Kukosekana kwa intaneti: Kebo moja ya intaneti ilikatwa mapema Jumapili katika Mji wa bandari wa Afrika wa Durban, je ni hujuma?

Meneja Wa Makampuni

JF-Expert Member
Jul 7, 2020
6,509
8,503
Watumiaji wa intaneti nchini Tanzania, Kenya, Rwanda na Uganda wamekuwa wakilalamikia ukosefu wa intaneti huku watoa huduma kote Afrika Mashariki wakikiri kumekuwa na tatizo.

Screenshot_20240514_065610_Facebook.jpg


Wamesema wanajitahidi kurekebisha tatizo hilo.

Huduma hiyo ilikumbwa na hitilafu katika nyaya za chini ya bahari zinazounganisha eneo hilo na dunia nzima kupitia Afrika Kusini, mtaalam wa sekta hiyo Ben Roberts aliambia BBC.

Hali kama hiyo ilishuhudiwa katika sehemu za Magharibi na Kusini mwa Afrika mwezi Machi.

Cloudflare Radar, ambayo inafuatilia uunganishaji wa intaneti, imesema kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizoathirika zaidi na trafiki kushuka hadi asilimia 30 ya viwango vinavyotarajiwa.

Gazeti la Citizen la Tanzania lilieleza kilichotokea kama "kuzimwa kwa mtandao ambao kumeathiri njia kuu za mtandao".

Safaricom, pia nchini Kenya, ilisema "inakabiliwa na changamoto". Airtel Uganda imesema inafahamu kuhusu "huduma ya mtandao ya mara kwa mara".

Na MTN Rwanda ilisema kulikuwa na "suala la uharibifu wa uhusiano wa kimataifa". Malawi, Msumbiji na Madagascar pia zimeathirika kulingana na Cloudflare Radar.

Bw Roberts, kutoka kampuni ya pan-Africa ya Liquid Intelligent Technologies, alisema kuwa amethibitisha kuwa kebo moja inayopitia kando ya pwani ya Afrika Mashariki, inayojulikana kama Eassy, ilikuwa imekatwa mapema Jumapili katika Mji wa bandari wa Afrika wa Durban.

Kebo nyingine pia ilikatwa. Alipuuzilia mbali uwezekano kwamba huenda ni hujuma na uongeza kuha hali kama hiyo wakati mwingine hutokea kwa bahati mbaya.

Kebo zingine zinazounganisha Afrika Mashariki na Ulaya pia zinapatikana na hatua kwa hatua huduma inapaswa kuboreshwa kwani data inapitishwa tena.

Lakini kwa vile makampuni mengi makubwa yana vituo vya data nchini Afrika Kusini uharibifu wa kiungo muhimu ambacho Eassy hutoa ulikuwa na athari kubwa.

Chanzo: BBC
 
Kuna huduma zetu na kazi zetu tunazifanya kwa kutegemea internet, toka juzi kazi haziendi
 
Hamna hujuma na si mara ya kwanza undersea cable kupata shida, hili limetokea hwta kwa wenzetu. Tofauti wao wana repair crew iliyo sharp inafanya kazi in time. Pia wana backup
 
Watumiaji wa intaneti nchini Tanzania, Kenya, Rwanda na Uganda wamekuwa wakilalamikia ukosefu wa intaneti huku watoa huduma kote Afrika Mashariki wakikiri kumekuwa na tatizo.

View attachment 2989668

Wamesema wanajitahidi kurekebisha tatizo hilo.

Huduma hiyo ilikumbwa na hitilafu katika nyaya za chini ya bahari zinazounganisha eneo hilo na dunia nzima kupitia Afrika Kusini, mtaalam wa sekta hiyo Ben Roberts aliambia BBC.

Hali kama hiyo ilishuhudiwa katika sehemu za Magharibi na Kusini mwa Afrika mwezi Machi.

Cloudflare Radar, ambayo inafuatilia uunganishaji wa intaneti, imesema kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizoathirika zaidi na trafiki kushuka hadi asilimia 30 ya viwango vinavyotarajiwa.

Gazeti la Citizen la Tanzania lilieleza kilichotokea kama "kuzimwa kwa mtandao ambao kumeathiri njia kuu za mtandao".

Safaricom, pia nchini Kenya, ilisema "inakabiliwa na changamoto". Airtel Uganda imesema inafahamu kuhusu "huduma ya mtandao ya mara kwa mara".

Na MTN Rwanda ilisema kulikuwa na "suala la uharibifu wa uhusiano wa kimataifa". Malawi, Msumbiji na Madagascar pia zimeathirika kulingana na Cloudflare Radar.

Bw Roberts, kutoka kampuni ya pan-Africa ya Liquid Intelligent Technologies, alisema kuwa amethibitisha kuwa kebo moja inayopitia kando ya pwani ya Afrika Mashariki, inayojulikana kama Eassy, ilikuwa imekatwa mapema Jumapili katika Mji wa bandari wa Afrika wa Durban.

Kebo nyingine pia ilikatwa. Alipuuzilia mbali uwezekano kwamba huenda ni hujuma na uongeza kuha hali kama hiyo wakati mwingine hutokea kwa bahati mbaya.

Kebo zingine zinazounganisha Afrika Mashariki na Ulaya pia zinapatikana na hatua kwa hatua huduma inapaswa kuboreshwa kwani data inapitishwa tena.

Lakini kwa vile makampuni mengi makubwa yana vituo vya data nchini Afrika Kusini uharibifu wa kiungo muhimu ambacho Eassy hutoa ulikuwa na athari kubwa.

Chanzo: BBC
Hiki kiswahili Cha google translator ni shida kukielewa.
 
Back
Top Bottom