Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,498
- 113,604
Wanabodi,
Huu ni mwendelezo wa Tribute to Edward Lowassa ilianza wiki iliyopita TRIBUTE: Pumzika Lowassa. Kazi umekamilisha, umeacha alama, mwendo umeumaliza. Watanzania wazalendo tutakukumbuka daima-1
Kwa wasomaji wapya , huu ni mwendelezo wa jinsi nilivyokutana na Edward Lowassa nikihusisha visa na mikasa ya hapa na pale.
Wiki iliyopita tuliishia nikiwa TBC, umekuja mwaliko wa Wiki ya Maji, nika lobby trip, ofisi haina mtu wa camera, nikabeba camera yangu, kufika eneo la tukio, ili niweze kulipwa double na kurudishiwa nauli ya ndege ya watu wawili, nikam set kijana mmoja hawa wapiga picha kwenye mikutano na kuzipanga chini, nikamtengenezea kitambulisho cha mtu wa TBC, nikampa, dili ya kupiga pesa ikapita, jamaa alipovuta tuu ule mshiko, alitokomea kusiko julikana na kile kitambulisho.
Kumbe yule jamaa kile kitambulisho amekifanya dili, akatinga jijini Dar es Salaam na kuhudhuria matukio mbalimbali akijifanya ni mtu wa TBC!.
Sasa endelea
Lowassa Aokoa Maisha Yangu Rome Italy.
Baada ya kisa hicho, mimi na familia yangu niliamua kuhama nchi, nikaanzia UK, then US family ilasettle, mimi sasa nikawa na hanja hanja kutafuta wapi haswa kuna greener pastures. Nikajaribu Sweden, Germany, Holland, Swiss, nikatua Rome Italy.
Watanzania ni watu wenye upendo sana wawapo ughaibuni, Lowassa alianzisha harambee ya papo kwa papo, na ubalozi wetu Rome, ukatia mkono, ukaingilia kati kuanzia vipimo, bili yote ya hospitali, nikapimwa nikatibiwa nikookolewa maisha yangu!.
Balozi Mahalu akamua assign afisa ubalozi wetu pale Rome, Adolf Nchemwa, akashughulikia bili zote za Hospital na nilitoka akanichukua kukaa kwake na familia yake yenye mke na watoto wawili mabinti.
From there mimi nikageuka ni Mgeni wa ubalozi nikagharimiwa kila kitu mpaka niliporejea nyumbani Tanzania. Yote haya yalifanyika kwasababu ya Lowassa!, Balozi Mahalu na Adolf Mchemwa!.
Somo hapa Watanzania tuwapo ughaibuni, tujenge utamaduni wa kujitambulisha ubalozini just incase of anything, ubalozi una taarifa zako. Mimi kilichoniokoa kule Italy ni press pass na nilipata msaada kwa hisani tuu ya Lowassa, lakini endapo ningejitambulisha ubalozini ukikutwa na jambo lolote ni rahisi kusaidiwa.
Harusi ya Binti Lowassa
Wakati Lowassa akiwa Waziri Mkuu alioza binti, Binti Lowassa na mimi nilitafutwa kuwa MC wa main event ya harusi ya binti Lowassa. Serikali nzima ilihudhuria na ikatokea tukawa marafiki na Bwana harusi.
From there mimi nikawa kama ni mtu wa Lowassa, hata kashfa ya Richmond ilipoibuka bado tulisimama na Lowassa.
Kufuatia kuwepo kwa dhana ya uchawa kwenye kuwaunga mkono wanasiasa tunaokubali na kuna watu ni wafuasi wa Lowassa wanajiita "Friends of Lowasa" mimi kwa bahati mbaya sikuwa mfuasi wa Lowassa wala siko kwenye kundi la friends of Lowasa kwasababu mimi ni independent, Lowassa akikosea ninamkosoa.
Harakati mbalimbali za Kisiasa za Lowassa Ikiwemo Safari ya Matumaini
Kuna msemo usemao rafiki wa kweli ni wakati wa dhiki, wakati Lowassa anaugua, yale makundi ya watu hayakuonekana tena, hata friends of Lowasa nimekuja kuwaona msibani!, waliokuwa wanahangaika nae ni mkewe, watoto na familia, na marafiki wachache na serikali kumhudumia kwa mujibu wa sheria taratibu na kanuni.
Somo la Kifo cha Lowassa
Somo Kuu la kwanza la kifo cha Mwamba huu ni kijifunza kuweka akiba ya maneno, nikisikiliza baadhi ya clips za wanasiasa jinsi walivyokuwa wanamsema vibaya Lowassa akiwa hai, na sasa wamekuja msibani na kugeuza maneno bila aibu!, tujifunze kuweka akiba ya maneno na sometimes ni bora kunyamaza kimya.
Somo la pili ni kuwa determined, ukidhamiria jambo lako lishikilie, usikubali kukatishwa tamaa. Lowassa was a very determined person.
Somo la tatu ni Lowassa ni mwalimu mkubwa wa siasa za kuwa na kiasi, alikuwa CCM, akafanyiwa figisu akalatwa kwa figusu, akahamia Chadema. Akiwa Chadema hakuisema vibaya CCM, na aliposhindwana na Chadema na kurejea CCM, Lowassa hakuisema vibaya Chadema!. Ni wanasiasa wachache sana wana haiba ya namna hii. Leo kwenye msiba wa Lowassa CCM na Chadema wanashindana kumuenzi kwa kumzungumza kwa wema.
Pumzika Lowassa Pumzika, ulikuwa ni mtu miongoni mwa watu (of the people) na ukawatumikia watu kwa uwezo wako wote kwa kushirikiana na watu (by the people) na ukautoa uhai wako kwa ajili ya watu wako, kwa kifupi ni Lowassa ni ametufia (for the people)
Mwendo umeumaliza, imani umeilinda
Bwana Alileta, Bwana Ametwaa
Jina lake Lihimidiwe...
Adios....
Amigos...!
Paskali
Huu ni mwendelezo wa Tribute to Edward Lowassa ilianza wiki iliyopita TRIBUTE: Pumzika Lowassa. Kazi umekamilisha, umeacha alama, mwendo umeumaliza. Watanzania wazalendo tutakukumbuka daima-1
Kwa wasomaji wapya , huu ni mwendelezo wa jinsi nilivyokutana na Edward Lowassa nikihusisha visa na mikasa ya hapa na pale.
Wiki iliyopita tuliishia nikiwa TBC, umekuja mwaliko wa Wiki ya Maji, nika lobby trip, ofisi haina mtu wa camera, nikabeba camera yangu, kufika eneo la tukio, ili niweze kulipwa double na kurudishiwa nauli ya ndege ya watu wawili, nikam set kijana mmoja hawa wapiga picha kwenye mikutano na kuzipanga chini, nikamtengenezea kitambulisho cha mtu wa TBC, nikampa, dili ya kupiga pesa ikapita, jamaa alipovuta tuu ule mshiko, alitokomea kusiko julikana na kile kitambulisho.
Kumbe yule jamaa kile kitambulisho amekifanya dili, akatinga jijini Dar es Salaam na kuhudhuria matukio mbalimbali akijifanya ni mtu wa TBC!.
Sasa endelea
Somo hapa ni mtu unaweza kutenda kitendo kidogo tuu cha deal mbuzi ili kuvuta pesa mbuzi kikaja kukugharimu big time kwenye career yako au maisha yako!..
Kumbe yule jamaa kile kitambulisho amekifanya dili, akatinga jijini Dar es Salaam na kuhudhuria matukio mbalimbali akijifanya ni mtu wa TBC!.
Za mwizi 40, siku ya siku jamaa katinga tukio na kitambulisho chake fake, kajisajili, kumbe siku hiyo aliyepangwa tukio hilo ndio yule Cameraman mwenyewe ambae kanjanja anatumia jina lake. Mtu halisi wa TBC alipojisajili akaambiwa huyu jamaa ameisha jisajili hatuwezi kukusajili mara mbili, hivyo akakataliwa kuingia.
Ilikuwa ni tukio la muhimu likinuhusisha kiongozi mmoja kati ya wale viongozi wetu wakuu, hivyo TBC hawawezi kuikosa hiyo story, tukio likaripotiwa ofisini, ofisi ikaripoti polisi, kanjanja akasakwa, akasakwa akawekwa chini ya ulinzi, mtu halisi wa TBC akaruhusiwa kuingia ku cover story.
TBC Moto Ukaniwakia!
Yule jamaa katika mahojiano akanitaja, hivyo na mimi nikafuatwa ofisini niunganishwe kesi ifunguliwe.
Kumbe kuna mlolongo wa tarajiwa za kijinai za kumshitaki mtumishi wa umma permanent and personable, wakati taratibu za kujinai zinaendelea, yule jamaa akajiongeza, akawapanga polisi, wakapangika akaachiwa!, hapa naamini utakuwa ni unajua ni nini kilifanyika!.
Wakati taratibu za kuniunganisha zimekamilika, kule polisi kukakutikana hakuna ushahidi wowote, faili halionelani, na yule jamaa ameyeyuka kwenye mahabusu ya polisi, no any records, atakuwa ameshauriwa salama yake ni apotee!, ahame mji asionekane popote, kweli jamaa akapotea issue ikafa.
Japo issues ilipotezewa kule polisi, huku kazini kwangu TBC moto uliendelea kuniwakia, kwenye taarifa yangu ya utendaji wa kazi, zile fomu zangu za OPRAS zikachafuliwa vibaya sana!, mimi nikagoma kusaini, najua sheria inanilinda na inamruhusu mtumishi kutosaini fomu zile ukijiona hujaridhika na ile assessment yako.
Nikaitwa kwa Mkurugenzi na meneja na mkuu wa Idara na kuelezwa the consequences za kukataa amri halali ya kulazinmishwa kusaini opras, nikajibu I'm ready!. Kilichofuatia baada ya hapo ni barua ya Summary Dismissals kwa kosa la insubordination!. That was my sad ending with TBC!.
Lowassa Aokoa Maisha Yangu Rome Italy.
Baada ya kisa hicho, mimi na familia yangu niliamua kuhama nchi, nikaanzia UK, then US family ilasettle, mimi sasa nikawa na hanja hanja kutafuta wapi haswa kuna greener pastures. Nikajaribu Sweden, Germany, Holland, Swiss, nikatua Rome Italy.
Ndipo Lowassa akasema huyu Mayalla japo sio mtumishi wa serikali lakini ni Mtanzania mwenzetu, tunamfahamu, tena kile kipindi chake cha Kiti Moto, nilikuwa nakipenda sana, sijui kwanini kilikufa?!. Balozi tafuta namna ya kumsaidia na mkikwama kabisa nijulisheni tutafanya jambo!.Kote ninamopita najichanganya na Watanzania na bado na maintains Press Card yangu always to gain the easy access ya tukio lolote.
Nikiwa Rome, kukafanyika mkutano wa Kimataifa wa World Food Day 10-years After, Tanzania ikatuma a very strong delegation. Mimi nika register kama Journalist from Tanzania.
Siku ya mwisho ya mkutano, I don't know what really happened to me mpaka kesho, nikiwa press gallery ni with my mac computer, camera, na begi, I just passed out!.
Kuzinduka ni nazinduka niko Hospital kubwa ya Rome, nimezungukwa na kundi kubwa la watu, Waziri Lowassa, Waziri Anna Tibaijuka, Balozi wa Tanzania nchi Italy wakati huo, Balozi Prof. Costa Rick Mahalu.
Ndio naelezwa nikiwa chumba cha waandishi nilizimika ghafla nikaanguka, nikakimbizwa hospital . Press pass yangu ikaonyesha ni Mtanzania, ubalozi wakaarifiwa ndio kisa cha kuzungukwa vile.
Hapo Hospital nimepatiwa tuu huduma ya kwanza, sikuwa na travel insurance, and not part of Government Delegation. Nikaulizwa hali yangu, najisikia Fresh tuu, natakiwa kufanyiwa uchunguzi wa kina sina bima.
Lowassa akamuuliza Balozi Mahalu ubalozi unaweza kusaidiaje?. Balozi akamjibu kwa kawaida ubalozi unasaidia watumishi wa umma on official visit, huyu sio mtumishi wa umma na hapa Rome yuko kivyake tuu!.
Watanzania ni watu wenye upendo sana wawapo ughaibuni, Lowassa alianzisha harambee ya papo kwa papo, na ubalozi wetu Rome, ukatia mkono, ukaingilia kati kuanzia vipimo, bili yote ya hospitali, nikapimwa nikatibiwa nikookolewa maisha yangu!.
Balozi Mahalu akamua assign afisa ubalozi wetu pale Rome, Adolf Nchemwa, akashughulikia bili zote za Hospital na nilitoka akanichukua kukaa kwake na familia yake yenye mke na watoto wawili mabinti.
From there mimi nikageuka ni Mgeni wa ubalozi nikagharimiwa kila kitu mpaka niliporejea nyumbani Tanzania. Yote haya yalifanyika kwasababu ya Lowassa!, Balozi Mahalu na Adolf Mchemwa!.
Somo hapa Watanzania tuwapo ughaibuni, tujenge utamaduni wa kujitambulisha ubalozini just incase of anything, ubalozi una taarifa zako. Mimi kilichoniokoa kule Italy ni press pass na nilipata msaada kwa hisani tuu ya Lowassa, lakini endapo ningejitambulisha ubalozini ukikutwa na jambo lolote ni rahisi kusaidiwa.
Harusi ya Binti Lowassa
Wakati Lowassa akiwa Waziri Mkuu alioza binti, Binti Lowassa na mimi nilitafutwa kuwa MC wa main event ya harusi ya binti Lowassa. Serikali nzima ilihudhuria na ikatokea tukawa marafiki na Bwana harusi.
From there mimi nikawa kama ni mtu wa Lowassa, hata kashfa ya Richmond ilipoibuka bado tulisimama na Lowassa.
Kufuatia kuwepo kwa dhana ya uchawa kwenye kuwaunga mkono wanasiasa tunaokubali na kuna watu ni wafuasi wa Lowassa wanajiita "Friends of Lowasa" mimi kwa bahati mbaya sikuwa mfuasi wa Lowassa wala siko kwenye kundi la friends of Lowasa kwasababu mimi ni independent, Lowassa akikosea ninamkosoa.
Harakati mbalimbali za Kisiasa za Lowassa Ikiwemo Safari ya Matumaini
Kuugua.
Kwenye uchaguzi mdogo wa jimbo la Arumeru, mimi nilisimama na Sioi Sumari, nikamshauri Lowassa Ushauri: Edward Lowassa asikanyage Arumeru, atamponza Sioi ushauri huu haukusikilizwa.
Safari ya Matumaini
Lowassa alipoianza ile safari ya matumaini, tulisimama nae na tukaeleza wazi wazi kumuunga mkono Elections 2015 - Kuelekea 2015: Kama CCM Itamsimamisha Edward Lowassa...
Japo chaguo la wengi kwa mgombea wa uchaguzi Mkuu wa 2015 alikuwa ni Edward Lowassa, nilipopenyezewa hii Elections 2015 - Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John Pombe Magufuli tuliishusha.
Tukawaandaa wafuasi kisaikolojia Elections 2015 - Edward Lowassa sio lazima yeye tu ndiye awe Rais wetu 2015, Rais wetu wa 2015 ni...
Tukawaeleza Elections 2015 - Licha ya kukubalika, Jina la Lowassa halitafika hata CC!
Na kweli muda ulipowadia ni kweli jina la Lowassa lilikatwa na kwanza tukashauri Elections 2015 - Ushauri wa Bure Kwa Lowassa: Kwa Vile ni Magufuli, Kubali Matokeo, Vunja Kambi, Jisalimishe!
Kisha licha ya kukatwa CCM, bado tulisimama nae Elections 2015 - Kukatwa kwa Lowassa, ni mwisho wa ile safari, au ni mwanzo wa Safari Halisi ya Matumaini?
Tumewashauri Chadema wampokee Ujio wa Lowassa CHADEMA: Kuna kundi wamesusa, wanapanga kurejea CCM!
Tukawasisitizia Chadema kuwa Lowassa ni mtaji Elections 2015 - Mabadiliko Chanya ya Ujio wa Lowassa: CHADEMA Kuhama Ufipa!, Kuwa Makao Yake, Kituo cha TV na Redio!
Wakati wote wa kampeni tulisimama nae Elections 2015 - Hii 'Vox Populi' ni 'Vox Dei' Kuhusu 'Jiwe Walilolikataa Waashi'?
Na tukamtabiria Lowassa ushindi Kama kipimo cha ushindi ni idadi ya watu, Lowassa ndiye rais wetu
Kusema ukweli kabisa siasa ni mchezo mchafu, Kwa Hali Niliyoishuhudia Leo Old Bagamoyo Rd: There is No Way CCM Inaweza Kushinda! na bado kwenye matokeo ya mwisho akishindwa!.
Baada ya matokeo kutangazwa Lowassa akalalamika kuwa ni yeye aliyeshinda, tukasimama nae Elections 2015 - Kama Hii ni Kweli, Then, Serikali Yetu ni Serikali Dhalimu?, Haramu?. Hukumu ya Karma ii Juu Yake!
Ila pia tukamshauri ENL, CHADEMA na UKAWA, Tuyakubali Matokeo!, Tushukuru Kwa Yote!, Life Goes On!.
Hivyo alipoitwa Ikulu tulishangaa Kama hiki ndicho Lowassa alichoitiwa Ikulu, Then tuna Rais wa ajabu! Kama ni Uongo, Lowassa ashitakiwe kwa Uchochezi!
Ila pia tukamshauri Ushauri wa bure kwa Lowassa, japo it's now just a matter of time kabla... Tafadhali sana tunakuomba kwanza kanusha tamko hili!
Kuna msemo usemao rafiki wa kweli ni wakati wa dhiki, wakati Lowassa anaugua, yale makundi ya watu hayakuonekana tena, hata friends of Lowasa nimekuja kuwaona msibani!, waliokuwa wanahangaika nae ni mkewe, watoto na familia, na marafiki wachache na serikali kumhudumia kwa mujibu wa sheria taratibu na kanuni.
Somo la Kifo cha Lowassa
Somo Kuu la kwanza la kifo cha Mwamba huu ni kijifunza kuweka akiba ya maneno, nikisikiliza baadhi ya clips za wanasiasa jinsi walivyokuwa wanamsema vibaya Lowassa akiwa hai, na sasa wamekuja msibani na kugeuza maneno bila aibu!, tujifunze kuweka akiba ya maneno na sometimes ni bora kunyamaza kimya.
Somo la pili ni kuwa determined, ukidhamiria jambo lako lishikilie, usikubali kukatishwa tamaa. Lowassa was a very determined person.
Somo la tatu ni Lowassa ni mwalimu mkubwa wa siasa za kuwa na kiasi, alikuwa CCM, akafanyiwa figisu akalatwa kwa figusu, akahamia Chadema. Akiwa Chadema hakuisema vibaya CCM, na aliposhindwana na Chadema na kurejea CCM, Lowassa hakuisema vibaya Chadema!. Ni wanasiasa wachache sana wana haiba ya namna hii. Leo kwenye msiba wa Lowassa CCM na Chadema wanashindana kumuenzi kwa kumzungumza kwa wema.
Pumzika Lowassa Pumzika, ulikuwa ni mtu miongoni mwa watu (of the people) na ukawatumikia watu kwa uwezo wako wote kwa kushirikiana na watu (by the people) na ukautoa uhai wako kwa ajili ya watu wako, kwa kifupi ni Lowassa ni ametufia (for the people)
Mwendo umeumaliza, imani umeilinda
Bwana Alileta, Bwana Ametwaa
Jina lake Lihimidiwe...
Adios....
Amigos...!
Paskali