Kisbo imepitwa hapa mapema tu!

Kisbo imepitwa hapa mapema tu!

Jamani nilishauriwa humuhumu JF ili nifike Dar kutoka Mwanza kwa siku moja nipande basi la Kisbo, wanaJF wakasisitiza hakuna basi linalokimbia kama Kisbo, nami kweli nikakata tiketi ya hilo basi.

Sasa ajabu leo tumetoka Nyegezi stand tumevuka tu Buhongwa Kisbo ikapitwa basi fulani linaitwa Master, sasa nimeanza kupata wasiwasi kama kweli nitafika leo manake uongo umeanza kudhihirika.
Shuka utembee kwa miguu uenda ukawahi
 
Basi za mwanza-mbeya ligi ilikua nzuri zaman,sahv hamna kitu...Basi zote vimeo!!
 
ni kweli sio yule wa kwanza, sasa naona huyu aliyeingia ni mdogo wake Michael Schumacher. jamaa ananyoosha mguu hadi raha
Ntakukatia ticket siku moja ya bombadia ili utupe live stream kati ya precision na bombadia nani zaidi.
 
Sasa hivi ndio muda wa madereva kuonyesha uwezo. Hakuna torch. Hapo ni uwezo wa dereva tu kuona usiku na kupishana bila ya kupunguza speed
 
Huyo jamaa aliyeipita kisbo hapo buhongwa, kwa uzoefu wangu, hata toboa shinyanga bila ya kukutwa na kupitwa.
Uzuri wa kisbo hailali kituoni, kula ni dk 4 hadi 5, ukizembea utaachwa. Kuns kamsemo chao wale madereva na mautingo "kisbo haimuachi abiria, bali abilia ndo anaiacha kisbo"
Nimeupenda huo msemo
 
Giza limeingia [HASHTAG]#sexer[/HASHTAG]
haoni maeneo, tumia google map mkuu!
 
ni kweli sio yule wa kwanza, sasa naona huyu aliyeingia ni mdogo wake Michael Schumacher. jamaa ananyoosha mguu hadi raha
Au kaingia yule jamaa wa transporter reloded?
Nahisi mpo moro kwa sasa
 
Kuna basi moja la Osaka, ni scania ila nawaonea huruma wanaopandaga, linapiga kelele hatari. Lile ukipanda lazima uwe unatafuna big G kuepuka masikio kuuma.
 
baada ya singida hakuna aliyekatisha, wale waliotupita shy tulibambana singida walikuwa wanaenda arusha. nadhan huko mbele yetu kuna kidia one, katagi sijajua anaenda wapi make naye alipopita hajaonekana tena.
kudia na katagi dom Zilikuwa nyuma yenu
 
baada ya singida hakuna aliyekatisha, wale waliotupita shy tulibambana singida walikuwa wanaenda arusha. nadhan huko mbele yetu kuna kidia one, katagi sijajua anaenda wapi make naye alipopita hajaonekana tena.
kudia na katagi dom Zilikuwa nyuma yenu
 
dodoma ilikuwa saa 9. nilishawahi toka dar to mwanza na zuberi, saa mbili niko mwanza tena buzuruga nikaangalia na taarifa ya habari

Ila siku hizi safari ya mwanza ni mateso tu. Nakumbuka kuna siku tulifika shinyanga saa tano na nusu usiku Traffic Police wakaizuia bus ikabidi watu walale mpaka asubuhi
 
Jamani nilishauriwa humuhumu JF ili nifike Dar kutoka Mwanza kwa siku moja nipande basi la Kisbo, wanaJF wakasisitiza hakuna basi linalokimbia kama Kisbo, nami kweli nikakata tiketi ya hilo basi.

Sasa ajabu leo tumetoka Nyegezi stand tumevuka tu Buhongwa Kisbo ikapitwa basi fulani linaitwa Master, sasa nimeanza kupata wasiwasi kama kweli nitafika leo manake uongo umeanza kudhihirika.
Umenikumbusha ligi ya Tawaqal na Kiswele enzi hizo Dar to Songea, huku kuna giriki kule yuko Yogi palikuwa hapatoshi!
 
Tulia hapo hapo, tochi zimeshapaki, ni mwendo wa kunyoosha goti tu saa hizi, saa tatu usiku moro, saa tano na nusu usiku ubungo........

Ndugu Habari ya masiku?
 
Kwanza ukianza kuuliza gari gani ya kupanda ambayo huta lala njiani,gari uli shauriwa na wadau wengi ndio uliyo panda .saa 12 alfajiri ukawajuza wadau mwenendo wa safari yako kuwa na hadi sasa uko nasi began kwa bega kuhusu mwenendo wa safari yako.vp mkuu jirani yako uliye kaa naye seat mmoja ana kusaidia kuiona safari fupi kwa kukupa ushirikiano wa story .

nilidhan wanaJF waliniingiza chaka. kumbe walinishaur vizuri
 
Jamani nilishauriwa humuhumu JF ili nifike Dar kutoka Mwanza kwa siku moja nipande basi la Kisbo, wanaJF wakasisitiza hakuna basi linalokimbia kama Kisbo, nami kweli nikakata tiketi ya hilo basi.

Sasa ajabu leo tumetoka Nyegezi stand tumevuka tu Buhongwa Kisbo ikapitwa basi fulani linaitwa Master, sasa nimeanza kupata wasiwasi kama kweli nitafika leo manake uongo umeanza kudhihirika.
Subili utatuambia kufika singida nani yuko mbele. No pm nikwambie siri
 
Back
Top Bottom