Rare Sapphire
JF-Expert Member
- Jul 24, 2021
- 576
- 1,626
Wakuu,
Katika harakati za kutafuta nyumba kwa ajili ya shughuli mbalimbali madalali wamekuwa wakitumika kufanikisha jambo hilo. Wenye nyumba hutafuta madalali ili kuweka wepesi katika kupata wateja, na imekuwa rahisi kwa wapangaji kufikia maeneo hayo kirahisi kupitia madalali.
Ambapo, baada ya kufanikisha zoezi la kupata mteja mpangaji anatakiwa kulipa kodi ya mwezi mmoja kwa dalali kama ujira wake, na asipolipa atafanyiwa figisu mpaka ashindwe kupata sehemu hiyo au ataletewa mtu mwingine na yeye kulazimika kuhama
Sasa swali linakuja hapa, nani anatakiwa kulipa ujira wa dalali? Kama dalali amepewa kazi na mwenye nyumba kwanini ujira alipe mpangaji? Kwanini asilipe mwenye nyumba aliyetoa shavu hilo kwa dalali?
Swali la nyongeza, kwanini mpangaji atakiwe kulipa kodi ya mwezi mmoja? Yaani gharama ile ile kwa mwenye mali inatakiwa iende sawa na kwa aliyetoa taarifa juu ya uwepo wake!
Ina maana imekosekana kabisa njia ya kumpa mpangaji unafuu na kumpunguzia, ikiwezekana kumuondolea kabisa mzigo huo? Lukuvi akiwa Waziri wa Ardhi alipiga marufuku madalali kuwadai wapangaji kodi ya mwezi mmoj akiita kitendo hiko kuwa ni ujambazi, akisema mwenye nyumba ndio alipe pesa hiyo.
Katazo hili liliishia wapi? Ilikuwa ni kauli tu ya kisiasa kufurahisha watu huku wakiaacha wananchi waendelee kuumia?
Wakuu mnazungumziaje suala hili.
Katika harakati za kutafuta nyumba kwa ajili ya shughuli mbalimbali madalali wamekuwa wakitumika kufanikisha jambo hilo. Wenye nyumba hutafuta madalali ili kuweka wepesi katika kupata wateja, na imekuwa rahisi kwa wapangaji kufikia maeneo hayo kirahisi kupitia madalali.
Ambapo, baada ya kufanikisha zoezi la kupata mteja mpangaji anatakiwa kulipa kodi ya mwezi mmoja kwa dalali kama ujira wake, na asipolipa atafanyiwa figisu mpaka ashindwe kupata sehemu hiyo au ataletewa mtu mwingine na yeye kulazimika kuhama
Sasa swali linakuja hapa, nani anatakiwa kulipa ujira wa dalali? Kama dalali amepewa kazi na mwenye nyumba kwanini ujira alipe mpangaji? Kwanini asilipe mwenye nyumba aliyetoa shavu hilo kwa dalali?
Swali la nyongeza, kwanini mpangaji atakiwe kulipa kodi ya mwezi mmoja? Yaani gharama ile ile kwa mwenye mali inatakiwa iende sawa na kwa aliyetoa taarifa juu ya uwepo wake!
Ina maana imekosekana kabisa njia ya kumpa mpangaji unafuu na kumpunguzia, ikiwezekana kumuondolea kabisa mzigo huo? Lukuvi akiwa Waziri wa Ardhi alipiga marufuku madalali kuwadai wapangaji kodi ya mwezi mmoj akiita kitendo hiko kuwa ni ujambazi, akisema mwenye nyumba ndio alipe pesa hiyo.
Katazo hili liliishia wapi? Ilikuwa ni kauli tu ya kisiasa kufurahisha watu huku wakiaacha wananchi waendelee kuumia?
Wakuu mnazungumziaje suala hili.