Kuna Viongozi wasaliti CHADEMA - Mbowe

Kuna Viongozi wasaliti CHADEMA - Mbowe

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman Mbowe amesema chama hicho hivi sasa kinakumbana na viongozi wasaliti wasiojua wajibu wao wa kulikomboa Taifa.

Akihutubia kongamano la wadau na viongozi wa Kanda ya Kaskazini kiongozi huyo amesema sababu kubwa ya usaliti huo ni uroho wa madaraka kwa baadhi ya watu.

Mwenyekiti huyo anayeongoza chama kikuu cha upinzani nchini amesema kwa sasa chama hicho hakitavumilia viongozi wasaliti na badala yake watakuwa wanaelezana ukweli na kuchukua hatua stahiki kila inapobidi.

Kauli hii ya Mbowe itakuwa msumari wa moto kwa baadhi ya viongozi wanafiki na wanaotumika kutaka kuvuruga chama hicho.

Mbowe ni kiongozi ambaye anaungwa mkono na idadi kubwa ya wafuasi wa CHADEMA kote nchini kutokana na kazi kubwa anayofanya kuimarisha chama hicho kiasi ambacho Mwenyekiti wa CCM Rais Kikwete akiwahutubia watendaji wa CCM hapo jana amehofia chama chake kuondolewa madarakani kupitia sanduku la kura mwaka 2015.

Source:ITV Habari
 
Kazi nzuri mwenyekiti Mbowe,wewe ni jemedari wa vita na tunakuunga mkono katika harakati zako kwakuwa Chadema iko salama ikiwa chini ya uenyekiti Wako. Wengine bado hawajajipambanua kama ni baridi au Moto!
 
chiaguzi za ngazi tofauti katika chama zapaswa kufanyika,sanduku la kula litaamua nani anahitajika katika ngazi mbalimbali chamani,haiwekani mtu anashikilia nafasi miaka 10 no uchaguzi hii sio democrasia,chama cha siasa ni chama cha watu na sio cha ukoo au familia furani,ukifanyika uchaguzi hao wanaotwa wasaliti watatoweka.
 
Maneno ya mfa maji haya. Hivi leo kaweza kwenda kuzungumza na wananchi pamoja na kupigwa ngumi na Mwigamba jana?
 
IMG_5154.JPG
The picture is worth a thousand words.
 
Mfano wa kazi inayofanywa na Mwenyekiti wa Chadema unapaswa uigwe na viongozi wengine maana wasaliti ndani ya chadema hawana tofauti na wanaohujumu uchumi wa nchi kwa rushwa, kuchezea nyara za umma na ufisadi. Heko Mwenyekiti Mbowe
 
chiaguzi za ngazi tofauti katika chama zapaswa kufanyika,sanduku la kula litaamua nani anahitajika katika ngazi mbalimbali chamani,haiwekani mtu anashikilia nafasi miaka 10 no uchaguzi hii sio democrasia,chama cha siasa ni chama cha watu na sio cha ukoo au familia furani,ukifanyika uchaguzi hao wanaotwa wasaliti watatoweka.

Mkuu,

Kuna familia imewekeza pesa zake nyingi kuendesha shughuli za chama hiki. Ukiwaambia waachie uongozi utakuwa unatafuta ugomvi nao.

Chama cha wote kinajulikana.
 
CHADEMA Kuitoa CCM madarakani ni ndoto chini ya huyu mtu.Hapendi kabisa kukosolewa au kuulizwa jambo lolote linalohusiana na fedha au uvunjaji wa kanuni na katiba ya Chama.CHADEMA nilitaka sana uchukue utawala wa hii Nchi lakini naona hilo halitawezekana tena.I will have to think of my political position again,I will become an Independent I guess.
 
Aksante papaa kachanchabuseta,
nashauri ule waraka wenye mawasiliano kati ya zito na yale masisiemu uchapishwe kt magazeti ya kesho pia mitandao yote ili watanzania wengi wamfahamu kiundani uyu chui zzk alojivika ngozi ya kondoo ajue katu hatutadanganyika nae any more
 
Mkuu,

Kuna familia imewekeza pesa zake nyingi kuendesha shughuli za chama hiki. Ukiwaambia waachie uongozi utakuwa unatafuta ugomvi nao.

Chama cha wote kinajulikana.


ah ah, wewe kwa pumba tshakuzoea, wala hatushuguliki na wewe, kwan we cant argue with the fool ze marcopolo, yani wewe ni more than NICAMPOOP
 
chiaguzi za ngazi tofauti katika chama zapaswa kufanyika,sanduku la kula litaamua nani anahitajika katika ngazi mbalimbali chamani,haiwekani mtu anashikilia nafasi miaka 10 no uchaguzi hii sio democrasia,chama cha siasa ni chama cha watu na sio cha ukoo au familia furani,ukifanyika uchaguzi hao wanaotwa wasaliti watatoweka.

Chadema kamwe hakitaongozwa na mawazo kutoka Lumumba! Yule ambaye Lumumba hawamtaki ndiye atakayeongoza Chadema!
 
CHADEMA Kuitoa CCM madarakani ni ndoto chini ya huyu mtu.Hapendi kabisa kukosolewa au kuulizwa jambo lolote linalohusiana na fedha au uvunjaji wa kanuni na katiba ya Chama.CHADEMA nilitaka sana uchukue utawala wa hii Nchi lakini naona hilo halitawezekana tena.I will have to think of my political position again,I will become an Independent I guess.

Chadema haitafuata masharti ya vibaraka wa Lumumba.Ninachokushauri kapumzike tu kwani kazi uliyopewa hutaiweza!
 
Back
Top Bottom