Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,748
- 50,170
Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) ni chombo kinachosimamia maslahi ya waislamu Tanzania lakini lisilokubalika na baadhi ya kizazi kipya cha waislamu.
Vijana wengi wa kiislamu hulishutumu Baraza hilo kutumiwa kisiasa kufanikisha maslahi ya CCM.
Miaka ya hivi Karibuni BAKWATA walibadili mfumo wao wa kupata masheikh wa mikoa kutoka masheikh wa kuchaguliwa na waislamu wa mkoa husika hadi masheikh wa kuteuliwa toka makao Mkuu ya BAKWATA.
Mfumo huo mpya ambao umelipa mamlaka Baraza la maulamaa kuteua masheikh wa mikoa, umeleta hofu na sintofahamu.
Kanisa la Kilutheri la Kiinjili Tanzania (KKKT) na lenyewe liko kwenye harakati za kubadili Katiba ya kanisa hilo kumpa mamlaka Mkuu wa kanisa mamlaka ya kuhamisha na kuteua Maaskofu.
Nasikitika kuwaambia KKKT mpango wa kubadili Katiba yao na kumpa mamlaka Mkuu wa kanisa kuteua na kuhamisha Maaskofu, umekaa kisiasa zaidi na utawagharimu.
Siku Katiba hiyo ikipitishwa, ndiyo KKKT itaanza kutumiwa kisiasa na CCM. Hivi Maaskofu wenye fikra huru kama Bagonza watasalimika kweli?
Vijana wengi wa kiislamu hulishutumu Baraza hilo kutumiwa kisiasa kufanikisha maslahi ya CCM.
Miaka ya hivi Karibuni BAKWATA walibadili mfumo wao wa kupata masheikh wa mikoa kutoka masheikh wa kuchaguliwa na waislamu wa mkoa husika hadi masheikh wa kuteuliwa toka makao Mkuu ya BAKWATA.
Mfumo huo mpya ambao umelipa mamlaka Baraza la maulamaa kuteua masheikh wa mikoa, umeleta hofu na sintofahamu.
Kanisa la Kilutheri la Kiinjili Tanzania (KKKT) na lenyewe liko kwenye harakati za kubadili Katiba ya kanisa hilo kumpa mamlaka Mkuu wa kanisa mamlaka ya kuhamisha na kuteua Maaskofu.
Nasikitika kuwaambia KKKT mpango wa kubadili Katiba yao na kumpa mamlaka Mkuu wa kanisa kuteua na kuhamisha Maaskofu, umekaa kisiasa zaidi na utawagharimu.
Siku Katiba hiyo ikipitishwa, ndiyo KKKT itaanza kutumiwa kisiasa na CCM. Hivi Maaskofu wenye fikra huru kama Bagonza watasalimika kweli?