Kuelekea 2015: Changamoto Kuu za CHADEMA ni nini?

Ame! umesema vema,hizi point ni kusaidai magamba kujua strategic plan za CDM,naunga mkono uliyoyaandika !
 
I am not sure MMM kama sincere members wa CDM watatoa siri zao in public kuijenga CDM!
Ujenzi wa Chadema ya ushindi 2015 hautafanikiwa kwa siri bali kwa uwazi; kwa maana nyingine, siri ya mafanikio katika ushindani wa siasa chini ya demokrasia ya uliberali sio siri bali uwazi;
 
Mkuu nilishangaa sana Dr slaa alipotoa comment kuhusu uchanguzi wa ccm week mbili zilizopita,je ilikuwa sawa au ni makosa,nafikiri kiongozi mkubwa kama Dr slaa anatakiwa kuwa na washauri kwa ukaribu na lolote atakaloleta publick wahakikishe wamelipitia na kuangalia reaction itakuwaje

Dr. Slaa yupo makini; pamoja na uanachama wangu wa CCM, i have to admit kwamba watu kama Mnyika, Lissu na Slaa ni hazina kubwa sana kwa taifa letu;
 
Dr. Slaa yupo makini; pamoja na uanachama wangu wa CCM, i have to admit kwamba watu kama Mnyika, Lissu na Slaa ni hazina kubwa sana kwa taifa letu;

sawa Mkuu naona umeamua kuja kutusaidia,lakini vilevile hatuna imani na wewe nahisi unataka mambo yawekwe peupe,usisahau nyie ccm mna hamu sana ya kujua mienendo ya Chadema
 
Wanaotutawala tumewachoka na wanaotaka kuchukuwa dola nao hatuwaanini...sijui tufanyaje.
 
Dr. Slaa yupo makini; pamoja na uanachama wangu wa CCM, i have to admit kwamba watu kama Mnyika, Lissu na Slaa ni hazina kubwa sana kwa taifa letu;

Well said mkuu. Lakini nimeupitia uchambuzi wako kwa kina na ninasita kuamini kwamba wewe ni CCM kweli!!!
 
Baadhi ya changamoto nizionazo mimi ni hizi:
-CHADEMA inategemea mno RUZUKU itolewayo na serikali. Haina wanachama watakaokiwezesha kuishi ruzuku hii ya zaidi milioni 233 kila mwezi ikipungua au kusitishwa kwa namna yoyote ile;
-CHADEMA inategemea mno umaarufu na umashuhuri wa VIONGOZI wake wa sasa. Nikipewa mimi Uenyekiti wa CHADEMA leo wengi watakihama chama hiki ingawa naweza kuwa kiongozi mzuri kuliko Mbowe;
-KATIBA ya sasa ya JMT, vyombo vya DOLA na namna tunavyopiga kura kuchaguana bado ni changamoto kubwa;
-Bado hatujaingia kikamilifu kwenye mfumo wa vyama vingi.
 
sawa Mkuu naona umeamua kuja kutusaidia,lakini vilevile hatuna imani na wewe nahisi unataka mambo yawekwe peupe,usisahau nyie ccm mna hamu sana ya kujua mienendo ya Chadema

Ni mawazo yangu tu mkuu, ila kimsingi naelewa hoja juu ya umuhimu wa kufanya mikakati ya chama kuwa ya siri hasa katika mazingira haya ya siasa za kuviziana; Mimi nilikuwa nazungumzia tu kwa ujumla wake ambapo ushindani wa siasa katika mfumo wa demokrasia ya uliberali hauendeshwi kwa siri bali mikakati iliyo wazi hasa kutokana na uwepo wa ushindani unaotegemea sana tofauti za itikadi; Lakini ndani ya mazingira yetu ya ombwe la itikadi miongoni mwa vyama vyote vya siasa Tanzania (including CCM), hoja ya usiri katika mikakati ina mashiko kwani ushindani upo based on mambo mengine ambayo yanakaribia kuwa ya udaku;
 
Well said mkuu. Lakini nimeupitia uchambuzi wako kwa kina na ninasita kuamini kwamba wewe ni CCM kweli!!!

Asante mkuu; Utambulisho wangu wa kwanza ni Utanzania, ambapo nina vitambulisho viwili - pasi ya kusafiria na kadi ya kupiga kura; kadi ya CCM haina tofauti sana na kadi ya kuingia club kwenye VIP section kwa maana ya kwamba suala la siasa, starehe ni masuala secondary, primary ni utaifa wangu; Kwa maana hii, ni rahisi sana mimi kupigia kura diwani, mbunge au rais kutoka chama chochote cha siasa; Isitoshe, katika Jimbo langu la Kawe, uchaguzi wa 2010 nilimpigia kura Halima Mdee kwa sababu sikuridhika na mgombea wetu wa CCM; Hata mwaka 1995, Mwalimu Nyerere alimpigia kampeni mgombea wa NCCR Mageuzi Musoma Mjini kutokana na kutoridhishwa na mgombea wa CCM;

Vinginevyo kweli, mimi ni mwanachama wa CCM lakini sio mwanachama wa kutetea maovu na kuona Chadema ni wabaya wakati nguvu yao inatokana na mwitikio wa UMMA; Na hauwezi kujua, pengine siku moja nitakuwa mwanachama wa Chadema kwani nina haki ya kufanya hivyo kikatiba;
 
Katika kuangalia changamoto hizo nina presume kuwa watu wanakubaliana katika mengi mazuri ambayo yamekwisha fanya hadi hivi sasa na CDM.

Unaamini kuna changamoto kubwa....

MMM naona umebana kidogo wigo kwa kurudia sana neno 'changamoto' kwa vivumishi tofauti.

Tatizo kubwa, sio changamoto, ni RUSHWA ktk ngazi zote na hasa ktk chaguzi. Rushwa ni ya wazi wazi na vitendo vyake 'huratibiwa' na Taasisi Nyeti za Umma. Hili ni ovu mno.

Kwa nini rushwa? Tumeona ubutu wa TAKUKURU, uadhaifu wa TISS, uhalifu wa POLISI, kukosa umakani kwa JWTZ (mnajua waliingizwa kwenye siasa punde kabla ya uchaguzi uliopita), udhaifu wa Tume ya Uchaguzi, wabunge na mawaziri kuhongana na kununuana nk nk.......yote hayo ni kwa sababu watu wana bei na CCM imeweka utaratibu wa kuwanunua.

Rushwa inaweza kabisa kuufanya uchaguzi wa 2015 usiwe uchaguzi.
 
Ujenzi wa Chadema ya ushindi 2015 hautafanikiwa kwa siri bali kwa uwazi; kwa maana nyingine, siri ya mafanikio katika ushindani wa siasa chini ya demokrasia ya uliberali sio siri bali uwazi;
Ni kweli sana. Watu wanafikiria kujadili changamoto za CDM hadharani ni kuisaidia CCM; kivipi mimi sielewi bali ni woga usio na sababu.
 
Ni mawazo yangu tu mkuu, ila kimsingi naelewa hoja juu ya umuhimu wa kufanya mikakati ya chama kuwa ya siri hasa katika mazingira haya ya siasa za kuviziana; Mimi nilikuwa nazungumzia tu kwa ujumla wake ambapo ushindani wa siasa katika mfumo wa demokrasia ya uliberali hauendeshwi kwa siri bali mikakati iliyo wazi hasa kutokana na uwepo wa ushindani unaotegemea sana tofauti za itikadi; Lakini ndani ya mazingira yetu ya ombwe la itikadi miongoni mwa vyama vyote vya siasa Tanzania (including CCM), hoja ya usiri katika mikakati ina mashiko kwani ushindani upo based on mambo mengine ambayo yanakaribia kuwa ya udaku;

mambo yanyowekwa hadharani ni sera baada ya kuwa reviewed siyo crude thing...Hata invention na innovation huwa haiwekwi wazi mpaka ifikie level ya marketing..Lakini hata hivyo hiyo forum sijasema iwe siri inakuwa na public access kupost opinions na strategies ili ziwe reviewed na viongozi na zikija public zinakuwa zimechujwa kwa manufaa ya chama siyo tuchanganye kila kitu...Wenye malengo yao yakisiasa kui haribu CDM na wale wenye maono na vision sahihi ya chama hata kama yatakuwa yanakosoa baadhi ya mambo ya ndani kabisa ya chama....

Hata Mungu pamoja na uumbaji wake hakuweka miyoo na akli ya watu wazi kwanini sisi tusiige hiyo architecture ya Mungu mwenyewe?
 
Mchambuzi....Muhimu: Chini ya kanuni ya sasa ya mshindi ni mshindi - CCM hata ikimsimamisha Sofia Simba 2015 itapita kwa uhalali;.....
Asante kwa maneno mazuri, ingawa najua walio ndani ya CDM hawatapost wala kujibu haya hapa hadharani, inawezekana kwa nia na sababu njema, ila sisi wapenda maendeleo tunasema "msg send" cha ajabu hata mashabiki wao wamekaa kimya.
1. Katiba mpya ni tatizo sana kwa sababu inaweza isiwe tayari hadi 2015, lakini pia draft inaweza ikaleta shombo hivyo kuleta mjadala na uchaguzi usifanyike 2015.
2.katiba mpya inaweza ikaleta jambo jipya (mojawapo mgombea binafsi) Hapo kutakuwa na changamoto kubwa sana, ingawa joto litakuwa kali kwa CCM, bado majimbo ya CDM yatapungua kuliko kama hilo halitakuwepo.

3. Kuanzia sasa CDM inahitajika kuwapat middle class kwa wingi, changamoto ni kwamba lazima watoe hadharani mfumo na uendeshaji wao wa nchi kama watapata dola!!! ukianzia lile la majimbo/kanda mfumo mzima wa uendeshaji, wizara, nk bila kusahau jinsi ya kuendesha uchumi.....haijalisha kama ni uliberali ubepari na masoko au ubia PPP!!!
4.Tume ya Uchaguzi; hatuna kwa sasa anaeongelea mabailiko yoyote kwenye tume ya uchaguzi, tuna subiri katiba hili jambo kama halitakuwe vile tunavyo tarajia, kwa maana ya tume kufanyiwa mabadiliko makubwa, ikiwemo kjinsi ya kumpata kiongozi wake mkuu, majukumu, mamlaka na uendeshaji wake, vinginevyo ni tatizo.

Mwisho naona kivuli na wingu zito juu ya katiba mpya yenye serikali mbili ( serikali kuu na mitaa) kuewepo kwa sheria na uchaguzi mpya, na pindi utakapo rudiwa kutumia sheria mpya, au kungoja katiba ndo kufanya uchaguzi kwa pamoja.
Mchambuzi, kwa nini umemtumia m/kiti wa UWT?
:confused2:
Wakatabahu
 
Ni kweli sana. Watu wanafikurua kujadili changamoto za CDMhadharani ni kuisaidia CCM; kivipi mimi sielewi bali ni woga usio na sababu.
Nilikuwa naamka alfajiri saa 10 kuangalia zile debate tatu za Obama na Romney. Romney wa Republicans alikuwa hafichi kitu juu ya nini atafanya akiingia madarakani. Hapa tunawachagua watu hata ambao hawajui kwa nini wanautaka UONGOZI wa nchi yetu!
 
Imani kwa CDM inazidi kupanda kwa mifano michache tu ya Madiwani walioboronga Arusha na kule Mwanza, hilo tu linatosha kuona mwanga kwamba, japo inauma ila CDM ilisimamia maadili tofauti na ccm.
 
Mchambuzi....Muhimu: Chini ya kanuni ya sasa ya mshindi ni mshindi - CCM hata ikimsimamisha Sofia Simba 2015 itapita kwa uhalali;.....
Asante kwa maneno mazuri, ingawa najua walio ndani ya CDM hawatapost wala kujibu haya hapa hadharani, inawezekana kwa nia na sababu njema, ila sisi wapenda maendeleo tunasema "msg send" cha ajabu hata mashabiki wao wamekaa kimya.
Nashukuru kwa kuliona hilo, kwani inanishangaza sana kuona makamanda wangu kama kina Samson Mwigamba wakiwa hawaelewi wala kusikia neno lingine zaidi ya Chadema 2015 Ikulu njia ni nyeupe; Binafsi nitafurahi hilo kutokea nikiwa bado hai kwani itakuwa ni ukomavu mkubwa wa demokrasia katika taifa letu, na sio jambo la ajabu kwa vyama kupeana vijiti kutokana na matakwa ya umma; Huo ndio msingi wa demokrasia; CCM tukishindwa, tujipange, and actually tutakuwa na nafasi nzuri zaidi ya kujipanga kwani watakaobakia CCM iwapo itaanguka 2015 watakuwa ni wale wenye mapenzi ya dhati na chama hiki;

Vinginevyo reforming or rebranding CCM ikiwa ipo madarakani ni upotevu wa muda na resources; Chama kimeshakataa kubadilika, na matokeo ya chaguzi za ndani za CCM zinazidi kudhihirisha hilo;

Mchambuzi, kwa nini umemtumia m/kiti wa UWT?

Ni jina lililonijia haraka kichwani kutokana na mtiririko wa matukio ndani ya chama chetu cha CCM hivi karibuni, kwani iwapo ni kweli kwamba CCM inafikiria mpango wa kuweka mgombea Urais mwanamke 2015 kama njia ya kuua makundi, basi majina kama Sofia Simba ni miongoni mwa majina hayo in my humbe view, hasa iwapo Mama zetu, wake zetu, dada zetu na shangazi zetu ndani ya CCM wameona yeye ndiye anayefaa zaidi kubeba bendera ya chama kupitia UWT; Isitoshe, kwa CCM, lolote linawezekana;
 
Kwanza nitambue mchango mzuri sana wa MCHAMBUZI, kwa kweli unastahili sifa na pongezi. unakaa na kufikiria sana kabla ya kwenda kwenye keyboard. huwa napenda kusoma michango yako ambayo inazama kwa kina. tatizo ni kwamba wengi wetu hatupendi vitu vinavyozama. tunapenda vitu vya kiudaku udaku hivi! lakini pia niseme katika hilo kwamba wako wengi tu hapa JF ambao wanazama na kuchambua mambo kwa kina.

Pili nimpongeze aliyeleta mada hii, MM. heshima kubwa mzee.

Nitachangia katika maeneo mawili: Kwa Watanzania wote, na pili kwa CHADEMA. Nianze na yale ambayo nadhani ni muhimu sisi sote Watanzania, tukiongozwa na hali yetu ya Utaifa, Uzalendo, Utanzania, tunatakiwa kufanya. Pamoja na mengi ambayo uongozi thabiti wa chama kama CHADEMA unaweza kufanya, naamini kwamba viongozi hao watakuwa bora zaidi pale tu watakapopata changamoto njema na yenye afya kutoka kwa wingi wa Watanzania. ni watanzania wenyewe, hasa walio na uchungu kwamba mambo hayaendi sawa katika nchi yetu, hao ndio wanaweza kuielekeza CHADEMA na kuiwezesha ifanye kile kinachotakiwa. tunaweza kufanya haya siyo hasa kwa kununua kadi, ambalo nalo ni jambo jema tu, lakini nazungumzia hapa kufanya kazi za kujitolea kujenga chama. kila mtu katika kada yake na uzoefu wake na ujuzi wake anaweza kuangalia anawezaje kuchangia mabadiliko? wataalamu wa IT wanaweza kusaidia katika kufuatilia taarifa, maoni, na mambo yanayojitokeza na yenye umuhimu kwa chama, na kuyawasilisha kwa uongozi. Haya tunayojadili hapa ni mojawapo ya ushiriki, lakini unahitajika uwe mpana zaidi. Tusione kwamba kuna wenye chama ambao ni CHADEMA, na sisi ni watu tofauti. yetu macho! tunasubiri wakosee tuwaseme. Nadhani CHADEMA inahitaji sana ushiriki mpana wa watanzania ili kuwawezesha kuwa chama bora zaidi. Na hasa kama kuna uwezekano mkubwa wa CHADEMA kuwa mshindi katika sanduku la kura hapo 2015. Jinsi uwezekano huu unavyozidi kuwa mkubwa, ndivyo wale ambao kazi yao ni kutafuta tiketi ya kupata mafanikio binafsi na jamaa zao, watakavyojazana katika chama ili wajipange kuendeleza ulaji chini ya chama kipya. Business as usual! Tunaweza kukabili hali kama hii kwa wale wenye nia njema kushiriki kwa vitendo na kuacha kuwa watazamaji.

Pili, kwa CHADEMA, nikirejea mchango wa MCHAMBUZI kuhusiana na itikadi. suala la Itikadi ni muhimu sana kwa sababu linatoa mwanga wa mwelekeo wa chama katika kutekeleza kazi zake. lakini hapa nadhani tunahitaji kuwa na sehemu mbili tofauti. Itikadi ya chama na mwelekeo wa taifa. Chama cha TANU na baadae CCM, kilkuwa na itikadi yake. baadae CCM wameacha itikadi iliyoelezwa vizuri katika Azimio la Arusha, wakaingia katika itikadi ya siri lakini ambayo kutokana na tunayoyaona, ni aina ya uliberali ambao naomba niuite ULIBERALI KOKO. tumefika mahali tunahitaji kama taifa tuwe na mwelekeo. Kwa hali hiyo, pengine si jambo zuri sana kuachia mambo ya itikadi kwa chama. tukifanya hivyo tutaacha uwezekano wa chama kinachochukua madaraka kutuvuruga mno. tunahitaji kuamua ni mwelekeo gani tunautaka, kisha tujiimarishe hapo. itikadi za vyama zibakie ni kwa vipi watatufikisha tunapotaka kwenda kwa haraka, uhakika na gharama ndogo zaidi.
 
Mindi,

Asante kwa mchango wako kupitia bandiko namba 37; Nakubaliana na hoja yako kuhusu umuhimu wa itikadi, lakini zaidi, kutenganisha baina ya itikadi ya vyama na dira ya taifa; Ni muhimu sana kama taifa tukawa na self - determination inayolenga destination tunayotaka kwenda kama taifa; na hii ni lazima itokane na dira ya taifa ambayo ni home grown, sio ya kuletewa na nchi wahisani, ambayo itashirikisha wananchi kupitia wawakilishi wao/vyama vya siasa, civil society, private sector na serikali kwa pamoja; Tukishakubali tunataka kwenda wapi, ushindani sasa uwe kupitia itikadi za vyama vyetu, huku kila chama kikijinadi kuwa na njia bora na sio bora njia kufika tunapolenga kwenda;

Swali linalofuatia ni je, katika mazingira ya sasa, vyama vyote vya siasa, asasi za kiraia, sekta binafsi n.k, je wanakubaliana katika mambo gani ya msingi ambayo ni beyond party politics? Kila taifa lina masuala kadhaa ya msingi ambayo yanabakia intact bila ya kujalisha chama gani kinaingia madarakani, na kazi kubwa ya kila chama ni kuyalinda hayo; Lakini kwetu Tanzania, inaonyesha kila chama kina mambo yake kutegemeana viongozi wake wana amka vipi siku inayofuatia; Ni muhimu tukatatua hili, na sidhani kama ni suala la kuogopa kwa wadau wote hawa kukaa pamoja na kuamua juu ya hilo, na muhimu zaidi, suala hili lisiwe politicized...;

Kuhusu Uliberali KOKO, nimependa hoja yako juu ya hilo; Na uliberali huu KOKO ndio umetuzalia mabepari uchwara ambao wanatajirika kupitia 10% wanazowekewa kwenye mabenki ya Uswisi, badala ya taifa kujenga indigenous entrepreneurs and capitalists wenye value addition kwa uchumi wa taifa letu;
 
1.KATIBA
2.TUME YA UCHAGUZI
3.MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA(TENDWA)
4.JESHI LA POLISI(JWTZ nao ni-kama wameanza kuingia kwenye huo mkumbo)
...hizo ndo changamoto zinazokikabili chama kilichobeba matumainia ya watanzani "CHADEMA"...
Mkuu umesahau na USALAMA WA TAIFA
 
Nilikuwa naamka alfajiri saa 10 kuangalia zile debate tatu za Obama na Romney. Romney wa Republicans alikuwa hafichi kitu juu ya nini atafanya akiingia madarakani. Hapa tunawachagua watu hata ambao hawajui kwa nini wanautaka UONGOZI wa nchi yetu!

Wengine wanasema wananchi hawahitaji kujua nini watafanya; kwamba waingiae madarakani kwanza halafu tutajua baadaye
 
Back
Top Bottom