Kiswahili kinaliangamiza taifa

Naomba nikuulize maswali yafuatayo:
Je, ni lugha gani kati ya kiingereza na kiswahili, inamchango mkubwa katika maendeleo ? na ni kwa nini?
Hivi Mkuu una uelewa wa namna gani? mbona hata maswali yako hayana mshiko? Unauliza lugha yenye mchango mkubwa katika maendeleo kati ya Kiswahili na Kiingereza bila ya kutaja mchango wa maendeleo gani na nchi gani, unatarajia ujibiwe vipi? Unataka useme maendeleo yaliyoko uchina, Ujerumani, Urusi, Italia, Ufaransa, na nchi kibao zisizozungumza hicho kiingereza unachokiabudu yaliletwa kwa kuzungumza Kiingereza? Ni viongozi wenye mawazo kama yako ndiyo walioididimiza lugha hii kuwa kama ilivyo, wameshindwa kuchukua hatua thabiti kuiimarisha. Inashangaza lugha inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 100 waliosambaa katika mataifa zaidi ya kumi wewe unasema si lugha ya kimataifa! Nasisitiza tena ukikiona Kiingereza ni kipana, kirefu au kinapendeza ujue nyuma ya pazia wapo watu wanaokifanya kionekane hivyo.

 
ndugu yangu!haya unayozungumza umefanyia utafiti kweli?hivi lugha ndio kikwazo cha sisi kuto tambulika au kuto kuwa na maendeleo?naomba nitofautiane na wewe kwa hilo.mimi na amini fikra sahihi huja kwa lugha sahihi inayoeleweka kwa jamii husika.nilisha wahi fika china,kwakweli wale jamaa ni kichina kwa kwenda mbele unaweza shindwa nunua kitu dukani au kwenda mahali fulani kwa kuwa mmeshindwa kuelewena kwa lugha lakini hebu angalia walivyopiga hatua kimaendeleo kwa kila nyanja!hivyo basi usitukuze lugha za kigeni na kuacha za kwako kisa eti hatutaendelea,jaribu kuja na mbinu mbadala ya sisi wapi tumekosea ila hili la lugha hapana!


kweli kabisa kaka jidu(kama sijakosea) cha msingi ni kuwa na msimamo, haina maana kuwa kiingereza tukiache la hasha!! tujifunze kama lugha ya pili lakini si ifanye tupuuze lugha yetu!!! mfano tanzania ni nchi tajiri sana kwa madini,na mali asili nyigine, madini kama tanzanite huwezi yapata popote isipokuwa tanzania, hivyo ni jukumu la viongozi kusimamia kuwa mikataba haiwezi kufungwa kwa lugha tofauti na kiswahili tuone kama hawatakuja kuwekeza!!!!!!
 
masauni hoja yako haina mashiko, ndio maana hata wewe mwenyewe hukijui hicho kiswahili, kumbuka nguo ya kuazima haisitiri ******!
tunahitaji kiswahili kwa mawasiliano ya ndani na umoja wetu lakini pia tunazihitaji lugha za kigeni sio kiingereza tu kwa mawasiliano ya kimataifa
hiyo mifano uliyotoa ya aljazera na tb joshua ni sehemu ndogo tu ya dunia wanaotazama, usizuzuke na ule wingi wa watu! nimebahatika kuizunguka kidogo dunia hivyo vipindi havipo sehemu kubwa ya nchi nilizopata kufika
KUKIDHARAU KISWAHILI NI KUJIDHARAU NI KUJISHUSHA THAMANI KAMA MTANZANIA
 
Hata waziri wetu wa Elimu ....Mulugo alituaibisha South Africa kwa kuchapia Kiingereza
 
Nimepita haraka haraka kwenye tovuti ya Benki ya Dunia, miongoni mwa mataifa maskini 20 duniani zimo Haiti, Niger, Sierra Leone, Zimbabwe, Malawi, Togo, Liberia na Uganda, nchi ambazo ni wazungumzaji wa Kiingereza tokea mwanzo.
Mtoa mada nahisi umevurugwa...
 
mleta mada kungekuwa na kitufe cha """"UNLIKE""" ningekubonyezea...we kingereza unakijua kwanza???
 
Upuuzi mtupu kuleta takataka zako humu jf, huo muda ungeutumia kulala tu na sio kuweka takataka zako humu jamvini
 
Mkuu kwanza hongera kwa bahati (au jitihada) ya kipekee kuishi nje ya Tanzania. Pili, sidhani kama kiingereza kinapuuzwa hapa Tanzania na ndio maana kwanza kinafundishwa kama somo ngazi za awali na ndio lugha rasmi ya kufundishia ngazi ya sekondari na kuendelea.

Pili kulegalega kwa kiingereza isichukuliwe ni kutokana na kupuuzwa kwake kwani hata hicho kiswahili chenyewe wala hakina au hakifundishwi kwa ubora unaotakiwa.

So, generally, tatizo halipo kwenye kiingereza bali tuna tatizo zaidi ya lugha. Ni almost kila kitu hatukiwezi karibu kila nyanja ya maisha. Kwa mfano, hivi hata kuweka mazingira yetu safi ili tusisumbuliwe na kipindupindu kila wakati tunahitaji kiingereza? Hivi kondakta wa daladala anahitaji kujua kiingereza ili asimnyanyase mwanafunzi? Hivi tunahitaji kujua kiingereza ili tusijisaidie ovyo mitaani? Hivi tunahitaji kujua kiingereza ili tusikwepe kodi au kuiba mali ya umma, ufisadi, n.k?

Tatizo sio lugha bali mfumo. Na mfumo, nionavyo mimi, unahusisha tabia zetu, desturi zetu, siasa zetu, mila zetu (imani za kishirikina, n.k.), mahusiano yetu, na hata dini zetu. Kama wachina waliweza kwa lugha yao na "sasa hivi" ndio wanajifunza lugha za kigeni kwa nini sisi tushindwe? Ni maoni yangu.

Wewe ndio umemaliza kila kitu maana nchi kama nchi inatambua umuhimu wa kiingereza tena kinafundishwa tangu darasa la 3 kikubwa kuna sehemu tumeteleza tukashindwa kukipa msukumo mkubwa ili kila mtu akielewe pia na masomo mengine pia yamechakachuliwa, lakini bado na kiswahili chetu kinatakiwa kipewe kipaumbele ili kusiwe na gap la kimawasiliano kati ya tabaka moja la watu na wengine. Ukiondoa Zambia na ukienda tu nchi za jirani kama Kenya na Uganda utakuta ndio watu wengi waliopita katika elimu ya kawaida wanajua kiingereza lakini bado kuna watu wengine wengi hawajui hiyo lugha matokeo yake mtu mwingine anazungumza Kinyankole hajui Kiingereza wala Kiswahili. (unakuta hakuna consistence katika matumizi ya lugha)

Point na mbili ya mleta uzi kiukweli kuna baadhi ya vitu ni kwa ajili ya wenyeji kwa kuwa wengi ndio wanatumia barabara na mitaa hiyo hivyo hata kama Kiingereza ni lugha ya kimataifa ila kuna wakati mwingine mgeni nae anatakiwa ajifunze utamaduni wa wenyeji wake ikiwemo na lugha ya mahali husika (baisic).

Mie nadhani hoja hapa ni kutoa michango ya namna gani ya kuboresha ufundishaji na matumizi ya lugha hii ya kiingereza ikiwa pamoja na kuhakikisha mitihani yetu katika mashule mwanafunzi hasa ya kiswahili, kiingereza na hata kama kifaransa mbali ya kufanya written kuwe na maksi kiasi flani zinatolewa kwa mtihani kwa oral but baada ya kuhakikisha tunatengeneza waalimu wa kutosha maana tatizo lililopo hata hao walimu hasa wa shule ya msingi wengi walipata maksi za chini karibu masomo yote including English (hasa hawa waalimu kuanzia 1998 - 2012 ambapo utaratibu ule wa kuchaguliwa moja kwa moja ulipofutwa though sio wote)

Kikubwa nafikiri ni ku-promote watu wafanye kazi kwa bidii ili wajijenge kiuchumi huku juhudi za ku-promote English na kuboresha mazingira ya ufundishaji hasa primary school maana pamoja na kufundishwa english tangu darasa la 3 bado wengi wana-gain wakianza sekondary which means tukikomaa shule ya msingi tutakomaa
 
Am not surprised! utakuta mara nyingi wasio jua kingereza ndo wakwanza kusema hatuhitaji kingereza! utajuaje kama hukuhitaji wakati hukijui?
Ukiangalia the 'bigger picture' information na elimu tunayohitaji kuendelea ipo katika lugha ya kingereza au lugha zingine zilizoendelea zaidi kama kifaransa na kichina.
wachina na wafaransa wameweza kuendelea na lugha zao kwasababu lugha zilikuwepo toka 'industrial revolution' na zimekua kwa pamoja na utandawazi, tusisahau kwamba ni wangapi duniani wanaongea kichina na kifaransa? watu zaidi ya 1 billion wanaongea na kuandika kichina na zaidi ya 500 million wanaongea kifaransa vizuri, na 1.5 billion kingereza. swahili 30 million. ila we demand to give it equal share!
Unaweza kutrain daktari/enginneer/lawyer from scrach kwa kifaransa au kichina bila kutumia neno hata moja la kingereza je itagharimu miaka mingapi na shingi ngapi kufanya hivyo kwa kiswahili?! vitu kama matokea ya research kibao zinaandaliwa kwa kingereza, sasa ebu niambieni kama huwezi ukaelewa haya matokeo si utapoteza mda kufanya research yako? ambayo ni marudio?

Mtu anasema proudly kwamba wawekezaji wakija walazimishwe kujifunza kiswahili!!! huoni kwamba ni kupoteza mda na hela kibao, we need to get our priorities right!

Tanzania is not an island but we spend so much time and enrgy trying to make it one, acting like we dont need the rest of the word, trying to impose swahili like its the corner stone to mankind! really?!
 
Nimepita haraka haraka kwenye tovuti ya Benki ya Dunia, miongoni mwa mataifa maskini 20 duniani zimo Haiti, Niger, Sierra Leone, Zimbabwe, Malawi, Togo, Liberia na Uganda, nchi ambazo ni wazungumzaji wa Kiingereza tokea mwanzo.
Mtoa mada nahisi umevurugwa...
usiwe mwepesi kuropoka!!!, soma mada, elewa, tafakari, jibu.
 
Tena kama tungejitahidi tukatumia kiswahili hata mpaka chuo kikuu elimu yetu ingekuwa ya uelewa zaidi kuliko sasa hivi ambapo tunatumia kiingereza kucram vitu tusivyovielewa kwa kiingereza

Nchi haiwezi kuendelea na kuwa na amani Kwa kutumia lugha za kigeni.Huo ni ujinga ambao ni mwafrika tu anayeutukuza.
anza kwa kuchapisha kitabu cha chemistry kwa kiswahili. no! kwanza tafuta hilo somo kwa kiswahili linaitwaje, na usiseme 'kemia'. kemia sio kiswahili
 
hydrogen sahihisha taarifa zako kwanza.
Watu wanaosema na kuandika Kiswahili sio Milioni 30, ni kati ya Milioni 120 na 150 hivi kwa mujibu wa tafiti zilizochapishwa na BBC mwaka 2005, inawezekana namba hiyo imeongezeka miaka ya karibuni.
Halafu unaweza kunisaidia idadi ya wasemaji wa Kijerumani, Kireno na Kihispania ili tufanye utafiti linganifu kuliko kulumbana kutokea hewani?
 
Last edited by a moderator:
Hata chemisty sio Kiingereza, ni Kilatini.

duh! Tipical!!

ok. lengo sio kujua chemistry ni kilatini/ kiingereza. tusiongee tu ili tuonekane kama si tuwazalendo sana au ndo tunapenda mila zetu kuzidi watu wote...... kutafsiri vitabu vinavyotumika secondary na vyuoni itachukua miaka mingapi na kutugharimu sisi walipa kodi shi'ngi ngapi? je tuko tayari kugharamika na kusubiri au ni maneno tu? maana yangu ilikua kwamba its imposible kufundisha hasa masomo ya sayansi kwa lugha ya kiswahili. na information ndio power ya maendeleo. so, Mphamvu nilitaka nikuonyeshe kwamba lugha yetu bado changa na sio kujua neno chemistry ni lugha gani, labda kwa kukufahamisha tu ni kwamba chemistry is greek origin not latin!
 
Sasa nani kakuzuia kujifunza lugha ya kigeni? Tatizo la Tanzania si Kiswahili kingi bali ni Kiswahili kidogo. wewe mwenyewe hujui Kiswahili wataka kujua Kiingereza? Watu hurahisisha hawalahisishi.
Wageni hawa unaowataka ni wageni wapi? Mbona tanzania imezungukwa na majirani wazungumzao Kiswahili? Anza kusafiri kwanza halafu ndio uandike.
 
ndugu yangu!haya unayozungumza umefanyia utafiti kweli?hivi lugha ndio kikwazo cha sisi kuto tambulika au kuto kuwa na maendeleo?naomba nitofautiane na wewe kwa hilo.mimi na amini fikra sahihi huja kwa lugha sahihi inayoeleweka kwa jamii husika.nilisha wahi fika china,kwakweli wale jamaa ni kichina kwa kwenda mbele unaweza shindwa nunua kitu dukani au kwenda mahali fulani kwa kuwa mmeshindwa kuelewena kwa lugha lakini hebu angalia walivyopiga hatua kimaendeleo kwa kila nyanja!hivyo basi usitukuze lugha za kigeni na kuacha za kwako kisa eti hatutaendelea,jaribu kuja na mbinu mbadala ya sisi wapi tumekosea ila hili la lugha hapana!

Haina haja ya kufanya research kwa mambo ambayo tunayaishi. China sio Tanzania. Wale wanajitosheleza kwa teknolojia na hawana haja ya kuomba misaada kama tufanyavyo.

Ni mtumwa ndio hujifunza lugha ya bwanaake. Sisi ni wategemezi na utegemezi wetu ndio unatugharimu. Usiniambie kuwa tuna jeuri ya kujifunza kwa lugha ya kiswahili huku entry requirements za vyuo vya ulaya tunavyokimbilia kusoma vinataka uwe na intermediate level ya Kiingereza.

Achana na kampeni za kina Makih Hassan na BAKITA yao. Hapa hapa tu ukiwa huna fluency ya kiingereza hupati kazi, leo hii mtu akutie ujinga eti kiswahili, we usijidanganye.
 
duh! Tipical!!

ok. lengo sio kujua chemistry ni kilatini/ kiingereza. tusiongee tu ili tuonekane kama si tuwazalendo sana au ndo tunapenda mila zetu kuzidi watu wote...... kutafsiri vitabu vinavyotumika secondary na vyuoni itachukua miaka mingapi na kutugharimu sisi walipa kodi shi'ngi ngapi? je tuko tayari kugharamika na kusubiri au ni maneno tu? maana yangu ilikua kwamba its imposible kufundisha hasa masomo ya sayansi kwa lugha ya kiswahili. na information ndio power ya maendeleo. so, Mphamvu nilitaka nikuonyeshe kwamba lugha yetu bado changa na sio kujua neno chemistry ni lugha gani, labda kwa kukufahamisha tu ni kwamba chemistry is greek origin not latin!

Hoja imetoka kwa kukurupuka, ngoja na sisi tuoneshe mwitikio huo huo.
Uingereza wapo mataahira wa kutosha, nadhani kwa ujuvi wao wa Kiingereza wanafaa kuajiriwa kuliko wasomi wetu wanaozungumza brokeni Inglish...
Si eti eh?
 
Hivi sasa dunia ni kijiji kimoja watu wanafanya bidii kuelewa lugha inayounganisha dunia nzima nyie mmepinda na miradi yenu ya kifisadi ya kuandika vitabu vya chuo kikuu kwa kiswahili. Hao wanafunzi wa kusoma kwenye hivyo vyuo hawatakiwi kuwa wa kimataifa? Leo mnatumia internet ya kiswahili? au ndio mana wengine hamuwezi kuchangia mada za kiingereza? kwenye face book mnaandika vishotishoti hata sentensi haikamiliki? vyuo vikuu vinatumika vitabu mpaka walivyoandika kina Plato na kina Pythagoras navyo mtavitafsiri? hayo ni mawazo mgando na naomba kuunga mkono hoja
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom