Kuelekea 2015: Changamoto Kuu za CHADEMA ni nini?

Kuelekea 2015: Changamoto Kuu za CHADEMA ni nini?

1. CHADEMA ijipange kwa dhati kukabiliana na propaganda za udini zinazoenezwa na CCM. CHADEMA lazima itafute credibility kwa jamii ya Kiislam. 2. Namna ya kukabiliana na vyombo vya dola hasa katika uchakachuaji wa matokeo. 3. Kujenga network vijijini kwa kujenga office na kufungua matawi. 4. Kuwa makini na wanachama pandikizi hasa wale wanaotoka CCM.
 
Nilikuwa naamka alfajiri saa 10 kuangalia zile debate tatu za Obama na Romney. Romney wa Republicans alikuwa hafichi kitu juu ya nini atafanya akiingia madarakani. Hapa tunawachagua watu hata ambao hawajui kwa nini wanautaka UONGOZI wa nchi yetu!

Hapa lengo sijui kama ni kuiuliza CDM itafanya nini ikiingia madarakani..Unless I miss something! Ni kuhusu changamoto ni kama kusema mtu yuko kwenye mashindano ya urembo alafu wakati anaji advertise basi ndiyo mumpe changamoto za vitu vinavyomwangusha....


Huyo contestant anatoa sera za republicans zilizochujwa na vichwa na kabla ya kutoka kwenye mdomo wake zimehakikiwa ki-science zisije zua contradictions na kupunguza kura za wapigaji....
 
Mkuu nilishangaa sana Dr slaa alipotoa comment kuhusu uchanguzi wa ccm week mbili zilizopita,je ilikuwa sawa au ni makosa,nafikiri kiongozi mkubwa kama Dr slaa anatakiwa kuwa na washauri kwa ukaribu na lolote atakaloleta publick wahakikishe wamelipitia na kuangalia reaction itakuwaje

Binafsi nafikiri Dr Slaa alifanya vyema ku-comment kufuatia uchaguzi wa CCM maana aliwasaidia Watanzania wengi zaidi kujisogeza karibu na siasa chafu za magamba ili wazifahamu kwa undani na kisha kuitosa CCM wakiwa na uhakika na maamuzi yao.

Changamoto pekee ninayoiona ni Watanzania INFLUENCIAL ambao wamekaa kimya bila kuonesha msimamo wao kwenye siasa zinazoendelea. Nalitegemea watu hawa wenye ushawishi kwenye jamii zetu waweke wazi misimamo yao ili kuchagiza ushiriki wa watanzania wengi zaidi kwenye siasa. Maana, (hofu yangu) ni kuwa , Watanzania hawa wenye ushawishi wanavyokaa kimya, wanasababisha Watanzania wanaowaamini kuendelea kuchukia siasa na wanasiasa.

(sitaji majina lakini nawapa mifano: Wakurugenzi wa Mabenki kama Barclays, NBC, NMB, Exim, Standard Chattered etc, Mobosi wa makampuni makubwa makubwa na kadhalika-wangefuata mfano wa Sabodo -simaanishi wote wapigie debe chadema bali waweke wazi misimamo yao ya kisiasa)
 
Wengine wanasema wananchi hawahitaji kujua nini watafanya; kwamba waingiae madarakani kwanza halafu tutajua baadaye

MMM umesema mwenyewe kuwa CDM haitakiwi kuwaambia CCM wapi wanakosea ili ijirekebishe sasa humu kwani CCM hawezi kupata hiyo opportunity ya kujua hizo challenge za CDM na ku-capitalize katika hayo ili yenyewe iendelee kuwepo? Siyo kwamba wasifanye public awareness na dessimination ya sera zao laa..Ila inapokuja kwa real challenges zingine zimo humo ndani mwao so ukiwaambia hapo hiyo lipistic ya red umeweka kwenye macho badala mdomoni huku yeye anatafuta mchumba what mesage unatoa kwa wale wanaotegemewa kuchumbia? lol!

Lakini pia wazo lako ni sahihi kwani kuna mambo ambayo wakiyapata sasa yatasaidia sana..Mfano kama kusema rushwa ndiyo challenge kubwa tatizo litakuja yes ni challenge unaiondoaje hiyo challenge? Maana si kusema tu challenge ni hii bila kuwasaidia jinsi ya kukabiliana nazo..So it would be useful to them kuwa na foruma yenye public access inayotoa feed back baada ya mambo yanayoingia kuchujwa kama wengi wa wamiliki wa blog wanavyofanya kwa mesages kutoka kwa readers wao...
 
Binafsi nafikiri Dr Slaa alifanya vyema ku-comment kufuatia uchaguzi wa CCM maana aliwasaidia Watanzania wengi zaidi kujisogeza karibu na siasa chafu za magamba ili wazifahamu kwa undani na kisha kuitosa CCM wakiwa na uhakika na maamuzi yao.

Changamoto pekee ninayoiona ni Watanzania INFLUENCIAL ambao wamekaa kimya bila kuonesha msimamo wao kwenye siasa zinazoendelea. Nalitegemea watu hawa wenye ushawishi kwenye jamii zetu waweke wazi misimamo yao ili kuchagiza ushiriki wa watanzania wengi zaidi kwenye siasa. Maana, (hofu yangu) ni kuwa , Watanzania hawa wenye ushawishi wanavyokaa kimya, wanasababisha Watanzania wanaowaamini kuendelea kuchukia siasa na wanasiasa.

(sitaji majina lakini nawapa mifano: Wakurugenzi wa Mabenki kama Barclays, NBC, NMB, Exim, Standard Chattered etc, Mobosi wa makampuni makubwa makubwa na kadhalika-wangefuata mfano wa Sabodo -simaanishi wote wapigie debe chadema bali waweke wazi misimamo yao ya kisiasa)

Hawatakaa wafanye unavyotaka hata nchi makini hawawezi ingia huo mtego..Huwa wanaangalia upepo wakiona unaenda vizuri CDM then kwa siri wana saidia na wao..Wakiona opinion polls zimeegemea kwa mafisadi na wao wanjisogeza kwao haraka sana..Maana wako ki biashara zaidi kuliko kisiasa na ki-imani lol!
 
wao wanasafiri zaidi kwenda uk na usa lakini wanasahau wana kazi kubwa zaidi nyumbani,hao jamaa wa uk na usa hawapigi kura,huku wanamsema kikwete kwa kusafiri sana.sometimes wanakatisha tamaa sana hawa jamaa

huwezi jua katiba itakuwaje! Wameona mbali, diaspora ndo wapelelezi na wakusanya data! Ndo wadhamini wa chama.
 
BAWACHA kujipanga na kuwahamasisha wanawake kwa ajili ya mabadiliko,maana hili nalo ni kundi kubwa
linahitaji kuhamasishwa ili waendane na vuguvugu la mabadiliko.

haswaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!
 
Chadema iimarishe baraza la wazee na baraza la wanawake! Itakuwa vyema sana kama John Heche anavyoshambulia jukwaa, wawepo na wengine.
 
vijijini bado elimu ya uraia haitoshi na sera za CHADEMA bado hazijaenezwa ipasavyo. tufanye hivo wote wenye mapenzi nacho tusisubiri viongozi wakuu.
 
Je mfumo wa kuchuja na kupata wagombea wa ngazi mbalimbali ni mzuri ba unapaswa kuendelea ulivyo?
 
Nashukuru kamanda MM kwa uzi huu, ni uzi mujarabu na umeletwa kwa wakati unaofaa, mimi nikiwa kama mdau mkubwa wa mabadiliko, lakini zaidi nikiwa mwanachama na kamanda kindakindaki wa CHADEMA, ninaona changamoto zifuatazo ambazo zinaikabili chama changu CHADEMA. Nimezigawanya kwenye makundi mawili, yaani zile zinazoundwa na maadui wa CHADEMA, na zile zinazotokana na sisi wenyewe CHADEMA;

A. ZINAZOTOKA KWA MAADUI WA CHADEMA NA MABADILIKO

  1. UDINI NA UKABILA: Hii ni changamoto tunayopigana nayo mpaka sasa, ni changamoto inayoonekana kuwa haikuwa na nguvu sana miaka michache iliyopita, ila kwasasa inaweza kupata nguvu sana hasa kutokana na mabadiliko yanayoonekana ndani ya jamii yetu kwasasa. Udini umepamba moto kwasasa hapa nchini kwetu, na kwahakika umeenza kuligawa Taifa vipande viwili vilivyo wazi. Pengine nguvu inahitajika zaidi kupambana na changamoto hii kuliko hata ilivyokuwa miaka 10 iliyopita. Nachoshukuru MUNGU, ni changamoto iliyopuuzwa sana na watanzania wataka mabadiliko. Na hii inatokana na ukweli kwamba hoja hii ya UDINI na UKANDA ilitumika na wabaya wa mabiliko kuiangusha CUF miaka 10 iliyopita. Kwa hoja ya UKANDA, nayo inakosa mashiko kwasasa, japo nayo inahitaji nguvu kupambana nayo.
B.CHANGAMOTO NDANI YA CHADEMA YENYEWE
  1. KUKIPELEKA CHAMA VIJIJINI: Hii imekuwa ni changamoto kwa muda mrefu, ila kwa siku za karibuni na hasa baada ya kuzinduliwa kwa operesheni M4C angalau sasa tumeweza kuzifikia kata na vijiji kadhaa hapa nchini. Bado nguvu inahitajika kujenga imani kwa watanzania na hasa wa vijijini, ambao bado wamejenga imani kwa CCM na serikali yake. Na hii inatokana na mfumo ulijengwa na CCM kwa muda mrefu. Tukumbuke kuwa asili ya binadamu ni kuzuia mabadiliko na hasa asipofahamu hayo mabadiliko yana lengo gani. Wananchi wengi wa vijijini wanaamini kuwa CHADEMA ni chama cha vurugu, na CCM wanapokuwa huku wanawaaminisha kuwa ukichagua mabadiliko NCHI ITAINGIA KWENYE VITA. Nguvu zaidi inahitajika kuwaambia watanzania sababu za wao kuchagua mabadiliko.
  2. MABADILIKO YA UONGOZI: Nashukuru kwasababu kamanda wa anga, amiri jeshi mkuu Kamanda Freeman Mbowe ametangaza kutogombe tena na alisema kuwa ni wakati wa yeye kumuachia mwingine na yeye alipeleke hili gurudumu mbele. Hakuna asiyetambua mchango wa Dr Slaa na Mbowe kwenye ujenzi wa CHADEMA. Wamekuwa wakijotelea kwa mali na hali kuijenga CHADEMA yenye neema kwa muda mrefu sana, na hata mie sikushangaa wazee wa chama walipomuomba Kamanda Zitto ajitoe kumpisha Mbowe amalize mipango yake. Nadhani wana-CHADEMA hatukuchemsha kumpa kamanda Mbowe miaka mingine mitano ya kuongoza jahazi letu. Nadhani changamoto ya kujipanga kiuongozi ni ya muhimu kwasas, na hasa ukizingatia wabaya na maadui wa CHADEMA watatumia mwanya huu kutuangamiza kwa kuweka vibaraka wao au watu wasio makini kwa kisingizio cha DEMOKRASIA.
  3. UCHAGUZI WA CHAMA 2013: Tunayoyaona ndani ya CCM leo ni kengele kwa CHADEMA, hakuna changamoto kubwa kama uchaguzi wa chama 2013. Huu ndio utaamua mustakabli wa CHADEMA kwa miaka mitano(5) na hasa kwenye chaguzi za serikali za mitaa 2014 na uchaguzi mkuu 2015. Tukichagua vibaya ndio mwanzo wa kukiangamiza chama chetu. Hoja za UDINI, UKABILA, UKANDA zitatawala sana wakati huo, ni vyema tukajipanga kuona namna ya kucheza na changamoto hizi.

Nawasilisha.
 
Baadhi ya changamoto nizionazo mimi ni hizi:
-CHADEMA inategemea mno RUZUKU itolewayo na serikali. Haina wanachama watakaokiwezesha kuishi ruzuku hii ya zaidi milioni 233 kila mwezi ikipungua au kusitishwa kwa namna yoyote ile.

Hapana CDM inazaidi ya wanachama Milion 1 ambao hukichangia chama kwa ukawaida ambapo wakitoa sh 500 tu nusu yao hiyo ruzuku ni cha mtoto.
 
Nilikuwa naamka alfajiri saa 10 kuangalia zile debate tatu za Obama na Romney. Romney wa Republicans alikuwa hafichi kitu juu ya nini atafanya akiingia madarakani. Hapa tunawachagua watu hata ambao hawajui kwa nini wanautaka UONGOZI wa nchi yetu!
Acha kupotosha mkuu,ameshindwa kusema ni kivipi ata deal na deficit,na kuuendeleza uchumi bila ya kupandisha kodi za middle class, ameshindwa kusema na kabakia kudai watu wacheki kwenye website yake.Musipende kupindisha mambo kwasababu ya agenda zenu.Ni afadhali ungesema mwenzake ndiye aliyeweka wazi kuwa the rich will be taxed a bit more.Hakuna uwazi kihivyo kwenye mambo hayo.

Mleta mada mwenyewe anadai eti si wakati wa kuendelea kuwapatia ccm cha kufanya kwa kutumia ukosoaji,sasa kuna tofauti gani kama wakiweka plani zao wazi vs kukosoa?Maana chadema wakikosoa si huwa wanasema nini ni mbadala na ndiyo hapo ccm wanazitumia mbinu hizo?Nawashangaa sana tu.
Mzee Mwanakijiji said:
Kuna ambao wanaridhika na CDM kama chama cha upinzani; wakikosoa utawala wa CCM, wakikosoa watawala wa CCM na wakitoa ushauri mbalimbali kwa serikali na hawa hufurahia na kuridhika pale ambapo serikali inapochukua mapendekezo ya CDM. Je inatosha kuwa chama cha upinzani chenye kukosoa na kushauri serikali na taasisi zake? Je inatosha kwa viongozi wa upinzani kukosoa wale wa CCM na kuisaidia serikali itawale?

Niliwahi kuandika huko nyuma mada ya kwamba jukumu la chama cha upinzani siyo kusaidia serikali kutawala bali ni kuhakikisha wanaiangusha serikali iliyoko madarakani ili wao wapate nafasi ya kuingia kwenye uongozi huo na kutekeleza sera zao. Mada hiyo ya Aprili 2011 inaeleza kwa kina kuwa siyo jukumu la CDM kuikosoa serikali ili itawale vizuri. Lengo lolote la kukosoa serikali ni kuidhoofisha ili hatimaye ianguke (collapse) au wananchi waikatae kwenye uchaguzi mkuu.
Sasa ukiweka mambo yako wazi kuna utofauti gani na kutoa ushauri?

Lets say utasema "sitoi ushauri",lakini hivi ndivyo nitakavyofanya",hapo kuna tofauti gani kati ya statement hizo mbili?
 
Hapana CDM inazaidi ya wanachama Milion 1 ambao hukichangia chama kwa ukawaida ambapo wakitoa sh 500 tu nusu yao hiyo ruzuku ni cha mtoto.

wanachama milioni 1? mbona huu si mtaji mzuri katika kupiga kura? Maana CCM inao kama miliioni 5 hivi...
 
only83,

Mkuu wangu hoja yako ya kwanza kuhusu UDINI.. Hili ni tatizo kubwa sana kuliko watu mnavyolifikiria. CUF haikupachikwa Udini bali imejiingiza yenyewe. Ni sawa na mtu alosingiziwa kutembea nje ya ndoa, kisha akachukia na kutembea kweli halafu anajitetea mlinilazimisha kufanya hayo..

Huwezi kunambia kwamba CUF sio chama cha Kidini hilo sikubaliani na wewe pamoja na kwamba mimi Muislaam. Nakaa nao, nakula nao, na natembea nao na nasema kwa uhakika CUF kimekuwa chama cha UDINI wakitumia Uzanzibar.. Ajizi hili lisije tu kutupata hata Chadema maana dalili za kuamini hivyo zinaanza kujtokeza. Na sintosema mengi sana lakini tujihadhari na mbegu hii ilopandwa nasi tukajikuta tunavuna matunda yake tukatoa mbegu na kuzipanda maana wataalam wanasema mbegu hupandwa chini japo mbegu hizo hutoka ndani ya tunda.
 
Mkuu nilishangaa sana Dr slaa alipotoa comment kuhusu uchanguzi wa ccm week mbili zilizopita,je ilikuwa sawa au ni makosa,nafikiri kiongozi mkubwa kama Dr slaa anatakiwa kuwa na washauri kwa ukaribu na lolote atakaloleta publick wahakikishe wamelipitia na kuangalia reaction itakuwaje

Mimi nadhani dr. alikuwa sasa katika mtazamo kuwa alibeza kile ccm walichofanya kwa kuwapitisha mafisadi na hapa alionyesha umma udhaifu ambao ccm wameounyesha kuwa hawana nia ya dhati kushughulikia mafisadi bali ni maigizo na hii alert ya Dr. Kikwete ameithibitisha kwa lawama anazotoa refer uchaguzi wa UWT na UVCCM. Imeonyesha kweli Dr alikuwa sahihi kwamba wamechemka maana hata m/kiti na raisi anaogopa watoa rushwa ndo akaishia kulaumu wamama na kuwahasa vijana nao wakampuuza wakaendelea kupiga dili m/kiti alilianzisha 2005.
 
Acha kupotosha mkuu,ameshindwa kusema ni kivipi ata deal na deficit,na kuuendeleza uchumi bila ya kupandisha kodi za middle class, ameshindwa kusema na kabakia kudai watu wacheki kwenye website yake.Musipende kupindisha mambo kwasababu ya agenda zenu.Ni afadhali ungesema mwenzake ndiye aliyeweka wazi kuwa the rich will be taxed a bit more.Hakuna uwazi kihivyo kwenye mambo hayo.

Mleta mada mwenyewe anadai eti si wakati wa kuendelea kuwapatia ccm cha kufanya kwa kutumia ukosoaji,sasa kuna tofauti gani kama wakiweka plani zao wazi vs kukosoa?Maana chadema wakikosoa si huwa wanasema nini ni mbadala na ndiyo hapo ccm wanazitumia mbinu hizo?Nawashangaa sana tu.
Sasa ukiweka mambo yako wazi kuna utofauti gani na kutoa ushauri?

Lets say utasema "sitoi ushauri",lakini hivi ndivyo nitakavyofanya",hapo kuna tofauti gani kati ya statement hizo mbili?


Inabidi uhakikishe kwanza umeelewa kinachosemwa au kilichosemwa; usidhani kimesemwa nini. Kuna uhusiano gani kati ya changamoto zinazoikabili CDM na kuikosoa CCM na serikali yake?
 
Inabidi uhakikishe kwanza umeelewa kinachosemwa au kilichosemwa; usidhani kimesemwa nini. Kuna uhusiano gani kati ya changamoto zinazoikabili CDM na kuikosoa CCM na serikali yake?
Sina shida na heading,bali ni contents,ningeomba ujibu nilichouliza.Kama ni changamoto mbona wanazo nyingi tu?Hakuna chama cha kisiasa chenye kujitambua na chenye wanachama na ambacho bado kinakuwa na kisiwe na changamoto.

Swali langu la msingi umeliona,ungelijibu badala ya kung'ang'ania kwamba sijaelewa maana ya changamoto.

Mbali na ukweli kuwa kuna maelfu ambao hawajakikubali kama ulivyoainisha,pia kuna changamoto kwamba maelfu walioko vijijini bado hawajafikiwa na chama hicho.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom