kugombea nafasi hiyo achana na kazi ya kujenga mtandao na mikakati kabambe ya siasa chafu unazopanga na kutekeleza kwa kushirikiana na Rose Mayemba wa RUCO, Hemmed Hassan Masood wa Unguja, Zainabu Haroub wa Chake Chake Pemba, Getrude Ndibalema wa UDOM, Mashuve Aron (Mwenyekiti wa BAVICHA Tanga), Josephat Issango (Mwenyekiti wa vijana Singida), Fred Ndajo wa Kigoma, Danny Mela wa Kilimanjaro, Exaud Mamuya wa Arusha, Olevarayo Noel wa Arusha, Renatus Pamba Diwani wa Sinza,Mlebele wa Mwanza (huyu ndiye aliyesema alitumiwa hela na Mchange), Edward kinabo anayefanya Kazi John Hopkins na Mjumbe wa Baraza Kuu,Mikael Aweda Mwenyekiti wa Chadema Ukonga (mjumbe wa Baraza kuu) na wengineo
Kumbuka propaganda ya ukabila ina nguvu sana na ni vyema ukapima hili kwa maslahi ya chama chetu kuliko ulivyofanya kipindi kile ukaishia kuenguliwa
Tuhuma za ukabila na ukanda zimetolewa sana na akina Mwampamba, Mchange, Shonza, Kafulila na hata Chacha Wangwe huko nyuma na hii ndiyo inayoonekana inatumika kumtenga Zitto. Kama wewe siyo Mroho wa Madaraka basi hicho kisirani chako cha kuitaka Bavicha kwa udi na uvumba achana nacho.
UCHAGUZI UJE, Idumu CHADEMA