Kiswahili kinaliangamiza taifa

Tanzania ni nchi maskini bado hivyo tusitegemee lugha yetu kukua kwa haraka labda mtu ajifunze kea ridhaa yake na ili sisi tafanikiwe ktk nyanja mbali mbali tunahitaji kujifunza kingereza kwa namna moja au nyingine kitasaidia kujikwamua ktk hatua kadhaa tunazokutana nazo maishani

Mkuu, elimu yako ni ndogo sanaaaaaaaaaa au umesoma na hukelimika. Kwahiyo unatakakutuambia kuwa Uingereza kwamfano walianza na Kihaya au Kiswahili? Umasikini wetu umeletwa na Lugha za kigeni kwakuwa tunawekeza zaidi ya 56% ya kisomo chetu kwenye kiingereza hasa baada ya elimu ya msingi.

Hivi kuchimba madini, kuuza samaki wetu, kuu, .... kunahitaji Kiingereza? Baada ya kushindwa kidato cha nne, cha sita, au ata baada ya kuajiriwa mfano wewe ulipoajiriwa una kitumia kiingereza kwa kwa siku mara ngapi kama si Kiswangilish?
 
Ndugu yangu nakubaliana kuwa lugha za kigeni kikiwemo Kiingereza ni muhimu katika internaional forums na mawsiliano ya kimataifa kwa ujumla. Lakini si kweli kwamba maenedleo duni katika nyanja za uchumi na maendeleo katika Tanzania yanasababishwa na mataumizxi ya lugha ya Kiswahili.Wewe unasema unakaa je unakaa nch gani wewe? Mimi nimetembea almost the whole of Europe, North and South America pamoja na Asia. Utafiti wa Kisayansi unaonesha kuwa hakuna hata nchi moja Duniani iliyoendelea kwakutumia lugha ya nchi nyingine. Nimefika ufaransa, Norway, taly hukutimtu anaongea lugha nyingine zaidi ya lugha zao wenyewew mbaya zaidi hata kama anafahamu Kiingereza hataki kuongea hata ukienda Ujerumani ni hivyohivyo. Nimefika Istanbul-Turkey, hakuna hata bango moja lililokuwa limeandikwa kwa Kiingereza yote ni Kiturkish tu na nchi inayoendelea sana kiviwanda sasa hivi na wanatumia lugha yao tu kwenye shule zote, ukienda Rusia wanatumia kirusi. Angalia nchi jirani kama Zambia na Malawi na hata Uganda ambao wanatumia lugha za nje lakini hakuna maendeleo ya kuridhisha kiuchumi na hata asisi tuko mbele yao. Angalia Nigeria pamoja na Kiingereza na utajiri mkubwa wa mafuta lakini asilimia kubwa wako below ppovert line na hata Lagos pale huwezi kukaa 24 hrs bila umeme kukatika na ukitoka nje kidogo tu ya Lagos unaona umasikini mubwa. Sasa tatizo la umasikini na hali mbaya ya uchumi haliletwi na lugha ya kiswahili. Ila nakili kwamba lugha hususani ya Kiingereza ni muhimu bado kwa mawasiliano ya kimataifa ila si kweli kwamba Kiswahili kinatufanya tuwe tulipo, na still ninapendekeza lugha si ya Kiingereza tu bali hata international languages zingine zifundishwe kuanzia shule za awali ili tupate better understanding ya lugha lakini si kwasababu ya kutuletea maendeleo ya kiuchumi na kuondoa umaskini kwakuwa hata nchi nyingi za Kiafrika zinazotumia lugha za nje either Kiingereza au Kfaransa bado ni masikini sana pamoja na kuwa na language advantae. Naomba tukienzi Kiswahili, tufanye juhudi za makusudi kuondoa ufisadi na tuongeze uwajibikaji ili kukuza uchumi wetu na kuondoa/kupunguza umasikini uliokithiri.

Ndugu yangu mimi nakaa nje ya Tanzania kwa miaka mingi sasa. kabla ya kuondoka Tanzania nilikuwa proud sana na kiswahili lakini baada ya kukaa nje nimegundua viongozi wetu walikosea sana kusisitiza kiswahili na kupuuza kiingereza!! Ndugu yangu narudia tena kwa nchi masikini kama Tanzania, lugha ya kiingereza ni muhimu sana.
 


Hapo kwenye mstari...ni kweli au urongo???

Hivi mjerumani(mwenye uchumi unaoongoza barani ulaya) ametumia kiingereza kufika hapo alipo???!!!

Nadhani maendeleo ni zaidi ya lugha...kama hatusomi, hatufanyi kazi kwa bidii, hatulei na kukuza ubunifu, sifikiri kama lugha pekee itatufikisha kwenye nchi ya kanaani!!!

Nakumbuka tukiingia sekondari miaka ya mwanzo wa tisini, tulikutana na vijana kutoka Arusha School ambao walikuwa wakisakata kimombo kweli kweli...lakini baada ya muda nasi tukiwa tayari kimombo kimenza kukubali...tulikuwa level moja na hatimaye baadhi yao tukawapiku, siri ikiwa ni kujituma na kusoma kwa bidii.

Niseme kwamba, tunakihitaji sana kizungu na kwa maneno ya Mh Lowasa, tunakihitaji kichina. Lakini bado bila ya vitu hivyo nimevitaja hapo juu...Lugha si lolote si chochote.

Ndg. yangu umesema kweli tupu, wengi wanaopigia upati english ni watumwa wa ukoloni, nilikutana na mwl. mmoja kazini, wakati huo ndiyo kwanza nimemaliza degre yangu ya kwanza, alikuwa shabiki sn wa english humwambia kitu kuhusu kiswahili, mpaka siku moja alinitukana na kuniita kuwa mimi sio msomi kwa 7bu nashabikia kiswahili badala ya english, ila baadae nilijua tambua kuwa alikuwa amesimamishwa masomo pale UDSM kwa utovu wa nidhamu, naona yule jamaa ni sawa na mtoa mada hii. hivi kilichomfikisha hapo alipo ni english au ni elimu aliyo nayo. hapa BONGO tumejichanganya wenyewe tatizo la umaskini wetu sio lugha

tusiwe na mawazo mgando, hata sasa ukiamua ujue kichina utajua tu, lakini hutapata maendeleo kwa kujua kichina, maendeleo yakuja kwako kwa kufanya kazi kwa bidii basi na si vinginevyo!!!!!!!!!!!1
 
Tena kama tungejitahidi tukatumia kiswahili hata mpaka chuo kikuu elimu yetu ingekuwa ya uelewa zaidi kuliko sasa hivi ambapo tunatumia kiingereza kucram vitu tusivyovielewa kwa kiingereza

Nchi haiwezi kuendelea na kuwa na amani Kwa kutumia lugha za kigeni.Huo ni ujinga ambao ni mwafrika tu anayeutukuza.
 
Ninaomba kuanzisha hii mada baada ya kusikia kwamba kuna mahali walimu wamefukuzwa kwa sababu ya kuongea kiswahili katika mazingira ya shule.
Niseme tu kwamba naunga mkono jambo hilo kwa asilimia mia. Sababu ni hizi hapa.

1. Tutambue kuwa kiswahili ni lugha inayozungumzwa sana Tanzania na ukitoka nje ya mipaka ya Tanzania kiswahili chako unaweka mfukoni! Lazima tujufunze lugha za kimataifa(English) ili tulahisishe mawasiliano na mataifa mengine.
Hoja hii umeitoka kwa kukurupuka,hujatuonesha madhara yake. Kwahiyo ina matatizo gani sasa!!! Au ulitaka kumaanisha kuwa ukifika China na hela yako huwezi kununua bidhaa? kwahiyo watanzania wajifunze Lugha zot e za dunia hii kwamba ukitaka kwenda Rwanda, Angola, SA, Brazil, Korea, China.... ujifunze lugha zao kwanza. Au unamaanisha hakuna wakarimani? Ukienda kuomba omba at?

2. Wageni wakija Tanzania wanapata taabu kweli, matangazo ya biashara yameandikwa kwa kiswahili, barabara nazo unakuta vibao vimeandikwa kwa kiswahil mfano PITA KUSHOTO. Sasa jamani wageni wetu ambao wengi wanakuja kwa maswala ya biashara inakuwa ngumu sana.Mgeni kuendesha gari tanzania ni ngumu sana. Mgeni kufanya biashara Tanzania ni ngumu sana!! Kuna jamaa wafanyabiashara wengi sana nawafahamu wanaprefer kwenda Kenya na Uganda kuchukua bidhaa kuliko Tanzania na sababu wanazozitoa ni ugumu wa Lugha.wanasema kwenda Tanzania ni gharama zaidi maana inabidi umtafute mkalimani ambaye utamlipa.

Hoja hii ni kichekesho, kwakifupi hiyo ndo ajira ya watu wetu kufanya kazi ya ukarimani. Nadhani hujui kuwa pengine hawana wakitakacho na kama kingekuwepo basi wataitumia lugha yetu mara moja. Alafu Sasa tukitoka hapo tutakuomba upendekeze tutafsiri ata majina yetu, mitaa yetu..... hii ni hatari, kisa tuwapendezeshe wageni. Wanaenda kenya si kwakuwa kunatumika Kiingereza bali ni sera na taratibu nzuri za uongozi wa Kenya. Huku serikali imelala. Ni ufisai kwenda mbele. na kwa taarifa yako wakija huku wanaenda kwa wamasai na si UDSM mf!


3. Kenya inatangaza mlima kilimanjaro kwa sababu ya Lugha wanayotumia inaeleweka duniani kote. Sisi tunatangaza mlima kilimanjaro kwa kiswahili wataelewa nini wageni?
Hoja hii si ya kweli. Nadhani hujafanya itafiti au umetumwa kuinusuru CCM na ulalaji usingizi na kukosa ubunifu. Hapa bila kuuma uma maneno ni uzembe wa Serikali na idara ya utalii hasa wizara nzima. Hakuna anayewazuia kutangaza kwa lugha zote za dunia hii. Wamelala.

4.Tunawasanii wazuri sana wa muziki, tamthiliya, vichekesho, ambao wangesaidia sana kuitangaza nchi yetu kimataifa na wao pia kufaidika, lakini wamebaki eti wasanii wa BONGO. (Kwa wale mliobahatika kuangalia stand up Zambia kilichorushwa na Africa magic channel mtakubaliana na mimi wale jamaa 3 walioshinda sasa hivi ni comedian wakimataifa wanazunguka nchi mabalimabali sababu ni lugha tu, maana kwa ukweli hawawezi kumfikia Joti, Masanja.
Ndugu yangu, tatizo hujanijibu maswali yangu ya awali, una mambo mengi huyajui, nakusaidia, Kazi yoyote ni lazima uisomee. kama hujaisomea uifanye kwa kiwango cha kimataifa. Kina masanja wanaifanya kwa kiwango cha Bongo hasa Dar na Uswazi tu. hawa jamaa wamekuja tu toka mtaani na wasanii wetu wengi hawajaona ata ubao! Sasa unataka wafanye maajab gani hapo. Unawajua waswana na mziki wao ambao unapendwa dunia nzima? Wanatumia lugha gani? Wanakijua Kiingereza? Unakumbuka wale Makirikiri walitinga hadi ufunguzi wa kombe la dunia. Unamjua msomi Mr. Bean? Anasaidiwa na Lugha?



5.Tuna wachungaji wazuri sana(Pastors) lakini mahubiri yao ni kwa kiswahili. T.B Joshua anajulikana kila mahali kwa sababu mahubiri yake ni ya kiingeraza. Si kwamba Joshua unaupako kuliko wengine.
Hihi nayo kaili. Sasa Unailinganisha Nigeria na TZ? hawa jamaa wameanza usanii muda mrefu sana. TB Joshua ni msanii alafu promo tu! Ila ni bora ukumbuke Kuwa babu wa loliondo alivuta watu wengi kwa usanii wake bila shaka na si kwa kiingereza. pia mambo ya imani uendana na inani ya watu. Watu wanaenda yesu alipozaliwa na kumalizia maisha yake si kwakiingereza. Au waislam hawaendi Saudia kwakujua lugha. Hoja yako ni dhaifu na niya kitoto.

6. Mikataba mibovu tunayoingia na wawekezaji ni kwa sababu ya lugha tunashindwa kuilewa vizuri Wawekezaji wanapokuja ilitusionekane ni mbumbumbu wa kiingereza tunabaki kusema YES, YES YES.
Si bure wewe umetumwa na magamba, hivi mkuu unasema kweli hapo! Acha hoja za kipuuzi wewe, hapo ni ufisadi tu. Nakuomba uwatake radhi kina Prof. Shivj, Dr. Nshala, Prof. Majamba, kuwa hawajui kusoma mikataba. Tumia kichwa vizuri unapotaka kudanganya au kuwazuga watu. Ebu angalia Ndg. yangu, Karamagi hajui kiingereza? Kwahiyo ukijua kiingereza unaijua sheria tayari!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Unachanganya lugha na utaalamu au??????


7. Kwa watazamaji wenzangu wa aljazeera kuna kipindi kinaitwa 'Tea cafe (kama sijakosea)kinaongelea maswala mbalimbali yanayohusu nchi husika kipindi hicho kinapofanyika. Kipindi hicho kimefanyika,Kenya, Uganda zambia lakini Tanzania hakuna na hata katika ratiba yao Tanzania haimo simply because hakuna watu kama wanasiasa na baadhi ya watu mahalufu ambao wako tayari kujadili kwa kimombo! Sasa dunia itatuelewa vipi matatizo na mipango yetu ?

Acha ujinga wako wewe, haya matusi ya kusema hakuna watanzania waliotayari kuhojiwa si kweli. Mimi na wewe mbona tuko tayari. lkn ata hivyo wakarimani wapo.

maoni yangu ya msgingi,
  1. ni lazima serikali iweke mkazo kwenye somo la kiingereza tangua shule ya msingi kiasi kwamba anayemaliza std 7 awe na uwezo wakuongea kiingereza.
  2. masomo yote nchini yafundishwe kwa kwa Kiswahili chuo kikuu ila tuwe strict kwenye somo la kiingereza kama tufanyavyo kwenye hesabu.
  3. kuwepo kuwepo mkakati wa haraka kubadirisha lugha ya kufundishia kwakuwa watoto wanao toka shule za kiwahili hutumia muda wa miaka 2 hd 3 au sekondari ya wali yote kujifunza Kiingereza na kukariri baadala ya kupata elimu na walio wengi hutoka kapa
 
Paul Kijoka
Narudia kusema tena na tena nchi masikini hatutaendelea kama hatutakubali kubadilisha lugha ya mawasiliano na kuwa kiingereza. Natambua vizuri sana kuwa kuna other factors zinazochangia maendeleo ya nchi lakini pia Lugha ni one of the factor inayochangia katika maendeleo ya nchi na mtu mmoja mmoja. Na pointi yangu nimeijenga katika msingi huo. Nchi kama Japan,china na german kunatofauti kubwa sana na sisi. Ni kupe mfano mzuri, unajua zaidi ya 50% ya watu wote wa dunia hii wanazungumza english lakini wazungumzaji wa kiswahili hawafiki ata 1% ya watu wote duniani. hii 1% haiwezi ikawa peke yake na lugha yake itafika mahali itashindwa kuendelea. tunatakiwa tuwe na mawasiliano mazuri na hiyo 50% ili shughuli za maendeleo zifanyike kwa urahisi.

Jamani si vibaya kuiga mambo mazuri ya mataifa ya wengine mfano nigeria, kenya, zimbabwe wanalugha zao lakini huwezi ukakuta kijana anashindwa kuzungumza kiingereza. Tuachane na fikra za kusema kila kitu tukiiga cha wazungu tunatafsiri kama neo colonialism. Tunashindwa kuangalia mahali tunapokosea tunabaki kusema wazungu wazungu.
 
Last edited by a moderator:
Quote by Jidu
ndugu yangu!haya unayozungumza umefanyia utafiti kweli?hivi lugha ndio kikwazo cha sisi kuto tambulika au kuto kuwa na maendeleo?naomba nitofautiane na wewe kwa hilo.mimi na amini fikra sahihi huja kwa lugha sahihi inayoeleweka kwa jamii husika.nilisha wahi fika china,kwakweli wale jamaa ni kichina kwa kwenda mbele unaweza shindwa nunua kitu dukani au kwenda mahali fulani kwa kuwa mmeshindwa kuelewena kwa lugha lakini hebu angalia walivyopiga hatua kimaendeleo kwa kila nyanja!hivyo basi usitukuze lugha za kigeni na kuacha za kwako kisa eti hatutaendelea,jaribu kuja na mbinu mbadala ya sisi wapi tumekosea ila hili la lugha hapana!
Quote by Masauni
Wewe ulifika china miaka gani? Nataka kukuhakikishia kuwa sasa hivi wanajifunza kwa bidii sana! Naomba ulewe hivi unaweza kuwa na ideas nzuri sana very constructive ideas lakini usipoweza kuzielezea hizo ideas kwa watu wakazielewa utamarginalized yourself. Dunia imekuwa ni kama kijiji. Maendeleo katika nchi yanaletwa katika kuwasiliana na si kuwasiliana sisi kwa sisi tu na watu wa nchi nyingine pia. Tukubali tusikubali Kiingereza ndio lugha ya kimataifa lazima tuifahamu kama tunahitaji kupiga hatua katika maendeleo
Tatizo ni kwamba hata watetezi wa Kiingereza hawakijui sawasawa wanafuata mkumbo tu! Ukweli ni kwamba Kiswahili kina uwezo tosha kabisa wa kujifunza isipokuwa kunakosekana msukumo wa kisiasa. Nilitazama siku moja mdahalo wa lugha ya kiingereza juu ya lugha gani itumike kufundishia nilicheka hadi mchozi kunitoka kwani waliojifanya eti wanatetea kiingereza walizungumza kiingereza kibovu kweli kweli! isitoshe eti ndiyo walikuwa walimu! Si ajabu sana kwa watu kutetea lugha ya mtawala wao kwani hata waingereza wenyewe kiingereza hakikuwa lugha yao rasmi ya kufundishia na waliihusudu sana lugha ya wakoloni wao wafaransa na kilatini. Utawala wa kule ulipofanya maamuzi ya kutumia lugha ya kiingereza pekee kufundishia inasemekana wapo waliopinga hadi mmoja wa maprofesa kuamua kujiua ili asiishi kuishuhudia aibu ya kuporomoka kwa elimu! Natamani mjinga yule angerudi leo aone jinsi watanzania wanavyojikomba kwa waingereza sawa na yeye! Wachina wamefika walipofika baada ya kufanya maamuzi magumu ya kuachana na lugha za wageni kufundishia na kuamua kutumia lugha yao! Mtu mmoja tu aliibadilisha hali hiyo; Mao Tse Tung! Tatizo letu kubwa ni kufanya maamuzi nusu nusu, eti wanafunzi wasome darasa la kwanza hadi la saba kiswahili na kisha kiingereza la Tisa na kuendelea! Nasisitiza tena, tunahitaji viongozi wenye ubavu wa kufanya maamuzi magumu ili kufikia lengo la kukifanya kiswahili lugha rasmi ya kujifunzia, lakini si hawa wanaoinajisi na kuisaliti kila siku hadi Bungeni.
 
Paul Kijoka
Narudia kusema tena na tena nchi masikini hatutaendelea kama hatutakubali kubadilisha lugha ya mawasiliano na kuwa kiingereza. Natambua vizuri sana kuwa kuna other factors zinazochangia maendeleo ya nchi lakini pia Lugha ni one of the factor inayochangia katika maendeleo ya nchi na mtu mmoja mmoja. Na pointi yangu nimeijenga katika msingi huo. Nchi kama Japan,china na german kunatofauti kubwa sana na sisi. Ni kupe mfano mzuri, unajua zaidi ya 50% ya watu wote wa dunia hii wanazungumza english lakini wazungumzaji wa kiswahili hawafiki ata 1% ya watu wote duniani. hii 1% haiwezi ikawa peke yake na lugha yake itafika mahali itashindwa kuendelea. tunatakiwa tuwe na mawasiliano mazuri na hiyo 50% ili shughuli za maendeleo zifanyike kwa urahisi.

Jamani si vibaya kuiga mambo mazuri ya mataifa ya wengine mfano nigeria, kenya, zimbabwe wanalugha zao lakini huwezi ukakuta kijana anashindwa kuzungumza kiingereza. Tuachane na fikra za kusema kila kitu tukiiga cha wazungu tunatafsiri kama neo colonialism. Tunashindwa kuangalia mahali tunapokosea tunabaki kusema wazungu wazungu.

Naanza kukata tamaa na wewe masauni, ni vyema utumie akili yako na nina wasi wasi kama umesoma na kama umesoma umesomea nini??? Maendeleo hayaletwi na lugha ata siku moja. Kumbuka misingi angalau mikuu ya maendeleo kwa mujibu wa Baba wa Taifa 1. Raslimali Watu, 2. Siasa Safi, 3.Uongozi Bora na 4. Afya. Hii yako ni mpya ya lugha.
Kinachohitajika ni elimu bora na si lugha. . Mbali na mapungufu yake yote mzee Kingunge alipata kusemawkuwa wazungu waliotangulia (hawa tulikuwa sawa nao hadi karne ya 14) wajapani na ndg zao wakorea, waliamua kuiga elimu bora na kuwekeza kwenye viwanda. Akasema sisi (wa Africa) tukawekeza kwenye Lugha. (maneno haya hayajakaririwa moja kwa moja)
Alafu ukianzisha mada usome michango ya wadau. Nimegundua kuwa hujasoma au umesoma kwa juu juu mchango wangu. Mimi sijapinga watu kujua Kiingereza. Napinga kukitumia kufundishia na dhana ya kuwa kujua lugha ndo maendeleo. Wewe unakaa nchi gani sasa, wabongo wako vyema kwenye English sana tu. Tatizo ni mfumo mbaya wa elimu unaowafanya wahitimu wengi kushindwa lugha ya kiingereza.

Hivijaribu kufikiria kama bindau msomi sasa, kwakuwa watanzania ni chini ya Million 45 hivi, sasa jifanye tunawaondoa na kuwapeleka nchi za nje na kubadirishana na vilaza, mateja, majuha, mazezeta na kila aina ya wapuuzi hao lkn wanaojua Kiingereza. Nambie sasa, Tanzania itaendelea ndani ya Muda gani Mkuu?
 
Tatizo ni kwamba hata watetezi wa Kiingereza hawakijui sawasawa wanafuata mkumbo tu! Ukweli ni kwamba Kiswahili kina uwezo tosha kabisa wa kujifunza isipokuwa kunakosekana msukumo wa kisiasa. Nilitazama siku moja mdahalo wa lugha ya kiingereza juu ya lugha gani itumike kufundishia nilicheka hadi mchozi kunitoka kwani waliojifanya eti wanatetea kiingereza walizungumza kiingereza kibovu kweli kweli! isitoshe eti ndiyo walikuwa walimu! Si ajabu sana kwa watu kutetea lugha ya mtawala wao kwani hata waingereza wenyewe kiingereza hakikuwa lugha yao rasmi ya kufundishia na waliihusudu sana lugha ya wakoloni wao wafaransa na kilatini. Utawala wa kule ulipofanya maamuzi ya kutumia lugha ya kiingereza pekee kufundishia inasemekana wapo waliopinga hadi mmoja wa maprofesa kuamua kujiua ili asiishi kuishuhudia aibu ya kuporomoka kwa elimu! Natamani mjinga yule angerudi leo aone jinsi watanzania wanavyojikomba kwa waingereza sawa na yeye! Wachina wamefika walipofika baada ya kufanya maamuzi magumu ya kuachana na lugha za wageni kufundishia na kuamua kutumia lugha yao! Mtu mmoja tu aliibadilisha hali hiyo; Mao Tse Tung! Tatizo letu kubwa ni kufanya maamuzi nusu nusu, eti wanafunzi wasome darasa la kwanza hadi la saba kiswahili na kisha kiingereza la Tisa na kuendelea! Nasisitiza tena, tunahitaji viongozi wenye ubavu wa kufanya maamuzi magumu ili kufikia lengo la kukifanya kiswahili lugha rasmi ya kujifunzia, lakini si hawa wanaoinajisi na kuisaliti kila siku hadi Bungeni.
Mkuu mbona unaleta story za kusadikika? weka reference. Ndugu yangu tembea uone!! inawezekana wewe umezaliwa Dar, umesoma Dar, Umepata kazi dar, umeoa ukiwa dar. Ulimwengu unaoufahamu ni Dar es salaam tu!! Katika karne hii ya Science na teknolojia, tunahitaji lugha ya kimataifa. Ninawafahamu wasomi wazuri sana wa kitanzania ambao walishindwa kuiwakilisha Tanzania katika nyanja za utafiti na sayansi nje ya nchi kwa sababu ya lugha ya kiingereza lakini mkiwa mnajadili kwa kiswahili ni vichwa si mchezo.

Leo katika jumuia ya africa mashariki tunawaogopa sana wakenya na waganda(pamoja na sababu zingine lakini pia Lugha inachangia tuwaogope tukijua kwamba kupata kazi katika nchi hizo bila umombo ni ngumu)
Lugha ya kiiingereza ni pana sana na ndio maana inakuwa rahisi kufundishia kuliko kiswahili amabacho si kipana.
 
Ninaomba kuanzisha hii mada baada ya kusikia kwamba kuna mahali walimu wamefukuzwa kwa sababu ya kuongea kiswahili katika mazingira ya shule.
Niseme tu kwamba naunga mkono jambo hilo kwa asilimia mia. Sababu ni hizi hapa.

1. Tutambue kuwa kiswahili ni lugha inayozungumzwa sana Tanzania na ukitoka nje ya mipaka ya Tanzania kiswahili chako unaweka mfukoni! Lazima tujufunze lugha za kimataifa(English) ili tulahisishe mawasiliano na mataifa mengine.

2. Wageni wakija Tanzania wanapata taabu kweli, matangazo ya biashara yameandikwa kwa kiswahili, barabara nazo unakuta vibao vimeandikwa kwa kiswahil mfano PITA KUSHOTO. Sasa jamani wageni wetu ambao wengi wanakuja kwa maswala ya biashara inakuwa ngumu sana.Mgeni kuendesha gari tanzania ni ngumu sana. Mgeni kufanya biashara Tanzania ni ngumu sana!! Kuna jamaa wafanyabiashara wengi sana nawafahamu wanaprefer kwenda Kenya na Uganda kuchukua bidhaa kuliko Tanzania na sababu wanazozitoa ni ugumu wa Lugha.wanasema kwenda Tanzania ni gharama zaidi maana inabidi umtafute mkalimani ambaye utamlipa.

3. Kenya inatangaza mlima kilimanjaro kwa sababu ya Lugha wanayotumia inaeleweka duniani kote. Sisi tunatangaza mlima kilimanjaro kwa kiswahili wataelewa nini wageni?

4.Tunawasanii wazuri sana wa muziki, tamthiliya, vichekesho, ambao wangesaidia sana kuitangaza nchi yetu kimataifa na wao pia kufaidika, lakini wamebaki eti wasanii wa BONGO. (Kwa wale mliobahatika kuangalia stand up Zambia kilichorushwa na Africa magic channel mtakubaliana na mimi wale jamaa 3 walioshinda sasa hivi ni comedian wakimataifa wanazunguka nchi mabalimabali sababu ni lugha tu, maana kwa ukweli hawawezi kumfikia Joti, Masanja.

5.Tuna wachungaji wazuri sana(Pastors) lakini mahubiri yao ni kwa kiswahili. T.B Joshua anajulikana kila mahali kwa sababu mahubiri yake ni ya kiingeraza. Si kwamba Joshua unaupako kuliko wengine.

6. Mikataba mibovu tunayoingia na wawekezaji ni kwa sababu ya lugha tunashindwa kuilewa vizuri Wawekezaji wanapokuja ilitusionekane ni mbumbumbu wa kiingereza tunabaki kusema YES, YES YES!

7. Kwa watazamaji wenzangu wa aljazeera kuna kipindi kinaitwa 'Tea cafe (kama sijakosea)kinaongelea maswala mbalimbali yanayohusu nchi husika kipindi hicho kinapofanyika. Kipindi hicho kimefanyika,Kenya, Uganda zambia lakini Tanzania hakuna na hata katika ratiba yao Tanzania haimo simply because hakuna watu kama wanasiasa na baadhi ya watu mahalufu ambao wako tayari kujadili kwa kimombo! Sasa dunia itatuelewa vipi matatizo na mipango yetu ?

Nchi nyingi sasa hivi zinajifunza Kiingera hata china taifa kubwa wako busy kujifunza kiingereza Sisi masikini wakutupwa tunangangana na kiswahili ambacho mwisho wake ni mipakani tu! Viongozi wetu lazima pia waanalie hiyo watu waanza kufundishwa kiingereza tangu chekechea, maofisini lugha ya kiingereza isisitizwe, mikutano maofisini ifanyike kwa kiingereza. WITHOUT ENGLISH YOU ARE MARGINALIZED YOURSELF

Masauni, Salaam! Nimejizuia kwa muda mrefu sana nisichangie mada hii kutokana na jinsi ilivyojaa hoja potofu lakini nimeshindwa. Mchango pekee ninaoanza nao kwa leo ni kukutaka upitie upya maandishi yako hapo juu na urekebishe kwanza palipokozwa rangi nyekundu. Yamejaa makosa ya kimantiki na kileksika ambayo hayavumiliki. Baada ya kulifanya hilo, nitarudi nikufafanulie yaliyokupata baada ya wewe kukaa huko unakokuita 'nje'!
 
Wewe ulifika china miaka gani? Nataka kukuhakikishia kuwa sasa hivi wanajifunza kwa bidii sana! Naomba ulewe hivi unaweza kuwa na ideas nzuri sana very constructive ideas lakini usipoweza kuzielezea hizo ideas kwa watu wakazielewa utamarginalized yourself. Dunia imekuwa ni kama kijiji. Maendeleo katika nchi yanaletwa katika kuwasiliana na si kuwasiliana sisi kwa sisi tu na watu wa nchi nyingine pia. Tukubali tusikubali Kiingereza ndio lugha ya kimataifa lazima tuifahamu kama tunahitaji kupiga hatua katika maendeleo

The point is not about Wachina wanafundisha na kujifunza sana Kiingereza. Je, wanakifuta Kichina katika mfumo wao wa Elimu ili kukipisha Kiingereza?
Kama utachunguza mifumo ya elimu duniani utagundua kwamba mafanikio hupatikana kwa kuwa na mitaala mizuri na kufundisha vizuri lugha mbalimbali. Tunachojaribu kufanya hapa Afrika ni kuhakikisha kwamba wenye lugha zao (lugha kama Kiingereza, Kifaransa, Kireno, Kihispania, nk) wanatuona kwamba na sisi tumo bwana.
 
Paul Kijoka
Narudia kusema tena na tena nchi masikini hatutaendelea kama hatutakubali kubadilisha lugha ya mawasiliano na kuwa kiingereza. Natambua vizuri sana kuwa kuna other factors zinazochangia maendeleo ya nchi lakini pia Lugha ni one of the factor inayochangia katika maendeleo ya nchi na mtu mmoja mmoja. Na pointi yangu nimeijenga katika msingi huo. Nchi kama Japan,china na german kunatofauti kubwa sana na sisi. Ni kupe mfano mzuri, unajua zaidi ya 50% ya watu wote wa dunia hii wanazungumza english lakini wazungumzaji wa kiswahili hawafiki ata 1% ya watu wote duniani. hii 1% haiwezi ikawa peke yake na lugha yake itafika mahali itashindwa kuendelea. tunatakiwa tuwe na mawasiliano mazuri na hiyo 50% ili shughuli za maendeleo zifanyike kwa urahisi.

Jamani si vibaya kuiga mambo mazuri ya mataifa ya wengine mfano nigeria, kenya, zimbabwe wanalugha zao lakini huwezi ukakuta kijana anashindwa kuzungumza kiingereza. Tuachane na fikra za kusema kila kitu tukiiga cha wazungu tunatafsiri kama neo colonialism. Tunashindwa kuangalia mahali tunapokosea tunabaki kusema wazungu wazungu.

Masauni unakatisha tamaa kwa kutoweza kuyaangalia mambo kwa undani. Actually, inconsistencies and lack of logic in your writings is astonishing. Kwanza nami nikuambie, nakaa nje ya Tanzania, kwa miaka mingi, niseme miongo kadha. Usianze kudai tembea ujionee ukadhani wote ambao hawakubaliani nawe basi wamekaa Kiponzelo Iringa miaka yote. Na wala usije ukadhani wote wanaokitetea kiswahili au matumizi ya lugha nyingi kwamba ni watu wasioweza kusema Kiingereza vizuri. Nitakuambia ninawafahamu watu kadha ambao wanafundisha Kiingereza huko nje nao ni watetezi wakubwa wa Kiswahili.
Sasa, hebu tuangalie nchi zilizoendelea. Kila moja inatumia lugha yake ya asili. Na kama lugha zao si Kiingereza, basi wanafundisha PIA Kiingereza vizuri. Herufi kubwa hapa kusisitiza kwamba in addition to their languages. Hebu tuangalie nchi nyingine ambazo zimepiga hatua sana miaka ya karibuni. Korea, China, Vietnam, Indonesia, Malaysia, nk. Wanatumia lugha gani hasa katika elimu na shughuli za kiutawala? Wanatumia lugha zao. LAKINI wanafundisha PIA Kiingereza (hata na lugha nyingine). Na nyingine kama Malaysia, tunaambiwa miaka ya 50/60 (wakati wa uhuru) hazikuwa mbali sana na nchi za Kiafrika. Tofauti yetu ni nini? Sasa angalia nchi za Kiafrika kuhusu jambo hili. Sitaki kuleta hoja kwamba kumekucha kwa sababu jogoo amewika. Hoja hiyo wataalamu wa mantiki huisema kama: Est post hoc, ergo propter hoc.
Ukikumbatia tu mawazo ya kwamba huna chochote ila kukumbatia kila kitu kutoka nje kwa masters, huwezi kupiga hatua ya maendeleo. Na uchaguzi wa lugha hapa ni kielelezo (si chanzo kwa kiwango kikubwa, kwa maoni yangu), cha kukosa mawazo, vision, na mwelekeo ambao utatukwamua.
 
Unafikiri kwa kutumia masaburi




ninaomba kuanzisha hii mada baada ya kusikia kwamba kuna mahali walimu wamefukuzwa kwa sababu ya kuongea kiswahili katika mazingira ya shule.
Niseme tu kwamba naunga mkono jambo hilo kwa asilimia mia. Sababu ni hizi hapa.

1. Tutambue kuwa kiswahili ni lugha inayozungumzwa sana tanzania na ukitoka nje ya mipaka ya tanzania kiswahili chako unaweka mfukoni! Lazima tujufunze lugha za kimataifa(english) ili tulahisishe mawasiliano na mataifa mengine.

2. Wageni wakija tanzania wanapata taabu kweli, matangazo ya biashara yameandikwa kwa kiswahili, barabara nazo unakuta vibao vimeandikwa kwa kiswahil mfano pita kushoto. Sasa jamani wageni wetu ambao wengi wanakuja kwa maswala ya biashara inakuwa ngumu sana.mgeni kuendesha gari tanzania ni ngumu sana. Mgeni kufanya biashara tanzania ni ngumu sana!! Kuna jamaa wafanyabiashara wengi sana nawafahamu wanaprefer kwenda kenya na uganda kuchukua bidhaa kuliko tanzania na sababu wanazozitoa ni ugumu wa lugha.wanasema kwenda tanzania ni gharama zaidi maana inabidi umtafute mkalimani ambaye utamlipa.

3. Kenya inatangaza mlima kilimanjaro kwa sababu ya lugha wanayotumia inaeleweka duniani kote. Sisi tunatangaza mlima kilimanjaro kwa kiswahili wataelewa nini wageni?

4.tunawasanii wazuri sana wa muziki, tamthiliya, vichekesho, ambao wangesaidia sana kuitangaza nchi yetu kimataifa na wao pia kufaidika, lakini wamebaki eti wasanii wa bongo. (kwa wale mliobahatika kuangalia stand up zambia kilichorushwa na africa magic channel mtakubaliana na mimi wale jamaa 3 walioshinda sasa hivi ni comedian wakimataifa wanazunguka nchi mabalimabali sababu ni lugha tu, maana kwa ukweli hawawezi kumfikia joti, masanja.

5.tuna wachungaji wazuri sana(pastors) lakini mahubiri yao ni kwa kiswahili. T.b joshua anajulikana kila mahali kwa sababu mahubiri yake ni ya kiingeraza. Si kwamba joshua unaupako kuliko wengine.

6. Mikataba mibovu tunayoingia na wawekezaji ni kwa sababu ya lugha tunashindwa kuilewa vizuri wawekezaji wanapokuja ilitusionekane ni mbumbumbu wa kiingereza tunabaki kusema yes, yes yes!

7. Kwa watazamaji wenzangu wa aljazeera kuna kipindi kinaitwa 'tea cafe (kama sijakosea)kinaongelea maswala mbalimbali yanayohusu nchi husika kipindi hicho kinapofanyika. Kipindi hicho kimefanyika,kenya, uganda zambia lakini tanzania hakuna na hata katika ratiba yao tanzania haimo simply because hakuna watu kama wanasiasa na baadhi ya watu mahalufu ambao wako tayari kujadili kwa kimombo! Sasa dunia itatuelewa vipi matatizo na mipango yetu ?

Nchi nyingi sasa hivi zinajifunza kiingera hata china taifa kubwa wako busy kujifunza kiingereza sisi masikini wakutupwa tunangangana na kiswahili ambacho mwisho wake ni mipakani tu! Viongozi wetu lazima pia waanalie hiyo watu waanza kufundishwa kiingereza tangu chekechea, maofisini lugha ya kiingereza isisitizwe, mikutano maofisini ifanyike kwa kiingereza. Without english you are marginalized yourself
 
Ulichosema ni ukweli mtupu, ila tegemea kushambuliwa na watu ambao hawako tayari kuukubali hii fact. Tegemewa kuambiwa Wachina, Wajerumani, Wajapani, Wafaransa wanaongea lugha zao na wanaendelea.

Vile vile subiri kuambia kuwa unawaabudu wazungu.

Na mwisho kabisa, tegemea kuambiwa kuwa Nyerere aliasisi lugha takatifu ya Kiswahili - kwa hiyo anayekipinga anatenda dhambi kwa Mnyaz Mungu.

Read a book, please! Siyo kila anayetetea Kiswahili ana mawazo duni kama hayo unayoyatoa. Hayo umeyatoa wewe superficially ili ujidai kuonesha kwamba umeangalia upande wa pili. Kwa mfano, hakuna mwenye akili timamu na uelewa anaeyesema kwamba Kiswahili kiliasisiwa na Mwl Nyerere. That was a display of stupidity of the highest order. This was so low, I will not dignify the rest of your rant with some response.
Na kwa jamaa yako anayedhani kwamba kila anayetetea Kiswahili Tanzania maana yake hajasafiri.... well that is plain pathetic. Mimi naishi nje ya Tanzania kwa miongo kadha sasa.
 
jumamosi ya wiki jana nilibahatika kusikiliza makala ya lugha ya kiswahili katika redio moja iliyopo nairobi kenya.kitu nilicho ngundua ktk makala ile ni kwamba wakenya wanatuonea wivu sana watanzania na kiswahili chetu.profesa mmoja alienda mbali zaidi kwa kuponda tafiti za maprofesa wa kibongo zinazo dai kiswahili kilianzia mwambao wa pwani ya tanzania.yeye akadai kiswahili kilianzia mwambao wa pwani ya kenya(mombasa/malindi).sioni sababu kwanini sisi watanzania tusijivunie lugha yetu kiswahili japo sio kigezo pekee cha kutufanya tusijifunze lugha za mataifa mengine.
 
Alichoandika Masauni ( na Imani sio yule jamaa aliyetimuliwa UVCCM) ni matokeo ya fikra mgando zinazosababishwa na kuutukuza zaidi ukoloni na umagharibi! kwa taarifa yako tu Masauni kwa sasa wazungumzaji wa kiswahili duniani wanakaribia 5% na hizo nchi unazozishadidia kuwa ndio zilizoendelea kwa sasa wanajifunza kiswahili kwa bidiii sana. Nilikuwa Cambridge UK mwaka jana, na niliingia katika mgahawa mmoja nilikuwa jamaa ana darasa la pale anafundisha Kiswahili, that was extremly amazing! Marekai wameanzisha taasisi ya kukuza na kuendeleza kiswahili na tamaduni zake! ni ajabu sana wewe kupinga hili, japo ni kweli kuwa hatuwezi kuacha kujifunza lugha za kigeni hasa Kiingereza kwa ajili ya kurahisisha mawasiliano! Na si kweli kuwa wageni wanashindwa kufanya nasi biashara hapa nyumbani kwa ajili ya lugha! in contrary wageni hao hasa waingereza huwa wanatushangaa sana tunapolazimisha kuwasiliana nao kwa kiingereza tukiwa hapa TZ ilihali wao wanataka pia kujifunza Kiswahili, mifano ninayo!
 
Kama mfumo mzima tangu ukoloni ni kiingeleza basi kusingekuwepo mtu ata mmoja asiyejua kukiongea leo. Ila kila siku zinavyokwenda HALI INAZIDI KUWA MBAYA.
Anaye jua kukariri ndo anashinda mitihani na wenye akili wananabakia mtaani!!!

Wanaofungwa kwa kutengeneza Bunduki, au wale wanao fanya ufundi wa simu na ujenzi makini si wale walio katika mfumo rasimi wa elimu!!!! Ni wale waliopata zero la saba!!!
Mtu wa sayansi wa Form six hajui ata kubadiri balbu nyumbani kwao,
 
Kama mfumo mzima tangu ukoloni ni kiingeleza basi kusingekuwepo mtu ata mmoja asiyejua kukiongea leo. Ila kila siku zinavyokwenda HALI INAZIDI KUWA MBAYA.
Anaye jua kukariri ndo anashinda mitihani na wenye akili wananabakia mtaani!!!

Wanaofungwa kwa kutengeneza Bunduki, au wale wanao fanya ufundi wa simu na ujenzi makini si wale walio katika mfumo rasimi wa elimu!!!! Ni wale waliopata zero la saba!!!
Mtu wa sayansi wa Form six hajui ata kubadiri balbu nyumbani kwao,
 
countries where english is a dejure /official language (list of countries where english is an official language - wikipedia, the free encyclopedia)
countryregion
botswanaafrica
cameroonafrica
eritreaafrica
ethiopiaafrica
ghanaafrica
jamaicacaribbean
kenyaafrica
lesothoafrica
liberiaafrica
malawiafrica
namibiaafrica
nigeriaafrica
sierraleoneafrica
solomonislandsoceania
southafricaafrica
southsudanafrica
sudanafrica
swazilandafrica
tanzaniaafrica
thegambiaafrica
ugandaafrica
zambiaafrica
zimbabweafrica

hebu angalieni hizo nchi zinazoongea kiingereza. Wametuzidi nini?
Kiingereza sio muhimu kiviiile kwa maendeleo yetu. Ili tuendelee tunahitaji watu, ardhi, sera nzuri (siasa safi), na uongozi makini. Kiingereza is not one of the requirements. In fact, kama (kwa muujiza) tanzania ingekuwa economically superpower, majirani wote wangekuja tu kutafatua kazi na lazima wangejifunza kiswahili.
Hebu fikiria, kwa hapa nchini, inasemekana, kilimanjaro wameendelea zaidi kuliko sehemu nyingine. Je wanaongea kiingereza? Si wanaongea kichaga na kipare tu?

hapo ethiopia mh!
 
Kiingereza ni lugha ya kimataifa, kiswahili ni kitanzania. Kwa uhuru wa kuuelewa utandawazi kwa mapana yake, tusijidanganye, kiingereza kinahitajika mno.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom