Kulipa kodi kubwa sio sifa

Kulipa kodi kubwa sio sifa

Ndio kikubwa kila mmoja aishi kwa uwezo wake. Kipindi cha nyuma nilikurupuka kwenda kupanga nyumba ya gharama kidogo kulinganisha na kipato changu baada ya miezi sita ya kwanza kuisha pesa niliyonayo mkononi haitoshi nikaongea na mwenye nyumba nikaanza kulipa miezi mitatu asee ndani ya mwaka mzima sikufanya jambo lolote la maana kila nikigeuka kodi imefika nikawa kama nimekuja mjini kumfanyia mwenye nyumba kazi. Ikabidi nikimbie
Vijana hawawezi kukuelewa mkuu.

Pia huu ujinga na ulimbukeni wa vijana naona ni fursa kubwa wa kuwekeza nakuendelea kupiga pesa.
 
I'm a city boy hata nusu ya kipato changu nikilipa kodi ya pango sina presha na ndio kitu napenda..kulala pazuri raha mdogo wangu..

Nimekulia Majumba sita alafu Mwenge na Sinza.
Washua wakahamia madale 2005 .

Nikawa nawashangaa hata kama wamejenga. Ila kwanini wasingejenga mjini?.

Mm nimeanzia Maisha Kinondoni na Kijitonyama. Na nikawa na mentality kuwa mjini sihami ngo.

Ila mbeleni akili za kikubwa zikanijia.
Niko Goba na maisha naona yanasonga.

kukaa mjini na kulipa Kodi kubwa Sio ujanja. Kwanza hakuna utulivu.

Kama uko age flan ya kujipanga (25+) bora ukae mbali kidogo na mji. Kwa gharama nafuu kidogo ili ikupe mazoea na uone kawaida kujenga na kuwa na kwako pembezon mwa mji.

Ukiwa mentality ya kukaa mjini. Utazeeka haujajenga.
Maana kupata mill 200+ kumvua mtu nyumba its a not a joke.
 
Unaposema hivyo unakosea,kuna watu nawajua wanalipa kodi 10milion kwa mwezi na wanakaa kama wapo kwao

Ishu hapa kipato chako kipoje? Kuna watu hiyo hela ni ndogo sana kwao,kwahiyo usiwaone watu hawajui wanacho fanya
Mkuu naona haujaelewa issue sio kuwa na pesa.

Uzi unakumbusha kujimanage kidogo na kununua/kujenga nyumba haijalishi unapesa nyingi au kidogo.
 
Back
Top Bottom