KKKT Msikubali CCM iwageuze BAKWATA

KKKT Msikubali CCM iwageuze BAKWATA

Sisapoti hata kidogo wanachotaka kufanya kkkt, lkn kuhusu Yesu unaonekana hujui lolote, ila nitakusaidia mkuu.

Yesu hakuipinga serikali ya Roma iliyokuwa inatawala Israel kipindi chake Bali aliitambua kwa asilimia miamoja. Ndio mana aliwaambia wayahudi wanawajibika kulipa Kodi kwa Kaisari na vile vile kutoka sadaka kwa Mungu. (Ya Mungu mpeni Mungu na ya Kaisari mpeni Kaisari).

Waliomshitaki Yesu ni Wayahudi wenzie tena walimshtaki kwa maswala ya kiimani, ndio mana hata pilato(hakimu) hakuona kosa la Yesu kwa Sheria za kirumi akataka kumwachilia.

Pia hata askari wa kirumi Yesu aliwaasa wasiwachukulie watu Kodi Yao zaidi ya kiwango kilichowekwa (rushwa), hakuwaambia waondoke kurudi kwao ili Israel iwe huru.

Yesu hata aliwahi kuwaambia wayahudi kwamba vita vyake yeye ni vya kiroho (dhidi ya shetani) na sio vya kimwili (dhidi ya Dola ya Rumi).

Kwahiyo Yesu hakuipinga serikali, aliitambua japo ilikuwa haramu.
sawa, kama Bwana YESU alimpinga shetani, ni wazi pia kuwa aliipinga serikali haramu. Serikali haramu hutokana na huyo shetani.
 
Wataanza "kuwashughulikia" wale wenye mawazo huru.
 
anyway hizo porojo labda dhehebu la kipagani ndio wataelewa 🐒
Huko Lumumba hamnazo! yani nyie mama yenu hata avurude vipi na selikali yake haramu bado mnasifia na kutetea ujinga kweli njaa na uchawa mbaya sana
 
KKKT haifungamani na upande wowote na ndiyo msingi wa mafundisho ya kibiblia. Yesu alifundisha wapendeni adui zenu
 
Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) ni chombo kinachosimamia maslahi ya waislamu Tanzania lakini lisilokubalika na baadhi ya kizazi kipya cha waislamu.

Vijana wengi wa kiislamu hulishutumu Baraza hilo kutumiwa kisiasa kufanikisha maslahi ya CCM.

Miaka ya hivi Karibuni BAKWATA walibadili mfumo wao wa kupata masheikh wa mikoa kutoka masheikh wa kuchaguliwa na waislamu wa mkoa husika hadi masheikh wa kuteuliwa toka makao Mkuu ya BAKWATA.

Mfumo huo mpya ambao umelipa mamlaka Baraza la maulamaa kuteua masheikh wa mikoa, umeleta hofu na sintofahamu.

Kanisa la Kilutheri la Kiinjili Tanzania (KKKT) na lenyewe liko kwenye harakati za kubadili Katiba ya kanisa hilo kumpa mamlaka Mkuu wa kanisa mamlaka ya kuhamisha na kuteua Maaskofu.

Nasikitika kuwaambia KKKT mpango wa kubadili Katiba yao na kumpa mamlaka Mkuu wa kanisa kuteua na kuhamisha Maaskofu, umekaa kisiasa zaidi na utawagharimu.

Siku Katiba hiyo ikipitishwa, ndiyo KKKT itaanza kutumiwa kisiasa na CCM. Hivi Maaskofu wenye fikra huru kama Bagonza watasalimika kweli?
Wasigeuzwe mara ngapi na wamesha kuwa kitambo na hongo wanapokea
 
Hii ni baada ya CHADEMA kushindwa kuifanya KKKT kuwa tawi leo. Malasusa shikilia hapohapo.
 
Huko Lumumba hamnazo! yani nyie mama yenu hata avurude vipi na selikali yake haramu bado mnasifia na kutetea ujinga kweli njaa na uchawa mbaya sana
tuliza mihemko na porojo useless, haimsaidii wala kubadili chochote hiyo,
it's just hot air 🐒
 
Siyo kwamba wameshageuzwa BAKWATA? Si ndiyo askofu wao mkuu juzi alimtunuku Samia sijui nini, yule baba mjasiriamali anayejali tumbo lake tu? Ksema kweli mimi nanona yuko Bagonza tu mwenye msimamo, wengi ni chawa.
😆😆 Walikata jina la Bagonza kwenye uchaguzi wa askofu mkuu pamoja na kupata kura za wajumbe wengi, kama alivyofanyiwa Mtaka kwenye uchaguzi kamati ya olimpiki.

Kanisa linaloendeshwa kisiasa.
 
Kwamba kwenye kanisa la Lutheran ( KKKT)kila nchi wana uhuru wa kufanya mambo kwa taratibu tofauti na hakuna utaratibu mmoja unaotumika dunia nzima? .
Mwenye uelewa wa taratibu za Kanisa hilo anijuze.
 
Sijaona Cha ajabu kuwa na huo mfumo Ila kama wana mengine na CCM ndo ttzo pamoja na hayo KKKT ina mambo mengi hasa issue za uongozi ni mtiti haswa Ila mfumo mpya utakuwa vzr zaidi kwa watu wa matengenezo

Tuimbe kidogo

Nataka kuingia mjini kwa Mungu,

Nitashinda nitakaza mwendo nifike
 
Sisapoti hata kidogo wanachotaka kufanya kkkt, lkn kuhusu Yesu unaonekana hujui lolote, ila nitakusaidia mkuu.

Yesu hakuipinga serikali ya Roma iliyokuwa inatawala Israel kipindi chake Bali aliitambua kwa asilimia miamoja. Ndio mana aliwaambia wayahudi wanawajibika kulipa Kodi kwa Kaisari na vile vile kutoka sadaka kwa Mungu. (Ya Mungu mpeni Mungu na ya Kaisari mpeni Kaisari).

Waliomshitaki Yesu ni Wayahudi wenzie tena walimshtaki kwa maswala ya kiimani, ndio mana hata pilato(hakimu) hakuona kosa la Yesu kwa Sheria za kirumi akataka kumwachilia.

Pia hata askari wa kirumi Yesu aliwaasa wasiwachukulie watu Kodi Yao zaidi ya kiwango kilichowekwa (rushwa), hakuwaambia waondoke kurudi kwao ili Israel iwe huru.

Yesu hata aliwahi kuwaambia wayahudi kwamba vita vyake yeye ni vya kiroho (dhidi ya shetani) na sio vya kimwili (dhidi ya Dola ya Rumi).

Kwahiyo Yesu hakuipinga serikali, aliitambua japo ilikuwa haramu.

Mkuu TAI DUME, shukrani kwa mchango wako mzuri wenye mtazamo wa kihistoria na kimaandiko. Kwenye hoja yako ya msingi upo sahihi kwa asilimia kubwa: Yesu hakuwa mwanamapinduzi wa kisiasa aliyetaka kupindua Dola ya Roma kwa mtindo wa msituni au kijeshi. Alilenga mapinduzi ya kiroho. Hata hivyo, unachukulia mambo juujuu sana na unashindwa kuelewa maana halisi ya uanaharakati (activism) wa kimkakati. Ili kuweka kumbukumbu sawa na kuongeza nyama kwenye mjadala huu wa JF, kuna maeneo madogo ya kihistoria na kimaandiko yanayohitaji marekebisho kidogo (fine-tuning):
Kwanza, ulipomchanganya Yesu na Yohana Mbatizaji. Pale uliposema Yesu aliwaasa askari wasichukue kodi zaidi ya kiwango (rushwa), hapo umempa Yesu mistari ya Yohana Mbatizaji. Kimaandiko katika Luka 3:14, ni Yohana ndiye aliyewaambia askari waliomwendea: "Msidhulumu mtu, wala msishtaki kwa uongo; tena mtolewe na mishahara yenu."
Pili, kuhusu mtego wa kodi (Je, alitambua mamlaka ya Roma kwa 100%?). Siyo kwa asilimia mia moja mkuu. Ule mtego wa kulipa kodi kwa Kaisari haukuwa swali la kawaida tu la darasani kama unavyofikiria wewe hapo. Huo ulikuwa ni mtego mzito wa kijasusi na kisheria uliolenga kumgombanisha Yesu na Serikali ya Kirumi ili iwe rahisi kumfungulia mashtaka ya uhaini na kumnyonga. Waliomtega walijua fika: Kama Yesu angesema "Msilipe kodi," wangemkaba koo na kumpeleka kwa Gavana Pilato kama muasi wa serikali. Na kama angesema "Lipeni kodi," wananchi wa kawaida (raia wanyonge waliokuwa wananyonywa na kodi hizo za kikoloni) wangemwona Yesu ni msaliti na kibaraka, na harakati zake za kuwatetea zingekufa siku hiyo hiyo.
Akili kubwa ya uanaharakati wa kiwango cha juu (genius activism) wa Yesu ulionekana pale alipoutategua ule mtego wao kwa kuwauliza wao wenyewe sarafu ina sura na anwani ya nani. Walipomwambia ni vya Kaisari, akawapiga na ile punchline ya karne katika Mathayo 22:21: "Basi, mpeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na Mungu yaliyo ya Mungu." Kaisari alijiona yeye ni Mungu na kila kitu ni chake. Yesu kwa kutenganisha vitu vya Kaisari na vya Mungu, aliweka mipaka ya utii. Alimaanisha kuwa utii mkuu (dhamiri, ibada, na utu wa mtu) ni mali ya Mungu pekee, siyo ya serikali dhalimu ya Roma. Hapo aliwanyamazisha watesi wake, akalinda harakati zake mitaani, na akaonyesha kuwa serikali haina haki ya kuwadhulumu au kuwanyonga raia wake.
Tatu, kosa la kusulubiwa lilikuwa la kisiasa (Uhaini). Ni kweli viongozi wa Kiyahudi walimchukia kwa masuala ya kidini. Lakini walipompeleka kwa Pilato, walijua Pilato (Kama Gavana wa Kirumi) hawezi kumhukumu mtu kifo kwa makosa ya kidini ya Kiyahudi. Ndiyo maana walibadili mashtaka mbele ya Pilato yakawa ya kisiasa, wakidai Yesu anajifanya "Mfalme" na anazuia watu kulipa kodi (Luka 23:2). Roma ilimsulubisha Yesu kwa kosa la Uhaini (Sedition/Treason) dhidi ya Kaisari, na ndiyo maana msalabani wakaandika shtaka lake la kisiasa: "Mfalme wa Wayahudi."
Hitimisho:
Uko sahihi kabisa kwamba Yesu hakuwa mwanasiasa wa mrengo wa kushoto aliyetaka kuiondoa Roma kimwili ili Israel iwe huru. Lakini mafundisho na harakati zake zilikuwa hatari sana kwa watawala kwa sababu yalifundisha kwamba mamlaka ya Mungu yapo juu ya mamlaka yote ya kidunia. Kuwa mwanaharakati sio kuwa mjinga wa kukurupuka na fujo za kujipeleka gerezani kabla ya wakati. Yesu alikuwa mwanaharakati mwenye akili nyingi sana (strategic activist) aliyepambana na mifumo dhalimu kwa akili kubwa na akawashinda wote waliotaka kumziba mdomo!
Nawasilisha, Mkuu!


 
Back
Top Bottom