Mohammed wa 5
JF-Expert Member
- Jun 20, 2022
- 1,215
- 2,992
Pasaka njema kwa wakristo wote, naomba niwape kisa hiki cha ukweli kilichotokea kusini mwa Tanzania mkoa x katika nyumba moja ya Bibi mstaafu.
Jinsi nilivyo muonekano wangu, sio mfupi sana wala mrefu sana niko wastani,mweusi ila nina sura ya upole, sina ndevu nina mwili wa wastani sio mnene wala mwembamba, ukiniona uwezi kudhani kama nafanya kazi hiyo.
Mwaka 2013 baada ya kuamishwa kikazi nilipelekwa mkoa X kusini huko, baada ya kuripoti kituo kipya cha kazi na kukamilisha process zote kwenye kituo changu kwa ajiri ya kuanza majukumu ya kitaifa.
Nilipata chumba ni nyumba ya bibi mstaafu kidogo umri umeenda japo sio sana ana nguvu zake. Baada ya taratibu za mkataba na pango nikalipa miezi 6 Tsh 150,000 kwa mwezi mmoja pango ilikuwa 25,000. Nikamalizana na dalali kilichofuta ni kuamia tu maana mwenye nyumba alisema usafi wa chumba atafanya binti yake nikifika ntakuta chumba tayari.
Nilienda town kununua vitu mbalimbali vya geto kama kitanda, godoro, meza, na baadhi ya vitu muhimu vya geto nikahamia nikawa mpangaji wa rasmi wa nyumba ya yule bibi.
Ile nyumba Ina wapangaji 5 niliowakuta pale, mpangaji wa kwanza ni mama ana familia yake, wapili na watatu ni mabinti na wanne ni mwalimu na watano alikuwa na duka lake pande za town na mwisho ni mimi msela, jumla wapangaji sita.
Safari ya maisha na ile nyumba
Tuliishi vizuri Mana wapangaji wezangu walikuwa ni waelewa sababu umewakuta lazima ulete heshima kwenye kulipa luku, maji, usafi tulikuwa vizuri japo Kuna muda lazima kama wapangaji kugombana kunatokea ila mwenye nyumba alikuwa smart na matatizo yote alikuwa ana solve vizuri tu.
Kwenye ile nyumba mimi ndo nilionekana kijana mdogo na ukicheki umbo langu, wapangaji wenzangu Kama walianza dharau na maneno Mana kazi yangu ilikuwa haijajulikana.
Nilikuwa natoka asubuhi kama zamu yangu au jioni kama nina zamu ya usiku nilikuwa navaa juu jezi chini track ya mazoezi na sendo pamoja na begi langu,
Nikifika kazini nilikuwa navaa sare zangu na muda wa kutoka nilikuwa nabadilisha navaa nguo za kawaida tu, sare zangu nazibebe kwenye begi.
Lifestyle yangu ilikuwa ni ya hivyo sikutaka watu wajue nina fanya kazi gani....
Itaendelea nimechoka kuandika.
Jinsi nilivyo muonekano wangu, sio mfupi sana wala mrefu sana niko wastani,mweusi ila nina sura ya upole, sina ndevu nina mwili wa wastani sio mnene wala mwembamba, ukiniona uwezi kudhani kama nafanya kazi hiyo.
Mwaka 2013 baada ya kuamishwa kikazi nilipelekwa mkoa X kusini huko, baada ya kuripoti kituo kipya cha kazi na kukamilisha process zote kwenye kituo changu kwa ajiri ya kuanza majukumu ya kitaifa.
Nilipata chumba ni nyumba ya bibi mstaafu kidogo umri umeenda japo sio sana ana nguvu zake. Baada ya taratibu za mkataba na pango nikalipa miezi 6 Tsh 150,000 kwa mwezi mmoja pango ilikuwa 25,000. Nikamalizana na dalali kilichofuta ni kuamia tu maana mwenye nyumba alisema usafi wa chumba atafanya binti yake nikifika ntakuta chumba tayari.
Nilienda town kununua vitu mbalimbali vya geto kama kitanda, godoro, meza, na baadhi ya vitu muhimu vya geto nikahamia nikawa mpangaji wa rasmi wa nyumba ya yule bibi.
Ile nyumba Ina wapangaji 5 niliowakuta pale, mpangaji wa kwanza ni mama ana familia yake, wapili na watatu ni mabinti na wanne ni mwalimu na watano alikuwa na duka lake pande za town na mwisho ni mimi msela, jumla wapangaji sita.
Safari ya maisha na ile nyumba
Tuliishi vizuri Mana wapangaji wezangu walikuwa ni waelewa sababu umewakuta lazima ulete heshima kwenye kulipa luku, maji, usafi tulikuwa vizuri japo Kuna muda lazima kama wapangaji kugombana kunatokea ila mwenye nyumba alikuwa smart na matatizo yote alikuwa ana solve vizuri tu.
Kwenye ile nyumba mimi ndo nilionekana kijana mdogo na ukicheki umbo langu, wapangaji wenzangu Kama walianza dharau na maneno Mana kazi yangu ilikuwa haijajulikana.
Nilikuwa natoka asubuhi kama zamu yangu au jioni kama nina zamu ya usiku nilikuwa navaa juu jezi chini track ya mazoezi na sendo pamoja na begi langu,
Nikifika kazini nilikuwa navaa sare zangu na muda wa kutoka nilikuwa nabadilisha navaa nguo za kawaida tu, sare zangu nazibebe kwenye begi.
Lifestyle yangu ilikuwa ni ya hivyo sikutaka watu wajue nina fanya kazi gani....
Itaendelea nimechoka kuandika.