Kumbe Tanganyika bado ipo!

Cynic

JF-Expert Member
Jan 5, 2009
5,144
1,648
Wiki chache zilizopita nilitakiwa nitoe taarifa wazazi wangu walizaliwa lini na wapi. Nikataja mwaka na kwamba walizaliwa Tanzania. Jamaa akaniuliza nina uhakika mara tatu na mimi kwa kujiamini nikamwambia ndiyo. Baada ya muda akaniambia haiwezekani! Nikamwambia labda kwenye database yake itakuwa imeandikwa United Republik of Tanzania,
Akaniambia pia haiwezekani. Ndipo akaniuliza nchi yenu haijawahi kubadili jina? Ndipo akili zikanijia na kumwambia kwamba ilikuwa inaitwa Tanganyika. Ndipo system yake ikakubali, na copy ya printout kuonyesha walizaliwa Tanganyika.

Nilichojifunza hapa ni kwamba kumbe Tanganyika ipo na kumbe wengine bado wanaitambua. Na waTZ mliozaliwa kabla ya muungano msijisahau - hamkuzaliwa Tanzania
 
kwa tarifa yako Tanganyika ipo na itaendelea kuwepo,na kwa wale wasioipenda Tanganyika Mungu awataremshie lana katika maisha yao.
 
Hili jina Tanganyika hata mie huwa napata shida kuelewa ni wakati gani linakuwepo na wakati gani Tanganyika haipo.
Ukiangalia kwa mfano Chama cha wanasheria huitwa Tanganyika Law Society na siyo Tanzania.Hebu tuchanganue ni wapi Tanganyika ina apply..na ni wapi haipo.Kulikwa pia na Tanganyika Packers japo imekufa miaka ya mwanzo ya 80.
 
Wiki chache zilizopita nilitakiwa nitoe taarifa wazazi wangu walizaliwa lini na wapi. Nikataja mwaka na kwamba walizaliwa Tanzania. Jamaa akaniuliza nina uhakika mara tatu na mimi kwa kujiamini nikamwambia ndiyo. Baada ya muda akaniambia haiwezekani! Nikamwambia labda kwenye database yake itakuwa imeandikwa United Republik of Tanzania,
Akaniambia pia haiwezekani. Ndipo akaniuliza nchi yenu haijawahi kubadili jina? Ndipo akili zikanijia na kumwambia kwamba ilikuwa inaitwa Tanganyika. Ndipo system yake ikakubali, na copy ya printout kuonyesha walizaliwa Tanganyika.

Nilichojifunza hapa ni kwamba kumbe Tanganyika ipo na kumbe wengine bado wanaitambua. Na waTZ mliozaliwa kabla ya muungano msijisahau -
hamkuzaliwa Tanzania
Cynic,
Ni kweli TANGANYIKA ilikuwepo, ipo na itaendelea kuwepo na Muda si mrefu toka sasa Jinamizi lake liotaibuka kudai nafasi yake. Narudia Muda si mrefu toka sasa.................
 
duh nitafurahi ikiwa itarudi tunamuomba mungu irudi kama leo na kesho na sio kufichwa inajulikana kuwa tanganyika ipo na serekali yake ipo sasa hii ni kuonyesha kuwa mnawakandamiza wazenji tu
 
Hili jina Tanganyika hata mie huwa napata shida kuelewa ni wakati gani linakuwepo na wakati gani Tanganyika haipo.
Ukiangalia kwa mfano Chama cha wanasheria huitwa Tanganyika Law Society na siyo Tanzania.Hebu tuchanganue ni wapi Tanganyika ina apply..na ni wapi haipo.Kulikwa pia na Tanganyika Packers japo imekufa miaka ya mwanzo ya 80.

Ngoja nikuongezee na nyingine:
1. Medical Council of Tanganyika ( sijui madaktari wa Zanzibar kama wana yakwao tofauti na hii au hii ndio yenye kushughulikia kote)

2. Tanganyika Farmers' Association
 
Wiki chache zilizopita nilitakiwa nitoe taarifa wazazi wangu walizaliwa lini na wapi. Nikataja mwaka na kwamba walizaliwa Tanzania. Jamaa akaniuliza nina uhakika mara tatu na mimi kwa kujiamini nikamwambia ndiyo. Baada ya muda akaniambia haiwezekani! Nikamwambia labda kwenye database yake itakuwa imeandikwa United Republik of Tanzania,
Akaniambia pia haiwezekani. Ndipo akaniuliza nchi yenu haijawahi kubadili jina? Ndipo akili zikanijia na kumwambia kwamba ilikuwa inaitwa Tanganyika. Ndipo system yake ikakubali, na copy ya printout kuonyesha walizaliwa Tanganyika.

Nilichojifunza hapa ni kwamba kumbe Tanganyika ipo na kumbe wengine bado wanaitambua. Na waTZ mliozaliwa kabla ya muungano msijisahau - hamkuzaliwa Tanzania

kwa tarifa yako Tanganyika ipo na itaendelea kuwepo,na kwa wale wasioipenda Tanganyika Mungu awataremshie lana katika maisha yao.

Hili jina Tanganyika hata mie huwa napata shida kuelewa ni wakati gani linakuwepo na wakati gani Tanganyika haipo.
Ukiangalia kwa mfano Chama cha wanasheria huitwa Tanganyika Law Society na siyo Tanzania.Hebu tuchanganue ni wapi Tanganyika ina apply..na ni wapi haipo.Kulikwa pia na Tanganyika Packers japo imekufa miaka ya mwanzo ya 80.

Cynic,
Ni kweli TANGANYIKA ilikuwepo, ipo na itaendelea kuwepo na Muda si mrefu toka sasa Jinamizi lake liotaibuka kudai nafasi yake. Narudia Muda si mrefu toka sasa.................

duh nitafurahi ikiwa itarudi tunamuomba mungu irudi kama leo na kesho na sio kufichwa inajulikana kuwa tanganyika ipo na serekali yake ipo sasa hii ni kuonyesha kuwa mnawakandamiza wazenji tu

Ngoja nikuongezee na nyingine:
1. Medical Council of Tanganyika ( sijui madaktari wa Zanzibar kama wana yakwao tofauti na hii au hii ndio yenye kushughulikia kote)

2. Tanganyika Farmers' Association

Naona Wakuu mnajidanganya wote nyinyi jina la (Tanganyika) litabaki lakini halitatumika kama mnavyotaka nyinyi lakini suala la Muungano upo bado pale pale na hiyo Tanganyika imekufa kama zamani alivyo kufa Baba Wa Taifa Mwalim Nyerere na Mzee Abeid amani Karume ikiwa hao watafufuka na hiyo Tanganyika itafufuka na Unguja pia itafufuka lakini kama hawatafufuka mpaka siku ya hukumu yaani kiama basi hiyo Tanganyika na Unguja hayo majina hayatarudi kama zamani hizo ndio ndoto za Sakafuni.......................Asanteni sana


WANAOTAKA KUUVUNJA MUUNGANO BASI HAO NDIO NI MAFISADI.
 
Naona Wakuu mnajidanganya wote nyinyi jina la (Tanganyika) litabaki lakini halitatumika kama mnavyotaka nyinyi lakini suala la Muungano upo bado pale pale na hiyo Tanganyika imekufa kama zamani alivyo kufa Baba Wa Taifa Mwalim Nyerere na Mzee Abeid amani Karume ikiwa hao watafufuka na hiyo Tanganyika itafufuka na Unguja pia itafufuka lakini kama hawatafufuka mpaka siku ya hukumu yaani kiama basi hiyo Tanganyika na Unguja hayo majina hayatarudi kama zamani hizo ndio ndoto za Sakafuni.......................Asanteni sana


WANAOTAKA KUUVUNJA MUUNGANO BASI HAO NDIO NI MAFISADI.

Kwa tarifa yako wazanzibari sio mwehu wa kukana majina ya Unguja na pemba (zanzibar)sioni Ubaya wa jina Tanganyika kwanini linawaudhi watu kutamkwa, nawaombea wale wenye uchungu na Tanganyika siku moja Mmungu awape nguvu za kulimarisha jina asili la Tanganyika.
 
WANAOTAKA KUUVUNJA MUUNGANO BASI HAO NDIO NI MAFISADI.

We bwana mkubwa vipi? Kutaja neno Tanganyika ni ufisadi kwa vipi? Na hayo ya kuvunja muungano ni yako .. sijui yanakujaje hapa! Nadhani unafahamu fika kwamba December 9 huwa tunafunga ma osifi na tunasherehekea uhuru wa Tanganyika kwa magwaride rasmi ya majeshi ya ulinzi na usalama na viongozi wote wa kitaifa huwa wanaudhuria.
 
Tanganyika ipo, kuna ziwa, kuna wilaya huko DRC.

Ila nchi iliuawa katika muungano na Zanzibar katika mazingira ya kutatanisha na hesabu mpya za federation ambazo hazijawahi kuonekana tena dunia nzima.
 
Tanganyika will prevail forever!
Time talks,...and in no tym, we gonna see our beautiful Tanganyika!
 
Tanganyika ipo, kuna ziwa, kuna wilaya huko DRC.

Ila nchi iliuawa katika muungano na Zanzibar katika mazingira ya kutatanisha na hesabu mpya za federation ambazo hazijawahi kuonekana tena dunia nzima.
SWALI: Hivi timu ya taifa ya Zanzibar inapocheza mpira dhidi ya timu ya taifa ya bara kwenye Challenge inakuwa ni Zanzibar dhini ya Tanzania au Tanganyika? Mimi nadhani ni Zanzibar dhidi ya Tanganyika ila hawataki hilo jina litamkwe. Lakini nchi ipo.
 
mkisikika na wenye nchi mnasema Tanganyika mtakiona........

Moja ya laana inayowapata Wadanganyika ni kukataa asli yao na kulikana jina la nchi yao ya asli.

Poleni sana
 
Je wewe unayesema Tanganyika Itarudi umezaliwa lini? Nafikiri wewe ni Enzi ya Ruksa ndo maana hujui usemalo.........Asante
 
Naona tumekosa mambo ya kujadili! Kama kuna mtu atajisikia kuita Tanganyika au Tanzania Bara sioni kama kuna ubaya wowote, isipokuwa ijulikane nia yake ni nini! Dhambi ya ubaguzi itaendelea kuwatafuna, na mnastahili iwatafune vilivyo! Mkishamaliza kusema SISI WATANGANYIKA na kujitenga mtakuta hakuna mtu anayeitwa MTANGANYIKA! Kutakuwa na SISI WANYAMWEZI, WAO WASUKUMA! SISI WAPEMBA, WAO WAUNGUJA,.........Historia ndivyo ilivyo!
 
Back
Top Bottom