KARLO MWILAPWA
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 2,591
- 4,604
Kwenye mapendekezo ya bajeti Kwa mwaka wa fedha 2023/2024 baadhi ya tozo kama ile tozo ya kwenye miamala ambayo ni kilio Cha wanyonge wengi na Ile Kodi ya 'store' iliyopelekea mgomo Kariakoo zitaondolewa kabisa. Ukiachana na hizo Kodi, tozo na ushuru mbalimbali wa bidhaa zitapungua kabisa.
Kodi ni muhimu sana na Kwa vyovyote zisingeweza kuondolewa ikiwa mbadala wake haujajulikana ila Kwa kuwa mbadala umepatikana basi Serikali sikivu ya mama Samia imetupatia unafuu.
Tusipepese macho, mbadala wa tozo hizo ni matokeo na faida za uwekezaji zitakazopatikan katika bandari Kwa ushirikiano na DP WORLD. Makubaliano na DP WORLD yatakuja na fursa lukuki ikiwepo kuongezeka Kwa mchango wa mapato yanayochangiwa na bandari mpaka 67% kutoka 37% ya Sasa.
Hizi ni faida za mwaka wa kwanza tu, Sasa tufikirie mbali Zaidi faida zitakazokuwepo mwaka wa fedha 2024/2025-2025/2050. Naamini zitakuwa za kufurahisha.
Wanaopinga makubaliano haya watuambie kama hili sio jambo jema Kwa wananchi?
Je, Kuna mwananchi wa kawaida anayepinga makubaliano ikiwa yanampa faida za Moja Kwa Moja kama hizi?
Rai yangu, tumwache mama afanye kazi ,mipango na mikakati yake Kwa Taifa ni mikubwa Zaidi ya tunavyowaza au kufikiria.
Kodi ni muhimu sana na Kwa vyovyote zisingeweza kuondolewa ikiwa mbadala wake haujajulikana ila Kwa kuwa mbadala umepatikana basi Serikali sikivu ya mama Samia imetupatia unafuu.
Tusipepese macho, mbadala wa tozo hizo ni matokeo na faida za uwekezaji zitakazopatikan katika bandari Kwa ushirikiano na DP WORLD. Makubaliano na DP WORLD yatakuja na fursa lukuki ikiwepo kuongezeka Kwa mchango wa mapato yanayochangiwa na bandari mpaka 67% kutoka 37% ya Sasa.
Hizi ni faida za mwaka wa kwanza tu, Sasa tufikirie mbali Zaidi faida zitakazokuwepo mwaka wa fedha 2024/2025-2025/2050. Naamini zitakuwa za kufurahisha.
Wanaopinga makubaliano haya watuambie kama hili sio jambo jema Kwa wananchi?
Je, Kuna mwananchi wa kawaida anayepinga makubaliano ikiwa yanampa faida za Moja Kwa Moja kama hizi?
Rai yangu, tumwache mama afanye kazi ,mipango na mikakati yake Kwa Taifa ni mikubwa Zaidi ya tunavyowaza au kufikiria.