KUBENEA Vs LOWASSA

Safi sana Halisi na wote mnaomuunga Kubenea mkono. Habari za Lowasa zime dominate media kwa kuwa kila kitu anachofanya private na official ni cha Kifisadi. Hakuna fisadi kama Lowasa Tanzania nzima, RA ni cha mtoto. RA is the best friend of EL ili tu kupata mipitishio ya mipango yake. He is clever kuwa karibu na political shots. Hata mpaka niingie kaburini hakuna wa kunishawishi kuhusu ufisadi wa Lowasa. Naona tena mnataka kuzua uzushi kwa Kubenea kama yale ya Aziz Mongi kumfungia Kubenea kisa deni la 50,000 na kumtangaza ndani ya jamvi hili. Jamani heshimuni hili jamnvi ni takatifu si la wazushi na la vibaraka wa mafisadi.

Lowasa anatumia mbinu zote kutaka kumaliza uhuru wa vyombo vya habari. Anatamani avinunue vyote kama RA basi tu plan hizo in vain. Kweli nimeamini humu jamvini kuna sisi tunaopinga mafisadi na wengine wanatubeza.

Marekani kama kweli watafungia mafisadi kwenda kwao basi waanze na Lowasa. Big up Kubenea, cheers dedicated JF members and guests. Shame to Fisadi's na vibaraka wao.

Maane, hiyo ina maana kuliko watu watakavyoiona kwa juu juu. New Habari si ya RA.... kuna jambo zito ndani yake. Wamekwishaingia katika media nyingine wanataka kuzinunua na tusishangae wakamiliki TV na radio zenye nguvu kabla ya mwaka 2010. NINA UHAKIKA NA HILI tutaijadili katika wakati mwafaka
 
siamini kama mapambano haya tuliyonayo leo dhidi ya ufisadi yatafanikiwa iwapo tutaendelea na mbinu za sampuli hii.

Vita dhidi ya ufisadi haiwezi kufanikiwa kwa kumnyoshea kidole mtu mmoja(fisadi mmoja) , wala kikundi fulani tu cha mafisadi, ni lazima ziwepo juhudi za makusudi kabisa kukemea ufisadi popote unapofanyika. Kwenye hiyimisho la maranya hapo juu anasema hakuna kuwapa mafisadi nafasi ya kupumua. Lakini kwa staili hii tunawapa nafasi ya kupumua kwa sababu tuna concetrate kwa fisadi mmoja tu huku tukiwaacha mafisadi kibao wakipumua tena kwa raha mstarehe huku wakiendeleza ufisadi kwa kasi, nguvu na ari kubwa sana.

Hata katika mchezo wa mpiara, tazama jinsi timu pinzani inavyofungwa kirahisi kwa sababu tu wachezaji wanaconcetrate kumkaba mchezaji mmoja tu ambaye wao wanadhani ndiye mkali wa timu. Taifa stars ilipocheza na senegal wengi tuliamini mchezaji hatari alikuwa al-haji diouf na wengine wenye majina makubwa hivyo kuwakaba zaidi wao lakini kumbe kuna akina mamadou niang.

Kukoncetrate kwa lowassa kama sio deep thinker hauwezi kuona madhara yake. Akina rostam, nchimbi, d. Yona nk. Wanapumua vizuri sana na wanafanya ufisadi mkubwa tu.

Ninaendelea kusisitiza tupige vita ufisadi na mafisadi wote, lowassa ni fisadi lakini ufisadi sio lowassa.


wewe amekutuma uje uongee kwa niaba yake hapa?????
Anakulipa shilingi ngapi kwa kumpelekea data na kuongea kwa niaba yake?
 
Siamini kama mapambano haya tuliyonayo leo dhidi ya ufisadi yatafanikiwa iwapo tutaendelea na mbinu za sampuli hii.

Vita dhidi ya ufisadi haiwezi kufanikiwa kwa kumnyoshea kidole mtu mmoja(fisadi mmoja) , wala kikundi fulani tu cha mafisadi, ni lazima ziwepo juhudi za makusudi kabisa kukemea UFISADI popote unapofanyika. Kwenye hiyimisho la MARANYA hapo juu anasema HAKUNA KUWAPA MAFISADI NAFASI YA KUPUMUA. Lakini kwa staili hii TUNAWAPA nafasi ya kupumua kwa sababu tuna concetrate kwa fisadi mmoja tu huku tukiwaacha mafisadi kibao wakipumua tena kwa raha mstarehe huku wakiendeleza ufisadi kwa KASI, NGUVU na ARI kubwa sana.

Hata katika mchezo wa mpiara, tazama jinsi timu pinzani inavyofungwa kirahisi kwa sababu tu wachezaji wanaconcetrate kumkaba mchezaji mmoja tu ambaye wao wanadhani ndiye mkali wa timu. TAIFA STARS ilipocheza na SENEGAL wengi tuliamini mchezaji hatari alikuwa AL-HAJI DIOUF na wengine wenye majina makubwa hivyo kuwakaba zaidi wao lakini kumbe kuna akina MAMADOU NIANG.

Kukoncetrate kwa Lowassa kama sio deep thinker hauwezi kuona madhara yake. Akina ROSTAM, NCHIMBI, D. YONA nk. wanapumua vizuri sana na wanafanya ufisadi mkubwa tu.

Ninaendelea kusisitiza TUPIGE VITA UFISADI NA MAFISADI WOTE, LOWASSA NI FISADI LAKINI UFISADI SIO LOWASSA.
Ntaramuka,
Huwezi kulinganisha vita dhidi ya ufisadi na mchezo wa mpira wa miguu, tena timu yenyewe TAIFA STARS, hakuna hata professional player mmoja!Huyu Diouf unayemhusudu unaona anavyokamatwa kwenye ligi ya uingereza mathalani sunderland last week walikula 5-0 na Diouf akiwemo!na kwakuwa walijua kuwa yeye ndiye mbaya walimkaba hadi akashindwa kufurukuta kisha wakaanza kuwapiga mabao!Kwa taarifa yako kwenye mpira kuna FAIR PLAY. Mathalani mchezaji wa Taifa stars akiumia mchezaji wa senegal anatoa mpira nje ili huyu mpinzani atibiwe.Na akipona, mpira unaanzishwa kwa mchezaji wa taifa stars kumrushia wa senegal au anautoa nje ili senegal waanze kucheza ili kuleta iyo ktu inayoitwa fair play.
Kwenye ufisadi hakuna fair play, wala ufisadi sio sawa na mchezo.Michezo ni furaha,amani, upendo na mshikamano lakini ufisadi ni wizi, ujambazi uuaji, uporaji na kila aina ya uovu unaoweza kutajika.Ndiyo sababu tunasema ufisadi ni sawa na vita.Kwenye vita hakuna fair play kama kwenye mpira!mpinzani wako kadri anavyoishiwa nguvu ndivyo unazidisha mashambulizi ili upate ushindi, hakuna kumpa nafuu.Katiaka vita akiuawa kamanda ndio njia rahhisi ya kuwashinda wapinzani kwakuwa yeye ndiye anayetoa mbinu na kupanga mikakati ya mapambano.
Kwahiyo basi kuandikwa sana kwa fisadi lowasa ni katika juhudi za kumuua kamanda wa kikosi cha ufisadi Tanzania.Akishamalizwa huyo hawa wengine watkimbia tu ama watajifia wenyewe, hawatakuwa na jeuri yeyote wakati wanajua kamanda wao keshauwawa!
Kwahiyo ndugu yangu labda utuambie kwamba umetumwa nawewe uwasafishe.Maana fedha za mafisadi zinamwagwa kila kukicha hadi kwa wachunga kondoo wa MUNGU sembuse wewe!au wewe ndiye mchunga kondoo mwenyewe, kwahiyo unaendelea na majukumu uliyokabidhiwa na fisadiz?
 
Maane, hiyo ina maana kuliko watu watakavyoiona kwa juu juu. New Habari si ya RA.... kuna jambo zito ndani yake. Wamekwishaingia katika media nyingine wanataka kuzinunua na tusishangae wakamiliki TV na radio zenye nguvu kabla ya mwaka 2010. NINA UHAKIKA NA HILI tutaijadili katika wakati mwafaka


Mkuu nasikia Nchimbi alimnunua mwandishi wa IPP media ili amchafue Nape na kunyoosha maelezo juu ya jengo hilo ambalo lipo kwenye bifu sasa hivi.....Inasemekana Mungwana akaipata hii ishu kama ilivyo ikabidi ampigie cmu mkurugenzi wa IPP media na kumuuliza juu ya ishu hii....palikuwa hapatoshi sijui kama yule mwandishi kama anaendeleza libeneke pale IPP media.
Kama mnakumbuka vizuri mkurugenzi wa IPP media akaamua kutema cheche hivi karibuni kuwa mafisadi wanamnyemelea hata jana Mfanyabiashara maarufu Raza naye kaunga mkono hoja ya mkurugenzi huyo.
 
Ntaramuka,

at whatever cost ungemuunga mkono Kubenea kwani licha ya madhara makubwa alioyapata bado anaendelea kuexpose mafisadi kwa niaba ya sisi watanzania masikini .. laiti Mungu apishe mbali angedhurika zaidi ungefurahi wewe??? ... naona hata ukikutana na Kubenea na Lowasa ukaambiwa chagua basi utachagua Lowasa ... kuwa na utu japo kidogo ndugu yetu.

This guy is sacrifising his life for you as well
 
Kubenea kazi moja tu, kinara wa mafisadi lazima ashughulikiwe halafu tunawaambia wengine waanze kutia maji wakingojea zamu zao. Hakuna fisadi waku-relax mpaka wote watokomee. Lowasa ni lazima ashughulikiwe, akimshughulikia Nape naye ashughulikiwe na Kubenea mpaka atokomee. Na bdao sasa mafisadi wajue kuwa uvumilivu wa wadanganyika sasa umefikia kikomo na tunaingia barabarani huku ndiko liliko suluhisho.

Keep it up Kubenea
 
Siamini kama mapambano haya tuliyonayo leo dhidi ya ufisadi yatafanikiwa iwapo tutaendelea na mbinu za sampuli hii.

Vita dhidi ya ufisadi haiwezi kufanikiwa kwa kumnyoshea kidole mtu mmoja(fisadi mmoja) , wala kikundi fulani tu cha mafisadi, ni lazima ziwepo juhudi za makusudi kabisa kukemea UFISADI popote unapofanyika. Kwenye hiyimisho la MARANYA hapo juu anasema HAKUNA KUWAPA MAFISADI NAFASI YA KUPUMUA. Lakini kwa staili hii TUNAWAPA nafasi ya kupumua kwa sababu tuna concetrate kwa fisadi mmoja tu huku tukiwaacha mafisadi kibao wakipumua tena kwa raha mstarehe huku wakiendeleza ufisadi kwa KASI, NGUVU na ARI kubwa sana.

Hata katika mchezo wa mpiara, tazama jinsi timu pinzani inavyofungwa kirahisi kwa sababu tu wachezaji wanaconcetrate kumkaba mchezaji mmoja tu ambaye wao wanadhani ndiye mkali wa timu. TAIFA STARS ilipocheza na SENEGAL wengi tuliamini mchezaji hatari alikuwa AL-HAJI DIOUF na wengine wenye majina makubwa hivyo kuwakaba zaidi wao lakini kumbe kuna akina MAMADOU NIANG.

Kukoncetrate kwa Lowassa kama sio deep thinker hauwezi kuona madhara yake. Akina ROSTAM, NCHIMBI, D. YONA nk. wanapumua vizuri sana na wanafanya ufisadi mkubwa tu.

Ninaendelea kusisitiza TUPIGE VITA UFISADI NA MAFISADI WOTE, LOWASSA NI FISADI LAKINI UFISADI SIO LOWASSA.

Ebu nenda katibiwe makengeza yako kwanza. Yaani habari zote za ufisadi zinazoandikwa (hata kwenye MwanaHalisi) wewe umeona ya Lowasa tu? Soma vizuri MwanaHalisi, na magazeti mengine kama ukipenda, utabaini kuwa linaandika zaidi ya Lowasa
 
Ukweli unabakia pale oale kuwa jamii inayo haki ya kuangalia kama kuna connection kati ya Kubenea na Lowasa au la?

Tulishawahi kujiuliza humu ndani why kila kukicha magazeti ya Mengi ndio yako frontline kumuandika Mkapa ktk kila negative angle wanayodhani itawafaa, baadhi walitoa majibu na wengine bado walibisha kwa kejeli au kupuuziakabisa.

Lowassa kama mwanasiasa wa juu kabisa ktk jamii yetu achilia mbali madhira ya kisiasa aliyokutana nayo, kwa msingi huu anabaki kuwa ni sehemu ya muhimu kwa jamii yetu.

Mleta hoja anachojaribu ni kutupatia fursa wana JF kuangalia upande wa pili wa shilingi, waswahili wana kamsemo ka shari hivi" Nyundo iligongwa kabla ya kugonga"

Twende chini na tuangalie mzizi wa habari hizi maalum za Lowasa ktk kila front page ya Mwanahalisi takriban 90% tangu kuanzishwa kwa gazeti hili.

Tufungue milango ya kukubali kutofautiana kwa hoja na pengine kutokukubaliana waungwana.

Nampongeza mtoa hoja na wakati sasa wa kuangalia connection kati ya Lowasa na Kubenea, niwakumbushe tu kuwa Saed Kubenea alianza kung'ara ktk media zetu kwa kasi kuanzia February 2005 pale CCM waliposema sasa ruksa kwenda front kwa wagombea.

Baada ya ushindi wa kambi ya JK chini ya ukamanda wa Edward ndipo hapo Kubenea alianza kurusha live mitizamo yake dhidi ya wana mtandao na taratibu akaanza kuifikia target yake Edward Ngoyai Lowasa.

Jamvi hili lijitupe ndani na kutufumbua macho juu ya hawa mahasimu wawili kwa faida ya umma na kumhukumu mtoa hoja na wachangiaji wanaomuunga mkono,
He was our pm, still is our leader and people do have some respect for him.

Twende kazini wakuu
 
Halisi mungu akuweke pema yaani ningependa nikubebe mgongoni. Coolgirl kama unajua mafisadi wengine lete habari tuongeze msururu. This is an Olympic a special Olympic for Fisadis in Tanzania,
 
Kuandika sana,kuandika kidogo maana yake nini?Nani anajua kuandika sana?Je kila siku maana yake nini?NAUNGANA NA MWENDELEZO WA KUBENEA.Nchi hii lazima tujifunze kuchukia udhalimu.Kuvaa suti siyo kuongezeka akili wala kupungukiwa. Kama Kubenea anamwandika LOWASA bila ukweli wowote mbele ya halaiki ya WATANZANIA basi huo utakuwa UFISADI WA DAMU TENA YA MZEE.Maana ni heri ukatendewa isivyo haki kuliko wewe kutenda isivyo haki Mpaka sasa hajathibitishwa kwamba Kubenea analake jambo kwa nini wengine mnasema imetosha? Kutosha nini? Nani ametosheka? Kwa nini? Ki vip?
 
Inanikumbusha kisa (nilichojitungia) cha waandishi wa mwituni walioamua kuandika ufisadi wa simba; simba akawaambia mbona mnanifuata fuata kuniandika nikila tu swala mbona chui naye anakula vidigidigi vingi tu?. Waandishi wakamwambia kwa sababu wewe ni "mfalme wa mwitu"!
 
LOWASA amezidi acha asemwe hadi ajirekebishe ndipo aachwe kuandikwa KEEP IT UP KUBENEA
 
Nukumbuka ule wimbo wa Wanaume TMK {kumtushusha sisi kazi tu kazi tu.... nabado nabado... kumshusha KUBENEA kazi sana ... nabado nabado anaendeleza mapambano ya UFISADI
 
ntaramuka na wenzako,

....hakuna ubaya na ninyi mki-research ufisadi wa hao wengine, na hizo makala mkampelekea Kubenea au mkaandika magazetini yote ni sawa tu
 
Ukweli unabakia pale oale kuwa jamii inayo haki ya kuangalia kama kuna connection kati ya Kubenea na Lowasa au la?

Tulishawahi kujiuliza humu ndani why kila kukicha magazeti ya Mengi ndio yako frontline kumuandika Mkapa ktk kila negative angle wanayodhani itawafaa, baadhi walitoa majibu na wengine bado walibisha kwa kejeli au kupuuziakabisa.

Lowassa kama mwanasiasa wa juu kabisa ktk jamii yetu achilia mbali madhira ya kisiasa aliyokutana nayo, kwa msingi huu anabaki kuwa ni sehemu ya muhimu kwa jamii yetu.

Mleta hoja anachojaribu ni kutupatia fursa wana JF kuangalia upande wa pili wa shilingi, waswahili wana kamsemo ka shari hivi" Nyundo iligongwa kabla ya kugonga"

Twende chini na tuangalie mzizi wa habari hizi maalum za Lowasa ktk kila front page ya Mwanahalisi takriban 90% tangu kuanzishwa kwa gazeti hili.

Tufungue milango ya kukubali kutofautiana kwa hoja na pengine kutokukubaliana waungwana.

Nampongeza mtoa hoja na wakati sasa wa kuangalia connection kati ya Lowasa na Kubenea, niwakumbushe tu kuwa Saed Kubenea alianza kung'ara ktk media zetu kwa kasi kuanzia February 2005 pale CCM waliposema sasa ruksa kwenda front kwa wagombea.

Baada ya ushindi wa kambi ya JK chini ya ukamanda wa Edward ndipo hapo Kubenea alianza kurusha live mitizamo yake dhidi ya wana mtandao na taratibu akaanza kuifikia target yake Edward Ngoyai Lowasa.

Jamvi hili lijitupe ndani na kutufumbua macho juu ya hawa mahasimu wawili kwa faida ya umma na kumhukumu mtoa hoja na wachangiaji wanaomuunga mkono,
He was our pm, still is our leader and people do have some respect for him.

Twende kazini wakuu

FDR Jr, sidhani kama unakosea sana, ila ninachokiona kwako ni unapotosha kwa makusudi kwa hiyo hujakosea katika jitahada zako za kupotosha. Namkumbuka Lipumba wakati wa kampeni za mwaka 2000 alikua anasema hawezi kumuita Rais Mkapa mwongo, lakini alisema Mkapa hasemi kweli. Na wewe sasa naona hujakosea kwani umepatia kupotosha ambalo ndio lengo.


Ukweli unabakia pale oale kuwa jamii inayo haki ya kuangalia kama kuna connection kati ya Kubenea na Lowasa au la?

Anza wewe utupe hiyo connection, labda Lowassa alimchukulia mwanamke Kubenea maana walianza kusema waliommwagia acid waligombea mwanamke.

Tulishawahi kujiuliza humu ndani why kila kukicha magazeti ya Mengi ndio yako frontline kumuandika Mkapa ktk kila negative angle wanayodhani itawafaa, baadhi walitoa majibu na wengine bado walibisha kwa kejeli au kupuuziakabisa.

Hakuna magazeti yanayotwa 'ya mengi' kuna Nipashe, Thisday, Guardian, Kulikoni, Acha Umbeya na kadhalika.

Lakini suala la Mkapa halina tofauti na Lowassa. Mbona ZOmbe anaandikwa? Mbona Kasusura aliandikwa? Ninachotaka kukwambia ni kwamba suala si Mkapa wala Lowassa, hoja ni kwamba hawajaiba? Si mafisadi? Leta habari hapa ambayo Mkapa ama Lowassa kasingiziwa na haina ushahidi watu wajadili si kusema tu juu juu kwamba wanaandikwa sana. Kiwira Mkapa hakuhusika? NBC haijauzwa na Mkapa? Mtoto wa mke wake aliyezaa na Mramba (Peter Maro) hajakabidhiwa nyumba za TTCL aziuze na nusu hajamuuzia mama yake? kwa uchache tu. Lowassa hajahusika na Richmond? Lowassa hajahusika na jengo la UVCCM? Nagu, Lukuvi, Masilingi hawajamkana? Mbona wao hawajafukuzwa kama Nape? Sasa wanaondika au kusema ndio wanaokosea na wanaoiba au kuhujumu ndio washangiliwe?

Lowassa kama mwanasiasa wa juu kabisa ktk jamii yetu achilia mbali madhira ya kisiasa aliyokutana nayo, kwa msingi huu anabaki kuwa ni sehemu ya muhimu kwa jamii yetu.

Ni kweli ndio maana lazima ajadiliwe kwa maovu yake na kama akijenga shule kule Monduli ni wajibu wake, kwa tafsiri ya habari si habari ni sawa na mbwa kumng'ata mtu. Itakua habari ikiwa mtu atamng'ata mbwa.

Mleta hoja anachojaribu ni kutupatia fursa wana JF kuangalia upande wa pili wa shilingi, waswahili wana kamsemo ka shari hivi" Nyundo iligongwa kabla ya kugonga"

Hapo umepatia lakini njoo na HOJA ama jadili habari na gazeti husika si Kubenea, Mengi na Lowassa au Mkapa.

Twende chini na tuangalie mzizi wa habari hizi maalum za Lowasa ktk kila front page ya Mwanahalisi takriban 90% tangu kuanzishwa kwa gazeti hili.

Si kweli, kumekua na habari za watu wengi akiwamo Rostam, Jeetu Patel, Hosea, Karamagi, Msabaha na kadhalika na matokeo yake umeyaona kwa kamati ya Mwakyembe kupata nguvu na yeye kumwagiwa acid.

Tufungue milango ya kukubali kutofautiana kwa hoja na pengine kutokukubaliana waungwana.

Nakubaliana na wewe kwa HOJA na habari husika

Nampongeza mtoa hoja na wakati sasa wa kuangalia connection kati ya Lowasa na Kubenea, niwakumbushe tu kuwa Saed Kubenea alianza kung'ara ktk media zetu kwa kasi kuanzia February 2005 pale CCM waliposema sasa ruksa kwenda front kwa wagombea.

Si kweli, Kubenea ameanza kung'ara baada ya kumwagiwa acid na gazeti lilianza kupanda chati baada ya uchaguzi 2005 na si kabla yaani feb, 2005.

Baada ya ushindi wa kambi ya JK chini ya ukamanda wa Edward ndipo hapo Kubenea alianza kurusha live mitizamo yake dhidi ya wana mtandao na taratibu akaanza kuifikia target yake Edward Ngoyai Lowasa.

Jamvi hili lijitupe ndani na kutufumbua macho juu ya hawa mahasimu wawili kwa faida ya umma na kumhukumu mtoa hoja na wachangiaji wanaomuunga mkono,
He was our pm, still is our leader and people do have some respect for him.

Hapa umeshindwa kujificha kwa kumuita Lowassa kamanda na kwa kweli kwa kusema Lowassa na Kubenea ni MAHASIMU WAWILI. Hapo umejivua nguo
 
Kubenea kama upo hapa,

Please usikate tamaa. Najua matangazo ndo yanalipatia faida gazeti lakini kwako kupata hayo matangazo yanatakiwa watu kama akina Slaa. Naomba mobile ya Kubenea ili ikiwezekana nipate special price above 400tshs per copy. Najaribu kumtafuta through hizi za kawaida lakini may be anahisi ni waleeee.

Please mwenye nayo anitumie offline.

Asante sana
 
hata mimi inanikera ,fisadi ni lowasa peke yake?kubenea sema ulilonalo moyoni kila siku lowasa tulio wengi tumechoka na nyinyi waandishi mmezidi kopotosha umma wa watanzania!

He cool girl,
Are you serious??!!!!

Kama kuandika Lowassa ni fisadi katika makala kadhaa ni upotoshaji umma. Nini basi usahihi wa mambo!? Maana yawezekana tunachojua, na kuendelea kujulishwa na watu kama Kubenea na wenzie sicho ndicho!!

Na kama ndicho hicho, na wewe ni sampuli ya Lowassa (FISADI), unaogopa siku moja na wewe watakufikia. Na bila shaka watakufikia kwa sababu wameshakusikia.

Habari ndio hiyo.
 
Maane, hiyo ina maana kuliko watu watakavyoiona kwa juu juu. New Habari si ya RA.... kuna jambo zito ndani yake. Wamekwishaingia katika media nyingine wanataka kuzinunua na tusishangae wakamiliki TV na radio zenye nguvu kabla ya mwaka 2010. NINA UHAKIKA NA HILI tutaijadili katika wakati mwafaka


Halisi ni kweli kabisa usemayo. Jua kuwa Mafisadi hawa wa serikali kama Lowasa wanatumia influencial business people kama RA ili kufanikisha dili zao. Ndiyo maana mpaka kiama kije Lowasa na RA si rahisi sana kuachana. Wakiachana ujue kutakuwa na pigo kubwa sana kwao wote wawili. Kuna siri kubwa hapo. Hiyo ya kutaka kununua vyombo vya habari through the so called ununuaji wa HISA ndiyo gear ya kuingia. Then baadaye wamaliza kila kitu. Kwa usalama wao wakaanzishe vya kwao ila wajue kuwa media Tz imeamka sasa. Any way, ukifika wakati muafaka tulete hoja researched hapa jamvini kuhusuana na hizi plan za mafisadi na media tuanze kuwa pre-empty. Ila itabidi iwe mapema at the initial stages or plans ili tuzikomeshe. Wana JF waanze kukusanya data. We are tired with these FISADI's. Thanks.
 
Wana JF,
Ukiambiwa uhesabu hadi KUMI, unaweza kuanza 5,6,4,7... au 10,9,8,7.... au 1,2,3,4... Sasa hapa inategemea huyu Mwandishi wa kwanza ameandika ki-namna ili atuchemshe wote humu ndani yaani kaanzia 10,9,8.... na wote tumeichukulia hivyo. Angeliandika 1,2,3... yaani kwa kusema KUBENEA ENDELEA KUMUANDIKA LOWASA, sijui kama tungelijadili kiasi hiki. Hivyo akaanza 10,9,8,7..... na ona looooh, wote tumo ndani tukijadili.
Kwa mwandishi wa kwanza na wote mnaompinga, nafikiri ni VIZURI sana SIMBA WA NYIKA (kama asemavyo MKJJ) aendelee kusemwa kila kukicha. Zitumike mbinu zote watu wasilale kama tulivyolala tangu JKN aseme jamaa ni FISADI.
Kama Mwandishi kweli unadhamiria KUMSHAMBULIA kubenea na unakerwa na makala zake na gazeti lake kuandika kila kukicha FRONT PAGE juu ya Lowasa basi nakukumbusha tu kuwa kama hujasikia huu msemo basi ujue hii ndiyo maana yake. Ila kama upo Dar basi lazima umeshasikia. Msemo huo ni "NITAKOMAA NAYE HADI KIELEWEKE."
 
Hoja yenyewe ilivyokaa ni kifisadi fisadi kidogo. Kama ndugu ntaramuka upo kwenye payroll ya Lowasa, tuambiane. Pesa ngumu nchi hii.

Kubenea keep it up. Kuna sisi tunaokuunga mkono. Mimi sikosi kununua gazeti lako kila jumatano. Na la kesho nalisubiri kwa hamu.
 
Back
Top Bottom